Orodha ya mistari ya biblia kuhusu watoto.

Orodha ya mistari ya biblia kuhusu watoto.

Mistari ya biblia kuhusu watoto


Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/F1fZHcuNCB69aZsaGFpe3E

Tazama mistari hii, na chini kabisa utapata orodha ya masomo ya kujifunza kuhusu watoto, kwako wewe kama mzazi/mlezi.

Isaya 54:13 “Na watoto wako wote watafundishwa na Bwana; na amani ya watoto wako itakuwa nyingi”.

Mathayo 19:14 “Lakini Yesu akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu; wala msiwazuie; kwa maana walio mfano wa hao, ufalme wa mbinguni ni wao”.

Wakolosai 3:20 “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana”.

Mithali 1:8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,

9 Kwa maana hayo yatakuwa kilemba cha neema kichwani pako, Na mikufu shingoni mwako”.

Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.

2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,

3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”.

Luka 2:52 “Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu”.

3Yohana 1:4 “Sina furaha iliyo kuu kuliko hii, kusikia ya kwamba watoto wangu wanakwenda katika kweli”.

Marko 10:15 “Amin, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.

16 Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia”.

1Timotheo 4:12 “Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi”.

Zaburi 127:3 “Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, Uzao wa tumbo ni thawabu”.

Zaburi 34:11 “Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha Bwana”.

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”.

Mithali 22:15 “Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali”.

Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

Mithali 13:24 “Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema”.

Mithali 19:18 “Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini; Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake”.

Waebrania 12:11 “Kila adhabu wakati wake haionekani kuwa kitu cha furaha, bali cha huzuni; lakini baadaye huwaletea wao waliozoezwa nayo matunda ya haki yenye amani”.

Mithali 29:17 “Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako”.

Mithali 17:6 “Wana wa wana ndio taji ya wazee, Na utukufu wa watoto ni baba zao”.

Waefeso 6:4 “Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya Bwana”.

Mafundisho muhimu ya wazazi kwa watoto.

Rudi Nyumbani:

Je! utapenda mafundisho ya Neno la Mungu ya kila siku yawe yanakufikia kwa njia ya whatsapp au email yako? Kama ndio, basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Flora jovine urio
Flora jovine urio
10 months ago

Naomba nipate kwa njia ya whtsapp 0754941902

Diana Simeo
Diana Simeo
1 year ago

Mafudisho ya neno lamungu

Anonymous
Anonymous
1 year ago

Napenda niyapate masomo yenu kwanjia ya email

Anonymous
Anonymous
1 year ago
Reply to  Anonymous

Natak niyapate mafunzo yenu kupitia wattsap