JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu ukweli tangu zamani, na hataki kufanya hivyo au anapinga, huyo mtu atahukumiwa…Lakini kama huyo mtu ndio mara yake ya kwanza kuamini na kwa bahati mbaya akafa kabla ya kubatizwa, ataokolewa atafananishwa na yule mhalifu pale msalabani aliyekufa na Bwana.
Lakini Wapo watu baada ya kuujua ukweli, hawataki kuufanya uteule wao na wito wao imara kulingana na 2Petro 1: 10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.”
Kadhalika biblia inasema pia katika
Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. “
Soma tena hapa..
Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.
Hivyo masuala ya rohoni ni ya kuyatimiza kwa kuogopa na kutetemeka, na sio ya kuyachukulia tu kijuu juu.. Tunapoujua ukweli na mapenzi ya Mungu tunapaswa kuyafanya.
Wafilipi 2:12”…. utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka”.
Ubarikiwe.
Mada zinazoendana:
MADHARA YA KUUPIZIA MAAGIZO YA MSINGI MUNGU ANAYOKUPA.
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI:
UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.
WAKINYAMAZA HAWA, MAWE YATAPIGA KELELE.
My fellow brothers and sisters in Christ I greeet you in the name of the Most high God .I hope you are very fine as your spirit nourishes hope your physical is also the same.May God bless you Am actually blessed by the good work you are doing in The Kingdom of God.
Tutamshukuru Mungu kwa ajili yako, kwa mchango wako, ili kuifanya injili hii isonge mbele Tuma sadaka yako kwa namba hizi:
Airtel:+255789001312 -Devis Magembe
Mpesa: +255767992434-Denis Magembe
About the author