JINSI YA KUUHARIBU UJANA WAKO.

by Admin | 29 January 2022 08:46 pm01

Hizi  ni baadhi ya njia zitakazokusaidia kuuharibu ujana wako kwa wepesi.

  1. Pendelea makundi yasiyojenga.

Wahuni ni ndio wawe marafiki zako, wazinzi ndio wawe kampani yako, walevi ndio wawe watu wa kukupa raha, wanawake wasengenyaji ndio wawe wajoli wako, njia hii ukiitumia vizuri itakufanikisha haraka sana kwenye malengo yako. Huna haja ya kukaa na vijana  wenye hekima, wanaomcha Mungu ya nini?

Ukiliondoa neno hili katika akili yako utafanikiwa..

Zaburi 1:1 Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

2) Usimpende Mungu, wala usilitii Neno lake.

Wakati wale vijana wengine washamba wanajibidiisha kumpendeza Mungu, sawasawa na

Zaburi 119:9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.

Basi wewe, nenda kinyume tu, kataa kulifuata neno la Mungu. Tafuta namna nyingine ya kuisafisha njia yako, Pale unapoambiwa usizini, ona kama huo ni udhaifu, kazini na kila kahaba au mwanamume unayemwona, kwasababu wewe ni mrembo sana,  si ndio? kijana maji ya moto.

3) Fanya chochote unachojisikia kufanya.

Kile roho yako inapenda, huna haja ya kujizuia. Usijizuie wala usiwe na kiasi, Ukijisikia kwenda Disko nenda, ukijisikia kuvuta sigara vuta, ukijisikia utukane, fanya hivyo, ukijisikia kutembea nusu uchi barabarani tembea, ukijisikia kujichubua tumia mikorogo yote, kwasababu andiko linalokusapoti kufanya hivyo;

Mhubiri 9:8 Mavazi yako na yawe meupe sikuzote; wala kichwa chako kisikose marhamu.

9 Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote za maisha yako ya ubatili, ulizopewa chini ya jua; siku zote za ubatili wako, kwa maana huo ni sehemu yako ya maisha; na katika taabu zako ulizozitaabika chini ya jua.

10 Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; KWA KUWA HAKUNA KAZI, WALA SHAURI, WALA MAARIFA, WALA HEKIMA, HUKO KUZIMU UENDAKO WEWE.

4) Endelea kufikiria wewe ndio bora kuliko watu wote duniani, hakuna mwingine kama wewe:

Kati ya watu 7,00,000,000 waliopo duniani leo, zidi kufikiri hakukuwahi kuwa na warembo zaidi yako wewe, na wakajuta, wazuri kupita wewe, wote hao waliokufa walikuwa wadhaifu sana, endelea kudharau maonyo ya waliokutangulia, ona mawazo yao ni ya kizee,

Hata hili andiko usilizingatie,

Mhubiri 12: 12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo;..”

Biblia iendelee kuwa kwako ni kitabu cha wazee,

5) Usipende kujishughulisha na chochote, kwasababu muda sikuzote unao.

Kwasababu kujishughulisha na kazi ya Mungu ni ushamba kwako, basi hata na mambo mengine, hayana haraka sana, si umri bado mdogo, utasoma tu siku moja, sasahivi ponda starehe, utafanya kazi tu siku moja, kesha kwenye muvi, chat instagramu, zururazurura, ruka ruka tu huku na huko, kwasababu muda bado upo, .

Wale wanaolishika hili neno achana nao.

Waefeso 5:15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

Ukiyafanikisha haya kwa bidii ,mafanikio yako yapo mbioni.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Hizi  ni baadhi ya njia zitakazokusaidia kuuharibu ujana wako kwa wepesi.

  1. Pendelea makundi yasiyojenga.

Wahuni ni ndio wawe marafiki zako, wazinzi ndio wawe kampani yako, walevi ndio wawe watu wa kukupa raha, wanawake wasengenyaji ndio wawe wajoli wako, njia hii ukiitumia vizuri itakufanikisha haraka sana kwenye malengo yako. Huna haja ya kukaa na vijana  wenye hekima, wanaomcha Mungu ya nini?

Liondoe kabisa neno hili akilini mwako, utafanikiwa..

Zaburi 1:1 Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.

2) Usimpende Mungu, wala usilitii Neno lake.

Wakati wale vijana wengine washamba wanajibidiisha kumpendeza Mungu, sawasawa na

Zaburi 119:9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.

Basi wewe, nenda kinyume tu, kataa kulifuata neno la Mungu. Njia yako utaisafisha vizuri sana, Pale unapoambiwa usizini, ona kama huo ni udhaifu, kadange na kila kahaba au mwanamume unayemwona, kwasababu wewe ni mrembo sana,  si ndio? kijana maji ya moto.

3) Fanya chochote unachojisikia kufanya.

Kile roho yako inapenda, huna haja ya kujizuia. Ukijisikia kwenda Disko nenda, ukijisikia kuvuta sigara vuta, ukijisikia utukane, fanya hivyo, ukijisikia kutembea nusu uchi barabarani tembea, ukijisikia kujichubua tumia mikorogo yote, kwasababu andiko linalokusapoti ni hili;

Mhubiri 9:8 Mavazi yako na yawe meupe sikuzote; wala kichwa chako kisikose marhamu.

9 Uishi kwa furaha pamoja na mke umpendaye, siku zote za maisha yako ya ubatili, ulizopewa chini ya jua; siku zote za ubatili wako, kwa maana huo ni sehemu yako ya maisha; na katika taabu zako ulizozitaabika chini ya jua.

10 Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; KWA KUWA HAKUNA KAZI, WALA SHAURI, WALA MAARIFA, WALA HEKIMA, HUKO KUZIMU UENDAKO WEWE.

4) Endelea kufikiria wewe ndio bora kuliko watu wote duniani, hakuna mwingine kama wewe duniani:

Kati ya watu 7,00,000,000 waliopo duniani leo, zidi kufikiri hakukuwahi kuwa na warembo zaidi yako wewe, wazuri kupita wewe, wote hao waliokufa walikuwa wadhaifu sana, endelea kudharau maonyo ya waliokutangulia, ona mawazo yao ni ya kizee, Kwasababu wewe ni wewe..

Hata hili andiko usilizingatie,

Mhubiri 12: 12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo;..”

Biblia ni kitabu cha wazee,

5) Usipende kujishughulisha na chochote, kwasababu muda sikuzote unao.

Kwasababu kujishughulisha na kazi ya Mungu ni ushamba kwako, basi hata na mambo mengine, hayana haraka sana, si umri bado mdogo, utasoma tu siku moja, sasahivi ponda starehe, utakuja kufanya kazi tu siku moja, kesha kwenye muvi, chat instagramu, zururazurura, ruka ruka tu huku na huko, kwasababu muda bado upo, .

Wale wanaolishika hili neno achana nao.

Waefeso 5:15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

Ukiyafanikisha haya kwa bidii bado,mafanikio yako yapo mbioni.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

Je! Ni dhambi kwa kijana aliyeokoka kuvaa suruali za kubana (model), kunyoa mitindo (mfano kiduku), ?

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/01/29/jinsi-ya-kuuharibu-ujana-wako/