Title January 2022

Je! Ni kanisa lipi sahihi kumuabudia Mungu?

Imekuwa changamoto kubwa kwa mtu anayeokoka mara ya kwanza, au kwa yule mtu ambaye anahitaji kumwabudu Mungu katika njia sahihi, kutambua kanisa sahihi la kumfanya yeye amwabudu Mungu wake  katika Roho na kweli.

Hiyo ni kutokana na kuzuka kwa imani nyingi potofu, na watu wenye nia mbaya, ambao lengo lao ni kuwapoteza watu na sio kuwaokoa.

Hivyo wewe kama mkristo huna budi kuwa mchunguzi sana, na Mungu pia ameruhusu tuwe watu wa namna hiyo sawasawa na (1Timotheo 4:1 )..kwasababu hizi ni zama za uovu.

Lakini pamoja na kwamba kuna makanisa na imani nyingi za uongo ulimwenguni, bado suluhisho sio kukaa nyumbani..kwasababu ni agizo la Bwana kwamba tusiache kukusanyika pamoja na wengine, kumwabudu yeye(Waebrania 10:25)..Na faida zake ni nyingi sana, tofauti na utakavyokwenda mwenyewe mwenyewe, wakati wote. Hata ukutanapo na jiwe katika chakula haikufanya wewe umwage chakula chote..utalitoa lile jiwe utaendelea kula..Vivyo hivyo na katika habari ya makanisa.

Lakini pia kumbuka kujiunga na kanisa sio tiketi ya wewe moja kwa moja kwenda mbinguni..lakini kanisa sahihi lina sehemu kubwa sana ya kukusaidia wewe kufika mbinguni.

Makanisa yanafananishwa na SHULE. Kwamfano mwanafunzi anayehitimu shule ya msingi..akienda sekondari, huwa anakutana na chaguzi nyingi sana za shule zikimwita..na kila shule inajinadi kuwa ina ufauluji mzuri, na mazingira mazuri ya kusomea..

Hivyo ni wajibu wa mwanafunzi mwenyewe kufanya uchunguzi wake mwenyewe je, ni kweli shule hiyo ina vigezo vya kumsaidia kufaulu? .Uchaguzi wa shule mbaya utamweka katika hatari kubwa sana ya kufeli haijalishi atakuwa na akili nyingi kiasi gani.

Lakini pamoja na kwamba shule itakuwa na ubora na ufauluji mzuri, bado bidii ya mwanafunzi mwenyewe binafsi inahitajika..

Hivyo vyote viwili vinasaidiana na vina umuhimu, na vinakwenda sambamba. Tengeneza picha mwanafunzi anayesema mimi siendi shule..nitatafuta tu namba yangu ya mtihani wa mwisho siku hiyo ikifika nikafanye.. nitakuwa najisomea peke yangu nyumbani kwa miaka yote hiyo.. Jiulize mwanafunzi kama huyo atafaulu kweli..lengo la shule kuwekwa ni kumsaidia mwanafunzi ufauluji wake, kwa kukutanishwa na waalimu wa kumsaidia na kumpa nidhamu ya usomaji bila kuvutwa na mambo mengine..

Halikadhalika ukristo na kanisa ni vitu vinavyokwenda sambamba, na ni wajibu wako kuchagua kanisa sahihi litakalokusaidia kufanikisha safari yako ya wokovu hapa duniani.

Mpaka hapo naamini umepata picha..hivyo vifuatavyo ni vigezo muhimu sana vya kuukusaidia kutambua kanisa sahihi ni lipi

1) YESU KRISTO ndio kiini cha imani hiyo.

Tunapouzungumzia ukristo, tunamzungumzia Yesu Kristo, kanisa lisilomfanya Kristo peke yake ndio msingi wa imani hiyo. Ni kanisa la uongo. Ukiona halimtaji Kristo kwa kila kitu..Kimbia hilo kanisa..ikiwa jina la nabii au kiongozi ndio linatamkwa na kupewa heshima kubwa kuliko Kristo..ondoka haraka sana hapo..

Vilevile ukiona Bwana Yesu analinganishwa na watakatifu wengine, kana kwamba na wenyewe ni wapatanishi wa dhambi zetu kama yeye..mfano wa Yosefu na Maria. Ondoka pia hapo, haijalishi litakuwa na wafuasi wengi au zuri kiasi gani.

Wakolosai 2:18-19
[18]Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;
[19]wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukiruzukiwa na kuungamanishwa kwa viungo na mishipa, hukua Kwa maongeo yatokayo kwa Mungu.

   2) Pili, kanisa la kweli Linaamini Biblia Takatifu tu ndio mwongozo wake.

Ni lazima liamini Biblia yenye vitabu 66, na si zaidi wala pungufu..yapo madhehebu ambayo yameongeza vitabu vya Apokrifa katika biblia na kuifanya iwe na vitabu 73.

Ukiona dhehebu hili ondoka hapo, vitabu vyovyote nje ya vile vinavyojulikana yaani 66 havijaviviwa Roho Mtakatifu.

Ufunuo wa Yohana 22:18
[18]Namshuhudia kila mtu ayasikiaye maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mtu ye yote akiyaongeza, Mungu atamwongezea hayo mapigo yaliyoandikwa katika kitabu hiki.

Halikadhalika yapo mengine yanaamini katika mapokeo, kama vile waaminivyo bibila takatifu hayo pia yakimbie ni upotevu na udanganyifu mwingi upo ndani yake.

Utapotezwa tu..

     3) Tatu linafundisha mafundisho yanayolenga ufalme wa mbinguni.

Yohana mbatizaji alipoanza kuhubiri alisema tubu kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia..Bwana Yesu naye alihubiri kwa kusema tubuni kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia(Mathayo 3:2, 4:17)…mitume nao walihubiri na kufundisha vivyo hivyo.

Nasi pia tujue ukristo, ni habari za ufalme wa mbinguni na sio ufalme wa duniani..Ikiwa utakuwepo mahali unafundishwa na kushinikizwa tu juu ya mambo ya ulimwenguni wakati wote..yaani mali, na vitu vya ulimwenguni..hiyo ni ishara kuwa kanisa hilo ni la uongo..hivyo ondoka hapo.

Ndio zipo nyakati, hayo nayo yatafundishwa katika kanisa lakini sehemu yao iwe ndogo sana, yasiwe kiini cha mtu kuwepo kanisani kumwabudu Mungu. Kanisa ni habari za ulimwengu ujao.

   4) Utakatifu na Upendo:

Huu nao ni msingi mwingine wa kanisa hai la Kristo, kufundishwa utakatifu na Upendo ambavyo vyote viwili ndio vinatajwa kama malango ya kumuona Mungu sawasawa na (Waebrania 12:14, na 1Yohana 4:7-8 ).

Kanisa ambalo, watu wake wanamwabudu Mungu watakavyo, wanawake na vijana wanavaa hohe hahe, wanaenda kanisani kama vile disco na hawaambiwi chochote, hawakemewi dhambi, hawaonywi..hilo sio kanisa hai.

  5) Karama za Roho:

Alipo Roho Mtakatifu, atadhihirisha na uwepo wake pia, kama kanisa haliruhusu karama kama za uponyaji wa Roho, unabii, uinjilisti, lugha, maombi n.k. ni dalili kuwa hilo sio kanisa la Kristo.

Yapo ambayo yanaamini lakini hayahimizi, haya yanaweza yasiwe na shida..lakini yapo ambayo hayaamini kabisa kiasi kwamba lolote likitokea waweza fukuzwa kanisani..haya ndio uyakimbie, kabisa kwasababu yatakuua kiroho, ushindwe kumtumikia Mungu kwa karama aliyoiweka ndani yako.

1 Wakorintho 12:7-11
[7]Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.
[8]Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule;
[9]mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja;
[10]na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha;
[11]lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.

Hivyo kwa vigezo hivyo, naamini utakuwa umepata mwanga wa kujua kanisa la kweli ni lipi.

Hivyo chukulia kwa uzito suala hili, lipime kanisa lako, kwasababu wengi wameshafungwa katika kamba za makanisa ya uongo na bado wanaendelea nayo..Usiogope kutoka kwasababu atakayehukumiwa ni wewe sio hilo dhehebu.

Nikitakie uchaguzi mwema.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Maji ya Farakano ni nini katika biblia?

Kama jina lake lilivyo “Maji ya Farakano”…maana yake ni maji yanayoondoa mafarakano.

Mtu yeyote katika Israeli ambaye alikuwa amejitia unajisi kwa kugusa maiti ya mtu, alikuwa amejifarakanisha na Mungu, hivyo hana budi kujitakasa, ili akubalike mbele za Mungu.

Na kitu pekee kilichokuwa kinaweza kumtakasa ni maji hayo maalumu, yaliyojulikana kama MAJI YA FARAKANO.

Maji hayo yalikuwa yanatengenezwa kwa majivu ya Ng’ombe mwekundu, ambaye hajazaa bado, wala hajatiwa nira, wala hajakamuliwa maziwa.

Ng’ombe huyu alikuwa ni maalumu kwa ajili ya upatanisho Wa dhambi za wana wa Israeli.

Baada ya kuchinjwa na kuteketezwa, majivu yake yalihifadhiwa na kuchanganywa na maji safi, sasa maji hayo ya majivu ya huyo ng’ombe ndio yaliyoitwa maji ya Farakano.

Endapo mtu yeyote atagusa maiti basi atajitakasa kwa kunyunyiziwa maji hayo ya farakano na atakuwa safi. Na mtu yeyote asiyejitakaswa na maji hayo sheria ilikuwa ni kuuawa.

Hesabu 19:1 “BWANA akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,

2 Hii ndiyo amri ya sheria BWANA aliyoagiza, akisema, Waambie wana wa Israeli wakuletee ng’ombe mke mwekundu asiye na kipaku, mkamilifu, ambaye hajatiwa nira bado;

3 nanyi mtamleta kwa Eleazari kuhani, naye atakwenda naye nje ya kambi, na mtu mmoja atamchinja mbele yake;

4 kisha Eleazari kuhani atatwaa katika damu yake kwa kidole chake, na kuinyunyiza damu yake kuelekea upande wa mbele wa hema ya kukutania mara saba;

5 kisha mtu mmoja atamchoma moto huyo ng’ombe mbele yake; ngozi yake, na nyama yake, na damu yake, pamoja na mavi yake pia atachoma moto;

6 kisha kuhani atatwaa mti wa mwerezi, na hisopo, na sufu nyekundu, na kuvitupa katika huo moto unaomchoma ng’ombe.

7 Ndipo kuhani atazifua nguo zake, na kuoga mwili wake majini, kisha baadaye ataingia kambini, naye kuhani atakuwa najisi hata jioni.

8 Na huyo aliyemchoma moto ng’ombe atazifua nguo zake majini, na kuoga mwili wake majini, naye atakuwa najisi hata jioni.

9 Kisha mtu mmoja aliye safi atayazoa majivu ya huyo ng’ombe, na kuyaweka yawe akiba katika mahali safi nje ya kambi, nayo yatatunzwa kwa ajili ya mkutano wa wana wa israeli, kuwa ndiyo maji ya farakano; ni sadaka ya dhambi.

10 Na yeye ayazoaye majivu ya huyo ng’ombe atazifua nguo zake, naye atakuwa najisi hata jioni; na jambo hili litakuwa amri ya milele, kwa wana wa Israeli, na wa mgeni akaaye kati yao.

11 Mtu agusaye maiti ye yote atakuwa najisi muda wa siku saba;

12 naye atajitakasa kwa yale maji siku ya tatu, na siku ya saba atakuwa safi; lakini kama hajitakasi siku ya tatu, ndipo na siku ya saba hatakuwa safi.

13 Mtu awaye yote agusaye maiti wa mtu aliyekufa, asijitakase, yuatia unajisi maskani ya BWANA; na mtu huyo atakatiliwa mbali na Israeli; maana, hayo maji ya farakano hayakunyunyizwa juu yake, atakuwa najisi; unajisi wake ukali juu yake bado”.

Lakini katika agano jipya hatuna sheria hiyo, kwamba tukigusa maiti tunakuwa najisi mpaka tunyinyuziwe maji hayo.

Unajisi katika agano jipya sio kushika maiti, wala si kula bila kunawa, si kukaa bila kuoga, wala si kuingia kanisani bila kutawadha..ni vizuri kufanya hayo kwa lengo la usafi tu!, Lakini haitusogezi karibu na Mungu n.k.

Bali unajisi hasa ambao unatuweka mbali na Mungu ni kutoa maneno machafu mdomoni mwetu, na kuwaza mabaya moyoni mwetu.

Marko 7:15,18-23 “Hakuna kitu kilicho nje ya mtu ambacho kikimwingia chaweza kumtia unajisi, bali vile vimtokavyo, ndivyo vimtiavyo unajisi yule mtu…..

18 Akawaambia, Hivi hata ninyi hamna akili? Hamfahamu ya kwamba kila kitu kilicho nje ya mtu, kikimwingia, hakiwezi kumtia unajisi;

19 kwa sababu hakimwingii moyoni, ila tumboni tu; kisha chatoka kwenda chooni? Kwa kusema hivi alivitakasa vyakula vyote.

20 Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi.

21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,

22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.

23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”

Mambo haya ndio yanayotufarakanisha sisi na Mungu na kutufanya kuwa najisi mbele zake.

Na unajisi huo hautakaswi kwa Maji ya Farakano, bali kwa Neno la Mungu.

Waefeso 5:25 “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;

26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;

27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa”.

Na neno la Mungu, ambalo ndio maji yatutakasayo linasema..

Matendo ya Mitume 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”

Hilo ndilo Neno la Mungu litusafishalo na kutuondolea UNAJISI WOTE!. Na ndio maji yetu ya Farakano katika agano jipya.

Je umetubu na kubatizwa kwa jina lake Yesu Kristo?..Je umepokea Roho Mtakatifu?..Kama bado unangoja nini?.

Hizi ni siku za mwisho na Bwana yu karibu kurudi, na walio najisi wote hawataurithi uzima wa milele.

Maran atha!.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je mwanamke anaruhusiwa kupanda madhabahuni akiwa katika siku zake?

Nini maana ya usimfunge ng’ombe kinywa apurapo nafaka!.(Kumbukumbu 25:4)

JIEPUSHE NA UNAJISI.

TATIZO LA NDANI LINALOWASUMBUA VIJANA, WALIOOKOKA.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi nyumbani

Print this post

Je suruali ni vazi la kiume tu?

Ni wapi katika biblia panaonyesha kuwa suruali ni vazi la kiume tu? Na vipi juu ya kanzu!, mbona kama ni mfano wa gauni lakini linavaliwa na wanaume, kwanini Suruali isivaliwe pia na wanawake!


Jibu: Vazi la Suruali mara ya kwanza katika biblia lilivaliwa na Makuhani.

Mungu aliwapa amri makuhani watengeneze suruali ambazo zilitofautiana kimaumbile, waliambiwa watengeneze suruali fupi (yaani kaptula), Na vile vile walikuwa wanavaa zile ndefu ambazo zilifika kabisa mpaka chini kwenye viiko vya miguu.

Kutoka 28:41 “Nawe mvike huyo nduguyo Haruni na wanawe nao mavazi hayo; nawe watie mafuta, na kuwaweka kwa kazi takatifu, na kuwatakasa, ili wapate kunitumikia mimi katika kazi ya ukuhani.

42 Nawe wafanyie SURUALI ZA NGUO YA KITANI, ili kufunika tupu ya miili yao; suruali hizo zitafika tangu kiunoni hata mapajani;

43 na Haruni na wanawe watazivaa, hapo watakapoingia katika hema ya kukutania, au hapo watakapoikaribia madhabahu ili watumike katika mahali patakatifu; wasije wakachukua uovu, wakafa; hii itakuwa ni amri ya milele kwake yeye, na kwa wazao wake”.

Na katika Israeli hakukuwa na Kuhani Mwanamke!, Makuhani wote walikuwa ni wanaume. Hivyo lilikuwa ni vazi la kiume. (Soma pia Kutoka 39:27, na Walawi 6:10)

Vile vile tunaweza kulithibitisha hilo kipindi kile cha akina Shedraka, Meshaki na Abednego. Wakati Mfalme Nebukadneza alivyowatupa katika lile tanuru la moto, maandiko yanasema walitupwa kule hali wamevaa suruali zao na kanzu zao na joho zao.

Danieli 3:21 “Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa SURUALI ZAO, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.

22 Basi kwa sababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto ukawaua wale watu waliowashika Shadraka, na Meshaki, na Abednego”.

Sasa Shedraka, Meshaki na Abednego hawakuwa wanawake, bali wanaume!, na hakuna popote katika biblia panataja au kuonyesha mwanamke kavaa suruali, kama hawa wakina Shedraki au kaagizwa kuvaa suruali kama hawa Makuhani.Hakuna!!. Ikifunua kuwa hilo ni vazi la kiume!

Maandiko yanasema.

Kumbukumbu 22:5 “Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako”.

Mwanamke yeyote kuvaa suruali ni machukizo mbele za Mungu, Suruali sio vazi la kumsitiri mwanamke, hakuna mwanamke yeyote anayevaa suruali na kuonekana kama kajisitiri, badala yake ataonekana kama kajidhalilisha au kajifunua..Na maandiko yanasema wanawake na wavae mavazi ya kujisitiri.

1Timotheo 2:9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani”

Hivyo mwanamke yeyote hapaswi kuvaa suruali, wala vimini wala nguo zozote zinazochora maungo yake.

Na pia Kanzu, halikuwa vazi la kike!, kanzu lilitumika kama vazi la Nje!, kama vile mtu anavyovaa koti!.. Ndio maana utaona hapo wakina shedraka, Meshaki na Abednego walikuwa wamevaa suruali na kanzu kwa nje. Kwahiyo Kanzu halikuwa gauni, Gauni ni vazi la kike lililotengenezwa mahususi kufuatia maumbile ya mwanamke!. Na ndilo wanawake wa kikristo wanapaswa walivae.

Sasa inawezekana ulikuwa hulijui hili kuwa hilo ni vazi la kiume, lakini leo umejua na ndani ya kabati lako kumejaa suruali, nataka nikuambie, usingoje kesho, leo leo zitoe kazichome moto!, wala usimpe mtu!.. zichome na tafuta magauno au sketi ndefu!, usiogope kuonekana mshamba mbele ya ulimwengu!. Ni heri uonekane mshamba lakini unakwenda mbinguni kuliko kuonekana wa kisasa lakini sehemu yako ni katika lile ziwa la moto!.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

USIYAACHE MAVAZI YAKO NA KWENDA UCHI!

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

VAZI LA YESU HALIGAWANYWI.

Rudi nyumbani

Print this post

Mzushi ni nani kibiblia? (Tito 3:10).

Kibiblia mzushi ni mtu anayezusha jambo au mada ambazo lengo lake ni kuleta MIGAWANYIKO!.

Mtu anayezuka katikati ya kanisa na kuzusha mada ambazo anajua kabisa zitaishia kuleta migawanyiko ndani ya kanisa la Kristo, mtu huyo ni Mzushi kibiblia. Kwa lugha ya kiingereza (divisive person).

Na biblia imetoa maelekezo juu ya watu hao, kwamba tuwakatae, (maana yake tusiwape nafasi).

Tito 3:10 “Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae;

11 ukijua ya kuwa mtu kama huyo amepotoka, tena atenda dhambi, maana amejihukumu hatia yeye mwenyewe”.

Mfano wa mada zinazoleta migawanyiko ndani ya kanisa ndio hizo Mtume Paulo alizoziorodhesha katika Tito 3:9..

Tito 3:9 “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana”.

Mashindano ya dini, hayo yanasababisha kiburi na mwishowe migawanyiko katika kanisa kwasababu yanawaharibu wale wanaosikia…

Kwasababu ndani ya kanisa kuna ambao pia bado ni wachanga katika Imani, sasa endapo wakisikia watu wanashindana (kila mmoja anajiona mjuzi) ni rahisi Imani zao kudhoofika na hata kuiacha ile Imani, au kuegemea upande mmoja na kuudharau mwingine, hivyo tayari migawanyiko imeshaingia.

2Timotheo 2:14 “Uwakumbushe mambo hayo, ukiwaonya machoni pa Mungu, wasiwe na mashindano ya maneno, ambayo hayana faida, bali huwaharibu wasikiao”.

1Timotheo 6:4 “..amejivuna; wala hafahamu neno lo lote; bali ana wazimu wa kuwazia habari za maswali, na mashindano ya maneno, ambayo katika hayo hutoka husuda, na ugomvi, na matukano, na shuku mbaya”

Na sisi kama wakristo hatuna budi kujihadhari na Uzushi, vile vile watu ambao ni wazushi katika kanisa, baada ya kuwaonya mara ya kwanza na ya pili, na hawataki kubadilika maandiko yametupa ruhusu ya kujiepusha nao!, maana yake kutowapa nafasi yoyote ya kusema au kuchangia chochote!, wabaki kimya au wazungumze wao wenyewe.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

UFUNUO Mlango wa 2: Sehemu ya pili.

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

KUWA RAFIKI WA DUNIA NI KUWA ADUI WA MUNGU.

Neno “Uchungu wa mauti” lina maana gani kibiblia?

TWAENENDA KWA IMANI NA SI KWA KUONA.

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.

Hizi  ni baadhi ya njia zitakazokusaidia kuuharibu ujana wako kwa wepesi.

  1. Pendelea makundi yasiyojenga.

Wahuni ni ndio wawe marafiki zako, wazinzi ndio wawe kampani yako, walevi ndio wawe watu wa kukupa raha, wanawake wasengenyaji ndio wawe wajoli wako, njia hii ukiitumia vizuri itakufanikisha haraka sana kwenye malengo yako. Huna haja ya kukaa na vijana  wenye hekima, wanaomcha Mungu ya nini?

Ukiliondoa neno hili katika akili yako utafanikiwa..

Zaburi 1:1 Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

2) Usimpende Mungu, wala usilitii Neno lake.

Wakati wale vijana wengine washamba wanajibidiisha kumpendeza Mungu, sawasawa na

Zaburi 119:9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.

Basi wewe, nenda kinyume tu, kataa kulifuata neno la Mungu. Tafuta namna nyingine ya kuisafisha njia yako, Pale unapoambiwa usizini, ona kama huo ni udhaifu, kazini na kila kahaba au mwanamume unayemwona, kwasababu wewe ni mrembo sana,  si ndio? kijana maji ya moto.

3) Fanya chochote unachojisikia kufanya.

Kile roho yako inapenda, huna haja ya kujizuia. Usijizuie wala usiwe na kiasi, Ukijisikia kwenda Disko nenda, ukijisikia kuvuta sigara vuta, ukijisikia utukane, fanya hivyo, ukijisikia kutembea nusu uchi barabarani tembea, ukijisikia kujichubua tumia mikorogo yote, kwasababu andiko linalokusapoti kufanya hivyo;

Mhubiri 9:8 Mavazi yako na yawe meupe sikuzote; wala kichwa chako kisikose marhamu.

9 Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote za maisha yako ya ubatili, ulizopewa chini ya jua; siku zote za ubatili wako, kwa maana huo ni sehemu yako ya maisha; na katika taabu zako ulizozitaabika chini ya jua.

10 Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; KWA KUWA HAKUNA KAZI, WALA SHAURI, WALA MAARIFA, WALA HEKIMA, HUKO KUZIMU UENDAKO WEWE.

4) Endelea kufikiria wewe ndio bora kuliko watu wote duniani, hakuna mwingine kama wewe:

Kati ya watu 7,00,000,000 waliopo duniani leo, zidi kufikiri hakukuwahi kuwa na warembo zaidi yako wewe, na wakajuta, wazuri kupita wewe, wote hao waliokufa walikuwa wadhaifu sana, endelea kudharau maonyo ya waliokutangulia, ona mawazo yao ni ya kizee,

Hata hili andiko usilizingatie,

Mhubiri 12: 12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo;..”

Biblia iendelee kuwa kwako ni kitabu cha wazee,

5) Usipende kujishughulisha na chochote, kwasababu muda sikuzote unao.

Kwasababu kujishughulisha na kazi ya Mungu ni ushamba kwako, basi hata na mambo mengine, hayana haraka sana, si umri bado mdogo, utasoma tu siku moja, sasahivi ponda starehe, utafanya kazi tu siku moja, kesha kwenye muvi, chat instagramu, zururazurura, ruka ruka tu huku na huko, kwasababu muda bado upo, .

Wale wanaolishika hili neno achana nao.

Waefeso 5:15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

Ukiyafanikisha haya kwa bidii ,mafanikio yako yapo mbioni.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Hizi  ni baadhi ya njia zitakazokusaidia kuuharibu ujana wako kwa wepesi.

  1. Pendelea makundi yasiyojenga.

Wahuni ni ndio wawe marafiki zako, wazinzi ndio wawe kampani yako, walevi ndio wawe watu wa kukupa raha, wanawake wasengenyaji ndio wawe wajoli wako, njia hii ukiitumia vizuri itakufanikisha haraka sana kwenye malengo yako. Huna haja ya kukaa na vijana  wenye hekima, wanaomcha Mungu ya nini?

Liondoe kabisa neno hili akilini mwako, utafanikiwa..

Zaburi 1:1 Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

2) Usimpende Mungu, wala usilitii Neno lake.

Wakati wale vijana wengine washamba wanajibidiisha kumpendeza Mungu, sawasawa na

Zaburi 119:9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.

Basi wewe, nenda kinyume tu, kataa kulifuata neno la Mungu. Njia yako utaisafisha vizuri sana, Pale unapoambiwa usizini, ona kama huo ni udhaifu, kadange na kila kahaba au mwanamume unayemwona, kwasababu wewe ni mrembo sana,  si ndio? kijana maji ya moto.

3) Fanya chochote unachojisikia kufanya.

Kile roho yako inapenda, huna haja ya kujizuia. Ukijisikia kwenda Disko nenda, ukijisikia kuvuta sigara vuta, ukijisikia utukane, fanya hivyo, ukijisikia kutembea nusu uchi barabarani tembea, ukijisikia kujichubua tumia mikorogo yote, kwasababu andiko linalokusapoti ni hili;

Mhubiri 9:8 Mavazi yako na yawe meupe sikuzote; wala kichwa chako kisikose marhamu.

9 Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote za maisha yako ya ubatili, ulizopewa chini ya jua; siku zote za ubatili wako, kwa maana huo ni sehemu yako ya maisha; na katika taabu zako ulizozitaabika chini ya jua.

10 Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; KWA KUWA HAKUNA KAZI, WALA SHAURI, WALA MAARIFA, WALA HEKIMA, HUKO KUZIMU UENDAKO WEWE.

4) Endelea kufikiria wewe ndio bora kuliko watu wote duniani, hakuna mwingine kama wewe duniani:

Kati ya watu 7,00,000,000 waliopo duniani leo, zidi kufikiri hakukuwahi kuwa na warembo zaidi yako wewe, wazuri kupita wewe, wote hao waliokufa walikuwa wadhaifu sana, endelea kudharau maonyo ya waliokutangulia, ona mawazo yao ni ya kizee, Kwasababu wewe ni wewe..

Hata hili andiko usilizingatie,

Mhubiri 12: 12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo;..”

Biblia ni kitabu cha wazee,

5) Usipende kujishughulisha na chochote, kwasababu muda sikuzote unao.

Kwasababu kujishughulisha na kazi ya Mungu ni ushamba kwako, basi hata na mambo mengine, hayana haraka sana, si umri bado mdogo, utasoma tu siku moja, sasahivi ponda starehe, utakuja kufanya kazi tu siku moja, kesha kwenye muvi, chat instagramu, zururazurura, ruka ruka tu huku na huko, kwasababu muda bado upo, .

Wale wanaolishika hili neno achana nao.

Waefeso 5:15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

Ukiyafanikisha haya kwa bidii bado,mafanikio yako yapo mbioni.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Je! Ni dhambi kwa kijana aliyeokoka kuvaa suruali za kubana (model), kunyoa mitindo (mfano kiduku), ?

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi nyumbani

Print this post

NI NINI BWANA ANATAZAMIA KILA TUNAPOSHIRIKI MEZA YAKE.

Biblia inamfananisha Bwana wetu Yesu Kristo na Melkizedeki kuhani wa Mungu aliye hai.. Na hiyo yote ni Kutokana na jinsi alivyofanana na Kristo kwa kila tabia aliyokuwa nayo.

Waebrania 7:1-3
[1]Kwa maana Melkizedeki huyo, mfalme wa Salemu, kuhani wa Mungu aliye juu, aliyekutana na Ibrahimu alipokuwa akirudi katika kuwapiga hao wafalme, akambariki;

[2]ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi ya vitu vyote; (tafsiri ya jina lake kwanza ni mfalme wa haki, tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;

[3]hana baba, hana mama, hana wazazi, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake, bali amefananishwa na Mwana wa Mungu); huyo adumu kuhani milele.

Sasa kama wewe ni msomaji wa biblia utajiuliza ni kwanini siku ile Ibrahimu alipotoka kumwokoa ndugu yake Lutu ambaye alikuwa tayari ameshatekwa na maadui, Melkizedeki hakumpa zawadi nyingine zaidi ya MKATE NA DIVAI..

Jiulize ni kwanini iwe mkate na Divai, na ni kwanini uwe ni wakati ule? Na si mwingine..kwanini Melkizedeki asingempa Dhahabu na Lulu kama pongezi, au kwanini asingempa kondoo na mbuzi kama zawadi kwake..badala yake anampa divai na makate, kitu kidogo tu.. kuna nini?

Mwanzo 14:17-20
[17]Abramu aliporudi kutoka kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni Bonde la Mfalme.
[18]Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana.
[19]Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.
[20]Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.

Kama tulivyotangulia kuona kuwa Melkizedeki anafananishwa na Yesu Kristo kwa kila kitu..Habari hiyo inajirudia kwa Kristo alipokuwa anaondoka duniani..

Hakuwaacha hivi hivi tu mitume wake, bali aliwapa uzima wake kwa mfano wa mkate na divai akasema huu ndio mwili wangu na damu yangu imwagikayo kwa ajili ya ondoleo la dhambi, kuleni huu, na nyweni hii kwa ukumbusho wangu na kutangaza mauti yake inayowaokoa watu (Mathayo 26:28)

Sasa tarajio lake kubwa ni kutuona sisi tunashiriki ipasavyo..anatarajia kutuona tupo katika mazingira kama ya Ibrahimu..ambaye yeye hakuona vema kukaa tu hivi hivi angali ndugu yake Lutu amechukuliwa mateka..aliamua kutoka aende kumkomboa, kutoka mikononi mwa wale wafalme wa mbali.

Na ndipo Mungu alipouona moyo huo wa Ibrahimu akaona anastahili kushiriki mwili na damu ya Yesu Kristo.

Lakini je! Tujiulize na sisi tangu tulipoanza kwenda makanisani, na kushiriki meza ya Bwana mara zote hizo..Je! Ni ushuhuda gani Kristo anauona ndani yetu aone kwamba tumestahili kuishiriki meza yake.

Kila tendo la rohoni lina kanuni yake.. Ili ule uzima ambao Bwana Yesu alisema utaingia ndani yetu pale tu tunaposhiriki meza yake, uingie, ni lazima tujue kanuni zake vinginevyo tutakuwa tunafanya kazi bure tu.

Yohana 6:53-54
[53]Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
[54]Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.

Hivyo, tukumbuke hilo pia tukaribiapo nyumbani kwa Bwana anatazamia tuwaangazie na wengine nuru yetu ya wokovu tuliyoipokea..Ndipo tustahili vema kushiriki meza yake. Lakini kama tutakuwa ni watu wa kuingia kanisani na kutoka, baada ya hapo hatuna habari tena na Mungu. Ni heri tuache tu.

Bwana atasaidie katika hilo.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.

Je tunapaswa tushiriki Meza ya Bwana mara ngapi?

Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu?

Rudi nyumbani

Print this post

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe,

Leo tutajifunza jinsi ya kuuvuta uwepo wa Roho Mtakatifu karibu nasi. Yapo mambo makuu matatu yanayovuta uwepo wa Mungu karibu nasi.

  1. MAOMBI

Hili ni jambo la kwanza linalohifadhi uwepo wa Roho Mtakatifu ndani yetu. Tunapoingia kwenye maombi Roho Mtakatifu anazidi kusogea karibu nasi,  anasogea kuomba pamoja na sisi (Warumi 8:26) na vile vile anasogea kuzungumza na sisi.

Kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka kipindi, Bwana Yesu anabatizwa katika mto Yordani na Yohana, utaona Roho Mtakatifu alishuka juu ya Bwana kwa mithili ya HUA (Yaani Njiwa).

Lakini katika tukio hilo kuna siri moja imejificha pale, ambayo ukisoma kwa haraka haraka unaweza usiigundue. Na siri yenyewe ni MAOMBI!. Utaona baada ya Bwana kutoka majini, na kusogea pembeni utaona alianza KUOMBA!, na wakati akiwa katika maombi, ndipo Mbingu zilipofunguka na Roho Mtakatifu kushuka juu yake.

Luka 3:21 “Ikawa, watu wote walipokwisha kubatizwa, na Yesu naye amebatizwa, NAYE ANAOMBA, mbingu zilifunuka;

22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili, kama hua; sauti ikatoka mbinguni, Wewe ndiwe Mwanangu, mpendwa wangu; nimependezwa nawe”.

Umeona? Ni wakati alipokuwa anaomba ndipo Roho Mtakatifu alishuka juu yake, na sio wakati anabatizwa tu peke yake.

Vile vile utaona kipindi cha Pentekoste, Mitume na wanafunzi wengine wapolikuwa wamekusanyika mahali Pamoja katika ghorofa wakidumu katika kusali, na kule kule ndipo Roho Mtakatifu akashuka juu yao na kuwajaza nguvu (Soma Matendo 1:13-14, Matendo 2:1-2).

Na sehemu nyingine nyingi, utona kuwa Roho Mtakatifu alishuka wakati watu wakiwa kwenye maombi..

Matendo 4:31 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri”.

Vile vile na sisi tukitaka kuuvuta uwepo wa Roho Mtakatifu hata tumuhisi ndani yetu, au katikati yetu basi hatupaswi kuyakwepa MAOMBI, kadhalika tukitaka tumsikie anataka nini kwetu au anasema nini, njia pekee ni Maombi!

Sasa inawezekana hujui namna ya kuomba, ni rahisi sana.. Kama utatamani kupata mwongozo wa namna ya kuomba basi tutumie ujumbe inbox, ili tuweze kukutumia somo linalohusu “Njia bora ya kuomba”

  1. KUSOMA NENO.

Hii ni njia nyingine ya Muhimu ya kuuvuta uwepo wa Roho Mtakatifu karibu nasi. Kazi mojawapo ya Roho Mtakatifu ni kutuongoza na kututia katika Kweli yote (Yohana 6:13-14), na Kweli ni Neno la Mungu (Yohana 17:17). Hivyo tunapotenga muda wa kuishika biblia na kuisoma kwa lengo la kujifunza, basi Roho Mtakatifu anasogea karibu nasi sana. Ni lazima atusogelee kwasababu ndio kazi yake yeye kutufundisha na kutufunulia maandiko.

Tunaweza kujifunza kwa yule Mkushi aliyekuwa anarudi nchini kwao, ambapo njiani alijikuta anafungua kitabu cha Isaya 53, kilichokuwa kinazungumzia Habari za Masihi, Yesu lakini hakuwa na ufunuo wowote juu ya hilo, Ndipo Roho Mtakatifu akaingia kazini kujisogeza karibu naye ili amtie katika kweli yote!!..

Roho Mtakatifu akaanzaa kuzungumza kwanza na Filipo siku kadhaa kabla hata ya Mkushi huyo kufikiria kusoma hilo andiko, Roho Mtakatifu akaanza kutengeneza njia ya kumkaribia Mkushi huyo, akamwambie Filipo ashuke njia ya jangwa, na alipokutana na yule Mkushi yupo matatani haelewi maandiko, ndipo Roho Mtakatifu akaanza kuzungumza kupitia kinywa cha Filipo. Na hatimaye kumfunua macho yake na kumtia katika kweli yote.

Matendo 8:29 “Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.

30 Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma?

31 Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.

32 Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.

33 Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.

34 Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?

35 Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.

36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?

37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]

38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.

39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi”.

Roho wa Yesu ni yule yule na tabia zake ni zile zile, tukitaka atukaribie, tumsikie, au tumwone basi ni lazima pia tuwe wasomaji wa Neno.

  1. KUHUBIRI/KUSHUHUDIA.

Agizo kuu ambalo Bwana alilotupatia ni kupeleka injili ulimwenguni kote.

Marko 16:15 “Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.

16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Kwanini kuhubiri/kumshuhudia Yesu kunamsogeza Roho Mtakatifu karibu nasi?. Kwasababu kila tunapofika mahali na kushuhudia tunafanyika vyombo vya Roho Mtakatifu, Hivyo Roho Mtakatifu hana budi kila wakati kuwa nasi kwasababu wakati wote tunatumika kama vyombo vyake, hakuna wakati uwepo wake utakaa mbali na sisi!..

Mathayo 10:18 “nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.

19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

20 KWA KUWA SI NINYI MSEMAO, BALI NI ROHO WA BABA YENU ASEMAYE NDANI YENU”.

Kwahiyo kama wakati wote tutakuwa katika hayo mazingira ya kumshuhudia Kristo, maana yake wakati wote, kinywa kitakachokuwa kinasema ndani yetu ni kinywa cha Roho Mtakatifu, hivyo uwepo wake utakuwa nasi muda wote!, lakini kama hatutakuwa katika mazingira yoyote ya kumshuhudia Kristo ni ngumu Roho Mtakatifu kuwa na sisi, kuzungumza kupitia vinywa vyetu, au kusema nasi!.

Je! Na wewe leo Umempokea Yesu?

Na kama ndio je! Wewe ni MWOMBAJI?..wewe ni MSOMAJI WA NENO?…wewe ni MSHUHUDIAJI?. Kama hufanyi hayo basi, uwepo wa Roho Mtakatifu utawezaje kuusikia?, vile vile sauti yake utaweza kuisikia?!.

Leo shetani kawafanya wakristo wengi wasiwe Waombaji?..utakuta mkristo mara ya mwisho kutenga angalau lisaa limoja kuomba yeye binafsi hata hakumbuki!, (yeye atakuwa anapenda kusikiliza na kusoma mahubiri tu!, na kuombewa lakini kuomba mwenyewe hataki/hawezi), Utakuta mkristo mara ya mwisho kusoma Neno binafsi ni muda mrefu sana, leo hata ukimuuliza mkristo biblia ina vitabu vingapi hajui, ukimpa biblia afungue kitabu cha Yeremia atapepesuka nusu saa hajui kilipo mpaka akaangalie kwenye index, hiyo ni kuonesha ni jinsi gani biblia ni kitabu-baki tu kwake!, na si kila kitu kwake!.

Leo hii ukimwuliza mkristo mara ya mwisho kuzungumza na mtu mwingine Habari za wokovu, au kumshuhudia Kristo, hana hiyo kumbukumbu!, lakini shuhuda za mipira, na za Maisha ya watu wengine zimejaa katika kinywa chake!..

Kumbuka Bwana anatamani yeye kuwa karibu na sisi kuliko sisi tunavyotamani yeye awe karibu nasi, hivyo ni wajibu wetu kuongeza bidii katika kuomba, kusoma Neno, kushuhudia Pamoja na kuishi Maisha matakatifu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni kiumbe gani kinachosujudiwa hapo katika Warumi 1:25?

Tusome,

Warumi 1:25 “Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina”.

Kiumbe ni kitu chochote chenye uhai kilichoumbwa na Mungu. Katika dunia viumbe hai ni Wanadamu, Wanyama na mimea.

Kwahiyo maandiko hapo yaliposema kuwa “wameibadili kweli ya Mungu kuwa uongo na kukisujudia kiumbe inamaanisha ni kiumbe chochote kile, na si kimoja maalum!..kinaweza kuwa mtu au mti, au mnyama Fulani. Maeneo ya Korea kaskazini watu wanaabudu MTU kama Mungu, maeneo ya India watu wanaabudu Nyoka na Ng’ombe, Maeneo ya Marekani ya kusini na watu wanaabudu Chui na maeneo ya Afrika watu wanaabudu Miti n.k. Hawa wote wanaabudu viumbe vilivyoumbwa na Mungu, jambo ambalo ni machukizo makubwa mbele za Bwana.

Na mbaya zaidi wengi wanaofanya hivyo maandiko yanasema wanafanya hivyo kwa kujua kabisa! Kwamba vitu hivyo si Mungu, na dhamiri zao zikiwashuhudia, lakini hawataki kubadilika.

Warumi 1:20 “Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru;

21 kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.

22 Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika;

23 wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo.

24 Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.

25 Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina”.

Je na wewe unaabudu watu? Kumfanya mtu tegemeo lako asilimia mia hakuna tofauti na kumwabudu!, kumwogopa mtu na kumfanya kinga yako kiasi kwamba hata anaweza kukuamulia siku ya kuabudu na ukatii huko hakuna tofauti na kumwabudu (Unakiabudu kiumbe), kumtumikia mtu mpaka unakosa muda wa kwenda kumfanyia Mungu wako ibada angalau hata mara moja kwa wiki, huyo mtu ni mungu wako.

Yeremia 17:5 Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.

6 Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.

7 Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.

 8 Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda”.

Je Bwana ni tegemeo lako au viumbe?

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

Rudi nyumbani

Print this post

Vitimvi ni nini kibiblia?

Vitimvi ni mipango inayopangwa kwa siri na  kikundi cha watu ili kufanya uasi juu ya mtu au watu.

Katika biblia Mitume wa Bwana Yesu walifanyiwa vitimvi vingi sana vya kuwaangamiza, mfano wa hao utaona ni Mtume Paulo..

Matendo 20:2 “Naye akiisha kupita pande zile na kuwafariji kwa maneno mengi, akafika Uyunani.

3 Alipokwisha kukaa huko miezi mitatu, na Wayahudi KUMFANYIA VITIMVI, alipotaka kwenda Shamu kwa njia ya bahari; basi akaazimu kurejea kwa njia ya Makedonia”.

Na pia utaona kuna wakati Paulo alipokuwa amefungwa kule Yerusalemu, baadhi ya wayahudi kama 40 hivi walijifunga kiapo kwamba hawatakula wala kunywa hata watakapomwua Paulo (Matendo 23:12). Sasa mipango hiyo ndiyo inayoitwa vitimvi!

Matendo 23:27 “Mtu huyu alikamatwa na Wayahudi, wakawa karibu kumwua, ndipo nikaenda pamoja na kikosi cha askari nikamwokoa, nilipopata habari ya kuwa yeye ni Mrumi.

28 Nami nikitaka kulijua lile neno walilomshitakia, nikamtelemsha nikamweka mbele ya baraza;

29 nikaona kwamba ameshitakiwa kwa ajili ya maswali ya sheria yao, wala hakushitakiwa neno lo lote la kustahili kuuawa wala kufungwa.

30 Hata nilipopewa habari kwamba PATAKUWA NA VITIMVI JUU YA MTU HUYU, mara nikampeleka kwako, nikawaagiza na wale waliomshitaki, wanene habari zake mbele yako. Wasalamu”.

Na kama wakristo wa kanisa la kwanza walipitia Vitimvi, kutokana na Imani yao, kadhalika na wakristo wa kweli wa siku hizi za mwisho ni lazima wapitie vitimvi kama wa kanisa la kwanza, kwasababu Roho ni yule yule, Bwana na yule yule hajabadilika.

Ni lazima upitie maudhi kwaajili ya Imani yako, ni lazima upitie kuhuzunishwa, ni lazima upangiwe visa, ni lazima wakati mwingine utenge au uchukiwe au hata kupigwa na kufungwa!. Hizo ndizo chapa za Yesu ambazo tunazopaswa kuzichukua..

Wagalatia 6:17 “Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Dini ni nini, na Imani ya kweli ni ipi?

YEYE ALIYEUWASHA HUO MOTO LAZIMA ATALIPA.

MWISHO WA MAVUNO, NI MWISHO WA DUNIA.

Kuhusuru ni nini kibiblia? (Luka 19:43)

Neno “Uchungu wa mauti” lina maana gani kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

FUNDISHO KUU LA NEEMA YA MUNGU KWETU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia, chakula cha uzima wa roho zetu.

Maandiko yanasema kuwa tunaokolewa kwa Neema na si kwa matendo,

Waefeso 2:8 “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu;

9 wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu”.

Maana yake ni kwamba hakuna tunachoweza kukifanya sisi kwa matendo yetu, kikatufanya tuwe na haki ya kuokolewa, haijalishi tutajiona tunafanya mema kiasi gani, bado tuna mabaya mengi tunayoyafanya pasipo sisi kujijua. Mbwa anaweza kujiona yupo sawa katika njia zake zote, lakini wewe mwanadamu bado utamwona anazo kasoro nyingi. Na kwa Mungu wetu ni hivyo hivyo, kamwe hatuwezi kujisifu kwa matendo yetu kwake, haijalishi tutajiona ni wasafi kiasi gani, kwake yeye bado tutakuwa na kasoro nyingi tu!.

Lakini katika kasoro zetu hizo bado anatupa wokovu. Sasa kitendo hicho cha kupewa Wokovu bure! Pasipo matendo yetu ndicho kinachoitwa NEEMA!..

Lakini sasa hii NEEMA, ambayo inatupa wokovu bure pasipo matendo, inayo DARASA. Maana yake inafundisha!.. Kuna kitu inataka kutoka kwetu!. Ambapo ikikikosa hicho kitu kutoka kwetu basi na yenyewe inatukataa sisi.

Sasa kitu hicho ni kipi??

Tusome,

Tito 2:11 “Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa;

12 NAYO YATUFUNDISHA KUKATAA UBAYA NA TAMAA ZA KIDUNIA; TUPATE KUISHI KWA KIASI, NA HAKI, NA UTAUWA, KATIKA ULIMWENGU HUU WA SASA;

13 tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu”

Umeona hapo mstari wa 12?. Kitu gani neema ya Mungu inatufundisha au inachotaka kutoka kwetu?.. inatutaka sisi KUUKATAA UBAYA NA TAMAA ZA KIDUNIA!!!. Hicho tu!.. Inatutaka sisi tuwe wanafunzi bora juu ya hilo!. Tukiweza kufanikiwa kujifunza jambo hilo basi Neema ya Mungu itakaa na sisi milele!..

Haitatazama kasoro nyingine ndogo ndogo tulizo nazo. Mbwa anayekubali mafunzo ya Bwana wake ya kutotoka nje kuzurura na anapokubali kuwa na nidhamu, Bwana wake atampenda, kasoro nyingine ndogo ndogo alizonazo atazifumbia macho!, lakini Mbwa anayekataa mafunzo machache ya Bwana wake, hataki kufundishika, ni mzururaji huko na kule, Bwana wake atamchukia na kumfukuza!.

Na neema ya Mungu ni hivyo hivyo, tukitii FUNZO lake hilo la KUUKATAA ULIMWENGU NA UBAYA WOTE!, Zile kasoro nyingine ndogo ndogo tulizonazo neema ya Mungu haitaziona, tutahesabika tu kuwa tumestahili mbele zake.

Wengi leo hawapendi kuishi Maisha ya kuukataa ulimwengu.. huku wakiamini au kuaminishwa kuwa “tunaokolewa kwa neema na si kwa matendo”..pasipo kujua NEEMA YA MUNGU, nayo kuna kitu inataka kutoka kwetu!

Ukitaka Neema ya Mungu ikae nawe ni lazima ukatae fashion za kiulimwengu.

Ukitaka Neema ya Mungu ikae nawe ni lazima ukatae anasa za kiulimwengu

Ukitaka Neema ya Mungu ikae nawe ni lazima ukatae kujichubua, kuvaa wigi, kuweka rasta, hereni, kupaka wanja, lipstick, kuvaa suruali kwa wanawake, kuvaa vimini na nguo za kubana.

Ukitaka Neema ya Mungu ikae nawe ni lazima ukatae ulevi, kusikiliza miziki ya kidunia, kujichua, kuzini kutukana, kuiba na mambo yote yanayofanana na hayo.

Usidanganyike kuwa NEEMA YA MUNGU, inakubaliana na UDUNIA!.. Neema ya Mungu na udunia ni vitu viwili tofauti!..

Je! Umeukataa ubaya?..umeukataa Udunia?

Kama bado, basi fahamu kuwa Neema ya Mungu inakufundisha hivyo leo. Tubu dhambi leo na mpokee Yesu, na ukabatizwe katika ubatizo sahihi kwa maji tele na kwa jina la Yesu Kristo na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kweli yote, na kukusaidia kulitii agizo hilo la Neema ya Mungu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

USIWE MSIKIAJI TU! BALI MTENDAJI.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Je! Kuna dhambi kubwa na ndogo, na kama hakuna je! Mtu aliyeua na aliyetukana je watapata adhabu sawa?

Amri zilizo ndogo alizozizungumzia Yesu ni zipi?

Neema ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post