Hivyo unachopaswa kufanya ni KUTUBU KWANZA KWA KUDHAMIRIA KUACHA DHAMBI Zako zote. Unadhamiria kuacha uasherati, uwongo, ulevi, rushwa, pornography, wizi, uvaaji mbaya, utukanaji, utoaji mimba, anasa na mambo yote uliyokuwa unayafanya yasiyompendeza Mungu, Na baada ya kufanya hivyo nenda ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kimaandiko wa kuzamishwa mwili wako wote kwenye maji na kwa jina la YESU KRISTO kulingana na (Matendo 2:38, 8:16, 10:48, na 19:5,) ili upate ondoleo la dhambi zako..Na kisha Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu atakayekusaidia kushinda dhambi na kukuongoza katika kuijua kweli yote ya kimaandiko..