Category Archive Ubatizo

TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU

Jina la Bwana na Mwokozi Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.

Je kuna utofauti wowote ya Ubatizo wa Yohana na ule wa Bwana Yesu?,

Jibu ni kwamba hakuna utofauti wowote, ubatizo ni ule ule mmoja  wa toba, lakini kinachoutofautisha ule wa Yohana na ule wa Bwana Yesu ni “jina” Lakini ubatizo ni ule ule.

Kumbuka kabla ya Bwana Yesu kuja watu walikuwa wanasali, walikuwa wanafanya maombezi, na vitu vingine lakini walikuwa hawalitumii jina lolote, kwasababu hawakupewa maagizo hayo na Mungu. Hali kadhalika na Yohana alipokuja na ufunuo mpya wa ubatizo, alibatiza pasipo kuhusisha jina lolote. Maana yake baada ya watu kutubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zao, ishara ya mwisho ya wao kutakasika ilikuwa ni “kuzamishwa katika maji, na kuibuka juu” pasipo kutaja jina lolote.

Lakini Bwana Yesu alipokuja, mambo yalibadilika.. Kila kitu cha KIMungu ni lazima kifanyike kwa jina lake yeye..

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, KWA NENO AU KWA TENDO, FANYENI YOTE KATIKA JINA LA BWANA YESU, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Kutokana na maagizo hayo, Mitume na wanafunzi wengine wa Bwana Yesu, walianza kulitumia jina la Yesu katika mambo yote yote ya kiMungu watakayoyafanya kwa NENO na kwa MATENDO.

Mfano wa MANENO ambayo walianza kutamka kwa jina la Yesu ni SALA zote NA MAOMBI  NA MAHUBIRI …ndio maana utaona walipokwenda kutoa pepo, na kuombea watu wenye magonjwa na madhaifu mbali mbali walitumia jina la Yesu,..

Luka 16:17 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; KWA JINA LANGU watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya”.

Vile vile utaona walipoenda kuhubiri na kufundisha, walifundisha kwa jina la Yesu..

Luka 24:46 “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa KWA JINA LAKE habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu”.

Soma pia Matendo 4:18

Mfano wa matendo hayo yalikuwa ni ubatizo!..

Hayo yalikuwa ni Maneno, sasa utauliza vipi kuhusu Matendo..je! kuna matendo yoyote ambayo yalikuwa yanafanywa kwa jina la Yesu?.. Jibu ni ndio!

Kumbuka ubatizo si yohana peke yake aliyekuwa anafanya, bali na wanafunzi wake pia walikuwa wanawabatiza watu..kwasababu Yohana aliwafundisha hivyo, na zaidi sana utaona pia Adrea kabla ya kuwa Mwanafunzi wa Bwana Yesu alikuwa ni mwanafunzi wa Yohana. Hivyo alikuwa anaujua ubatizo vizuri na alikuwa akibatiza, kabla hata ya Bwana Yesu.

Lakini baada ya Bwana YESU kuja, na kufahamu kuwa mambo yote, ni lazima yafanyike kwa jina la Bwana Yesu, ikiwemo ubatizo pia, ndipo wote wakaacha kubatiza kama Yohana, kwa kuzamisha bila kutaja jina lolote, na wakaanza kubatiza kwa jina la Yesu.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Umeona?.. kumbe hata ubatizo, ni lazima uwe kwa jina la Bwana Yesu ili ulete matokeo.. Ndio maana Mtume Paulo, alipokutana na wale watu kipindi wapo Efeso, aliwaambia wakabatizwe upya kwa jina la Yesu, ijapokuwa tayari walikuwa wameshabatizwa kwa ubatizo wa Yohana.

Matendo 19:1 “Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko;

2 akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia.

3 AKAWAULIZA, BASI MLIBATIZWA KWA UBATIZO GANI? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana.

4 Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, Yesu

5 WALIPOSIKIA HAYA WAKABATIZWA KWA JINA LA BWANA YESU.

6 Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.”

Ndugu unayesoma ujumbe huu, fahamu kuwa kama hutabatizwa katika ubatizo sahihi, baada ya kuujua ukweli, utakuwa umemkataa Mungu moja kwa moja!!!.. na kuna madhara makubwa sana ya kutokubatizwa kwa jina la Bwana Yesu, (siku zote usilisahau hilo kichwani mwako).

Ikiwa bado hujampokea Yesu, kumbuka hizi ni siku za Mwisho, Kristo anarudi hivyo ni vizuri ukayatengeneza maisha yako kabla nyakati za hatari hazijafika.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

UMUHIMU WA KUBATIZWA.

Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue?  Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

Rudi nyumbani

Print this post

“Lakini nina ubatizo unipasao kubatiziwa” (Luka 12:50) Ni ubatizo gani huo?.

Jibu: Tusome,

Luka 12:49 “Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi?

50 LAKINI NINA UBATIZO UNIPASAO KUBATIZIWA, nami nina dhiki kama nini hata utimizwe!”

Ubatizo Bwana Yesu aliokuwa anaumaanisha hapo, ni kile kitendo cha  KUZIKWA na KUFUFUKA kwake. Kwasababu maana yenyewe ya Neno ubatizo ni KUZIKWA.

Hivyo kwa kupitia mauti ya Bwana Yesu, Deni la dhambi zetu limefutwa/LIMEZIKWA. Na kama vile alivyofufuka katika upya na utukufu, pasipo mzigo wa dhambi zetu, vile vile na sisi tunapomwamini yeye na kubatizwa kwa njia ya maji, kama ishara ya kuakisi ubatizo wake yeye (wa kuzikwa na kufufuka kwake) tunakuwa tunakufa kwa habari ya dhambi na tunafufuka katika upya.

Wakolosai 2:12 “MKAZIKWA PAMOJA NAYE KATIKA UBATIZO; NA KATIKA HUO MKAFUFULIWA PAMOJA NAYE, KWA KUZIAMINI NGUVU ZA MUNGU ALIYEMFUFUA KATIKA WAFU.

13 Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote”.

Kwahiyo ubatizo wa Maji ni kivuli cha Ubatizo wa Bwana Yesu, (wa kuzikwa kwake na kufufuka kwake). Kama vile Bwana alivyozikwa katika makosa yetu na kufufuka pasipo makosa yetu, na sisi tunapozama katika maji na kuibuka juu… katika ulimwengu wa roho, tunakuwa tumekufa katika utu wa kale na tumefufuka katika utu upya. (Dhambi zetu zinakuwa zimeondolewa, Matendo 2:38).

Tunakuwa tunatembea katika utukufu ule ule ambao Bwana Yesu alitembea nao baada ya kufufuka kwake.. Na katika ulimwengu wa roho tunakuwa tumeketi naye..

Waefeso 2:5 “hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.

6 AKATUFUFUA PAMOJA NAYE, AKATUKETISHA PAMOJA NAYE KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, katika Kristo Yesu”

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Ubatizo Bwana alioumaanisha katika Luka 12:50 ni KUZIKWA na KUFUFUKA KWAKE. Na kabla ya huo kutimizwa ilipasa Bwana apitie mateso mengi (dhiki), kwa kukataliawa na kuteswa Kalvari, ndio maana anamalizia kwa kusema “nami nina dhiki kama nini hata utimizwe!”

Luka 9:22 “akisema, Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi, na kukataliwa na wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa NA SIKU YA TATU KUFUFUKA”.

Kufuatia maandiko hayo utaona ni jinsi gani ubatizo wa maji ulivyokuwa wa muhimu, na wala si wa kuupuuzia hata kidogo, Na maandiko yanasema mtu asipozaliwa kwa Maji na kwa Roho, (Yohana 3:5) hawezi kuurithi uzima wa milele. (na Kuzaliwa kwa maji ni ubatizo wa Maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo).

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

Rudi nyumbani

Print this post

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Je unajua ubatizo unaua na vile vile unaokoa?.

Ipo siri kubwa sana katika ubatizo ambayo laiti watu wengi wangeijua wangeutafuta kwa bidii zote.

Hebu tusome mistari ifuatayo,

1 Petro 3:20 “watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, WALIOKOKA KWA MAJI.

21 MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO, UNAOWAOKOA NINYI PIA SIKU HIZI; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo”.

Hapo kuna vitu 3 vya kuzingatia katika mistari hiyo..na tutatazama kipengele kimoja baada ya kingine.

  1. WATU WANANE WALIOKOKA KWA MAJI.

Hapa tunachoweza kuona ni kwamba..“kumbe maji ni njia ya wokovu?”. Nuhu pamoja na mkewe na wanawe watatu na wake zao, jumla nafsi 8, waliokoka kwa maji!!!!! 

Wakati wengine wasioamini wanaangamia kwa maji, Nuhu aliyeamini, maji hayo hayo yanamwokoa na ghadhabu ya Mungu. Hili ni jambo la kwanza la kuzingatia…hebu tulitazame jambo la pili.

2. MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO, UNAOWAOKOA NINYI PIA SIKU HIZI.

Kumbe kama Nuhu alivyookoka kwa Maji zamani hizo, na sisi siku hizi hatuna budi kuokoka kwa kupitia maji hayo hayo? Yaani kwa Kubatizwa. Si ajabu Bwana Yesu alisema katika Marko 16:16 kuwa..“Aaminiye na kubatizwa ataokoka”..na si “atakayeamini tu peke yake”

Huu ni ufunuo mkubwa sana ambao Mtume Petro alifunuliwa na Roho Mtakatifu..

Kumbe wakati sisi tunasoma habari za gharika ya Nuhu kama gazeti, kumbe nyuma yake kuna ufunuo wa ubatizo..

Si ajabu na Yohana Mbatizaji pengine naye alitolea ufunuo wa ubatizo humu humu.
Unapomwamini Yesu (Ni sawa na umeingia ndani ya safina kama Nuhu)..unapobatizwa kwa kuzamishwa katika maji mengi na kuibuka juu (Ni sawa na umeingia kwenye gharika ukiwa ndani ya safina na umetoka salama).

Na kama vile baada ya gharika Mambo yote yakawa mapya kwa Nuhu, akaingia katika ulimwengu mpya na kuanza maisha mapya, yale ya kwanza yenye shida na dhuluma na maasi yamepita. (Kwa ufupi uchafu wote wa kwanza ukaondoka).

Vivyo hiyo na sisi tunapobatizwa katika roho tunaondoa uchafu wote unaozunguka maisha yetu ya kiroho… Yale maisha ya kale yanazikwa, zile dhambi za kale zinaisha nguvu, kile kiburi cha kale kinafifia n.k
Faida hii kuu inatupeleka katika kipengele cha tatu na cha mwisho.

 3. SIYO KUWEKEA MBALI UCHAFU WA MWILI, BALI JIBU LA DHAMIRI SAFI MBELE ZA MUNGU.

Kumbe lengo la ubatizo sio kuondoa uchafu wa mwilini kama JASHO au VUMBI..bali ni kuondoa uchafu wa rohoni ambao huo ndio jibu la Dhamiri zetu safi mbele za Mungu.

Swali ni Je! umebatizwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu kulingana na Matendo 2:38?.

Kama bado unasubiri nini na tayari umeshajua faida zote hizi?..Haraka sana katafute ubatizo sahihi, kwa gharama zozote baada ya wewe kumwamini Bwana Yesu na kutubu dhambi zako.

Kama unapata ugumu kupata sehemu ya ubatizo, basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba zilizopo chini ya somo, tutakusaidia, kukuelekeza mahali karibu na ulipo.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

Je! Unaweza kubatizwa na usipokee Roho Mtakatifu?. Na Je! Unaweza kupokea Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono?

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Rudi nyumbani

Print this post

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

Kabla ya kufahamu ubatizo ni nini…Hebu jiulize mtu katokea na akakuuliza “kuzamisha maana yake ni nini?”..utamjibuje?…Bila shaka utamwelezea kwa kina kwamba ni kitendo cha kukitosa kitu chote kwenye kimiminika Fulani au kitu Fulani, pasipo kubakisha sehemu ambayo ipo wazi. Meli iliyopata ajali na kushuka chini ya bahari, tunasema meli hiyo imezama baharini. Mtu anayechimba shimo la taka akachimba chini sana na kuzitupa humo na kuzifukia, hapo ni sawa na kusema kazizamisha/kazizika.

Sasa mpaka hapo tutakuwa tumeshajua maana ya neno “KUZAMA au KUZAMISHA”..Sasa ukilichukua neno hilo “kuzamamisha”  ukalitafsiriwa kwa lugha ya kigiriki linakuwa ni BAPTIZO…Ni sawa uchukue Neno la kiswahili “kanisa” na kulitafsiri kwa kiingereza na kuwa “CHURCH”…Vivyo hivyo Neno “kuzamishwa” likitafsiriwa kwa kigiriki linakuwa ni Baptizo..neno hilo hilo likipelekwa kwa lugha ya kiingereza linakuwa ni “IMMERSION”..na linaweza kutafsiriwa kwa lugha mbali mbali..

Kwahiyo mtu anayesema “leo naenda chachi”..ni sawasawa na mtu aliyesema “leo naenda kanisani”…neno “chachi” sio Kiswahili, na wala sio kiingereza fasaha lakini utakuwa umemwelewa amemaanisha nini kusema hivyo.

Vivyo hivyo mtu akikuambia “leo nime batizwa kwenye maji” utakuwa umemwelewa kwamba amemaanisha leo kazamishwa kwenye maji…kwa lengo Fulani.. (katumia tu msemo wa kigiriki lakini utakuwa umeshamwelewa).

Kwahiyo mpaka hapo utajua kuwa hakuna mtu atakayekuambia kwamba kabatizwa kwenye maji halafu awe “amenyunyuziwa”…Mtu aliyenyunyuziwa hajabatizwa!…kwasababu kubatizwa sio kunyunyuziwa bali kuzamishwa kabisa. (mpaka hapo tutakuwa tumeshaelewa ubatizo ni nini)

TUKIRUDI KATIKA IMANI YA KIKRISTO.

Katika imani ya kikristo, yapo mambo ambayo yanafanyika kama ishara lakini yanafunua kitu kikubwa sana katika roho. Kwamfano utaona Bwana Yesu alitoa maagizo ya kushiriki meza ya Bwana, ambapo wakristo wakutanikapo wanakula mkate pamoja na divai. Hivyo ni vyakula vya kimwili lakini vinapolika kwa maagizo hayo ya Bwana Yesu vinakuwa vinafunua vitu vingine katika roho. Kwamba ni sawa na tunainywa damu ya Yesu na Mwili wake katika ulimwengu wa roho. Na alisema mtu asiyefanya hivyo basi hana uzima ndani yake. (maana yake hana ushirika na Yesu).

Yohana 6:53 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu”.

Umeona ni agizo dogo tu, la kula chakula cha kimwili, lakini lina maana kubwa sana katika roho, sio la kulipuuza wala la kulifanya isivyopaswa…Na hapo hajasema tuonje!..bali tuule..

Kadhalika Bwana Yesu alitoa maagizo mengine yanayofanana na hayo ya watu kuzamishwa katika maji kwa jina lake(au kirahisi kubatizwa), ambapo alisema kwa kufanya hivyo katika mwili..kunafunua jambo kubwa sana katika roho, ambalo jambo lenyewe ni “kufa na kufufuka pamoja naye”

Wakolosai 2:12 “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu”.

Umeona na hapo?..maana yake usipobatizwa (yaani kuzamishwa katika maji)..basi katika roho bado hujafa wala kufufuka pamoja naye…wewe bado si wake!. Vile vile kama hujazamishwa na badala yake umenyunyuziwa hapo bado hujabatizwa, unapaswa ukabatizwe tena katika maji mengi.. kwasababu ndio tafsiri ya neno ubatizo.

Sasa yapo maswali machache machache ya kujiuliza?

Je ina maana kama mtu hajabatizwa katika maji mengi na badala yake katika kunyunyiziwa hawezi kwenda mbinguni?..Na kama hawezi vipi Yule mwizi aliyesulibiwa na Bwana pale msalabani..mbona yeye aliokolewa na wala hakubatizwa?..mbona wakina Musa hawakubatizwa?…mbona wakina Eliya hawakubatizwa?…Majibu ya maswali haya yote utayapata hapa >> Mtu akifa bila kubatizwa atakwenda mbinguni?

Hivyo ndugu mpendwa kamwe usiudharau “ubatizo”..kama bado hujaelewa kwa undani ubatizo ni nini, na umuhimu wa ubatizo tafadhali rudia kusoma tena taratibu na nakuomba chukua muda mwingi…katafute kuuliza huko na huko na pia piga magoti peke yako mwulize Roho Mtakatifu, halafu kasome biblia yako atakupa majibu.

Na ubatizo sahihi ni wa Jina la Yesu kulingana na mistari hii; Matendo 2:38, 8:16,10:48 na 19:5. Jina la Yesu ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Kufahamu haya zaidi fungua masomo mwisho kabisa mwa somo hili (sehemu ya chini)..yanaelezea kwa kina masuala ya ubatizo.

Bwana akubariki.

Kama hujampokea Yesu saa ya wokovu ni sasa. Kristo yupo mlangoni kurudi kuwachukua wateule wake..hivyo ingia leo ndani ya neema hii, kabla mlango wa neema haujafungwa. Yesu anakupanda na anataka kukupa raha nafsini mwako leo kama utamkubali…sawasawa na neno lake hili..

Mathayo 11: 28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI:

BIBLIA TAKATIFU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Karibu tujifunze biblia na kujikumbusha mambo yale yale ambayo tumekwisha kujifunza huko nyuma kupitia sehemu mbalimbali..

Wengi wanajiuliza je ubatizo ni wa muhimu?..Jibu ni NDIO ni wa muhimu sana na si kidogo. Shetani hapendi wengi wajue siri iliyopo katika ubatizo sahihi kwasababu anajua madhara yake.

Wakati wana wa Israeli wanatoka Misri, Farao bado alikuwa anawafuatilia fuatilia..lakini walipovuka tu bahari ya shamu na majeshi ya Farao yote kuzama kwenye ile bahari ya shamu ndio ikawa mwisho wa Farao na majeshi yake kuwafuatilia wana wa Israeli.

Kutoka 14:26 “Bwana akamwambia Musa, Nyosha mkono wako juu ya bahari, ili maji yarudi tena juu ya Wamisri, juu ya magari yao, na juu ya farasi zao.

27 Musa akaunyosha mkono wake juu ya bahari, na kulipopambazuka, bahari ikarudi kwa nguvu zake; Wamisri wakakimbia mbele yake; na Bwana akawakukutia mbali hao Wamisri kati ya bahari.

28 Yale maji yakarudi yakafunikiza magari na wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja.

29 Lakini wana wa Israeli wakaenda katika nchi kavu katikati ya bahari; na hayo maji yalikuwa ni kuta upande wao wa kuume, na upande wao wa kushoto.

30 Ndivyo Bwana alivyowaokoa Israeli siku ile mikononi mwa Wamisri; Waisraeli wakawaona Wamisri ufuoni kwa bahari, wamekufa”.

Sasa siri ilikuwa ni nini mpaka Mwisho wa Farao ukawa kwenye hiyo bahari ya Shamu?..Jibu ni rahisi: Ni huo ubatizo wana wa Israeli waliobatizwa kwa kupita katikati ya bahari hiyo.

Utauliza je!..ina maana wana wa Israeli walibatizwa katika bahari ya Shamu?..Jibu ni ndio!..

1Wakorintho 10:1 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;

2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;”

Unaona hapo?..kitendo cha Wana wa Israeli kupitishwa katika yale maji ya Shamu, pasipo kupatikana na madhara ndiko kunakofananishwa na ubatizo. Hivyo ule ubatizo ndio uliohitimisha kazi ya shetani na majeshi yake kuwafuatilia, haijalishi kuwa tayari walishapewa ruhusu huko nyuma ya kuondoka.

Hali kadhalika, ubatizo sahihi wa maji mengi sasa unafanya kazi hiyo hiyo. Unapoingia katika yale maji na kubatizwa katika jina la Yesu na kutoka katika yale maji…wewe utatoka salama ukiwa na furaha, na amani lakini nyuma yako yale majeshi ya mapepo wabaya yaliyokuwa yanakufuatia yanakufa na maji huko nyuma.

Hivyo maji ni ishara ya wokovu kwako na maangamizi kwa shetani na majeshi yake. Ndio maana Bwana Yesu alisema katika Roho kwamba pepo amtokapo mtu hupitia mahali pasipo maji(maana yake mahali ambapo hapana maji) ili apumzike na akirudi na kukuta nyumba yake imefagiliwa anakwenda kuwachukua pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye, na hali ya mwisho ya Yule mtu inakuwa mbaya kuliko ya kwanza.

Maana yake ni kwamba pepo likimtoka mtu na Yule mtu kama hatachukua uamuzi wa kuukamilisha wokovu wake ikiwemo kubatizwa ubatizo sahihi wa kuzama mwili mzima kulingana na maandiko na kudumu katika usafi..Mtu huyo yupo hatarini kurudiwa na zile zile nguvu za giza zilizomwacha hapo kwanza. Hivyo ubatizo sahihi ni wa muhimu sana…Na ubatizo sio dini mpya bali ni maagizo ya  Bwana wetu Yesu…na kwa faida yetu kama ilivyokuwa kwa faida kwa wana wa Israeli wakati wanatoka Misri, kama sio yale maji Farao angeendelea kuwafuatilia daima.

Shetani na mapepo yake yataendelea kumfuata Yule mtu ambaye hajakamilisha wokovu wake…Na Bwana alishatuambia katika Neno lake, kwamba “aaminiye na kubatizwa ataokoka”..maana yake mambo hayo mawili yanakwenda pamoja, hayaachani, vinginevyo ni ngumu sana kuokoka na mkono wa Adui.

Kama unakumbuka kile kisa cha Yule mtu aliyekuwa na mapepo yaliyojitambulisha kama JESHI. Mtu Yule aliingiwa na mapepo, na mapepo yale yalipomtoka yaliwaingia nguruwe…Jinsi wale Nguruwe walivyokwenda kuangamia majini ni mfano wa Farao na majeshi yake yalivyozama majini…Kwahiyo unaweza kuona kuna uhusiano mkubwa sana wa maji na majeshi ya Adui. Hivyo ubatizo ni wa muhimu sana. Pale tu mtu anapoamini na kutubu anapaswa akabatizwe bila kuchelewa…

Itakuwa ni jambo la kushangaza, mtu utasema umeokoka, halafu miezi inapita, miaka inapita, bado hujabatizwa, unaishi kwa kanuni ipi ya wokovu?

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

SWALI: Naomba kufahamu Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena, tunaopaswa tuwe nao ni ule wa Roho Mtakatifu tu peke yake kama vile Yohana Mbatizaji alivyosema katika Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto”?


JIBU: Katika mistari hiyo hakuna mahali popote Yohana amesema sasa ndio watu waache ubatizo wa maji, wautazame ule wa Roho Mtakatifu peke yake..Hakuna na Hiyo yote ni kutokana na utafsiri mbaya wa maandiko ambao unasababishwa na baadhi ya waalimu ambao hawamtegemei Roho Mtakatifu katika kuyatafsiri maandiko.

Embu leo tuangalie mtu mmoja katika biblia ambaye alilielewa hilo andiko na akachukua hatua stahiki katika kuwaelekeza watu katika njia ya kweli.

Kama tukisoma kitabu cha Matendo sura ile ya 10 kwa ufupi pale tunaona habari ya mtu mmoja aliyeitwa Kornelio, ambaye alikuwa anamcha Mungu sana kwa sadaka zake, lakini siku moja akatokewa na malaika na kupewa maagizo ya kwenda kumuita Petro aje kuwaelekeza cha kufanya.. Ndipo Petro alipoeletewa taarifa akaenda na alipowakuta akaanza kuwaeleza habari za Yesu, pindi tu anaanza kuwaeleza habari zile Roho Mtakatifu alishuka palepale, na watu wote wakajazwa na Roho Mtakatifu wakaanza kunena kwa lugha mpya.

Matendo 10:44 “Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno.

45 Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu.

46 Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu,

47 Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?

48 Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha.

Sasa utaona hapo mara baada ya Petro kuona watu wamejazwa Roho Mtakatifu hakusema yatosha sasa, hakuna haja ya kubatizwa tena, Roho Mtakatifu anatosha kwasababu Yohana alisema hivyo…

Ukitaka kujua kuwa Petro naye aliufahamu huo mstari vizuri hata Zaidi yetu sisi, aliukumbuka pia hata alipokuwa palepale anawahubiria, Tunalithibitisha hilo mbele kidogo wakati sasa amesharudi Yerusalemu anawasimulia wayahudi tendo hilo la watu wa mataifa kupokea Roho Mtakatifu kama wao aliwaeleza mstari huo embu tusome alichokisema..

Matendo 11:15 “Ikawa nilipoanza kunena Roho Mtakatifu akawashukia kama alivyotushukia sisi mwanzo.

16 Nikalikumbuka neno lile la Bwana, jinsi alivyosema, YOHANA ALIBATIZA KWA MAJI KWELI, BALI NINYI MTABATIZWA KWA ROHO MTAKATIFU.

17 Basi ikiwa Mwenyezi Mungu amewapa wao karama ile ile aliyotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani niweze kumpinga Mungu?.

Unaona hapo?, Petro alilielewa hilo andiko kuwa hatupaswi kuuacha ubatizo wa maji, na ndio maana hata baada ya kuona Roho Mtakatifu alishuka juu yao kabla ya ubatizo bado aliagiza wakabatizwe. Hivyo na sisi pia agizo la ubatizo ni moja ya maagizo muhimu sana Bwana Yesu aliyotupa yanayoukamilisha wokovu wetu. Kila mtu aliyeamini hana budi kwenda kubatizwa haraka sana iwezekanavyo..Kama Bwana Yesu alivyosema..katika Marko 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Na tena katika ubatizo ulio sahihi wa mitume ambao ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23). na kwa jina la YESU KRISTO (Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5)..Ubatizo mwingine tofauti na huo ni batili. Mtu anapaswa akabatizwe tena.

Ubarikiwe.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo kwa njia ya whatsapp ya kila siku basi, bofya hapa uweze kujiunga >>> WHATSAPP Au tuandikie kwa namba hizi +255789001312

Maran atha


Mada Nyinginezo:

MTUMAINIE YESU ASIYEISHA MATUKIO.

KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

ROHO SABA ZA MUNGU NI ZIPI?

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

KIASI NI NINI KATIKA UKRISTO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

JIBU: Utendaji kazi wa Roho Mtakatifu ni kama ufuatavyo, Mungu anapomchagua mtu aliye dhambini, huwa anamtumia Roho wake mtakatifu kumvuta mtu yule ndio hapo mtu huyo anaanza kusikia kuhukumiwa dhambi zake moyoni, na hatimaye anafikia toba, sasa huyo ni Roho Mtakatifu siku hizo zote anakuwa anamvuta mtu yule, anakuwa anatembea na yule mtu kama rafiki yake wa pembeni, lakini bado hajaingia ndani yake, ni kama mwanamume anapokuwa katika hatua za awali za kumchumbia mwanamke, anakuwa anaweza kuwa karibu naye, kumpa zawadi chache chache, kuzungumza naye maneno mazuri, kumwonyesha vitu vyake n.k, hayo yote mwanamume anayafanya ili tu kumvuta yule mwanamke, lakini bado yule mwanamke sio mali yake mpaka siku atakayoamua kumkubalia na kufunga naye ndoa, ndipo siku hiyo atakuwa milki halali ya yule mwanamume.

 Na Roho Mtakatifu ndio hivyo hivyo, katika hatua za awali, Roho Mtakatifu anaweza akazungumza na mtu, wakati mwingine akampa hata maono,kumfanikisha katika mambo yake n,k lakini akawa bado hajaingia ndani yake, yote hayo Roho Mtakatifu anayafanya ili kuzidi kumshawishi kuielekea njia sahihi ya wokovu……Na kama mtu yule bado atakuwa hajachukua hatua ya kumkaribisha ndani ya moyo wake kwa kutubu kabisa kwa kumaanisha kuacha dhambi zake na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, ataendelea kumshiwishi ndani yake mpaka siku atakapokubali.. 

Sasa siku yule mtu yule atakapoamua kubatizwa katika ubatizo sahihi, siku ile ile yule Roho Mtakatifu ambaye alikuwa anatembea naye anaingia ndani yake na kuwa milki halali ya Roho Mtakatifu mwenyewe, wanakuwa ni kama wamefunga ndoa na Roho Mtakatifu, kwasababu ubatizo ndio kibali cha Roho Mtakatifu kuingia ndani ya mtu, ni ishara ya dhambi za mtu kuondolewa kwa damu ya Yesu, na ni muhimu sana na ndio maana Bwana aliyaagiza, sasa baada ya hapo ndipo Roho Mtakatifu anakuja kufanya makao ndani ya yule mtu. Biblia inasema Roho Mtakatifu ndio Muhuri wa Mungu, kama unavyojua barua yoyote isiyokuwa na muhuri halisi hiyo ni batili. Roho Mtakatifu ni kama Pete ya ndoa kwa wanandoa. 

Waefeso 4: 30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi”.

2Wakorintho 1: 22 “..naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu”. 

Na akishaingia ndani ya yule mtu anaanza kupitishwa madarasa mengine ya kiroho zaidi, na huyo mtu shetani hawezi kumpata tena kwasababu ni kama kashakatiwa leseni mbinguni kuwa milki halali ya Roho mtakatifu, Na pia maandiko yanasema katika ….Warumi 8:9 “……Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.”…kwa lugha nyepesi mtu yoyote ambaye hajafunga ndoa na Roho Mtakatifu kwa njia ya UBATIZO SAHIHI huyo sio wake, haijalishi Roho Mtakatifu anamwonyesha maono, anazungumza naye n.k bado huyo sio wake. 

Mwingine atasema mbona wapo ambao wamebatizwa huo ubatizo sahihi lakini bado ni waovu? je! wewe unamkosoa Bwana wako aliyekupa hayo maagizo kwamba alichokisema hakina umuhimu sana katika kazi ya ukombozi?..Mbona husemi hivyo kwa mitume waliobatizwa kwa njia hiyo?.. Nakushauri usiwaangalie wanadamu kama ni kipimo cha wokovu wako, hujui mtu huyo aliuendea ubatizo kwa kidini tu, au kuwaridhisha wanadamu, au kwa faida zake mwenyewe..Lakini fahamu kuwa Ubatizo sahihi wafaa sana kwa wokovu wako mwenyewe. 

Ubarikiwe.


Mada nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?

NINI MAANA YA KUTOKA KATIKA MADHEHEBU?

ROHO ZILIZO CHINI YA MADHABAHU:

MKATAE SHETANI NA MAWAZO YAKE YA KIBINADAMU.

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ubatizo wa moto ni upi?

JIBU: Ni kweli Yohana alibatiza kwa maji na alisema Bwana YESU atakapokuja atatubatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto..Sasa huu ubatizo wa moto ni upi?, kama tunavyofahamu moto hufanya kazi kuu tatu:

Ya kwanza: ni kuteketeza vitu dhaifu vyote visivyostahili. Kwamfano takataka..Vivyo hivyo Hatua hii ni ile Mungu anaichoma dhambi yote ndani ya mtu, hapo ndipo utakuta mtu tamaa ile ya kutenda dhambi aliyokuwa nayo kipindi cha nyuma inakufa yote, alikuwa anavuta sigara ghafla kiu ya sigara inakufa, alikuwa anakunywa pombe ghafla kiu ya pombe inakata, alikuwa ni mzinzi ghafla hata ile hamu ya kwenda kufanya uzinzi inakufa, alikuwa mtukanaji,ghafla anaanza kuona uzito tena kufungua kinywa chake na kutukana watu, alikuwa ni mwizi anajikuta hapendi tena uwizi, alikuwa msengenyaji ghafla dhamiri inamsuta akitaka kusengenya, alikuwa anatembea nusu uchi, ghafla anaanza kuona aibu hata kuzivaa hizo nguo n.k.

Ya pili: ni kuimarisha vitu vilivyo vigumu ili viwe vigumu na imara zaidi. kama vile dhahabu inapopitishwa kwenye moto.  

Hatua hii Roho Mtakatifu anapitisha mtu kwa lengo la kumuimarisha, Kama wafuaji wanavyofanya huwa wanayeyusha madini kwenye moto mkali ili baadaye yakishaganda yawe na mng’ao mzuri zaidi. , japo kwa nje yataonekana kama yanapitia dhiki ya hali ya juu kwa kuwekwa kwenye tanuru lakini yakishamalizwa kuchomwa matokeo yake yanaonekana kuwa bora zaidi kuliko yalipokuwa pale mwanzoni (Na ndio maana tunaona matofali ya udongo huwa yanachomwa kwanza, na ndipo yapelekwe kwa matumizi ya kujengea nyumba nzito,)..Hivyo kadhalika na kwa watoto wa Mungu..Tunapopokea Roho Mtakatifu..Mungu mwenyewe anaruhusu tupitie moto wa majaribu,ili kuihimarisha IMANI ZETU zisiwe dhaifu, hata tutakapopitia mambo magumu tusiweze kuanguka kirahisi.

Na ndio maana tunaona pale tu mtu anapoanza kuamini! mara anaanza kuona mambo ya nje yanabadilika, ghafla anakuchukiwa na ndugu au kutengwa, mwengine atapita misiba, mwingine magonjwa, mwingine vifungo, mwingine mapigo, mwingine anadorora kiuchumi, mwingine atatengwa n.k. mfano kama walivyopitia akina Ayubu, Yusufu n.k….Lakini Mungu kumpitisha mtu hivyo huwa sio kwa ajili ya kumwangamiza hapana bali ni kumuimarisha hivyo mtu kama huyo Bwana huwa anampa neema ya ziada kuyashinda hayo majaribu, kwasababu Mungu hawezi kuruhusu tujaribiwa kupita tuwezavyo

1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili”.

  Na pia Ukisoma…  

1Petro 1: 6 Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali; 7 ili kwamba KUJARIBIWA KWA IMANI YENU, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.”

  Hivyo huo ndio ubatizo wa Moto unaozungumziwa hapo..Kwahiyo mtoto yoyote wa Mungu ni lazima aupitie huo(Mitume walipitia, manabii walipitia na Bwana wetu Yesu Kristo alipitia kadhalika na sisi pia)..yaani ubatizo wa Maji pamoja na ubatizo wa Roho na wa moto .  

Na Hatua ya tatu: Ni kuchochea. Kwamfano moto ukiwashwa ndani ya bunduki, ile rasasi iliyo ndani yake ni lazima ifyatuke. Moto ukiwekwa chini ya sufuria yenye maji, yale maji ni lazima yatokote, Vivyo hivyo na moto wa Roho ukiachiliwa ndani ya mtu..Ni lazima atatoka na kwenda kuwahubiria injili wengine, hawezi kutulia..Na hicho ndicho kilichotokea ile siku ya Pentekoste mitume walipopokea ubatizo huu, muda huo huo walianza kuhubiri kwa kasi sana.

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

JE, KAMA HAUNA UBATIZO SAHIHI HAUWEZI KUWA NA ROHO MTAKATIFU?

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

JE! UNAWEZA KUBATIZWA NA USIPOKEE ROHO MTAKATIFU?. NA JE! UNAWEZA KUPOKEA ROHO MTAKATIFU KWA KUWEKEWA MIKONO?

MELKIZEDEKI NI NANI?

SEHEMU YA MAANDIKO ILIYOFICHWA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Moja ya maagizo muhimu sana ambayo Bwana YESU KRISTO aliyatoa kwa kanisa ni ubatizo.

Mengine yakiwemo kushiriki,kutawadhana miguu kwa wakristo,wanawake kufunika vichwa vyao wakati wa ibada.Kati ya hayo ubatizo ni muhimu sana kwa mwamini yeyote kwa ajili ya ondoleo la dhambi zake.Lakini ubatizo huu shetani ameuharibu usifanyike ipasavyo kwa sababu anajua una madhara makubwa katika kumbadilisha mkristo.na hiyo ndiyo imekuwa kazi ya shetani tangu awali kuyapindisha maneno ya Mungu na kuzuia watu wasimfikie Mungu katika utimilifu wote.

Makanisa mengi leo hii yanabatiza watu au watoto wachanga kwa kuwanyunyuzia maji. Wakibatiza kwa jina la BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU kulingana na mathayo 28:19. “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho mtakatifu”..swali ni je! hili jina linatumiwa ipasavyo kubatizia?

Kwa kukosa Roho ya ufunuo na uelewa wa maandiko viongozi wengi wa dini wameacha kweli. Na kugeukia mafundisho ya kipagani na kibaya zaidi wengi wao wanaujua ukweli lakini wanawaficha watu wasiujue ukweli kwa kuogopa kufukuzwa kwenye mashirika yao ya dini. Watu kama hawa ni adui wa msalaba

 Bwana aliowazungumzia akisema 

Mathayo 23:13″ ole wenu waandishi na mafarisayo, wanafki! kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamuingii wala wanaoingia hamwaachi waingie.”

 Tukirejea tena kwenye maandiko

Yohana 5:42-43 “walakini nimewajua ninyi ya kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu.Mimi nimekuja kwa JINA LA BABA YANGU, wala ninyi hamnipokei; mwingine akija kwa jina lake mwenyewe, mtampokea huyo.”

hapa tunaona dhahiri kabisa jina alilonalo Yesu ni jina la BABA yake. Kwa namna hiyo basi jina la baba yake ni Yesu.

Tukirudi tena kwenye maandiko yohana 14:26 Yesu Kristo alisema “lakini huyo msaidizi,huyo Roho mtakatifu ambaye baba atampeleka  KWA JINA LANGU, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.”na  hapa tunaona Roho Mtakatifu alitolewa kwetu kwa jina la Bwana Yesu. kwahiyo hapa biblia inatufundisha dhahiri kabisa kuwa jina la Roho Mtakatifu ni Yesu.

Na tena kwenye maandiko tunaona kuwa Roho Mtakatifu ndiye Baba mathayo 1:20 “…Yusufu, mwana wa Daudi usihofu kumchukua Mariamu mkeo maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu” kwahiyo Baba ndiye yule yule Roho na ndiye yule yule aliyechukua mwili na kuishi pamoja nasi kwahiyo hapa hatuoni ‘utatu’ wa aina yeyote ambao unahubiriwa leo hii na makanisa mengi.  Mungu ni mmoja tu!.

Kwahiyo jina la Baba ni Yesu na jina la Mwana ni Yesu na jina la Roho Mtakatifu ni Yesu; baba,mwana na roho ni vyeo na sio majina kwa mfano mtu anaweza akawa baba kwa mtoto wake,mume kwa mke wake,babu kwa mjukuu wake lakini jina lake anaweza akawa anaitwa Yohana na sio ‘baba,mume au mjukuu’ vivyo hivyo kwa Mungu.aliposema mkawabatize kwa jina la Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu alikuwa anazungumzia Jina la YESU KRISTO ambalo ndilo jina la baba na mwana na Roho Mtakatifu.

Katika biblia Wakristo na mitume wote walibatizwa na kubatiza kwa JINA LA YESU KRISTO na sio kwa JINA LA BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU. ubatizo huu wa uwongo ulikuja kuingizwa na kanisa katoliki katika baraza la Nikea mwaka 325 AD pale ukristo ulipochanganywa na upagani na ibada ya miungu mingi ya Roma.

Tukisoma matendo ya mitume 2:37-38 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao. wakamwambia Petro na mitume wengine , tutendeje, ndugu zetu? Petro akawaambia, tubuni mkabatizwa kila mmoja KWA JINA LAKE YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.”

Tukisoma tena  katika maandiko Filipo alipoenda Samaria na wale watu wa ule mji walipoiamini injili walibatizwa wote kwa jina lake Yesu Kristo matendo 8:12 ” lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habati njema za ufalme wa Mungu na  JINA LAKE YESU KRISTO  wakabatizwa wanaume na wanawake”

Na pia matendo 8:14-17  inasema ” Na mitume walipokuwa Yerusalemu, waliposika ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu.wakawapelekea Petro na Yohana ambao waliposhuka wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila WAMEBATIZWA TU KWA JINA  LAKE BWANA YESU”

Tukirejea tena.

Matendo 10:48  Petro alipokuwa nyumbani mwa Kornelio alisema maneno haya “Ni nani awezaye kuzuia maji,hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vilevile kama sisi? akaamuru WABATIZWE KWA JINA LAKE YESU KRISTO”

Tukisoma tena katika matendo 19:2-6  hapa Paulo akiwa Efeso alikutana na watu kadha wa kadha akawauliza.” je! mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini?, wakamjibu, la, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia. Akawauliza, basi mlibatizwa kwa ubatizo gani? wakasema, kwa ubatizo wa Yohana. Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani Yesu. Waliposikia haya WAKABATIZWA KWA JINA LA BWANA YESU”

Mitume wote hawa kuanzia Petro,Yohana,Filipo na mtume Paulo wote hawa walibatiza kwa jina la Yesu Kristo je? tuwaulize hawa viongozi wa dini wanaobatiza kwa jina la baba na mwana na roho mtakatifu wameutolea wapi??? na biblia inasema katika

Wakolosai 3:17 ” na kila mfanyalo kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote  katika Jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu baba kwa yeye”..

hii ina maana tukiomba tunaomba kwa jina la Yesu,tukitoa pepo tunatoa kwa Jina la Yesu, tukiponya watu tunaponya kwa jina la Yesu,tukifufua wafu tunafufua kwa jina la Yesu na tukibatizwa tunabatizwa kwa jina la YESU biblia inasema kwenye

Matendo 4:12 “…kwa maana hapana jina lingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”

na hakuna mahali popote katika biblia mtu alibatizwa kwa jina la Baba na Mwana na Roho mtakatifu

na maana ya neno ubatizo ni “kuzamishwa” na sio kunyunyuziwa, kwahiyo ni lazima kubatizwa kwa kuzamishwa kwenye maji sawasawa na maandiko na hakuna mahali popote katika maandiko watoto wachanga wanabatizwa. Ubatizo ni pale mtu anapoona sababu ya yeye kutubu na kuoshwa dhambi zake ndipo anapoenda kubatizwa kwa jina la Yesu kwa ondoleo la dhambi zake.

Ewe ndugu Mkristo epuka mapokeo ambayo Yesu aliyaita “chachu ya mafarisayo” penda kuujua ukweli ndugu mpendwa na ubadilike na umuombe Roho wa Mungu akuongoze katika kweli yote usipende mtu yeyote achezee hatima yako ya maisha ya milele, uuchunge wokovu wako kuliko kitu chochote kile,Mpende Mungu, upende kuujua ukweli,ipende biblia..Mwulize mchungaji wako kwa upendo kabisa kwanini anayafanya hayo huku anaujua ukweli na kama haujui mwambie abadilike aendane na kweli ya Mungu inavyosema kulingana na maandiko.

Kama hujabatizwa au umebatizwa katika ubatizo usio sahihi ni vema ukabatizwa tena kwa jina la YESU KRISTO kwa ondoleo la dhambi zako kwani ubatizo sahihi ni muhimu sana..ukitaka kubatizwa tafuta kanisa lolote wanaoamini katika ubatizo sahihi tulioutaja hapo  juu au unaweza ukawasiliana nasi tutakusaidia namna ya kupata huduma ya ubatizo sahihi, karibu na mahali ulipo 0789001312

 Mungu akubariki 

  jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP             

  (ubatizo sahihi wa kuzamishwa na KWA JINA LA YESU KRISTO)

Muhtasari wa maelezo haya kwa njia ya video unaweza kuyapata hapa chini.

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=kuCSAZcnM80[/embedyt]

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada zinazoendana:


Mada Nyinginezo:

MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI:

SAUTI AU NGURUMO

JE, KAMA HAUNA UBATIZO SAHIHI HAUWEZI KUWA NA ROHO MTAKATIFU?

JE! NI HATUA ZIPI MUHIMU ZA KUFUATA BAADA YA UBATIZO?

UBATIZO WA MOTO NI UPI?


Rudi Nyumbani

Print this post

UTAPENDA KUCHANGIA HUDUMA HII?

Tutamshukuru Mungu kwa ajili yako, kwa mchango wako, ili kuifanya injili hii isonge mbele Tuma sadaka yako kwa namba hizi:
Airtel:+255789001312 -Devis Magembe
Mpesa: +255767992434-Denis Magembe


This will close in 315 seconds