Title February 2019

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

Mtu ambaye ni mwepesi kuudhiwa, au mwepesi kulia, au mwepesi kukasirishwa basi mtu huyo mara nyingi anakuwa pia ni mwepesi kusahau makosa, au mwepesi kufurahi au mwepesi kucheka..Lakini mtu ambaye ni mzito kuudhika pale anapoudhiwa, au kukasirika au kulia au kuwaka hasira, basi mtu huyo vile vile mpaka afikie hatua ya kukasirishwa na baadhi ya mambo basi ujue kuwa itachukua muda sana kuituliza ghadhabu yake au hasira yake.

Tuchukulie tu mfano mtoto mdogo, kama ukimtazama kwa siku anaweza kulia hata mara tano au sita, utakuta kinachomliza ni vitu vidogo vidogo tu visivyo na maana, lakini mtu huyo huyo dakika chake mbeleni utakuta ameshasahau anacheza na wewe kana kwamba hujawahi kumuudhi kabisa..Lakini tuje kwa mtu mzima, anaweza asidondoshe chozi kwa hata kwa mamiaka, lakini siku ukimkuta analia basi ujue kuna jambo zito, tena zito sana tena sio jepesi hata kidogo, pengine utakuta ni msiba au kaumizwa sana,au kajeruhiwa sana, na hivyo mpaka hali hiyo imetokea ndani yake, basi haiwezi kuwa ni kitendo cha dakika chache kuondoka, pengine itamgharimu miezi au miaka ndipo iishe kabisa.

Hali kadhalika biblia imetuweka wazi kabisa, kuhusu hali ya Mungu wetu wa mbinguni tunaye mwabudu siku zote, yeye ni Mungu mvumilivu sana, ni mwingi wa rehema, ni mnyenyekevu, ni mwenye neema, ni mwingi wa huruma, haoni hasira haraka,..Na ni kweli ndivyo alivyo hata sisi wenyewe tunalishuhudia leo hilo pale tunapoona watu tunaona wanatembea barabarani uchi, watu wanamtukana Mungu hadharani lakini hasemi chochote, watu wanawachinja wenzao kama wanyama bila huruma na Mungu hafanyi lolote, watu wanawakata viungo watoto wadogo wasio na hatia wakiwa hai, na kuchukua viungo vya maalbino, wengine wanawachuna ngozi ili kwenda kuuza kwa waganga, mpaka tunajiuliza hivi Mungu hayaoni haya yote? Mbona hachukui hatua yoyote kali..Ingekuwa ni wewe au mimi ni Mungu ni wazi kuwa hakuna hata mmoja angesalia tungeshawateketeza wote.Lakini kwa Mungu haipo hivyo yeye alisema “..

Bwana si mwepesi wa hasira, (Nahumu 3:1)…Ni mpole wa Hasira, mwingi wa rehema (Hesabu 14:8)

Pia

Kutoka 34: 6 “….,Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli;

7 mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi;..”

Na pia Daudi anashuhudia hilo na kusema “Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, Zaburi 145:8” Na  ukisoma pia Yona 4:2 na Nehemia 9:17..utathibitisha jambo hilo hilo.

Unaona hiyo ndio sifa yake kuu.. Lakini yeye kuonyesha rehema zake hata kwa waovu sio kwamba anapenda kuendelea kuwaona wanafanya mambo yao maovu, bali kinyume chake anataka wote wafikie toba, na ndio maana kila siku anawahubiria watubu, Lakini wasipotaka kutubu, kama tulivyoona kuwa mtu Yule ambaye si mwepesi kuudhika, ikifika siku ameudhika basi jua kuwa ghadhabu yake haiishi leo wala kesho, ndivyo ilivyo kwa Mungu ukali wa hasira yake hakuna atakayeweza kuuzima, si kwa toba wala kwa kulia siku ile itakapofika..

Watu wa kipindi cha Nuhu walipuuzia sana uvumilivu wa Mungu kwao, walihuburiwa injili kwa miaka mingi, lakini waliona mbona hakuna dalili yoyote ya kuadhibiwa, kama vile Mungu hayupo, Mungu hawezi kuangamiza dunia yote na watoto ndani yake,ndivyo walivyokuwa wanajifariji, Nuhu alionekana kama kichaa anacheza lakini siku ile walipoingia kwenye safina, ndipo waovu walipojua kweli hasira ya Mungu ni kali…watu 8 tu kati ya mabilioni ya watu waliokuwa wanaishi duniani ndio waliopona…Vivyo hivyo ilikuwa katika siku za Lutu, na ndivyo itakavyokuwa katika SIKU ILE YA HASIRA YA BWANA kama Bwana alivyoifananisha siku ile na hizo, ambayo hiyo ipo karibuni sana kutokea. Kutakuwa na kulia lakini Mungu hatasikia, kutakuwa na maombolezo lakini Mungu hataokoa, utasema ni wapi tena jambo hilo lilishawahi kutokea kwenye Maandiko,? Wakati wana wa Israeli walipoonywa kwa mamia ya miaka waache maovu na wamgeukie Mungu, lakini hawakutaka, Bwana aliwaonya waache maovu wasije wakapelekwa utumwani hawakusikia, wakatenda maovu mpaka ikafikia hatua ya Mungu kutokusamehe tena..kikombe cha ghadhabu ya Mungu kilikuwa kimejaa juu yao, ulinzi wa kiMungu ukaondoka juu yao, Nebukadneza akaja akawachinja watu mbele ya macho kama kuku, na waliosalia akawapeleka utumwani Babeli.. Tunasoma hayo katika.

 2 Nyakati 36: 11 “Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja, alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka kumi na mmoja;

12 akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, Mungu wake; wala hakujinyenyekesha mbele ya Yeremia nabii aliponena kwa kinywa cha Bwana.

13 Tena akamwasi mfalme Nebukadreza, aliyemwapisha kwa Mungu; lakini akajifanyia shingo ngumu, akajitia moyo nguvu asimgeukie Bwana, Mungu wa Israeli.

14 Na zaidi ya hayo wakuu wote wa makuhani, na watu, wakakosa mno sawasawa na machukizo yote ya mataifa; wakainajisi nyumba ya Bwana aliyoitakasa katika Yerusalemu.

15 Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;

16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.

17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake”.

Soma tena mstari wa 15 na wa 16…inasema.. “Bwana aliwatumia wajumbe wake, kwasababu aliwahurumia lakini wakawacheka na kuwadhihaki, hata ilipozidi ghadhabu HATA KUSIWE NA KUPONYA”..Unaona kuna hatua inafika kutakawa HAKUNA KUPONYWA TENA!! Yaliyotokea yametokea, hayawezi kubadilika tena wala kubadilishwa.

Ndugu usidhani ukiachwa sasa kwenye UNYAKUO utakuwa na nafasi ya pili mbele za Mungu, kwamba utatubu na Mungu atakuhurumia, Fahamu nafasi ni moja tu nayo ni kwa Njia ya YESU KRISTO peke yake na sio kwa njia yako, ingekuwepo ipo nafasi nyingine, Yesu asingesema mtu haji kwa Baba isipokuwa kwa njia yangu mimi, badala yake angesema mtu haji kwa Baba isipokuwa kwa njia yangu au yako..Hautafika mbinguni ndugu kama chujio la UNYAKUO litakupita.. Na wote watakaobaki hakuta kuwa na lingine lililosalia kwao isipokuwa kukutana na ghadhabu ya hasira ya Mungu, na hiyo haina lengo lingine zaidi ya kuwaharibu watu wote waovu ambao, walikataa neema, walikataa kuishi maisha ambayo Mungu alikusudia kila mwanadamu ayaishi, ni mapigo ambayo hata mtu aombolezaje hawezi kusikiwa.

Kumbuka hiyo ni tofauti na dhiki ya mpinga-kristo, siku ya Bwana ni tofauti kabisa, ni wakati Mungu aliojitengea kujilipizia kisasi cha hasira yake. Usitamani uwepo huo wakati ukadhani kuwa utastahimili, au utaokoka..

Yoeli 2: kwa kuwa siku ya Bwana ni kuu, yenye kitisho sana; naye ni nani awezaye KUISTAHIMILI.

Bwana anasema tena Siku hiyo watu duniani wataadimika kuliko DHAHABU, kumbuka sio kama dhahabu, hapana! bali kuliko dhahabu…Tafakari hilo neno tunajua dhahabu ni jamii ya mawe, lakini upatikanaji wake sio wa kwenda tu nje na kuikota kama kokoto, ndivyo itakavyokuwa siku hiyo watu watakuwa wachache sana kama vile dhahabu ilivyoadimu, si ajabu hili taifa lote la Tanzania watasalia watu 2 au 3 tu au asisalie mtu kabisa…wakati wa gharika watu waliadimika kama dhahabu, alisalia Nuhu tu wanawe watatu na wake zao.

Isaya 13: 6 “Pigeni kelele za hofu; maana siku ya Bwana i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu.

7 Kwa sababu hiyo mikono yote italegea, na moyo wa kila mtu utayeyuka.

8 Nao watafadhaika; watashikwa na utungu na maumivu; watakuwa na utungu kama mwanamke aliye karibu na kuzaa; watakodoleana macho; nyuso zao zitakuwa ni nyuso za moto.

9 Tazama, siku ya Bwana inakuja, SIKU KALI, YA HASIRA NA GHADHABU KUU, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.

11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;

12 NITAFANYA WANADAMU KUADIMIKA KULIKO DHAHABU SAFI, na watu kuliko dhahabu ya Ofiri.

13 Kwa hiyo nitazitetemesha mbingu, na dunia itatikiswa itoke katika mahali pake, kwa sababu ya ghadhabu ya Bwana wa majeshi, na kwa sababu ya siku ya hasira yake kali.

 

Adhabu hiyo itakuwa ndani ya yale mapigo ya vitasa 7. (Ufunuo 16 :1-21). Embu tazama kwa ufupi yatakayo tokea.

Ufunuo 16:1 “Nikasikia sauti kuu kutoka hekaluni, ikiwaambia wale malaika saba, Enendeni, mkavimimine vile vitasa saba vya ghadhabu ya Mungu juu ya nchi.

2 Akaenda huyo wa kwanza, akakimimina kitasa chake juu ya nchi; pakawa na jipu baya, bovu, juu ya wale watu wenye chapa ya huyo mnyama, na wale wenye kuisujudia sanamu yake.

3 Na huyo wa pili akakimimina kitasa chake juu ya bahari, ikawa damu kama damu ya mfu, na vitu vyote vyenye roho ya uhai katika bahari vikafa.

4 Na huyo wa tatu akakimimina kitasa chake juu ya mito na chemchemi za maji; zikawa damu.

5 Nami nikamsikia malaika wa maji akisema, Wewe u mwenye haki, uliyeko na uliyekuwako, Mtakatifu, kwa kuwa umehukumu hivi;

6 kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe; nao wamestahili.

7 Nikaisikia hiyo madhabahu ikisema, Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, ni za kweli, na za haki, hukumu zako.

8 Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto.

9 Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu yamapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu.1

10 Na huyo wa tano akakimimina kitasa chake juu ya kiti cha enzi cha yule mnyama; ufalme wake ukatiwa giza; wakatafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu,

11 wakamtukana Mungu wa mbingu kwa sababu ya maumivu yao, na kwa sababu ya majipu yao; wala hawakuyatubia matendo yao.

12 Na huyo wa sita akakimimina kitasa chake juu ya mto ule mkubwa Frati; maji yake yakakauka, ili njia itengenezwe kwa wafalme watokao katika maawio ya jua.

13 Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.

14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.

15 (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)

16 Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni.1

17 Na huyo wa saba akakimimina kitasa chake juu ya anga. Sauti kuu ikatoka katika hekalu, katika kile kiti cha enzi, ikisema, Imekwisha kuwa.

18 Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo.

19 Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake.

20 Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.

21 Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno.

(Ikiwa utahitaji kufahamu kwa urefu juu ya vitasa 7 nitumie ujumbe inbox, nitukutumie uchambuzi wake wote.)…Sasa baada ya hayo mapigo kuisha kitakachofuata ni Hukumu kisha ziwa la moto.

Lakini hayo ni machache kati ya mengi yatakaowakuta wale wote ambao watakosa UNYAKUO sasa ambapo dalili zote zinaonyesha kuwa kizazi chetu hichi ndio kile Yesu alichokizungumzia kuwa hayo yote yatatimia..Ni saa gani hii tunaishi?..Kwanini huyathamini maisha yako ya milele?..Kwanini unaipuuzia hiyo neema iliyo juu yako? Unazini lakini Mungu hakusemeshi chochote, unatazama pornography kwa siri, lakini Mungu hakuadhibu kwa lolote, unafanya mambo machafu lakini Mungu kama vile hakuoni..sio kwamba anapendezwa na wewe au kwamba wewe ni mtu pekee sana kwake, na ndio maana hayakukuti mabaya sasa..

Lakini fahamu si mwepesi wa hasira ni Mwingi wa huruma..uvumilivu wake ndio unaokuvuta utubu..

2Petro 3:8 “Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.

9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, BALI HUVUMILIA KWENU, MAANA HAPENDI MTU YE YOTE APOTEE, BALI WOTE WAFIKILIE TOBA.

10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,”

Usipotubu leo upo wakati mbaya unakusubiria mbeleni usiokuwa na msamaha. Leo hii ukiwa tayari kuyakabidhi maisha yako kwa Bwana kwa kumaanisha kabisa, na sio nusu nusu, mguu mmoja huku na mwingine kule atakusamehe kabisa na kuyafuta makosa yako yote, kwasababu hicho ndicho anachokitafuta kwako.

Na ndio maana anasema:

Sefania 2: 3 “Mtafuteni Bwana, enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; HUENDA MTAFICHWA KATIKA SIKU YA HASIRA YA BWANA”.

Uamuzi ni wako, lakini maombi yangu leo utubu ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.Kisha baada ya hapo utakuwa umezaliwa mara ya pili, kwa Roho Mtakatifu atakayeingia ndani yako”

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo

 


Mada Zinazoendana:

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

KIKOMBE CHA GHADHABU YA MUNGU KINAJAA…NI WAKATI WA KUTUBU NA KUMGEUKIA MUNGU

MUNGU ANASEMA HATAGHARIKISHA DUNIA NA MAJI TENA,.KWANINI WATU WANASEMA DUNIA ITAANGAMIZWA?


Rudi Nyumbani

Print this post

SIRI YA MUNGU.

Shalom Mwana wa Mungu, karibu tujifunze biblia, chakula cha uzima, kitupacho afya rohoni, leo kwa Neema za Bwana tutajifunza kwa ufupi, juu ya SIRI YA MUNGU.

Biblia imetaja sehemu kadha wa kadha juu ya Siri ya Mungu, na leo tutajifunza hii siri ya Mungu ni ipi.

Warumi 16: 25 “Sasa na atukuzwe yeye awezaye kuwafanya imara, sawasawa na injili yangu na kwa kuhubiriwa kwake Yesu Kristo, sawasawa na ufunuo wa ile SIRI iliyositirika tangu zamani za milele”.

Unaona hapo, biblia imetaja kuwa ipo SIRI iliyokuwa imesitirika tangu zamani za milele.

Sasa kabla ya kwenda kujifunza hiyo siri ni ipi, ni vizuri kwanza tukaelewa neno SIRI lina maana gani kama lilivyotafsiriwa katika biblia yetu hii ya Kiswahili, Kumbuka lugha yetu ya Kiswahili haijajitosheleza kwa maneno mengi, kwamfano yapo maneno katika lugha ya kiingereza au kigiriki ambayo ukiyaleta katika lugha yetu ya Kiswahili yanakosa tafsiri. Na pia yapo maneno yetu ya lugha ya Kiswahili ambayo ukiyapeleka katika lugha ya kiingereza yanakosa tafsiri, kwa mfano neno “shikamoo” halina tafsiri kwa kiingereza. Lakini pia yapo maneno ya kiingereza yenye tafsiri zinazokaribiana sana hivyo yakiletwa katika lugha yetu ya Kiswahili yanatumia tafsiri moja, kwamfano neno la kingereza “mouse” na “rat” tafsiri yake kwa kiswahili ni moja tu ambayo ni panya, hali kadhalika maneno mengine kama “rabbit” na “hare” yote kwa Kiswahili tafsiri yake ni “sungura”

Lakini pia kuna maneno mawili ya kiingereza yenye maana zinazokaribiana sana lakini hayafanani..na maneno hayo ni “Secret” na “mystery”…yote tukiyaleta katika lugha yetu ya Kiswahili yana tafsiri moja yaani “SIRI” lakini yana maana mbili tofauti.

“Secret” ni neno la kiingereza lenye maana ya “kipande cha taarifa ambacho kinajulikana na mtu mmoja au zaidi ya mmoja, na kimehifadhiwa kisijulikane na watu wengine zaidi ya hao wanaokijua”…kwamfano wahalifu wawili wanapopanga njama ya kuvamia mahali fulani hiyo njama ni “siri”, au vikundi fulani vya upelelezi huwa vinafanya kazi zao katika siri, ikiwa na maana vina baadhi ya taarifa ambazo ni wao tu wanaozijua na hawampi mtu mwingine yeyote taarifa hizo, (wanafanya kazi zao katika siri).

Lakini tukirudi kwenye neno la pili la kiingereza linaloitwa “mystery” ambalo kwa Kiswahili limetafsiriwa hivyo hivyo “siri” lenyewe lina maana tofauti kidogo, neno hili mystery tafsiri yake halisi ni hii “ni taarifa ambazo hazijulikani na mtu hata mmoja, hazijulikani chanzo chake, wala sababu ya jambo hilo”..kwamfano mtu anapowasha taa na giza kuondoka, ulishawahi kujiuliza lile giza linakwenda wapi? Hakuna mtu anayejua, wala huwezi kupata jibu la hilo swali kwa mtu yeyote Yule, kwahiyo hiyo inajulikana kama mistery “Mystery”, ambapo kwa Kiswahili tunaweza kusema ni siri ya ndani sana isiyoweza kueleweka wala kuchunguzika.

Biblia inasema katika: 

Ayubu 38: 19“Iko wapi njia ya kuyafikia makao ya nuru? Na giza pia, mahali pake ni wapi?

20 Upate kuipeleka hata mpaka wake, Upate kuelewa na mapito ya kuiendea nyumba yake?

Ayubu 38: 24 “Je! Nuru hutengwa kwa njia gani, Au upepo wa mashariki hutawanywaje juu ya nchi?”

Hizo zote ni mystery au siri za ndani zisizoelezeka. Hali kadhalika jinsi mtoto anavyoumbika katika tumbo la mwanamke, hakuna ajuaye ni nani alipeleka mifupa migumu kule, ni nani aliingiza nywele, n.k. vyote hivyo vinabakia katika siri kuu sana (Mysteries), zisizojulikana na kushangaza watu.

Sasa baada ya kuelewa hayo, tukirudi kwenye biblia kuna kitu kinachoitwa SIRI YA MUNGU, kama tulivyotangulia kusema…sasa hiyo siri inayozungumziwa hapo sio siri yenye tafsiri ile ya kwanza “secret” bali ni siri yenye tafsiri ile ya pili “mystery”, Kwahiyo siri ya Mungu haikuwa ni kipande cha taarifa fulani kilichojificha kilichojulikana na baadhi ya watu wachache tu, na kwamba kisingepaswa kijulikane na watu wengine, hapana badala yake bali siri ya Mungu ilikuwa ni taarifa au jambo ambalo lililokuwa halijulikani na mtu awaye yeyote Yule hata MALAIKA wa mbinguni, walikuwa hawalijui wala hawalielewi, hakuna taarifa zozote kuhusiana na hilo jambo, mtu anaweza akakisia tu lakini asiwe na taarifa zozote sahihi kuhusiana na hilo jambo, kama tu vile tusivyoelewa giza huwa linakwenda wapi pindi mwanga unapokuja, na linatokea wapi pindi mwanga unapoondoka..wala hakuna mtu yeyote anaweza kutupa majibu ya hayo maswali, kadhalika na siri ya Mungu ndio ilikuwa hivyo hivyo(ilikuwa ni mystery na sio secret).

Sasa hii SIRI ya ajabu ya Mungu ilikuwa ni ipi?

Mtume Paulo alitoa majibu ya swali hilo kwa uwezo wa Roho.

Wakolosai 1:26 “SIRI ile iliyofichwa tangu zamani zote na tangu vizazi vyote, bali sasa imefunuliwa kwa watakatifu wake;

27 ambao Mungu alipenda kuwajulisha jinsi ulivyo utajiri wa utukufu wa SIRI HII KATIKA MATAIFA, nao ni KRISTO NDANI YENU, TUMAINI LA UTUKUFU

28 ambaye sisi tunamhubiri habari zake tukimwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtu katika hekima yote, tupate kumleta kila mtu mtimilifu katika Kristo”.

Unaona hapo, biblia inasema siri ambayo ilikuwa imefichwa tangu vizazi vyote, ikiwa na maana hakuna mtu aliyekuwa anaijua, lakini ilifunuliwa zamani za mitume, na siri hiyo haikuwa nyingine zaidi ya KRISTO YESU KUINGIA ndani yetu sisi watu wa MATAIFA. Haleluyaa!!

Tangu zamani yote, hakuna mtu angeweza kudhania kuwa sisi watu wa mataifa tungekuja siku moja kuwa wana wa Mungu, sisi tuliokuwa tunaitwa najisi, watu tuliokuwa mbali na Mungu, hakuna mtu angetegemea siku moja Wana wa Farao waliowatesa wana wa Israeli kwamba wangekuja kuitwa wana wa Mungu aliye juu, hakuna mtu angedhania kuwa wafilisti watu waliokuwa wanaitwa wasiotahiriwa kwamba siku moja watakuja kuitwa wana wa Mungu aliye juu, hakuna mtu angekuja kujua kuwa wamoabi waliowalaani wana wa Israeli wakati wanaelekea nchi ya ahadi, siku moja watakuja kuitwa wabarikiwa wateule wa Mungu aliye juu kwa kupitia Yesu Kristo, Ingekuwaje kuwaje kwanza ni sawasawa na sasahivi mtu akwambie kuna wakati utafika wachina wote wataitwa wamasai tena wamasai wa damu kabisa, ni jambo lisilosadikika. hakika hiyo ilikuwa ni siri ya ajabu ambayo isingeweza kudhaniwa na mtu yeyote, ni siri ambayo hata malaika walikuwa hawaijui. Lakini ilikuja kufunuliwa siku za mwisho.

Hakuna mtu angeweza kudhania kuwa MASIHI ambaye ametabiriwa kuja kuwaokoa wana wa Israeli peke yao, angekuja kwanza kuanza wokovu kwa watu wa mataifa, wanaoabudu sanamu, hakuna mtu au malaika angeweza kudhania kuwa siku moja Roho mwenyewe wa Mungu atakaa ndani ya watu wa mataifa. Hata malaika wa mbinguni hawakujua hiyo neema imetoka wapi, kama vile tusivyojua giza chanzo chake ni wapi, hiyo ni mystery.

Kwahiyo YESU KRISTO, kuja kutuokoa sisi watu wa MATAIFA hiyo ndiyo ilikuwa SIRI YA MUNGU, iliyofichika tangu zamani za milele, hata Musa alikuwa hajui kwamba siku moja Uzao wa Farao utamwabudu Mungu wa Israeli kupitia Masihi, hata Eliya alikuwa hajui kwamba siku moja wale alioomba moto ushuke juu yao watoto wao watakuja kumjua Mungu wa kweli na kupata kibali mbele za Mungu, Hata Daudi hakujua kwamba wale aliokuwa anawaimbia maadui maadui siku moja watakuja kuwa marafiki wa karibu wa Mungu kupitia BWANA WA UTUKUFU YESU KRISTO.

Waefeso 3:1 “Kwa sababu hiyo mimi Paulo ni mfungwa wake Kristo Yesu kwa ajili yenu ninyi Mataifa;

2 ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwa ajili yenu;

3 ya kwamba kwa kufunuliwa nalijulishwa SIRI HIYO, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache

4 Kwa hayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika SIRI YAKE KRISTO.

5 SIRI HIYO HAWAKUJULISHWA WANADAMU KATIKA VIZAZI VINGINE; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho;

6 YA KWAMBA MATAIFA NI WARITHI PAMOJA NASI WA URITHI MMOJA, na wa mwili mmoja, NA WASHIRIKI PAMOJA NASI WA AHADI YAKE ILIYO KATIKA KRISTO YESU KWA NJIA YA INJILI”

7 Injili hiyo ambayo nalifanywa mhudumu wake, kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake.

8 Mimi, niliye mdogo kuliko yeye aliye mdogo wa watakatifu wote, nalipewa neema hii ya kuwahubiri Mataifa utajiri wake Kristo usiopimika;

9 NA KUWAANGAZA WATU WOTE WAJUE HABARI ZA MADARAKA YA SIRI HIYO, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote;

10 ili sasa, kwa njia ya kanisa, hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi ijulikane na falme na mamlaka katika ulimwengu wa roho;

11 kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Mstari wa 9 unasema “NA KUWAANGAZA WATU WOTE WAJUE HABARI ZA MADARAKA YA SIRI HIYO”.

Ndugu unayesoma ujumbe huu, ukimjua Yesu Kristo, kwa mapana haya au zaidi ya haya, utaogopa!! Utajua ni jinsi gani hatukustahili lakini tumefanywa tustahili, utajua ni jinsi gani Neema ya Mungu inatisha,..kwasababu kama linafanyika jambo ambalo kwa namna ya kawaida haliwezekani, wala halielezeki, hiyo inatisha!! Hakuna mtu yeyote anayeweza kuelezea hii neema imetoka wapi? Kila mtu anashangaa hata malaika…iweje hawa watu wasiofaa wapokee kipawa cha neema kubwa namna hii? Manabii wa zamani na wenyewe walionjeshwa kidogo tu! Lakini bado hawakuielewa. Waliona tu lakini wasielewe chochote, pengine walidhani watu wa mataifa watakujua kumweshimu masihi tu, lakini sio kufanywa na wao warithi wa ahadi za Mungu.

 Ndugu, usiudharau msalaba, Kristo amehubiriwa kwako mara ngapi?..utapataje kupona usipouthamini wokovu MKUU namna hii?? Waebrania 2:3…kumbuka maisha yako ni kitabu na matendo yako ni kalamu yenye wino, yanaandika matendo yako kila siku, kila mwezi na kila mwaka,. siku inapopita ni unaanza aya mpya, kila mwezi ni unafungua ukurasa mpya, na kila mwaka ni unaanza sura mpya ya kitabu chako,. Na kitabu chako unaanza kukiandika siku unapozaliwa…na kinaanza na JINA LAKO kwa nje, ndio maana baada ya kuzaliwa tu unapewa jina, na pengine umeshaandika nusu ya kitabu chako mpaka kufikia sasa, jitathamini katika hiyo nusu uliyoiandika umeandika ipasavyo?, siku ile ya mwisho kitabu chako kitafunguliwa tena maandiko yanasema hivyo na kitalinganishwa na kile kitabu cha uzima kama matendo yaliyoandikwa kwenye kitabu chako hayafanani na matendo ya kile kitabu cha Uzima, sehemu yako itakuwa ni katika lile ziwa la moto. Huko ndiko kukosekana jina lako katika kitabu cha uzima. Na kumbuka mbinguni hakuna makaratasi, hivyo kitabu cha uzima sio makaratasi yaliyoandikwa majina kama nakala za ankra, hapana bali na chenyewe ni maisha yaliyoandikwa, na cha kuogopesha ni kwamba hayo maisha sio mengine zaidi ya maisha ya watu yaliyoandikwa kwenye biblia, maisha ya mitume, maisha ya Yesu Kristo, maisha ya watakatifu wote, na Maneno yao waliyoyahubiri katika Roho, Ndio maana unaona biblia ni kitabu kilichojaa habari za maisha ya watakatifu, watu siku ya mwisho ndio watahukumiwa kulingana na hayo. Paulo anasema katika kitabu cha Warumi 2:16 “katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu”

Ufunuo 20: 11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.

12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; NA VITABU VIKAFUNGULIWA; na kitabu kingine kikafunguliwa, AMBACHO NI CHA UZIMA; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao……

15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”

Kwahiyo usiidharau sauti ya Mungu inapozungumza nawe moyoni, Bwana anataka kukupa uzima wa milele na kukuepusha na hukumu inayokuja, tumefunuliwa hii siri ya Mungu, ambayo wakina Musa walitamani kuijua lakini hawakuijua, na manabii wengine wote vivyo hivyo, kwahiyo saa ya wokovu ni sasa, sio baadaye wala kesho, kama hujayakabidhi maisha yako kwa Bwana fanya hivyo leo, hata kama wewe ni muislamu au mbudha unasoma ujumbe huu, siku ile hutasema hukusikia, na kumpa Bwana maisha sio kumpa lisaa, au masaa au siku, hapana unampa maisha yako yote yaani kuanzia leo na kuendelea mpaka siku utakapoondoka duniani, unakusudia kuishi kwa kumfuata yeye, katika njia zake zote, unakusudia kuacha dhambi zote ulizokuwa unafanya kama uasherati, ulevi, anasa, usengenyaji, chuki, kutokusamehe, usagaji, utoaji mimba, ushoga, utazamaji pornography, masturbation, disco, uvaaji wa vimini na suruali, na upakaji wa makeup mpaka unatoka kwenye asili yako ya ubinadamu n.k .

Yeye anakubali wakosa na atakupa uwezo wa kushinda dhambi, , kwasababu kwa nguvu zako hutaweza kushinda dhambi hata kidogo….yeye ndiye atakuwezesha kwa namna ya ajabu utajikuta unashinda mambo hayo endapo utakubali kumfuata, wengine tulikuwa wabaya kuliko wewe lakini Bwana alitutengeneza, tulikuwa tunadhani ilikuwa haiwezekani kuishi bila kufanya hayo mambo, lakini tumeahakikisha maneno ya Mungu ni kweli kuwa ni rahisi na ni raha sana kuishi bila hayo mambo, na hatuna tena mizigo wa dhambi,na hakuna kiu tena hata kidogo ya hayo mambo, kama aliyafanya kwetu, atayafanya na kwako pia, isipokuwa Bwana anataka watu wanaomaanisha sio watu wanaositasita katika mawazo mawili, ukishakusudia kwa matendo kuacha hayo mambo haraka sana bila kupoteza muda nenda kabatizwe katika ubatizo sahihi kulingana na maandiko ambao ni wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa Jina la Yesu Kristo kulingana na (Matendo 2:38), ili upate ondoleo la dhambi zako. Na baada ya hapo utakuwa milki halali ya Roho wa Mungu, utafanyika kuwa hekalu la Mungu kwa Roho atakayeingia ndani yako.

Na kama ulirudi nyuma, shetani anataka urudi zaidi ya hapo, nia yake ni akupeleke kwenye ziwa la Moto, hiyo ndiyo ndoto yake kubwa, sasa usikubali ndoto ya shetani itimie juu ya maisha yako, ziwa la moto aliandaliwa yeye na malaika zake..lakini anataka na wewe uende huko, hivyo mpinge na Bwana atakuwa upande wako.

Mungu akubariki sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

INARUHUSIWA KULA NYAMA YA NGURUWE KWA MKRISTO WA KWELI?

KITABU CHA UZIMA

MJUE SANA YESU KRISTO.


Rudi Nyumbani

Print this post

MKUU WA GIZA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, libarikiwe sana. Karibu tujifunze Biblia, leo kwa Neema za Bwana tutajifuza juu ya Namna ya kutoka katika uvuguvugu wa kidunia.

Katika kitabu cha ufunuo sura ya pili na ya tatu tunasoma juu ya ufunuo wa yale makanisa saba, na kama tunavyojua makanisa yale yalikuwa ni makanisa halisi kabisa, yaliyozaliwa kutokana na Injili za Mitume hususani mtume Paulo aliyokuwa anaihubiri nyakati hizo, hata hivyo yalikuwa ni zaidi ya saba, lakini Roho aliyachagua hayo saba kwa kusudi maalum kuyafundisha makanisa ya siku za mwisho ambayo tunayoishi, utaona kulikuwa na makanisa mengine yaliyokuwa Korintho, Galatia, thesalonike, filipi nk. lakini hayajatokea katika kitabu cha ufunuo isipokuwa yale saba tu..

Hivyo kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa vipindi vya kanisa utakuwa unajua kuwa, tayari kuna vipindi sita vimeshapita vya kanisa tangu Bwana Yesu Kristo aondoke, na sasa tupo katika kipindi cha kanisa la saba, na kanisa tulilopo ndilo la saba na la mwisho linalojulikana kama LAODIKIA. Kama hujafahamu kabisa jambo hili au ndio mara ya kwanza unalisikia basi katafute kujua kwasababu ni jambo linalojulikana na wasomaji wengi wa biblia, au nitumie ujumbe inbox nikutumie uchambuzi wa nyakati hizi saba za kanisa na wajumbe wake.

Sasa tabia ya hili kanisa la LAODIKIA ni kanisa vuguvugu, kama tunavyosoma katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana mlango wa tatu.

Ufunuo 3: 14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.

15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu UNA UVUGUVUGU, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja name”.

Kanisa hili la Laodikia lilianza mwaka 1906, na litaisha siku unyakuo utakapofika, sasa hili kanisa ndilo lililoonyesha tabia ya hatari kuliko makanisa mengine yote ya nyuma, kwasababu mbele za Bwana limepimwa na kuonekana kuwa ni vuguvugu, nusu Mungu, nusu shetani, ni kanisa Nafki, na ndio inayopelekea kuonekana kuwa ni kanisa lililoharibika kuliko makanisa yote.

Sasa huu uvuguvugu unatoka wapi?..Huu uvuguvugu ni Pepo maalumu lililotoka kuzimu, na kutumwa duniani ili kufanya kazi maalumu ya ushawishi, na hili pepo halijatumwa kwa mtu mmoja hapana bali limetumwa kwa kizazi…Ni pepo lenye nguvu mara saba zaidi ya mapepo mengine yote..Ni pepo linalotenda kazi katika viwango vya juu kabisa vya utendaji kazi wa shetani, ambalo kazi yake hasa ni kuwakosesha wanadamu wa kizazi cha siku za mwisho wamkosee Mungu wao, ili Mungu awakatae kabisa kabisa na kuwakana.

Sasa tujifunze kwa ufupi hili pepo linatendaje kazi, kabla ya kuja kuona madhara atakayoyapata mtu yule endapo hatalishinda..

Biblia inasema katika Waefeso 6: 11 

“Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, JUU YA WAKUU WA GIZA hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho”.

Sasa Hawa wakuu wa giza wanaozungumziwa hapa wapo SABA, katika kila kanisa kulikuwa na mkuu mmoja, na katika hili kanisa la Laodikia yupo mmoja na ndiye mwenye nguvu kuliko wote. Na kama jina lake lilivyo “mkuu wa giza” anahakikisha kunakuwa na giza katika ulimwengu wa roho, anahakikisha hakuna nuru, na anahakikisha Nuru ya haki haiwazukii watu.

Na kauli mbiu yake aliyoipokea kutoka kwa shetani mkuu wake ni “KUHAKIKISHA WATU WOTE WANAKUWA VUGUVUGU DUNIANI”…kwahiyo anayo mapepo chini yake anayofanya nayo kazi kuhakikisha anatimiza lengo hilo. Kumbuka huyu mkuu wa anga, hatumshindi kwa kumkemea, hapana! Tutakuja kuona mbeleni namna ya kulishinda hili pepo.

Sasa anachokifanya ni kutumia nguvu za giza, na mapepo yake kuwafanya watu wawe vuguvugu, sio wanakuwa baridi wala moto! Hapana bali wanakuwa vuguvugu, hilo ndio lengo lake kubwa…Anahakikisha watu wamfahamu Mungu kidogo, na waufahamu uovu kidogo!..hataki kabisa mtu awe baridi hilo halitaki, anataka mtu awe hapo katikati..kwasababu anajua Mungu anamchukia mtu vuguvugu kuliko hata mtu yule aliye baridi..yaani kwa Mungu ni heri mtu awe mlevi na mwasherati moja kwa moja, kuliko mtu ambaye ni mwasherati kwa siri na bado anaenda kanisani au bado anasali..Huyo kwa Mungu anafananishwa na MATAPISHI!! Ni Bwana mwenyewe ndio alisema hivyo “ni heri ungekuwa moto au baridi kuliko kuwa vuguvugu”. Hivyo kule kuzimu katika vikao vyao ndio wameona wakifanikiwa kumfanya tu mtu awe vuguvugu, basi watakuwa wamemlaza kwa kila kitu.

Sasa hili pepo lenye nguvu mara saba kuliko mengine ndio lengo lake kubwa hilo!… wengi wanajua kuwa shetani mwanzoni alikuwa ni malaika mbinguni, lakini hawajui kuwa baada ya kulaaniwa hakunyanganywa nguvu zake na akili zake bali aliendelea kuwa nazo..Hivyo ni muhimu kujua kuwa yeye naye anatenda kazi kwa akili sana kiasi kwamba pasipo Roho wa Mungu, ni rahisi kuwadanganya hata yamkini walio wateule. Atahikikisha anatumia ushawishi mkubwa kumfanya mtu ajione yupo sawa na Mungu wakati bado ni mwasherati, mlevi, mla rushwa, anaishi na mwanamume au mwanamke ambaye hawajafunga ndoa, na bado mtu huyo ajione yupo sawa na Mungu n.k.

Huwa inauma sana unapokutana na mtu na unamwuliza umempa Bwana maisha yako na anakujibu NDIO, na unaendelea kumwuliza je! Bwana akija leo una uhakika wa kwenda naye mawinguni anakujibu NDIO nina uhakika kabisa, lakini ukija kumwangalia maisha yake utahuzunika kiasi cha kufa..

Kwamfano kuna mtu mmoja alinitumia ujumbe akaniambia mtumishi naomba uniombee kwasababu ni miaka mingi sasa sijapandishwa kazi, mimi ni kibarua tu,kazi yangu ni ya udereva, na bado ninafamilia, kwakweli alivyokuwa anaeleza alitilisha huruma sana huyu ndugu, nikamwuliza umempa Bwana maisha yako? akanijibu NDIO, nikazidi kumwuliza je! unauhakika Bwana leo akija utakwenda naye? Akajibu Ndio ninauhakika..Nikazidi kumwuliza tena je! una uhakika uovu wote haupo ndani ya maisha yako?.. namaanisha sio mlevi, sio mwasherati, hauna mwanamke unayetembea naye ambaye hamjaoana, sio mtukanaji, sio mla rushwa, sio mtazamaji wa pornography, sio mfanyaji masturbation n.k. akaniambia ndio hafanyi hayo yote!…na zaidi ya yote ameoa na ana mtoto, sasa lengo la kumwuliza vile sio kumweka kwenye mtego hapana! Bali kujua chanzo cha tatizo lake ili nijue namna ya kumsaidia kulingana na maandiko.

Baada ya kuniambia vile basi nikamwambia huna haja ya kuwa na hofu, wala usiogope! Maadamu upo katika mstari wa Bwana, Bwana hawezi kukutupa, Zidi kudumu katika haki subiri wakati wa Bwana, Bwana atakupatia kazi nzuri tu! mwamini yeye, akajibu amina!..Najua alitegemea nimwombee lakini sikufanya vile..

Baada ya siku kadhaa, nikaingia kwenye mitandao, nikakutana na post yake mahali.. “nguvu ziliniishia”…mambo anayo ya-post hata wasiomjua Mungu kabisa wanaona aibu kushiriki na wengine post hizo, ni picha chafu zisizoelezeka!!..Nilijihisi vibaya sana.

Nimekutana na watu wengi sana wa namna hiyo..wanahitaji Bwana awafanyie kitu fulani katika maisha yao, wanatamani wafanikiwe katika maisha, wawe matajiri, lakini hawajijui kuwa wao ni maskini wa roho, wanajiona kuwa ni matajiri wa roho kumbe ni maskini, wanajiona wapo sawa na Mungu kumbe hawamjui Mungu kabisa, ni lile lile pepo la Laodikia ndio lipo juu yao na ndilo linalowapusha wengi macho! Wasitambue ni hali gani mbaya ya kiroho waliyopo.

Nikakutana na dada mwingine nikamwuliza umempa Bwana maisha yako, akajibu ndio nampenda sana, nikamwuliza unamfahamu mtu fulani (nilimtaja tu mhubiri fulani maarufu wa zamani)..akajibu ndio namjua, nikamwuliza ulimsikia wapi..akanitajia nilimsoma kwenye agano la kale!..nikamwambia mbona huyo hayupo kwenye agano la kale,..akaniambiaa aah samahani nilimsoma kwenye agano jipya! Nikwambia hayupo hata kwenye agano jipya, akaniambia yupo wapi?, nikamwambi ni muhubiri tu aliyewahi kutokea miaka hamsini iliyopita nyuma..Huyu pia sikumwuliza kwa nia ya kumtega bali nilikuwa nataka nimfundishe kitu,…lakini tayari yeye alikuwa anajiona anajua kila kitu hana haja ya kitu kingine, baada ya muda mfupi nilijaribu kumpeleka kwenye maandiko nimfundishe, akakwazika akaondoka.

Nikakutana na mwingine tena, …nikamwuliza dada umempa Bwana Yesu maisha yako akanijibu ndio nimempa, ndio mwokozi wangu na ninampenda sana, nikamwambia akija leo una uhakika wa kwenda naye, akanijibu kabisa asilimia 100, nikamwuliza unamjua aliyeandika kitabu cha mhubiri? Akasema hamjui, nikamwuliza aliyendika kitabu cha wimbo uliobora je! akasema pia simjui, nikamwambia kama kweli unampenda Bwana ingekupasa kuyajua haya yote na zaidi ya haya, ila sikulaumu!..nikataka kujaribu kumfundisha msingi wa imani ya kikristo kwanza ndipo tuendelee mbele..hakutaka kuendelea kuongea akakatisha mazungumzo na kuondoka.

Hilo ndio tatizo la watu wengi katika kizazi chetu hichi cha Laodikia, Tunamwomba Mungu utajiri, na wakati ndani ya mioyo yetu ni Adui yetu, tangu lini mtu akaenda kumwomba adui yake gari, au mali au fedha?? Je! Atampa? Sharti apatane naye kwanza ndipo hayo yote apewe…Wengi leo wanapenda kwenda kumwomba Mungu mali wakati ndani ya mioyo yao wamekorofishana naye, ni matapishi mbele za Mungu, wapo mbali naye, ndani ya mioyo yao kuna kila aina ya uchafu..uasherati, ulevi, rushwa, anasa, mizaha, usengenyaji, pornography, punyeto n.k Biblia inasema ..” 

Mathayo 23:25 Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi.

26 Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi.”

Ni lile lile pepo la LAODIKIA linalotenda tenda kazi katika siku hizi za mwisho, kuwafanya watu wajione kuwa wana kila kitu katika roho, wakati ni maskini wa roho..

Bwana Yesu anasema maneno haya… “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”.

Ndugu unayesoma ujumbe huu, kamwe usiruhusu hii roho ya uvuguvugu, kila siku yachunguze maisha yako, shetani yupo kazini, kuhakikisha kuwa unakuwa hapo katikati, si moto wala si baridi…Na kama maandiko yalivyotangulia kusema, Ni heri uwe baridi kabisa…ni heri ukawe mwasherati na useme hujaokoka, ni heri uwe mvaaji vimini na mpakaji lipstick na wanja na useme hujaokoka, ni heri uwe unaenda disco kila siku au unaishi na mwanamke/mwanamume ambaye hamjaoana na useme sijaokoka na wala simjui Mungu, wewe adhabu yako siku ile haitakuwa kubwa, kuliko useme mimi nimeokoka na unampenda Bwana wakati bado unavaa vimini, tena bila aibu unauonyesha maungo yako wazi kwenye mitandao, bado unapaka wanja mfano wa Yezebeli na lipstick kiasi kwamba tofauti yako na mwanamziki maarufu wa kidunia hapa nchi hakuna. Unamdhihaki Mungu. Wewe mbele za Mbele za Mungu ni matapishi na kinyaa.

Ni heri ukatubu sasa, na kukusudia kuacha hayo mambo, usiruhusu fikra zako zipotoshwe na mkuu wa ulimwengu huu(shetani) kwa kupitia wakuu wake wa anga..

Waefeso 2: 1 “Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;

2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, NA KWA KUMFUATA MFALME WA UWEZO WA ANGA, ROHO YULE ATENDAYE KAZI SASA KATIKA WANA WA KUASI;

3 ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine.

4 Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda;”

Unaona? Bwana anaweza kukugeuza ukikusudia kumfuata kweli kweli, unachopaswa kufanya ni kutubu kwa kudhamiria kabisa kuacha dhambi, na kufanya maamuzi ya kutokuwa vuguvugu tena!! Hiyo ndio njia pekee ya kulishinda hili PEPO(MKUU WA ANGA)wa Laodikia…Ni kufanya maamuzi thabiti kwamba kuanzia leo mimi na dhambi basiii….lipstick basi, vimini basi, ulevi basi, uasherati basi, rushwa basi, anasa basi, marafiki wabaya basi, pornography basi,..Huo ndio ushauri wa Bwana alioutoa kwa kanisa la Laodikia…anasimama mlangoni na kubisha, hataingia mpaka wewe umefungua mlango, hatavunja mlango wa moyo wako na kuingia kwa nguvu, anasubiri wewe ufanye maamuzi ya kuacha dhambi, ndipo aingie. Na baada ya hapo fanya hima ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo. Usishirikiane kabisa na MKUU WA GIZA HILI, na Bwana mwenyewe atachukua nafasi ya kuhakikisha haujikwai.

Mungu akubariki. Tafadhali “share” ujumbe kwa wengine.
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Zinazoendana:

Print this post

NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO:

Waebrania 6:4 “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,

5 na kulionja neno zuri la Mungu, NA NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO.

6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri”.

Neno hili linatuonyesha kuwa kumbe licha ya mtu kuangaziwa nuru ya Mungu, yaani kupewa neema ya kumjua na kumwamini Yesu Kristo ambaye ndio Nuru yenyewe (Yohana 1:4-5), bado anaweza kuonja kitu kingine ndani yake, licha ya kuonja vipawa vya kimbinguni na kufanywa mshirika wa Roho Mtakatifu yaani kwa kuvuviwa karama za Roho kama vile Lugha, unabii, miujiza, utume, uchungaji, ualimu, uinjilisti n.k. mambo ambayo hapo kabla hayakuonekana kati ya watakatifu au kama yalionekana basi ni kwa sehemu ndogo sana, bado anaweza kuonja kitu kingine cha tofauti kabisa,.licha pia ya mtu kuliona Neno zuri la Mungu kama andiko hilo linavyotuambia, yaani Injili ya Yesu Kristo Bwana wetu ambayo kwa hiyo manabii wengi na wenye haki walitamani kuisikia lakini hawakupata neema kama sisi tunavyojua sasa, lakini bado lipo jambo lingine ambalo tunaambiwa mtu anaweza kulionja kwa wakati huu …Na jambo lenyewe KUONJA NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO..

Zamani zijazo ni nini?, Na nguvu zenyewe ndio zipi?

Biblia inapotumia Neno ZAMANI mara nyingi inamaanisha “nyakati fulani” au “kizazi fulani”..Na au kwa lugha rahisi ni “wakati wa Ulimwengu husika”..Hivyo inavyotumia Neno “Zamani hizi” inamaanisha kuwa wakati wa ulimwengu huu…Kwamfano pale Bwana Yesu alipowaambia wanafunzi wake.

“..Hakika nawaambia, hakuna mtu aliyeacha nyumba, au mke, au ndugu, au wazazi, au wana, kwa ajili ya ufalme wa Mungu,

30 asiyepokea zaidi mara nyingi katika ZAMANI HIZI, na katika ulimwengu ujao uzima wa milele. (Luka 18:29).”

Unaona, Hapo alimaanisha asiyepokea zaidi mara nyingi katika ulimwengu huu wa sasa, na katika ulimwengu ujao uzima wa milele.

Vivyo hivyo inavyosema ZAMANI ZIJAZO..inamaanisha kuwa “nyakati za ulimwengu ujao”..Yaani ulimwengu baada ya huu mbovu tunaoishi kupita.

Sasa tukitazama mifano michache kwenye biblia itatusaidia kufahamu nini maana ya kuonja nguvu za zamani zijazo, embu tutazame ile habari moja ya yule mwanamke mkananayo ambaye Bwana Yesu alimfananisha na Mbwa.Tunasoma:

Mathayo 15: 21 “Yesu akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.

22 Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24 Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26 Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28 Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Sasa katika habari hii sio kwamba Bwana alikuwa anamtukana kumfananisha na mbwa, au labda alikuwa anajaribu kumkatisha tamaa ili amwache, hapana bali kinyume chake alikuwa anamweleza uhalisia wa mambo jinsi yeye alivyo katika ulimwengu wa roho, na si yeye tu peke yake, bali pia watu wote ambao hawakuwa wayahudi kwa kuzaliwa. Na ndio maana hata ukisoma habari utaona japo yule mwanamke alitaka kuzungumza na Bwana lakini Bwana hakumjibu chochote, mpaka alipokuwa anasisitiza sana, ndipo Bwana akalazimika kufungua kinywa na kumkumbusha nafasi yake ni ipi katika majira aliyokuwa anaishi…

Sasa kumbuka hakukuwa na wakati wowote ambao watu wa mataifa walimtazamia Kristo aje kuwaokoa isipokuwa wayahudi tu peke yao. Japo unabii ulishatangulia zamani kwa vinywa vya manabii kuwa utafika wakati ambao mataifa nao watamtumainia huyo masihi, lakini sharti kwanza akataliwe na watu wake, na kuuawa ndipo damu ipatikane ya kuwasafisha watu wote mataifa ili nao wapokee kipawa cha neema kwa namna ile ile moja kama wayahudi, ni lazima kwanza dhabihu itolewe ili iondoe kile kiambazi cha kati kinachowatenga watu wa mataifa na wayahudi, hivyo wakati huo usingekuja kwanza kabla ya watu wake wenyewe kumkataa..

Lakini tunaona huyu mwanamke wa huko Tiro nchi ya mataifa ya kipagani, kwa sasa ni nchi ya LEBANONI kaskazini mwa Israeli, anakuja na kumfuata Bwana kabla ya majira yake na kumwomba ampe neema amponye mwanae ambaye alikuwa amepagawa na mapepo, lakini Bwana akamwambia asubiri kwanza watoto washibe (yaani wayahudi waipate hiyo neema kwanza),Bwana alimwambia sikutumwa ila kwa kondoo wa Israeli waliopotea, lakini yule mwanamke hakusikia badala yake aliendelea kung’ang’ania kana kwamba ni haki yake, mpaka mwisho wa siku baada ya Bwana kuiona imani yake jinsi ilivyokuwa kubwa akampatia alichokuwa anakitafuta kinyume na mipango iliyokuwa imewekwa kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, tunaona mtoto wake alipona saa ile ile na ule haukuwa tu uponyaji wa mwili wake bali pia hata wa roho yake… mbwa hajasubiria makombo

Sasa Jambo lililofanyika pale katika ulimwengu wa roho, ni kuwa imani ya yule mwanamke ilikwenda mpaka kipindi cha mbeleni kabisa Kalvari siku ambayo Bwana anasulibiwa, Imani ile ikaichukua ile damu iliyokuwa inamwagika katika mishipa ya Emanueli pale Kalvari, ikairudisha sasa mpaka wakati wa nyuma waliokuwepo pale Tiro katika mazungumzo, ikadai haki yake ya ukombozi ambayo ilishapata huko mbeleni kwa mateso yake..Na matokeo yake ikapokea sawasawa na ilivyotaka…

Ni sawa na mtu leo analazimisa alipwe sasa hivi mshahara ambao anapaswa aje kulipwa baada ya miaka 10 , na anang’ang’ania alipwe sasa mpaka analipwa.

Sasa kwa tukio hilo huyu mwanamke tunaweza kusema “Ameonja nguvu za zamani zijazo”..Nguvu za Wakati ambao bado haujafika lakini tayari kashaanza kuyafurahia matunda yake.

Na ndivyo ilivyo hata kwa wakati huu wa kipindi hichi cha mwisho tunachoishi, biblia inaweka wazi kabisa kuwa mtu anaweza kuonja nguvu za zamani zijazo au nguvu za ulimwengu ujao..

Sasa Nguvu za ulimwengu ujao ndio zipi?

Biblia inatueleza huko katika ulimwengu mpya, katika utawala wa amani wa miaka 1000 na Kristo hakutakuwa na magonjwa,wala shida, wala tabu wala vifo.

Isaya 33: 24 “Wala hapana mwenyeji atakayesema, MIMI MGONJWA; watu wakaao humo watasamehewa uovu wao.

Malaki 4: 2 Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, LENYE KUPONYA KATIKA MBAWA zake; nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa mazizini”.

Unaona?, leo hii unapoumwa ugonjwa ambao hautibiki na Yesu anakuponya, hujui kuwa unaonja nguvu za zamani zijazo ambazo udhihirisho wake wote utaonekana katika ulimwengu ujao. Furaha na amani unayoipata sasa katika wokovu, hiyo ni kidokezo kidogo sana, kitakuja kujidhihirisha katika utimilifu wote kwenye huo ulimwengu ujao, Huna hofu ya mauti tena kama zamani kwasababu maisha yako yapo mikononi mwa Bwana, unatumaini sasa la uzima wa milele baada ya kifo, hapo umeonja uzima ambao unakuja huko mbeleni ambapo huko kutakuwa hakuna kufa.

Lakini kwa jinsi tunavyoukaribia mwisho basi fahamu kuwa ndivyo zile nguvu za ulimwengu ujao zitakavyozidi kuongezeka, na kuwa dhahiri katikati ya watu, unapoona wafu wanafufuliwa unadhani ni picha gani hapo Mungu anakuonyesha?,

Yapo mambo ambayo Mungu atakwenda kuyaachia siku hizi za mwisho yahusianayo na nguvu hizi za ulimwengu ujao ili kutimiza ule unabii wa Yoeli 2:28. Na jambo ambalo tutamalizia nalo ni kubadilishwa kwa miili yetu na kuvaa kutokuharibika yaani miili ya milele

1Wakorintho 15.53 “Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.

54 Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda”.

Hivyo Bwana anatazamia kuiona Imani thabiti ndani ya watu wake, Imani ya kumwamini Yeye mpaka kufika hatua ya mauti kumezwa na uzima, hayo ni mambo ya ulimwengu ujao lakini ni sharti yaonekane sasahivi,ni sharti yaanzie hapa kwanza..Na ndio maana Bwana Yesu alisema….Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;

26 naye KILA AISHIYE na kuniamini HATAKUFA KABISA hata milele. Je! Unayasadiki hayo? (Yohana 11:25).

Unaona hapo?, yeye aishiye, na sio yeye aliyekufa..Hivyo tunapaswa tufikie kimo cha kumwamini huyu Bwana wa uzima, sisi tunaoishi sasa mimi na wewe, mpaka tuvionje vipawa hivi vya kutokuonja mauti kabisa, Henoko alivifikia kabla ya wakati, Eliya alivifikia kabla ya watu, lakini sisi tulio karibu kabisa na zamani zijazo, ndio tunapaswa tuvifikie, na watakaofikia Imani hiyo ndio wale watakaokwenda na Bwana kwenye UNYAKUO.. Itafika wakati kanisa litafikia hicho kiwango cha mauti kutokuwa na nguvu, litakapofikia hicho kiwango ndio unyakuo utakuwa umefika.

Je! mimi na wewe tumejiandaje?. Tunasema tunangojea Bwana, je! imani yetu kwake ina nguvu ya kuvuta mambo yajayo?..je! na wewe utakuwa miongoni wa watakaokuwa na imani ya kunyakuliwa?

Luka 18: …walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?

Mungu atusaidie sote.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine. Na Bwana atakubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze neno la Mungu, ambalo litatutoa sehemu moja hadi nyingine kiroho..Kama Daudi anavyosema..“Neno lako limesafika sana, Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda. (Zaburi 119:140)”..Neno la Mungu ndio chakula chetu, ndio silaha yetu na ndio ngao yetu. Biblia inasema Neno la Mungu ni kama upanga wenye makali pande zote mbili, sio upande mmoja kama haya mapanga tunayoyajua sisi, bali una makali pande zote mbili mfano wa SIME, linakata kuwili.

Waebrania 4: 12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote UKATAO KUWILI, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”.

Mtu akichomwa na kisu cha kawaida tumboni au kifuani kitaishia kwenye utumbo tu au mapafu, lakini Neno la Mungu ambalo ni kama upanga, biblia inasema linachoma na kuingia mpaka kwenye viungo vyote vya mwili…na mafuta yaliyo ndani yake, mafuta yaliyozungumziwa hapo ni mafuta yanayotengenezwa ndani ya mifupa (bone marrows), katikati kabisa ya mifupa mikubwa panapotengenezwa chembechembe hai za damu nyeupe, ndipo mafuta hayo yanapotengenezwa, Neno la Mungu kote huko linapita..Na aliishii kupenya huko tu…biblia inazidi kutuambia linapenya hata kizifikia nafsi na roho mahali siri za moyo zinapositirika, na linakata kata na tenganisha na kuharibu kabisa.

Kwahiyo unaweza ukaona Neno la Mungu ni silaha kubwa kiasi gani kama tukiweza kulitumia…

Lakini leo hatutaingia sana huko, bali tutajifunza somo la JINSI YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YAKO.

Kwanza ni muhimu kufahamu nini maana ya Neema, NEEMA ni kitu mtu anachopewa ambacho hakustahili kuwa nacho..tafsiri yake inakaribia sana kufanana na ZAWADI lakini sio zawadi..Neema tafsiri yake ni ya ndani kabisa..kwasababu zawadi mtu anapewa kwasababu kafanya kitu fulani kizuri…lakini Neema haiko hivyo, neema ni kitu mtu anapewa pasipo kustahili…kwamfano mtu anaweza kupewa nafasi ya kusomeshwa bure na serikali au mtu binafsi kwasababu pengine huyo mtu hana uwezo wa kujisomesha, au pengine amefaulu sana hivyo anapewa kama offer fulani ya kusomeshwa bure…Lakini Neema haipo hivyo, neema ni pale mtu anapewa nafasi ya kusomeshwa bure pasipo kuangaliwa yeye ni tajiri au ni maskini, au ana uwezo fulani au hana uwezo, amekidhi vigezo au hajakidhi. Hiyo ndiyo tunaweza kusema ni NEEMA.

Na kipawa cha Neema sisi wanadamu hatuwezi kuvitoa, ni ngumu sana kuvitoa kwasababu mara nyingi tunaangalia hali ya mtu ndipo tunamsaidia…Ni nani leo anaweza kwenda kutoa shamba lake na kumpa bure tajiri namba moja duniani? Kwa nia ya dhati kabisa na sio ya kujipendekeza?.. na baada ya kumpa anasahau?..utagundua hakuna au ni wachache sana wanaoweza kufanya hivyo wengi watakwambia..aa kama ni wema si afadhali ningeenda kumpa hilo shamba maskini fulani, kuliko  kumpa huyu mtu ambaye tayari ana mamilioni ya fedha, ndivyo mioyo yetu ilivyo sisi wanadamu. Lakini kwa Mungu haipo hivyo, NEEMA yake haina mipaka…haiangalii huyu ni tajiri au ni maskini, haiangalii huyu ni anacho au hana, anastahili kuwa nacho au hastahili.

Ndio maana wokovu na wenyewe ni NEEMA. Ingekuwa Mungu anaangalia hali fulani mtu aliyonayo ndio ampe wokovu, watu wengi wangeukosa..Tunaokolewa kwa NEEMA. Hakuna hali fulani tuliyonayo iliyomshawishi Mungu kutuokoa sisi zaidi ya NEEMA YAKE, …Ni buree kabisa tumeokolewa pasipo sababu. Sio kwa matendo yetu mema tumeokolewa, si kwa kusali kwetu sana tumeokolewa. Hapana.

Waefeso 2:8 “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;

9 wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu”.

Kwahiyo kama NEEMA ipo hivyo basi sio kitu cha kujisifia, kwasababu hakuna mtu kwa ajili ya sababu ndio amestahili au hakustahili kupewa.

Sasa Neema ya wokovu tumepewa wote, lakini pia kuna neema ya VIPAWA AU KARAMA, hii nayo ni vile vile, mtu hapewi kwasababu fulani fulani hivi..kwamba ni mtakatifu sana au kwamba si mtakatifu sana hapana! hii Mungu anampa mtu kama anavyotaka bila sababu yoyote na kama ni hivyo basi haipaswi kuwa ni ya kujisifia kwa namna yoyote, ukiona mtu anajisifia karama au kipawa, ujue huyo mtu bado hajauelewa UKRISTO hata kidogo, au ni mchanga sana kiroho.

Ukiona mtu anajisifia mimi ni mtu wa kusali sana, au mtakatifu sana, au nilimfanyia kitu fulani Mungu ndio maana naweza kufundisha, au ndio maana naona maono, au ndio maana ninaweza kunena kwa lugha, au ndio maana nina upako, nikimwekea tu mtu mikono anapona, tambua huyo mtu bado hajaelewa nini maana ya NEEMA, pengine atakuja kuelewa baadaye lakini kwa wakati huo anaojisifia bado hajaelewa maana ya neema.

Kwa ufupi Vipawa vya Mungu havitokani na juhudi zetu, baada ya kuamini tu na kubatizwa mtu unajikuta tu unapata uwezo wa kipekee katika kufanya jambo fulani la kimungu ndio hapo alikuwa hajui kama ana karama ya uponyaji, hivyo anapomwekea tu mtu mikono anapokea uponyaji n.k lakini sio jambo la kusema ni kwasababu fulani ndio maana ninao huu uwezo sasa..karama za Mungu sio zawadi kwamba tumefanya jambo fulani ndipo Mungu anatuzawadia kama pongezi, haiko hivyo karama za Mungu ni NEEMA unapewa pasipo sababu yoyote. Na Mungu anatoa jinsi anavyotaka yeye, huyu hivi yule vile.

Ukishindwa kuelewa hili, utajikuta unatamani kuwa kama mtu fulani ukidhani kuwa alifanya kajuhudi fulani mpaka kuwa vile, na unajikuta unashindwa kukaa katika nafasi yako, na kuanza kusifia watu, badala ya Mungu.

Sasa tukirudi kwenye kiini cha somo letu linalosema NAMNA YA KUITUMIA VYEMA NEEMA YA MUNGU ILIYO JUU YANGU, tutajifunza namna ya kuitumia vyema neema tulizopewa na kutuletea matokeo makubwa katika viwango vya kimbinguni.

Hebu tusome kwanza mistari ifuatayo na kisha tuendelee..

Luka 21 : 1-4

“1 Akainua macho yake akawaona matajiri wakitia sadaka zao katika sanduku la hazina.

2 Akamwona mjane mmoja maskini akitia mle senti mbili.

3 Akasema, Hakika nawaambia, huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote;

4 maana, hao wote walitia sadakani katika mali iliyowazidi, bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo”.

Katika habari hiyo Bwana aliona makundi mawili ya watu: la kwanza ni yule mwanamke mmoja MASKINI, ambaye kwa NEEMA, Mungu aliyompa hakuwa na kingi, lakini alitoa vyote Na kundi la pili aliloliona ni MATAJIRI ambao walitoa sadaka katika sehemu iliyowazidia.

 

Katika mfano huu, tunaweza tukamfananisha yule mwanamke mjane na wale watu ambao Bwana amewapa vipawa vinavyoonekana kama ni vya chini kabisa katika kazi ya Mungu, ambapo kiuhalisia hakuna kipawa chochote kisichokuwa na umuhimu katika mwili wa Kristo kwamfano kuna wengine hawana kitu lakini utakuta siku zote kanisa lipo katika hali ya usafi, wanahakikisha usafi wa kanisa katika viwango vyote, wanajitoa katika viwango vyote…wengine kazi yao ni kusambaza nakala tu za Neno la Mungu ingawa hawana kitu, lakini kwa bidii zote wanajitahidi..Sasa hawa wanafananishwa na huyu mwanamke ambaye alitoa vyote alivyo navyo kwa Mungu.

Lakini kundi lingine linalojiona lenyewe ndilo la muhimu sana, pengine mchungaji, au nabii au mwalimu ambaye kila siku anaonekana pale madhabahuni akifundisha lakini haitumii karama yake inavyopaswa anaangukia katika hili kundi la pili la matajiri waliotoa katika sehemu ya mali iliyowazidi, kwasababu wao wanadhani kukaa kuonekana na kusifiwa na watu ndio hivyo hivyo ilivyo hata mbele za Mungu.

Sasa siku ya mwisho wale wa mwisho watakuwa wakwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho. Kwasababu katika utajiri wao hawakutoa vyote.

Na mimi leo nakwambia wewe unayesoma ujumbe huu USINIE MAKUU bali jishughulishe na mambo madogo, usitamani yaliyo makubwa wakati haya madogo huyafanyi yanavyopasa…katika haya haya madogo, fanya kwa bidii, toa vyote ulivyonavyo kwa ajili ya Bwana, toa muda wako wote kuhakikisha injili inakwenda mbele hata kama huna fedha, hiyo ndio thawabu yenyewe, usijilinganishe na wale wengine kwasababu Macho ya Mungu sio kama ya kwetu sisi wanadamu.

Usidanganyike na INJILI Kutoka kuzimu zinazosema, utafute kwanza mali ndipo umtumikie Mungu, ndugu yangu Mungu hakuhurumii umaskini wa mwili wako!! Ana uhurumia kwanza umaskini wa roho yako….Ingekuwa anauhurumia kwanza umaskini wa miili yetu, yule mwanamke mjane aliyetoa senti mbili pale pale angeanza kumuhurumia na kusemaa ooo maskini yule mwanamke asitoe chochote maana ni mjane na ni kile tu alichobakiwa nacho…lakini badala yake unaona Bwana alimwacha atoe vyote alivyo navyo kwa ajili ya roho yake, pingine hata chakula cha mchana bibi yule hakupata, ilimradi tu ahakikishe nyumba ya Mungu ipo katika hali nzuri…Bwana hakuuangalia umaskini wake wa pale…Bali aliuangalia UTAJIRI WAKE KATIKA MBINGU MPYA NA NCHI MPYA…Si ajabu tunaweza kwenda kumkuta kule mbinguni ameketi na Bwana katika kiti chake cha enzi.

Kwahiyo hiyo achana na INJILI ZA MAFANIKIO YA KUZIMU!!... injili za kuonyeshwa milki zote za dunia ndani ya dakika moja, Zile shetani alizomuhubiria Bwana Yesu na kumwambia NITAKUPA VITU VYOTE UKIANGUKA KUNISUJUDIA!!. Biblia inasema Bwana hatatupungukia kabisa,

Waebrania 13: 5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa.

6 Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?”

Bwana atatupa utajiri kwa wakati wake na kwa kuchuma kidogo kidogo, sio za leo na kesho! Mithali 13:11.

Ni matumaini yangu kuwa NEEMA iliyo juu yako utaitumia inavyopaswa, utaitumia yote..pasipo kuangalia mazingira yoyote ya nje, kwasababu Bwana pia alikupa pasipo kuangalia hali yako. Na Mungu akubariki.

Kama hujampa Bwana maisha yako ayatawale, usipoteze muda, mlango wa Neema upo wazi, ila hautakuwa hivi siku zote, ni vyema ukafanya hivyo sasa, kwasababu saa ya wokovu ni sasa…usidanganyike kuwa watu hawaokoki leo, wokovu unaanzia hapa hapa duniani..hivyo kama Roho anakuhimiza kufanya hivyo sasa usikawie, unachopaswa kufanya ni kutubu dhambi zako zote kwa kudhamiria kuziacha, na baada ya kutubu kwako, basi haraka sana nenda katafute mahali utakapoweza kubatizwa ubatizo sahihi wa kimaandiko, yaani wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, na Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia kushinda dhambi na kuielewa biblia, na hapo utakuwa umezaliwa mara ya pili.

Mungu akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine, print ikiwezekana na Bwana akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP



Mada Zinazoendana:

USIMFANYIE JEURI ROHO WA NEEMA.

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

JIWE LA KUKWAZA

TABIA ZA ROHONI.


Rudi Nyumbani

Print this post

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.

Shalom! Mwana wa Mungu, Karibu tujifunze Neno la Mungu…ambapo leo tutajifunza mambo machache yahusuyo utendaji kazi wa Mungu. Tutajifunza ni wakati gani Mungu anatenda kazi kwa watu wake.

Swali ambalo limekuwa ni changamoto kueleweka, na linaloulizwa na wengi ni kuhusu siku gani inayopasa iwe ni ya kuabudia au ya kukutana na Mungu, je! ni jumapili, jumamosi au lini?…miongoni wa wanaosema jumamosi ndio siku ya kuabudu mstari mama wanaousimamia ndio huu:

Mwanzo 2: 3 “Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya”

Hali kadhalika pia miongoni mwa wanaosimamia kuwa jumapili ndio siku ya kuabudu, mstari huu ndio msingi wao.

Marko 16: 9 “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, alimtokea kwanza Mariamu Magdalene, ambaye kwamba alimtoa pepo saba”..

Kulingana na mstari huo siku ya kwanza ya juma ni jumapili, Hivyo hiyo ndio siku ya kupumzika na kuabudia kulingana na wao kwasababu ni siku ambayo walipata ushindi wao kwa kufufuka kwa Bwana Yesu.

Kumekuwa na kushindana kusikoisha kati ya makundi haya mawili, kila moja likitetea hoja zake..Lakini Biblia inasema Mungu ni Roho nao wamwabuduo imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Kwahiyo Mungu aliruhusu watu waishike sabato katika agano la kale, kufunua sabato halisi itakayokuja huko mbeleni (yaani pumziko la roho), kadhalika aliruhusu wana wa Israeli katika agano la kale wakati wanatoka Misri waishike pasaka (ile siku waliyotoka Misri), kufunua pasaka wetu halisi atakayekuja huko mbeleni yaani (Bwana wetu Yesu Kristo), ambaye kwa yeye tunapata ondoleo la dhambi na kutolewa kutoka katika utumwa wa dhambi. 1 Wakorintho 5: 7 “Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo;”

Kwahiyo katika agano jipya hatuna sheria yoyote ya lazima ya kushika sabato wala pasaka, wala sikukuu yoyote ile..Kwasababu tumepata ufunuo kamili wa mambo hayo yalikuwa yanamaana gani.

Wakolosai 2:15 “akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.

16 Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au SABATO; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo”

Pia jambo lingine la muhimu la kujua ni kuwa, Mungu hana siku maalumu ya kupumzika, kwa sababu yeye hachoki, Neno linaposema “katika siku ya saba aliacha kufanya kazi zake zote akapumzika” haimaanishi kuwa katika siku ya saba..shughuli zake zote alizisimamisha au zilisimama hapana!! bali alimaanisha kuwa katika siku hiyo “aliacha kufanya kazi ya kuumba vitu vipya”..

Kwasababu kama katika siku ya saba shughuli zake zote zilisimama basi mwanadamu pia angeacha kupumua kwasababu na yeye ni kazi ya Mungu, wanyama pia wangesimama kupumua, na kila kitu kingesimama, hata jua lingesimama..lisingekuchwa,na mito nayo ingesimama, kwasababu vyote hivyo ni kazi ya Mungu, unaona! lakini tunaona vitu vyote viliendelea kama kawaida hata katika hiyo siku ya saba, maji yaliendelea na mizunguko yake, jua liliendelea kusogea, miti iliendelea kuota n.k..kwahiyo kazi ya Mungu ilikuwa inaendelea…na inaendelea mpaka leo, yeye hapumziki anaendelea kutenda kazi.

Ndio maana wakati Fulani mafarisayo walitaka kumkamata Bwana Yesu kwa habari hiyo hiyo ya kuishika sabato, wakitaka kumwonyesha kuwa katika siku ya saba hapaswi mtu yoyote kufanya kazi kwasababu hata Mungu mwenyewe alistarehe katika siku hiyo akaacha kufanya kila kitu alichokuwa anakifanya..Lakini Bwana alikuwa na ufunuo mkubwa zaidi ya huo na kuwaambia…

Yohana 5:14 “Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya hekalu, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi.

15 Yule mtu akaenda zake, akawapasha habari Wayahudi ya kwamba ni Yesu aliyemfanya kuwa mzima.

16 Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato.

17 Akawajibu, BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA, NAMI NINATENDA KAZI”.

Umeona hapo?..Bwana anawaambia wale waliokuja kumshitaki kuwa siku ya saba hapaswi kufanya kazi…lakini Bwana akawaambia, BABA YAKE ANATENDA KAZI HATA SIKU HIYO, NA YEYE ANATENDA KAZI. Umeona hana siku ambayo anapumzika. Wao walitaka kumwambia siku ya saba Mungu alipumzika, lakini yeye akawaambia Baba yake anatenda kazi hata sasa. Kazi zake bado zinaendelea.

Bado anaendelea kuumba kimiujiza, bado anaendelea kutengeneza wanadamu kwenye matumbo ya wanawake, bado anaendelea kulitembeza jua kwa amri yake, bado anaendelea kutushushia mvua, bado anaendelea kuiumba miti na mimea, ndio maana ukiukata mti leo baada ya muda Fulani utaukuta umekua tena, hiyo ni kazi ya Mungu iliyo katika mwendelezo wake, haina pumziko, kama Bwana Yesu alivyosema “Baba yangu anafanya kazi hata sasa nami ninatenda kazi” kadhalika na sisi pia tunatakiwa tuseme maneno hayo Kama Baba yetu wa mbinguni anavyotenda kazi nasi pia TUNAZITENDA.

Na kazi hizo ni zipi?..Si nyingine zaidi ya zile zile Bwana Yesu alizozifanya.

Yohana 14 : 12 “Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, KAZI NIZIFANYAZO MIMI, YEYE NAYE ATAZIFANYA; NAAM, NA KUBWA KULIKO HIZO ATAFANYA, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba.

13 Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.

14 Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya”

Sasa Bwana Yesu alifanya kazi gani?; aliponya wagonjwa wa kila aina (wa mwilini na wa rohoni). Kama Baba naye anavyojishughulisha kuiponya dunia kila siku, hapumziki, Bwana Yesu alirudisha uhai wa mtu aliyekufa, aliumba macho ya mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa kwake n.k, aliwahubiriwa watu injiii, na sisi Bwana katuambia kazi hizo tunaweza kuzifanya kwa jina lake.

Kwahiyo nataka nikuambie wewe unayesoma ujumbe huu, hakuna UGONJWA, WALA SHIDA, WALA KIFUNGO CHOCHOTE CHA SHETANI Kitakavyoweza kusimama mbele yako kuanzia leo hii kama umeuelewa ujumbe huu, kama umemwamini Yesu Kristo kwa dhati kabisa kutaka moyoni mwako.

Kama ni ugonjwa Kristo anao uwezo wa kukuponya sasa hivi, sio kesho, na ametupa uwezo wa kuombeana sisi kwa sisi na kupokea uponyaji wetu. Kwahiyo kama una ugonjwa wowote sasahivi hapo ulipo, Weka mkono wako mahali penye tatizo na uambie huo ugonjwa maneno haya kwa sauti na kwa Imani  

“EWE UGONJWA!!, BABA YANGU WA MBINGUNI ANATENDA KAZI HATA SASA, NAMI NATENDA KAZI KAMA YEYE, ONDOKA KWANGU NA USIRUDI TENA KWA JINA LA YESU”

 Baada ya kusema hivyo AMINI! Na uhai wa huo ugonjwa utakuwa umeishia hapo hapo.

Utasema mbona sijawahi kumuona Baba akiniponya leo iweje aniponye kwa dakika moja? Nataka nikuambia ulishawahi kumwona akikuponya isipokuwa ulikuwa hujui tu kama ameshawahi kukuponya mara nyingi! Chukua mfano siku ile ulipojikata na kisu mkononi na baada ya wiki mbili ile ngozi ikajirudia tena vile vile, kama ilivyokuwa mwanzo huoni huo tayari ulikuwa ni uponyaji?..Hapo ni Baba yako anafanya kazi yake ya kukuponya kila siku, unapokata nywele na baada ya wiki mbili zinaota tena huoni huo ni uumbaji tayari… sasa kwanini na wewe usifanye kazi ya kutamka uponyaji juu yako na kwa watu wengine, hiyo ndio sababu iliyomfanya Kristo akafanye miujiza kila mahali pasipo kizuizi chochote sio cha sabato wala cha sikukuu yoyote, kwasababu aliona Baba hana mipaka kila siku anafanya kazi zake.

Kila siku katika maisha yako, likumbuke hilo neno, Mungu hapumziki katika kazi zake na wala hachoki,anafanya kazi kila dakika na kila sekunde…na hivyo nasi pia hatupaswi kupumzika katika kuzifanya kazi zake..Kila siku tunapaswa tuumbe jambo jipya moyoni mwetu na maishani mwetu, kama yeye anavyoumba watu wapya kila siku kwenye matumbo ya wanawake. Kwasababu huo uwezo tumepewa..Tukitamka tu! Kwa IMANI TUSIPOKUWA NA MASHAKA, Hilo tulilolisema ni lazima litokee..

Ndugu nakuambia hilo kwasababu mimi binafsi Bwana kanitendea katika maisha yangu, watu kadha wa kadha nimewaombea nao wamepona! Na mimi mwenyewe Bwana ameniponya mara nyingi kwa njia hiyo. Hivyo mwamini Mungu.

Bwana akubariki sana..

Tafadhali “share” ujumbe huu na wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

UPONYAJI WA YESU.

SABATO HALISI NI LINI, JE! NI JUMAPILI AU JUMAMOSI?, NI SIKU GANI ITUPASAYO KUABUDU?

JE! “MAJIRA NA SHERIA” MPINGA-KRISTO ATAKAYOKUJA KUBALISHA NI KUPINDUA SIKU YA SABATO NA KUWA JUMAPILI?


Rudi Nyumbani

Print this post

MLIMA WA BWANA.

Mara nyingi tunaposoma biblia katika agano la kale Mungu alipokuwa akitaka kukutana au kusema na watu wake, aliwaita milimani, hilo tunaliona tokea mbali kabisa jinsi Mungu alivyomwita baba yetu Ibrahimu katika ule mlima Moria amtolee sadaka na kumfanyia ibada, Tunakuja kuona tena baadaye Musa akiitwa na Mungu katika milima Sinai kupewa amri zote na hukumu na sheria kwa ajili ya wana wa Israeli, tunaona tena manabii wengi jinsi Mungu alivyokuwa akisema nao katika milima, mfano nabii Eliya Mungu alizungumza naye katika mlima Karmeli, na wengine wengi mfano wa Elisha ambao ukisoma habari zao mara nyingi utakuta walikuwa wakikutana na Mungu katika milima, 

Hivyo hiyo ilikuwa ni kama desturi yao kupanda milimani na kukutana na Mungu..Kwasababu iliaminika hivyo na ndivyo hata alivyofanya Mungu mara nyingi alipotaka kuzungumza na watumishi wake, alifanya kuwatenga kwanza kisha kuwapandisha milimani na baadaye kuzungumza nao. (Isaya 18:7). Na kama ukichunguza vizuri utaona kuwa wote waliokuwa wanaitwa kusema na Mungu milimani waliteuliwa na Mungu mwenyewe, sio kila mtu tu alikwenda, utakuta pengine wataanza safari wengi lakini mwisho wa siku wanaofikia kule juu mlimani ni wachache, ndivyo ilivyokuwa kwa Ibrahimu, Musa na manabii.

Tunaona hata kipindi cha Bwana wetu Yesu Kristo, mara nyingi alipokusudia kusali au kwenda kuzungumza na Baba yake alikuwa na desturi ya kupanda katika mlima wa Mizeituni, na tunaona pia wakati fulani alipotaka kuonyesha utukufu wake zaidi aliwatenga kwa kuwachagua baadhi ya mitume wake,(yaani watatu tu kati ya 12) kisha akawapandisha katika mlima MREFU sio mfupi, bali mrefu na huko huko ndiko alikowabadilikia sura..tunasoma..

Mathayo 17:1 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;

2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.

3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye”.

Sasa tukirudi kwenye kiini cha somo letu kinachosema “mlima wa Bwana”. Tunapaswa tujiulize ni kwanini Mungu alikuwa anawaita watu milimani na sio mahali pengine popote…kwanini asiwe anawaita katika mabonde azungumze nao, lakini badala yake aliwaita milimani?. Je! milima ina upako zaidi ya visiwa, au nyika?. Je! milima inakibali cha kipekee sana mbele za Mungu zaidi ya mahali pengine popote?. Kama sivyo basi ilifunua nini?

Ni wazi kuwa kila mmoja wetu alishawahi kupanda mlima na kama sio mlima basi angalau kajilima na kujionea jinsi hali ilivyo katika kuupanda..si kazi rahisi wala si kazi nyepesi, kama ilivyo katika kushuka mabondeni, au kutembea katika nchi tambarare, tunajua kabisa kupandisha mlima inachukua nguvu nyingi hivyo kama wewe ni mlegevu hutafika kileleni..Kupanda mlima ni lazima utoke jasho la kutosha, sio kama kushuka mabondeni.Wanaoweza kupanda milima mrefu sikuzote ni wachache sana na tena unapaswa uwe mtu wa mazoezi lakini kuteremka bondeni, kila mtu anaweza kufanya hivyo, tena ni raha iwe unazo nguvu au hauna hakuna asiyeweza kushuka bondeni..

Mambo hayo yanafunua nini katika Roho?

Sasa tukirudi katika agano jipya mambo ya mwilini yanafunua mambo yanayoendelea rohoni, Na ndio maana ukisoma mahali popote palipo na bonde utaona kuwa ni mauti inapatikana huko, BONDE LA UVULI WA MAUTI, bonde LINAFUA SHIMO LA KUZIMA, mahali makao ya shetani yalipo Na siku zote kushuka huko ni rahisi sana..Mahali Fulani Bwana alipowatoa pepo, walimsihi asiwaamuru waende shimoni, ikifunua kuwa ni sehemu ya hatari…Lakini katika vilele vya milima Mungu anapatikana, kwasababu Mungu anaketi Juu siku zote, sehemu za juu zilizoinuka.

Hivyo ndugu tukitaka leo hii kukutana na Mungu, ukitaka kuuona uso wa Mungu kwa namna nyingine na ile uliyoizoea, ukitaka Mungu aseme na wewe katika viwango vya juu sana ukitaka Mungu akufunulie njia zake kwa namna ambayo hujawahi kuona huna budi kupanda mlimani katika roho, huna budi kugharimika kuupanda mlima wa Bwana. Tena na kwa jinsi unavyopanda zaidi ndivyo utakavyofunuliwa uso wa Mungu katika viwango vya juu zaidi.

SASA TUNAPANDAJE PANDAJE MLIMA HUO, NA NI NANI ASTAHILIYE KUUPANDA MLIMA WA BWANA?

Biblia imetoa majibu yote tunaposoma kitabu cha Zaburi..

Zaburi 24:3-6 “Ni nani atakayepanda katika MLIMA WA BWANA? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?

4 Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila.

5 Atapokea baraka kwa Bwana, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.

6 Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao, Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.

Inasisitiza tena na kusema:

Zaburi 15:1 “Bwana, ni nani atakayekaa Katika hema yako? Ni nani atakayefanya maskani yake Katika KILIMA CHAKO KITAKATIFU?.

2 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu, Na kutenda haki. Asemaye kweli kwa moyo wake,

3 Asiyesingizia kwa ulimi wake. Wala hakumtenda mwenziwe mabaya, Wala hakumsengenya jirani yake.

4 Machoni pake mtu asiyefaa hudharauliwa, Bali huwaheshimu wamchao Bwana Ingawa ameapa kwa hasara yake, Hayabadili maneno yake.

5 Hakutoa fedha yake apate kula riba, Hakutwaa rushwa amwangamize asiye na hatia. Mtu atendaye mambo hayo Hataondoshwa milele”.

Unaona hapo?, vigezo vya kuuendea mlima huo?

1) Kwanza Ni mtu yule aendaye kwa ukamilifu, na kutenda haki, watu wengi wanaona shida kuishi maisha matakatifu, wanaona yatawasaidia nini? watapata faida gani, kujitaabisha kujizuia na tamaa, kutokunywa pombe, kutokufanya uasherati, kutokuvaa nguo za kizinzi, watapata faida gani?..wanaona ni ngumu sana mtu kuishi kwa namna hiyo, wanaona mtu kutenda haki, kutokula rushwa ni jambo ambalo ni gumu kutolifanya, lakini hawajui hizo ndizo gharama za kuupanda mlima wa Mungu, ambapo yeye yupo huko, mahali anapopatikana.

2) Biblia inasema pia mtu asemaye kweli kwa moyo wake, utakuta mtu kuwa muwazi wakati wote kwake ni shida, na bado anajiita mkristo, biblia inaendelea kusema Asiyesingizia kwa ulimi wake. Wala hakumtenda mwenziwe mabaya, Wala HAKUMSENGENYA JIRANI YAKE.

Unaona hapo?, utakuta mtu anajiita ni mkristo, na anahudhuria ibadani, na anasali, na anafanya kazi yote ya Mungu, lakini anaona ni vigumu kuuzia ulimi wake kutokuwazungumzia wengine vibaya, kusengenya watu kwake ni kama chakula chake,. Sasa mtu kama huyu asitazamie kumkaribia Mungu kwa namna yoyote ile hata kama atakuwa anafunga kiasi gani, hata kama atakauwa anatoa sadaka kiasi gani, hata kama atakuwa anahubiri kiasi gani..Hatoweza kupanda mlima wa Bwana..

3) Biblia inasema tena mtu ambaye macho yake huwaheshimu wamchao Bwana,

Mtu ambaye macho yake yanamfarahia yule tu anayejitaabisha kwa Bwana, na sio watu wengine,. Sasa Hapa utakuwa mtu ni Mkristo lakini hamu na Mungu hana hata kidogo, yupo tayari kuwa mshabiki wa mipira, kuwa mfuasi wa siasa, kuwa mshabiki wa watu maarufu wa kidunia hii, muda wote anapoteza kufuatilia mambo yao, lakini tukirudi katika upande wa Mungu, ukimuuliza hata historia ya kanisa la Kristo ilianzia wapi hajui, ukimuuliza nitajie ziara za mtume Paulo zilianzia wapi na kuishia wapi? Hajui, lakini ukimuuliza ziara za maraisi wote duniani na wasanii, atakutajia na yanayokuja na kitu gani kinaendelea sasahivi katika ulimwengu wa siasa atakutajia..Sasa hiyo ni roho ya kumkinai Mungu na watu kama hao biblia inasema hawataweza kufanya maskani yao katika mlima mtakatifu wa Mungu..Watu kama hao hata waseme wao ni wakristo kiasi gani, ndani ya maisha yao wanajijua kabisa kuwa wapo mbali na ufalme wa mbinguni.

4) Biblia inandelea kusema mtu ambaye hali rushwa.

Katika shughuli mkisto anazozifanya, je! Anakaa mbali na vitu kama rushwa na ukwepaji kodi?. Leo utashangaa ni mkristo lakini naye pia anatafuta njia za mkato za kukwepa kodi, mwingine anakuwa tayari kutoa rushwa ili afanyiwe jambo fulani..Sasa mambo kama hayo mtu akiwa nayo kadhalika asitarajie kumwona Mungu maishani mwake au Mungu kujifunua katika maisha yake, hata kama alibatizwa nakunena kwa lugha hiyo haijalishi, hatakaa amjue Mungu.

Hivyo Mungu kachagua sehemu ya juu iliyoinuka ili akutane na watu wake huko, sio rahisi kufika, inahitaji juhudi na bidii, kuacha usengenyaji sio rahisi kuliondoa kwa kuomba tu kama unavyodhani, inahitaji kuonyesha bidii yako binafsi kwa vitendo, mazungumzo yoyote unayoona yanakupelekea kumzunguzia mwingine kwa ubaya, ni kuyakwepa kwa namna zote, ukiudhiwa ni kuvumilia sio lazima uanze kutoa habari za mtu mwingine hadharani, unajizuia kwa nguvu, kila siku uendelee hivyo hivyo mpaka mwisho wa siku unajikuta inaumbika na kuwa ni tabia yako kutokuwazunguzia wengine vibaya..Hata na wale watu wanaokuletea hizo habari wakishakuona hauvutiwi na habari hizo, wao wenyewe watakuacha na kwenda kutafuta wanaoendana nao..Na kwa kufanya hivyo ndivyo unavyopiga hatua moja zaidi kuelekea mlima mtakatifu wa Bwana, Mungu alipo ili kusema na wale wote wamchao.

Kadhalika kutokufanya mambo ya ubatili, yaani uasherati, kampani mbovu zisizo na maana, kutokukaa wakati wote mitandaoni kuchati mambo yasiyo na maana, kutokwenda disco, kutofuata anasa za dunia hii, bali kinyume chake kujishughulisha na mambo ya Mungu, ni jinsi gani umpendeze yeye..Kumbuka Bwana anasema nikaribieni mimi nami nitawakaribia..Hivyo ukiwa unafanya bidii kukaa mbali na mambo maovu na kutafauta kujua habari zake, kwa kujifunza Neno, ndivyo unavyozidi kupanda kidogo kidogo mpaka kileleni alipo yeye..

Hizi ni siku za mwisho, na ndio kile kipindi ambacho Bwana Yesu alisema saa yaja ambayo waabuduo halisi watamwabudu Mungu katika roho na kweli.

Yohana 4.19 “Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.

21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu…

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.

Ndugu unaona hiyo saa ni sasa Kristo aliyokuwa anaizungumzia, wakati huo ndio huu, Mungu anakutafuta wewe na mimi tupande tukamwabudu yeye katika MLIMA WA ROHO, huko ndiko tutakapomwabudu katika roho na kweli. Hivyo tuanze kupanda mlima huo sasa, kwa kuacha mambo hayo mabaya tuliyoyaona hapo juu bila kuchoka, bila kukata tamaa, ni kweli jasho litakutoka kidogo, lakini ili uonekane kuwa umestahili kukutana na Mungu wako uso kwa uso zaidi ya wale wengine, huna budi kupanda mlima huo wa roho kwa ukakamavu.

Tazama Neno la Mungu linavyosema..

Isaya 2:2 “Na itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote watauendea makundi makundi.

3 Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana katika Yerusalemu.

4 Naye atafanya hukumu katika mataifa mengi, atawakemea watu wa kabila nyingi; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe.

5 Enyi wa nyumba ya Israeli, njoni, twende katika NURU YA BWANA.

Unaona siku hizi ndizo siku hizo za mwisho.

Ni maombi yangu kuwa mimi na wewe tutaanza kwenda katika nuru hii ya Neno la Mungu ili kutuongoza katika mlima huo wa Bwana.

Zaburi 43:3 “Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze, Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata maskani yako.

4 Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu”.

Zaburi 123:1 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.

2 Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele.”

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

SAYUNI NI NINI?

NYOTA YA ASUBUHI.

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.

UTAMBUE UJUMBE WA SAA UNAYOISHI.


Rudi Nyumbani

Print this post

MJI WENYE MISINGI.

Ibrahimu tunamwita ni Baba wa Imani, kutokana na Imani tunayoiona aliyokuwa nayo kwa Mungu wake licha ya kukaa kwa muda mrefu bila kupata mwana Mungu aliyekuwa amemuahidia akizingatia na huku umri umeshakwenda yeye na mke wake, hakukata tamaa kumwamini Mungu badala yake aliendelea kusubiria mpaka Mungu alipotimiza alichomuahidia na hata alipopata mwana, zaidi ya yote tunasoma katika uzee ule Mungu alimjaribu tena amtoe mwanawe kuwa sadaka ya kuteketezwa, Nalo hilo Ibrahimu halikumtikisa bali alidhubutu kumtoa, ndipo Mungu akavutiwa sana na Imani ya Ibrahimu..

Lakini hilo pekee tu pekee lingetosha Mungu kumfanya Ibrahimu kuwa baba wa imani na mtu wa kuigwa kwa vizazi vyote? Watu watakaokuja kumwamini yeye baadaye?..Lipo jambo lingine la ndani zaidi tunapaswa tulijue ambalo ndilo tutaligusia siku ya leo.

Tukisoma kitabu cha Waebrania tunapata kuona tabia nyingine tofauti ambayo Ibrahimu aliionyesha kwa Mungu wake. Tunasoma:

Waebrani 11:8 “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako.

9 KWA IMANI ALIKAA UGENINI KATIKA ILE NCHI YA AHADI, KAMA KATIKA NCHI ISIYO YAKE, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.

10 Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu”.

Sasa ukiyachunguza hayo maandiko kwa makini utaona kuwa Ibrahimu alikuwa na jicho lingine la mbele zaidi hata ya lile alilokuwa ameahidiwa na Mungu katika mwili..Na ndio maana siku zake zote maisha yake yote hakusumbuliwa na mambo yanayopita, hukusumbuliwa na kukawia kwake kupata mtoto,hakusumbuliwa na hata kutoa mwanawe Isaka kuwa sadaka kwa Mungu wake…

Embu Soma tena hapo anasema. 9 KWA IMANI ALIKAA UGENINI KATIKA ILE NCHI YA AHADI, KAMA KATIKA NCHI ISIYO YAKE,..

Kumbuka Mungu alimtoa Ibrahimu nchi ya mbali sana huko Uru ya Ulkadayo na kumleta Kaanani, mahali ambapo Mungu alimwahidia kumpa kila kitu ambacho ni chema, alimwahidia kuwa atamfanya kuwa taifa kubwa sana, atamfanya kuwa uzao hodari, uzao ambao utamiliki malango yote ya adui zake wote..Atamfanya kuwa taifa tajiri, na lenye nguvu sana..

Sasa embu jaribu kutengeneza picha ingekuwa hiyo nafasi umepewa wewe, Mungu anakuambia utakuwa na uzao hodari katika nchi fulani na kwa kupitia wewe mataifa yote duniani yatabarikiwa, hivi utajisikiaje?…Ni wazi kuwa utajiona kuwa ni mtu wa kipekee mbele za Mungu kuliko wengine wote, utatanua mbawa kidogo, utajiona kuwa wewe ni mtu muhimu sana mbele za Mungu kuliko wengine..Hata ukifika katika hiyo nchi Mungu aliyokuahidia utaimiliki pengine kwa kiburi fulani, utaishi kama mfalme fulani au chifu fulani hivi kwani Mungu tayari ameshakuridhia na kukupa wewe..hata watu wote wa huo mji wakitaka kupigana na wewe hutaogopa, kwasababu Mungu alishakupa wewe milki hiyo.

Lakini kwa Ibrahimu haikuwa hivyo, alikuwa na jicho la mbali zaidi, hakutazama Baraka hizo Mungu alizomwahidia za kitambo tu, hakutazama wingi wa uzao atakaokuwa nao duniani, hakutazama ukuu wa taifa atakalolizaa duniani, hakutazama utajiri wa kimwilini, kwa hili jicho la kimwilini, bali aliyatafakari maisha yake kwa utulivu sana, akiangalia jinsi Mungu alivyomtoa Nchi ya Ulkadayo na kumleta pale Kaanani, na jinsi Mungu alivyomwepusha katika taabu zote zile, za kungojea nchi ambayo Mungu amemwahidia, akajiuliza kama Mungu anao uwezo wa kunifanya taifa kubwa ndani ya dakika moja, kwanini anakawia hivi kunipa mwana? Sababu nini?..Ibrahimu alitaka kujua kusudi la maisha, nyuma ya haya yote kuna nini?.. Na ndipo akafahamu kuwa maisha yake ni picha ya mambo yatarajiwayo mbeleni yajayo baada ya ulimwengu huu kupita. Alifahamu kuwa maisha yake ni somo, maisha yake ni sauti Mungu anayozungumza naye juu ya mambo ya mbeleni sana..ng’ambo ya pazia..

Na ndio maana tunasoma Ibrahimu licha ya kupewa utajiri wote ule wa kimwilini, bado aliendelea kuishi katika nchi ile ambayo ni kweli ilikuwa ni haki yake kustarehe na kujifurahisha lakini biblia inatuambia aliishi mule kama vile siyo nchi yake, aliishi katika milki yake kama vile sio milki yake, kama vile mgeni nyumbani kwake mwenyewe..aliisha na mke wake Sara kwenye mahema, fikiria Ibrahimu alikuwa ni mtu tajiri sana mwenye mali nyingi alizopewa na Mungu lakini hakuishi kwenye makasri,..hiyo inafunua nini?..Inaonyesha ni jinsi alivyoishi kama mpitaji hapa duniani?.

Unadhani alikuwa hajipendi?. Hapana..Biblia inatuambia ni kwasababu alikuwa anautazama mji ulio bora, alikuwa anautazamia mji wenye misingi, sio ule wa Kaanani aliopewa ambao Mungu kweli alimpa kuwa milki yake, lakini huo ingempasa aweke misingi yeye iliyodhaifu, ingempasa aubuni yeye..Lakini badala yake Ibrahimu hakufanya hivyo bali aliutazamia mji wenye misingi ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu mwenyewe.. Na mji huo si mwingine zaidi ya YERUSALEMU MPYA ya mbinguni HALELUYA!!.

Jambo hilo ndilo lililomfanya Mungu apendezwe na Ibrahimu na kumfanya awe kielelezo cha kuigwa kwa watu wote, ikiwemo mimi na wewe.

Ndugu leo hii, umekuwa ukimsubiria Mungu aje kukufanikisha katika jambo fulani ambalo alikuahidia atakufanyia zamani, au tayari ameshakufanyia, pengine alikuahidia kukupa mtoto kwa muda mrefu na sasa amekupa, pengine alikuahidi utakapa mali amekupa, ulisubiria nyumba amekupa, ulingojea hiki au kile kwa muda mrefu sasa amekupa, Je! unadhani hayo ndio mapenzi ya Mungu kwako?.

Usipokuwa makini utakuwa unaona kila siku pale Mungu anapokufanikisha katika mambo yako ndio anapendezwa na wewe, ndio mrithi wake, utaona kila unalomwomba anakupa na wakati mwingine hata umetolewa unabii utakuja kuwa raisi, au mtoto wako atakuja kuwa bilionea wa kwanza duniani, Mungu kakuotesha utakuja kuwa kichwa cha ukoo wako mzima, wote wasiokupenda watakuja kukuinamia, ukadhani kuwa hayo ndio mapenzi ya Mungu kwako!!.

Ni kweli Mungu atatimiza Neno lake kwa alichokuahidia,lakini usipokuwa naUFAHAMU kama wa IBRAHIMU, Jua tu siku ile ikifika, hutaingia katika mji ule YERUSALEMU MPYA BIBI-ARUSI WA KRISTO. Siku ile kama Bwana Yesu alivyosema watatoka watu kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni; 12 bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. ( Mathayo 8:11)..Unaona hapo, wataketi na Ibrahimu, na Bwana hawezi kuwaketisha pamoja na Ibrahimu watu wasiofanana na Ibrahimu katika mienendo.

Hiyo Yerusalemu mpya, kwa tafsiri nyingine ni BIBI-ARUSI wa Kristo, yaani watakatifu wa Kristo, sasa sio kila mtu anayejiita ni mkristo atakuwa bibi-arusi wa Kristo, hapana, kama vile biblia inavyosema hawawi wote waisraeli walio wana wa Israeli, Vivyo hawawi wote wakristo, walio wa-kristo. Kuna tofauti kati ya suria na mke, wanawali wenye busara na wanawali wapumbavu, magugu na ngano. kadhalika mbele za Mungu, si kila mkristo ni bibi-arusi wa Kristo, si kila mtu ataujenga YERUSALEMU WA MBINGUNI. Bali ni wale tu waliokamilishwa katika wokovu.

Biblia inatumbia mji huo hakitaingia kilicho kinyonge, wala kidhaifu, ndugu ukiona umekosa tu unyakuo basi ufahamu kuwa wewe si miongoni mwa mji mtakatifu wa Mungu. Ukiona umekosa tu karamu ya mwanakondoo siku ile ya unyakuo basi hali yako ni itakuwa mbaya sana.

Ukisoma kitabu cha ufunuo sura ya 21 utaona ni jinsi gani hawa watu walivyo wa tofauti sana, wenye imani hii ya Ibrahimu, kundi hili dogo sana wanavyofananishwa na uzuri wa mji ule , ulipambwa ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu mwenyewe..Watu ambao Mungu amewajenga katika misingi iliyo imara..Na tunasoma misingi yenyewe ni mitume na manabii,(Biblia takatifu) na sio misingi ya pesa na mafanikio..sio misingi ya utajiri na ufahari, sio misingi ya urembo na umaarufu, sio misingi ya elimu ya dunia hii kama wengine wanavyodhani.

Mji huo unaonekana ukiwa na vipimo sahihi kabisa, urefu wake, na mapana yake, na kwenda juu kwake ni sawa sawa, kuonyesha uimara wake na umakini wa ujenzi wake, kuonyesha jinsi ulivyo FITI, kwa vifaa vilivyotumika kuujengea mji huo..jinsi watakatifu hao walivyostahili kwa utakatifu wao kujengwa juu ya misingi ya mitume na manabii (yaani BIBLIA) na sio katika mapokeo ya kibinadamu na madhehebu.

Mji huo unaonekana ukiwa umejaa dhahabu kote, ikiashiria utakatifu wa wateule..Unaonekana ukiwa umepambwa kwa vito vya thamani vya kila namna, ikiwakilisha wito na utumishi tofauti tofauti wa wateule wa Mungu.

Embu tusome kidogo tabia za mji huu..

Ufunuo 21:9 “Akaja mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na vile vitasa saba vilivyojaa yale mapigo saba ya mwisho, naye akanena nami, akisema, NJOO HUKU, NAMI NITAKUONYESHA YULE BIBI-ARUSI, MKE WA MWANA-KONDOO.

10 AKANICHUKUA KATIKA ROHO MPAKA MLIMA MKUBWA, MREFU, AKANIONYESHA ULE MJI MTAKATIFU, YERUSALEMU, UKISHUKA KUTOKA MBINGUNI KWA MWENYEZI MUNGU;

11 wenye utukufu wa Mungu, na mwangaza wake ulikuwa mfano wa kito chenye thamani nyingi kama kito cha yaspi, safi kama bilauri;

12 ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu, wenye milango kumi na miwili, na katika ile milango malaika kumi na wawili; na majina yameandikwa ambayo ni majina ya kabila kumi na mbili za Waisraeli.

13 Upande wa mashariki milango mitatu; na upande wa kaskazini milango mitatu; na upande wa kusini milango mitatu; na upande wa magharibi milango mitatu.

14 Na ukuta wa mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na katika ile misingi majina kumi na mawili ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.

15 Na yeye aliyesema nami alikuwa na mwanzi wa dhahabu, apate kuupima huo mji, na milango yake, na ukuta wake.

16 Na ule mji ni wa mraba, na marefu yake sawasawa na mapana yake. Akaupima mji kwa ule mwanzi; ulikuwa kama maili elfu na mia tano; marefu yake na mapana yake na kwenda juu kwake ni sawasawa.

17 Akaupima ukuta wake, ukapata dhiraa mia na arobaini na nne, kwa kipimo cha kibinadamu, maana yake, cha malaika.

18 Na majenzi ya ule ukuta wake yalikuwa ya yaspi, na mji ule ulikuwa wa dhahabu safi, mfano wa kioo safi.

19 Na misingi ya ukuta wa mji ilikuwa imepambwa kwa vito vya thamani vya kila namna. Msingi wa kwanza ulikuwa yaspi; wa pili yakuti samawi; wa tatu kalkedoni; wa nne zumaridi;

20 wa tano sardoniki; wa sita akiki; wa saba krisolitho; wa nane zabarajadi; wa kenda yakuti ya manjano; wa kumi krisopraso; wa kumi na moja hiakintho; wa kumi na mbili amethisto.

21 Na ile milango kumi na miwili ni lulu kumi na mbili; kila mlango ni lulu moja. Na njia ya mji ni dhahabu safi kama kioo kiangavu.

22 Nami sikuona hekalu ndani yake; kwa maana Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo, ndio hekalu lake.

23 Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo.

24 Na mataifa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa nchi huleta utukufu wao ndani yake.

25 Na milango yake haitafungwa kamwe mchana; kwa maana humo hamna usiku.

26 Nao wataleta utukufu na heshima ya mataifa ndani yake.

27 Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.”

Unaona hapo Yohana anaonyeshwa MKE WA MWANAKONDOO ambaye ndiye YERUSALEMU MPYA, na hapo mwisho kabisa anakuambia 21.24 “Na mataifa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa nchi huleta utukufu wao ndani yake”.

Sasa mwisho kabisa Mungu akishamaliza kuujenga huu mji ambao mpaka sasa anaujenga katikati ya watu wake na unakaribia kuisha, hapo ndipo maskani ya Mungu itakapokuwa na wanadamu, Hapo ndipo Mungu atakaposhuka na kukaa katikati ya wanadamu kwenye maskani yake..Na maskani yake ndio huu mji Yerusalemu mpya, ambayo inamwakilisha bibi-arusi kwa Kristo tu peke yake. Hivyo Mungu atakaa ndani ya hawa watu… Hawa watakuwa ni watu wa-kipekee sana mbele za Mungu, kama vile sisi tuwaonavyo malaika, ndivyo itakavyokuwa watu watakaopewa neema ya kuingia kule watakavyowaona hawa bibi-arusi wa Kristo..

Huo ndio mji ambao Ibrahimu alikuwa anautazamia.. licha ya kuahidiwa kuwa taifa hodari duniani hakujisumbua kulitazama hilo kama alivyolingojea hili kwa saburi zote..Swali ni je! Wewe nawe ni miongoni mwa mji mtakatifu wa Mungu ambao Mungu anauandaa sasa?..Yerusalemu mpya, bibi-arusi wa Kristo?..Je! Kristo akirudi leo unao uhakika wa kwenda naye?. Je! unaishi maisha ya kutazama mbinguni, au mambo tu ya duniani?.

 Je! umeoshwa dhambi zako, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, kama Neno lenyewe “ubatizo” linavyomaanisha, na kwa jina la YESU KRISTO?. na ikiwa umefanya hivyo vyote je! maisha yako yanauhakisi utakatifu? (Waebrania 12:14), maana biblia inasema hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao huo.

Ikiwa hayo hayapo ndani yako.. unao muda, sasa mji ule unakaribia kuisha ujenzi wake, fanya bidii uingie kabla mlango wa neema haujafungwa. Ulimwengu huu na mali zisiwe kisingizio siku ile. Kwasababu wapo waliokuwa na mali zaidi yangu na yako na waliokuwa na mafanikio kupita ya Ibrahimu lakini waliishi kama wapitaji tu hapa dunia.

Isaya 35: 8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; WASAFIRIO, WAJAPOKUWA WAJINGA, HAWATAPOTEA KATIKA NJIA HIYO.

Ni matumaini yangu utatubu leo na Bwana akujalie kuishi katika utakatifu na usafi.

Ubarikiwe sana.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

NJIA KUU YA KUINGIA KATIKA ULE MJI.

UFUNUO: Mlango wa 21

ALIPO NA ATAKAPOKUWEPO BIBI-ARUSI WA YESU KRISTO.


Rudi Nyumbani

Print this post

HUDUMA YA UPATANISHO.

2 Wakorintho 5: .17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

18 Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, ALIYETUPATANISHA sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho;

19 yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.

20 Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo mpatanishwe na Mungu.

Kuna sababu kadha wa kadha kwanini Yesu Kristo Bwana wetu, anajulikana kama Mwana wa Mungu, hiyo ni moja ya sifa yake kuu..Ingawa yeye alikuwa ni MUNGU katika mwili, lakini hilo halikuwa na umuhimu mkubwa sana kwetu kulifahamu , kuliko kumfahamu yeye kama mwana wa Mungu, ndio maana huoni mahali popote akitafuta kujionyesha yeye kuwa ni MUNGU. Hakutaka hilo, kwasababu hiyo sio sababu kubwa iliyomleta duniani, hakuja kutafuta kuabudiwa duniani…bali kutafuta kilichopotea. Kama ingekuwa amekuja kutafuta kuabudiwa kama Mungu, basi angekaa huko huko mbinguni kwenye utukufu wake angekuwa hana sababu ya kushuka huku duniani kwenye mavumbi..

Raisi anapokutana na familia yake cheo chake kinabadilika na kuwa Baba na MWANA-FAMILIA na sio raisi tena, hatamwadhibu mwanawe kwa kutumia vyombo vya dola, bali atatumia fimbo kama ikiwezekana, na Yesu Kristo alivyokuja duniani cheo chake cha kimungu kilibadilika na kuwa MWANA. Kwahiyo ilimpasa awe kama mwanadamu, ndio maana watu wasiomwelewa Bwana YESU wanapinga vikali kuwa yeye sio Mungu, Mungu gani anakufa? Analia? Anakula na kunywa?…Ni kweli kwa kumchunguza tu pasipo kuwa na ufunuo wa utendaji wake kazi hutaweza kuona uungu wowote ndani yake. Lakini akikujalia kupata ufunuo utamwelewa vizuri yeye ni nani. ukisoma Wafilipi 2:5-8, pamoja na 1Wakorintho 2:6-8, na Tito 2:13 na Timotheo 3:16, Utapata  picha halisi ya kuwa yeye ni nani. Na kwamba alikuja katika SIRI KUU SANA, ijulikanayo kama Siri ya utauwa..Na biblia inasema siri hiyo haijulikani kwa kila mtu bali kwa wakamilifu tu peke yao ya kwamba Kristo YESU ni MUNGU.

Lakini Bwana Yesu alipokuja duniani alitamani sana sisi tumjue yeye kama Mwana wa Mungu kuliko kumjua yeye kama Mungu, ndio maana aliwauliza wakati Fulani wanafunzi wake..”watu husema ya kuwa mimi ni nani?” wakasema wengine Eliya, wengine Yohana mbatizaji, wengine Yeremia n.k akawauliza na wanafunzi wake, na ninyi mnasema ya kuwa mimi ni nani? “PETRO AKAJIBU WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.

Unaona?  Bwana Yesu alimsifia Petro kwa ule ufunuo alioupata wa kumtambua Kristo kama mwana wa Mungu..

“Yesu akajibu, akamwambia, HERI wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni” (Mathayo 16:16-19)

Zingatia hilo neno “HERI” Ikiwa na maana kuwa amebarikiwa yeye alifahamuye hilo, unaweza ukajiuliza kwanini Bwana hakumrekebisha Petro na kumwambia hapana! Mimi si mwana wa Mungu, bali ni Mungu mwenyewe niliyekuja katika mwili. Unaona jambo ni lile lile, Yeye anataka tumwelewe ni kitu gani kilichomleta Duniani zaidi ya kuelewa ni kitu gani alichokiacha mbinguni.

Alifanyika kuwa MWANA WA MUNGU, ili kutuonyesha sisi NJIA ya jinsi mwana wa Mungu anavyotakiwa awe, ili siku atakapoondoka duniani, sisi tuliosalia kwa kuyaangalia maisha yake, tujifunze kwake, alikuja kutengeneza njia iliyoharibika..ili kwa kumtazama yeye tuyarekebishe maisha yetu. Ili yafanane na ya kwake ili nasi tuwe WANA WA MUNGU kweli kweli. Kama yeye alivyomtegemea Baba nasi tumtegemee Baba asilimia 100, kama yeye alivyokuwa mtakatifu hata akashuhudiwa mbinguni nasi tuwe hivyo hivyo, kama yeye alivyovumilia nasi tuvumilie majaribu, kama yeye alivyokuwa na upendo nasi tuwe na upendo.n.k Hizo ndio tabia za kuwa MWANA WA MUNGU. Sio kusema sisi ni wana wa Mungu lakini maisha yetu hata kidogo hayafanani na ya kwake, yeye ametupa kielelezo, kama yeye alivyofanya na kuishi na sisi pia tufanye na kuishi vilevile kama yeye..

Ni sawa na mwalimu aliyeona wanafunzi wake hawamwelewi akaamua kuvua cheo chake cha ualimu na kuvaa uniform za kiuanafunzi na kwenda kuketi pamoja na wanafunzi, na kujifanya yeye ni mwanafunzi na kusoma nao na kujiweka chini ya changamoto zote za kiuanafunzi ili tu kuwaonyesha njia bora ya kusoma inavyopaswa na kumwelewa mwalimu anapofundisha. Ndivyo na Bwana Yesu alivyofanya kuacha enzi na mamlaka kuja duniani. Ni kutuonyesha tu sisi njia!

Lakini tukiachana na hayo, tunaweza kujifunza pia sifa nyingine kuu ya KUWA MWANA WA MUNGU, Na sifa hiyo si nyingine zaidi ya UPATANISHO, Sifa hii ndio iliyobeba kiini cha somo letu leo…

Sasa sababu nyingine kubwa iliyomfanya Bwana Yesu kuwa mwana wa Mungu na si malaika ni KUTUPATANISHA SISI NA MUNGU. Kumbuka sisi tulikuwa tumepotea dhambini, na tulikuwa tayari wote ni wa kwenda kuzimu, hakuna hata mmoja wetu angepona hata Musa, hata Eliya, hata Yohana Mbatizaji hata Adamu mwenyewe wote walikuwa ni wakupotea…Lakini kwa kupitia damu ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu tumepatanishwa na Mungu. Tunakwenda mbinguni bure endapo tukimwamini yeye na kuyaishi maneno yake.

Hivyo basi ili na sisi tuwe wana wa Mungu ni lazima tuwe wapatanishi kama yeye. Utauliza? Na sisi kwahiyo inatupasa tumwage damu kama yeye?? Jibu! Damu ya Yesu inatosha!

ilishamwagika mara moja, lakini alitupa kielelezo kama yeye alivyotufanyia sisi na sisi tuyafanye kwa wengine, kwahiyo ndio wakati mwingine kama inabidi inatupasa na sisi kumwaga damu au kutoa uhai wetu kwaaajili ya wengine..maandiko yanasema hivyo katika kitabu cha 1 Yohana 3:16” Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu” HUO NDIO UPATANISHO, Na kwa kufanya hivyo tutaonekana tumekuwa WANA WA MUNGU,kwa macho yakimbinguni, tutafananishwa na MWANA WA MUNGU,Yesu Kristo aliyetoa uhai wake kwa ajili yetu. Biblia inasema katika kitabu cha Mathayo..

Mathayo 5:9 “HERI WAPATANISHI; Maana hao WATAITWA WANA WA MUNGU”

Upatanishi unaozungumziwa hapo juu, sio kuwapatanisha watu wanaogombana au watu waliokosana hapana! Bali kujitoa kwa hali na mali kwa ajili ya kuwapatanisha watu na Mungu wao, KWA KUWAPELEKEA HABARI NJEMA za wokovu na hata kugharimika kufa, ilimradi tu umpatanishe mtu na Muumba wake, kama Bwana Yesu alivyofanya. Maandiko yanasema..

2 Wakorintho 5: 17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.

18 Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, NAYE ALITUPA HUDUMA YA UPATANISHO;

19 yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; NAYE AMETIA NDANI YETU NENO LA UPATANISHO.

20 Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, KANA KWAMBA MUNGU ANASIHI KWA VINYWA VYETU; twawaomba ninyi kwa ajili ya KRISTO MPATANISHWE NA MUNGU.

Umeona hapo? Ndugu…Kristo,Mwana wa Mungu alitupatanisha sisi na Mungu ndio maana akaitwa Mwana wa Mungu, kwasababu heri walio wapatanishi hao wataitwa wana wa Mungu, na sisi Bwana ametupa huduma ya upatanisho..Ndiyo haya maneno yanayosema nawe sasa,…kama maandiko yanavyosema hapo katika mstari wa 20 “KANA KWAMBA MUNGU ANASIHI KWA VINYWA VYETU; twawaomba ninyi kwa ajili ya KRISTO MPATANISHWE NA MUNGU.”

Biblia inakusihi ndugu unayesoma ujumbe huu ambaye hujawa kiumbe kipya bado, ambaye ni vuguvugu katika imani, ambaye bado unaupenda ulimwengu, ambaye bado hujaacha anasa, wala usengenyaji, wala ulevi, wala tamaa mbaya…inakuomba upatanishwe leo na Mungu.

Mgeukie yeye leo ukanywe maji ya uzima, kama Bwana mwenyewe alivyosema katika Ufunuo 22:17 “Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.”..Ni bure kabisa yanapatikana…Utafika wakati haya maji hutayapata bure wala kwa fedha, yatakuwa hayapo…Na unajua madhara ya kukosa maji ya uzima baada ya kifo??..ni mabaya sana usitamani uyakose huko.

Kama hujatubu dhambi zako, bado hujachelewa, mwambie Bwana akusamehe, mahali popote ulipo, jitenge peke yako kwa muda kisha tubu! Mwambie Bwana kuanzia leo unahitaji kuwa kiumbe kipya, unahitaji kupatanishwa naye, wewe mwenye dhambi na kama umemaanisha kufanya hivyo yeye “anakubali wakosa” atakusamehe na atakupa amani ya ajabu moyoni mwako, hiyo amani ndio uthibitisho wa kusamehewa dhambi zako, na bila kupoteza muda haraka sana nenda katafute ubatizo sahihi wa kimaandiko, wa maji mengi na kwa JINA LA YESU KRISTO (kulingana na Matendo 2:38) ili dhambi zako ziondoke kabisa kabisa, Baada ya kufanya hivyo Bwana Yesu Mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia kushinda dhambi na kuilewa biblia vizuri..

Kwa kukamilisha hatua hizo utakuwa umezaliwa mara ya pili na kuwa kiumbe kipya…kama maandiko yalivyosema hapo juu..” MTU AKIWA NDANI YA KRISTO YA KALE YOTE YAMEPITA TAZAMA YAMEKUWA MAPYA”..Bwana mwenyewe atayafanya mapya maisha yako kwa kila NYANJA!

Mungu akubariki sana…Na kama tayari ulishakuwa ndani ya Kristo, yaani umeshazaliwa mara ya pili, Neno linasema TUMEPEWA HUDUMA YA UPATANISHO, hivyo ni wajibu wako pia kwenda KUWAPATANISHA WENGINE NA MUNGU WAO, yaani kwenda kuwaambia habari za Neema zilizopo ndani ya Yesu Kristo na Raha na Tumaini, na toba!. Huo ndio uthibitisho wa kuwa kweli umefanyika kuwa mwana wa Mungu, kumbuka Neno hili “heri wapatanishi maana hao wataitwa wana wa Mungu”.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO

MWANA WA MUNGU.

UHURU WA ROHO.


Rudi Nyumbani

Print this post

USIMWABUDU SHETANI!

Mungu alipomtuma Musa, kwa Farao, tunasoma habari alimpa maagizo ya nini cha kufanya atakapofika kwa Farao, na mojawapo ya maagizo hayo alimwambia akifika aitupe chini ile fimbo aliyokuwa nayo mkononi mbele ya Farao nayo itageuka na kuwa nyoka, na kisha aitwae tena mkononi mwake nayo itageuka kuwa fimbo kama mwanzo. Na pia tunaona Bwana alimfanyisha mazoezi kabisa akiwa kule kule mlimani kabla hata ya kwenda Misri kwa Farao, maana Mungu alimwambia palepale aitupe chini ile fimbo na alipoitupa ikageuka kuwa nyoka na Musa alipoona fimbo imegeuka kuwa nyoka alitaka kukimbia..

Bwana akamwambia akamshike Yule nyoka Mkia, kwa kusitasita na kutetemeka alikwenda na kumshika, na mara saa hiyo hiyo Yule nyoka akageuka na kuwa fimbo tena..Zoezi hilo lilimsadia kupata ujasiri, pindi atakapofika kwa Farao na kuitupa chini ile fimbo itakapogeuka na kuwa nyoka, asiigope kuishika na kuitwaa tena iwe fimbo.

Sasa swali la kujiuliza ni kwanini Mungu aitumie ile fimbo kuigeuza kuwa nyoka na wala si kitu kingine, kwanini hakutaka igeuke na kuwa chuma, au igeuke na kuwa sungura, au kiumbe chochote kile tofauti na NYOKA!.

Ili tuelewe hilo vizuri, turudi kidogo kujifunza histori ya Taifa la Misri, Misri ni Taifa lililopo kwasasa katika Bara la Afrika, kaskazini mashariki mwa Afrika, na asili ya Taifa hilo ilikuwa ni wana wa HAMU, aliyekuwa mwana wa Nuhu, Yule aliyeuona uchi wa Baba yake na asiusitiri, na hivyo akalaaniwa. Kwahivyo wana wa Hamu wakasafiri pande za kusini wakajenga miji huko, na Taifa mojawapo la wana hao wa Hamu ndio Misri. Mambo mengi yaliendelea hapo katikati hatuna muda wa kutosha wa kuyazungumzia yote lakini historia inasema ndio Taifa lililokuja kuwa na nguvu kuliko mengine yote kwa wakati huo.

Utamaduni wa Taifa hilo haikuwa kumwabudu Mungu wa Israeli, kwasababu walikuwa hawamjui Mungu wa Israeli bado, hivyo walikuwa wana miungu yao mingine mingi mingi tu!, waliabudu jua, mwezi na mambo mengine mengi…lakini moja ya miungu waliyokuwa wanaiabudu na kuipa heshima ya juu zaidi, ilikuwa ni NYOKA. Na aina ya nyoka hao waliokuwa wanawaabudu anajulikana kama COBRA. Walikuwa wanaamini kuwa nyoka aina ya Cobra ni mungu mkuu ambaye ana uwezo mkubwa sana katika kulilinda taifa lote la Misri dhidi ya Maadui zao, walitumia sanamu yake kama ishara kila mahali katika nyumba zao za kawaida na katika makasri yao makubwa ya kifalme. Hata katika kofia za kifalme za wafalme kulikuwa ni kijisanamu kidogo cha cobra kwenye kipaji cha uso kinachoangalia mbele, hicho kilikuwa kinavaliwa daima waliamini kuwa kama vile nyoka aina ya Cobra anavyotema mate ya sumu dhidi ya maadui zake usoni, vivyo hivyo cobra wanayemwabudu huyo huyo atawatemea moto maadui wa Farao wote wanaokuja mbele yao.

Kwahiyo ilikuwa ni imani iliyoheshimika sana, na ilikuwa inawapa matunda, kwasababu nyuma yake alikuwa ni shetani, na kama unavyojua shetani naye anawapa anaowapenda kama anavyotaka. Kwahiyo huyo mungu wao nyoka alikuwa anawapa ushindi mara nyingi ndio maana, Taifa hilo la Misri likainuka kuwa na nguvu kila mahali.

Wengi tunafikiri kuwa miungu hiyo ya Misri haikuwa na nguvu yoyote! Usidanganyike! Ilikuwa ina nguvu kama kawaida, na wamisri walikuwa wanaona inavyowasaidia, na endapo wakiwa hawaiabudu inavyopaswa ilikuwa inawaletea madhara, kwahiyo sio kwamba wamisri walikuwa wanaabudu kitu kisicho dhahiri!.. Ukitaka kujua walikuwa wanaabudu kitu kilicho dhahiri au la! Tazama yale mapigo, Musa aligeuza fimbo kuwa nyoka nao pia wakafanya hivyo hivyo, na baadhi ya mapigo pia waliweza kuiga, sasa kama hiyo miungu yao haikuwa dhahiri kwanini iliweza kufanya ile miujiza?? Jiulize hilo, na kama hiyo miungu yao ilikuwa na nguvu ya mpaka kuweza kubadilisha fimbo kuwa nyoka unadhani ingeshindwa vipi kutemea moto kwa maadui zao wakiwa vitani??..

Hata Israeli wakati Fulani walipokengeuka na kuanza kuabudu mabaali, sio kwamba walikuwa wanaabudu kitu kisichokuwepo, hapana! Walikuwa wanaabudu kitu kilicho dhahiri kabisa (ambacho ni shetani mwenyewe pasipo wao kujijua)..Na hata wakati ule walipojaribu kushusha moto mbele ya Eliya juu ya ile dhabihu usidhani ni kwamba walikuwa wanafanya kitu cha kujaribisha au kubahatisha, hapana! hiyo miungu yao kushusha moto sio jambo kubwa, Na ilishawahi kushusha hapo kabla, ndio maana unaona walipata ujasiri mbele ya Eliya kulileta lile shindano, lakini kilichowashtusha ni kama tu hicho kilichomshtusha Farao kuona nyoka wake wanamezwa mbele ya macho yake, na makuhani wa mabaali vivyo hivyo walishtuka kuona mbona moto haushuki kama siku zote!..

Kwahiyo Musa wakati anamwendea Farao, Mungu alitumia ishara ya nyoka, ili kuwaonyesha wa Misri kuwa mungu wanayemwabudu sio wa kweli, ingawa anawatendea miujiza , na kwamba nguvu zake zina mipaka, yupo mwenye nguvu kuliko mungu wao cobra wanayemwabudu, ndio maana alitumia ishara ya nyoka awali kabisa ili wamisri wamwelewe vizuri, kwasababu laiti angetumia ishara ya kugeuza fimbo kuwa sungura wamisri wasingeiamini kwasababu wao wanajua miungu ni mfano wa viumbe wakali kama nyoka, na ndio maana unaona nyoka wa Musa aliwameza wale nyoka wa Farao. 

Kwa ufupi ishara ile, ilitosha kabisa kumwaminisha Farao kuwa Mungu wa Israeli ni Mungu mkuu kuliko mungu wao. Hata wamisri wote baada ya kuiona ile ishara waliamini, kulikuwa hakuna haja ya kuendelea na ishara nyingine mbele…kwasababu mbele ya macho yao wameshuhudia mungu wao cobra wanayemweshimu na anayewasaidia siku zote katika vita, amemezwa na Mungu mwingine, ni ishara madhubuti kuwa endapo wakiendelea kushindana na huyo Mungu watamezwa vile vile, kama mungu wao alivyomezwa…Lakini kwasababu Mungu alitaka kuonyesha utukufu wake wote, ndiyo akaufanya moyo wa Farao usiamini, uwe mgumu. Lakini katika hali ya kawaida, Farao tayari alishaamini.

Ndugu kama uliwahi kuomba rozari na ikakupa majibu uliyoyaomba, uliiomba fedha ikakupa, uliiomba rozari ushindi ikakupa, na ukaiamini kiasi kwamba unatembea nayo kila siku shingoni, kwasababu haikuangushi……napenda nikwambie ndugu yangu mpendwa huyo sio Mungu ni shetani nyuma ya hiyo rozari, haijalishi hiyo rozari imekufanikisha kiasi gani, nataka nikuambie yupo Mungu aliye mkuu kuliko hiyo rozari atakayeimeza hiyo rozari unayoivaa na kuiomba kila siku, Hata Farao alitumia nyoka kuamini hakuna mungu zaidi ya huyo, na nguvu za Cobra zilimfanikisha kuliko mataifa yote duniani, lakini alipokuja Mungu wa miungu na kumkataa huyo. Misri iligeuka kuwa kama jalala la dunia.

Kama umekuwa ikiisujudia sanamu kanisani kwako pasipo kujua kuwa unamwabudu shetani na imekujibu maombi na kukupa kila unachokihitaji… Mungu hakuweza kukuhukumu kwasababu ulikuwa huujui ukweli, lakini leo umeujua ukweli, umgeukie yeye mwenye nguvu kuliko hiyo sanamu, itupe leo ivunje vunje leo, acha kuiabudu kwasababu yupo Mungu juu mwenye nguvu kuliko hiyo sanamu ya BIKIRA MARIA unayoiabudu na anataka kukubariki kuliko hata hapo ulipo. Anataka kukupa mafanikio kuliko hata hayo uliyonayo. Ambayo shetani amekupiga upofu kukudanganya kwamba ni mafanikio, kumbe ni mafanikio feki,…hiyo sanamu haiwezi kukupa raha nafsini mwako, hiyo sanamu haiwezi kukusamehe dhambi, hiyo sanamu haiwezi kukufanya uwe mtakatifu, hiyo sanamu haikupi kibali cha kuingia ufalme wa mbinguni, hiyo sanamu haiwezi kuondoa ulevi ulionao! Haiondoi uasherati ndani yako!! Hiyo sanamu sio Mungu wa kweli! Kwasababu ndivyo ilivyokuwa hata kwa Farao, wale nyoka aliokuwa anawaabudu walimpa utajiri lakini walikuwa hawamhukumu kuhusu tabia yake mbaya ya kuonea watu wasiokuwa na hatia! Mungu gani huyo!

Utasema huyo Mungu mbona watu wake ni maskini, nataka nikuambie hata Farao aliwaona wana wa Israeli ni maskini na kuwatesa kule kwenye mashimo ya matope! Lakini Misri yote ilishtuka kuona kuwa wale wanaowadharau kumbe ndio wanaomwabudu Mungu mwenye nguvu kuliko Mungu wao…..siku ile walipoona Misri yote imeteketea,…na wewe usiangalie hali ya watu wanaomwabudu Mungu wa Kweli ipoje, wapo vile kwasababu fulani tu, lakini hawatakuwa vile siku zote, ipo siku watang’aa kama jua, isikilize hii sauti ya Mungu inayozungumza nawe sasa…Mungu wa kweli sio nyoka, wala ekaristi, wala sanamu ya kiumbe chochote kile, wala sanamu ya mwanadamu yoyote Yule, wala Mungu wa kweli haabudiwi kwa kupitia sanamu ya Bikira Maria, wala chochote kile, Mungu wa kweli anaabudiwa juu mbinguni KATIKA ROHO NA KWELI.

Pengine umekwenda kwa waganga wa kienyeji na kwa kupitia wao umepata mafanikio, na wamekwambia wakristo hawamwabudu Mungu wa kweli, nataka nikuambia ndugu yangu, wamekudanganya na wamekupoteza..Wale nyoka walimpa Farao mafanikio makubwa sana kuliko uliyonayo wewe, lakini hao hao hawakuweza kumwokoa na hukumu ya Mungu iliposhuka juu ya Misri.

Na wewe siku hizi usiweke moyo wako mgumu, achana na hao waganga, kwasababu utaelekea kwenye ziwa la Moto, tupa leo hirizi zote walizokupa, choma moto, mvue mwanao hirizi zote ulizomvalisha kiunoni na shingoni na mikononi, tupa na wewe kila kitendea kazi ulichopewa na mganga wa kienyeji eti upate amani, fedha au utajiri, au vikulinde…hivyo vitendea kazi vitakulinda dhidi ya wachawi wenzako tu tena wenye nguvu kidogo kuliko mganga wako lakini wakija wachawi wengine wenye nguvu kuliko wewe na mganga wako watakuua na kukushinda tu!, na zaidi ya yote ni heri ingekuwa hivyo tu!! Ghadhabu ya Mungu bado inakungojea endapo ukikataa kutubu ndiyo itakayokuharibu kabisa kama ilivyomuharibu Farao, alipoteza fahari yake yote na kufiwa na mwanawe wa pekee.

Ukiyafahamu hayo ni wakati wa kugeuka, Bwana anakupenda na kukuhitaji, kama hujampa Bwana maisha yako, mlango wa Neema bado upo, ila hautakuwepo siku zote, biblia inasema utafika wakati mlango utafungwa, na watu watalia na kuomboleza wakiomba Bwana awafungulie, na Bwana hatawafungulia, Hivyo tubu leo kwa kumaanisha kuacha kabisa maisha ya dhambi uliyokuwa unayaishi huko nyuma, maisha ya usengenyaji, maisha ya rushwa, maisha ya uasherati, maisha ya utazamaji pornography, maisha ya usagaji, maisha ya ulawiti, maisha ya ushirikina, na uhudhuriaji wa waganga wa kienyeji,maisha ya aubuduji sanamu, maisha ya ulevi na sigara.n.k n.K

Na baada ya kufanya hivyo kama hujabatizwa nenda katafute ubatizo sahihi mahali popote pale kulingana na maandiko, na ubatizo sahihi ni wa maji mengi na kwa JINA LA YESU kulingana na Matendo 2:38, na baada ya hapo Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia kushinda dhambi, maana kwa nguvu zetu hatuwezi kamwe kushinda dhambi, na Roho huyo huyo atakusaidia kuielewa biblia na kukuongoza katika kweli yote usipotee kwa kuchukuliwa na upepo wa shetani. Na ukizingatia kufanya hivyo utakuwa umezaliwa mara ya pili, na kuwa na uhakika wa kuiona mbingu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali “share” ujumbe huu kwa wengine, na utakuwa umeshiriki katika kuisambaza injili ya Kristo.

Maran atha!

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

NEHUSHTANI (NYOKA WA SHABA)

UZAO WA NYOKA.

WANA WA MAJOKA.

BWANA YESU ALIMAANISHA NINI ALIPOSEMA TUWE NA BUSARA KAMA NYOKA?


Rudi Nyumbani

Print this post