UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

by Admin | 26 July 2020 08:46 pm07

Kabla ya kufahamu ubatizo ni nini…Hebu jiulize mtu katokea na akakuuliza “kuzamisha maana yake ni nini?”..utamjibuje?…Bila shaka utamwelezea kwa kina kwamba ni kitendo cha kukitosa kitu chote kwenye kimiminika Fulani au kitu Fulani, pasipo kubakisha sehemu ambayo ipo wazi. Meli iliyopata ajali na kushuka chini ya bahari, tunasema meli hiyo imezama baharini. Mtu anayechimba shimo la taka akachimba chini sana na kuzitupa humo na kuzifukia, hapo ni sawa na kusema kazizamisha/kazizika.

Sasa mpaka hapo tutakuwa tumeshajua maana ya neno “KUZAMA au KUZAMISHA”..Sasa ukilichukua neno hilo “kuzamamisha”  ukalitafsiriwa kwa lugha ya kigiriki linakuwa ni BAPTIZO…Ni sawa uchukue Neno la kiswahili “kanisa” na kulitafsiri kwa kiingereza na kuwa “CHURCH”…Vivyo hivyo Neno “kuzamishwa” likitafsiriwa kwa kigiriki linakuwa ni Baptizo..neno hilo hilo likipelekwa kwa lugha ya kiingereza linakuwa ni “IMMERSION”..na linaweza kutafsiriwa kwa lugha mbali mbali..

Kwahiyo mtu anayesema “leo naenda chachi”..ni sawasawa na mtu aliyesema “leo naenda kanisani”…neno “chachi” sio Kiswahili, na wala sio kiingereza fasaha lakini utakuwa umemwelewa amemaanisha nini kusema hivyo.

Vivyo hivyo mtu akikuambia “leo nime batizwa kwenye maji” utakuwa umemwelewa kwamba amemaanisha leo kazamishwa kwenye maji…kwa lengo Fulani.. (katumia tu msemo wa kigiriki lakini utakuwa umeshamwelewa).

Kwahiyo mpaka hapo utajua kuwa hakuna mtu atakayekuambia kwamba kabatizwa kwenye maji halafu awe “amenyunyuziwa”…Mtu aliyenyunyuziwa hajabatizwa!…kwasababu kubatizwa sio kunyunyuziwa bali kuzamishwa kabisa. (mpaka hapo tutakuwa tumeshaelewa ubatizo ni nini)

TUKIRUDI KATIKA IMANI YA KIKRISTO.

Katika imani ya kikristo, yapo mambo ambayo yanafanyika kama ishara lakini yanafunua kitu kikubwa sana katika roho. Kwamfano utaona Bwana Yesu alitoa maagizo ya kushiriki meza ya Bwana, ambapo wakristo wakutanikapo wanakula mkate pamoja na divai. Hivyo ni vyakula vya kimwili lakini vinapolika kwa maagizo hayo ya Bwana Yesu vinakuwa vinafunua vitu vingine katika roho. Kwamba ni sawa na tunainywa damu ya Yesu na Mwili wake katika ulimwengu wa roho. Na alisema mtu asiyefanya hivyo basi hana uzima ndani yake. (maana yake hana ushirika na Yesu).

Yohana 6:53 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu”.

Umeona ni agizo dogo tu, la kula chakula cha kimwili, lakini lina maana kubwa sana katika roho, sio la kulipuuza wala la kulifanya isivyopaswa…Na hapo hajasema tuonje!..bali tuule..

Kadhalika Bwana Yesu alitoa maagizo mengine yanayofanana na hayo ya watu kuzamishwa katika maji kwa jina lake(au kirahisi kubatizwa), ambapo alisema kwa kufanya hivyo katika mwili..kunafunua jambo kubwa sana katika roho, ambalo jambo lenyewe ni “kufa na kufufuka pamoja naye”

Wakolosai 2:12 “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu”.

Umeona na hapo?..maana yake usipobatizwa (yaani kuzamishwa katika maji)..basi katika roho bado hujafa wala kufufuka pamoja naye…wewe bado si wake!. Vile vile kama hujazamishwa na badala yake umenyunyuziwa hapo bado hujabatizwa, unapaswa ukabatizwe tena katika maji mengi.. kwasababu ndio tafsiri ya neno ubatizo.

Sasa yapo maswali machache machache ya kujiuliza?

Je ina maana kama mtu hajabatizwa katika maji mengi na badala yake katika kunyunyiziwa hawezi kwenda mbinguni?..Na kama hawezi vipi Yule mwizi aliyesulibiwa na Bwana pale msalabani..mbona yeye aliokolewa na wala hakubatizwa?..mbona wakina Musa hawakubatizwa?…mbona wakina Eliya hawakubatizwa?…Majibu ya maswali haya yote utayapata hapa >> Mtu akifa bila kubatizwa atakwenda mbinguni?

Hivyo ndugu mpendwa kamwe usiudharau “ubatizo”..kama bado hujaelewa kwa undani ubatizo ni nini, na umuhimu wa ubatizo tafadhali rudia kusoma tena taratibu na nakuomba chukua muda mwingi…katafute kuuliza huko na huko na pia piga magoti peke yako mwulize Roho Mtakatifu, halafu kasome biblia yako atakupa majibu.

Na ubatizo sahihi ni wa Jina la Yesu kulingana na mistari hii; Matendo 2:38, 8:16,10:48 na 19:5. Jina la Yesu ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Kufahamu haya zaidi fungua masomo mwisho kabisa mwa somo hili (sehemu ya chini)..yanaelezea kwa kina masuala ya ubatizo.

Bwana akubariki.

Kama hujampokea Yesu saa ya wokovu ni sasa. Kristo yupo mlangoni kurudi kuwachukua wateule wake..hivyo ingia leo ndani ya neema hii, kabla mlango wa neema haujafungwa. Yesu anakupanda na anataka kukupa raha nafsini mwako leo kama utamkubali…sawasawa na neno lake hili..

Mathayo 11: 28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI:

BIBLIA TAKATIFU.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/07/26/ubatizo-ni-nini/