Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

JIBU: Utendaji kazi wa Roho Mtakatifu ni kama ufuatavyo, Mungu anapomchagua mtu aliye dhambini, huwa anamtumia Roho wake mtakatifu kumvuta mtu yule ndio hapo mtu huyo anaanza kusikia kuhukumiwa dhambi zake moyoni, na hatimaye anafikia toba, sasa huyo ni Roho Mtakatifu siku hizo zote anakuwa anamvuta mtu yule, anakuwa anatembea na yule mtu kama rafiki yake wa pembeni, lakini bado hajaingia ndani yake, ni kama mwanamume anapokuwa katika hatua za awali za kumchumbia mwanamke, anakuwa anaweza kuwa karibu naye, kumpa zawadi chache chache, kuzungumza naye maneno mazuri, kumwonyesha vitu vyake n.k, hayo yote mwanamume anayafanya ili tu kumvuta yule mwanamke, lakini bado yule mwanamke sio mali yake mpaka siku atakayoamua kumkubalia na kufunga naye ndoa, ndipo siku hiyo atakuwa milki halali ya yule mwanamume.

 Na Roho Mtakatifu ndio hivyo hivyo, katika hatua za awali, Roho Mtakatifu anaweza akazungumza na mtu, wakati mwingine akampa hata maono,kumfanikisha katika mambo yake n,k lakini akawa bado hajaingia ndani yake, yote hayo Roho Mtakatifu anayafanya ili kuzidi kumshawishi kuielekea njia sahihi ya wokovu……Na kama mtu yule bado atakuwa hajachukua hatua ya kumkaribisha ndani ya moyo wake kwa kutubu kabisa kwa kumaanisha kuacha dhambi zake na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, ataendelea kumshiwishi ndani yake mpaka siku atakapokubali.. 

Sasa siku yule mtu yule atakapoamua kubatizwa katika ubatizo sahihi, siku ile ile yule Roho Mtakatifu ambaye alikuwa anatembea naye anaingia ndani yake na kuwa milki halali ya Roho Mtakatifu mwenyewe, wanakuwa ni kama wamefunga ndoa na Roho Mtakatifu, kwasababu ubatizo ndio kibali cha Roho Mtakatifu kuingia ndani ya mtu, ni ishara ya dhambi za mtu kuondolewa kwa damu ya Yesu, na ni muhimu sana na ndio maana Bwana aliyaagiza, sasa baada ya hapo ndipo Roho Mtakatifu anakuja kufanya makao ndani ya yule mtu. Biblia inasema Roho Mtakatifu ndio Muhuri wa Mungu, kama unavyojua barua yoyote isiyokuwa na muhuri halisi hiyo ni batili. Roho Mtakatifu ni kama Pete ya ndoa kwa wanandoa. 

Waefeso 4: 30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi”.

2Wakorintho 1: 22 “..naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu”. 

Na akishaingia ndani ya yule mtu anaanza kupitishwa madarasa mengine ya kiroho zaidi, na huyo mtu shetani hawezi kumpata tena kwasababu ni kama kashakatiwa leseni mbinguni kuwa milki halali ya Roho mtakatifu, Na pia maandiko yanasema katika ….Warumi 8:9 “……Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.”…kwa lugha nyepesi mtu yoyote ambaye hajafunga ndoa na Roho Mtakatifu kwa njia ya UBATIZO SAHIHI huyo sio wake, haijalishi Roho Mtakatifu anamwonyesha maono, anazungumza naye n.k bado huyo sio wake. 

Mwingine atasema mbona wapo ambao wamebatizwa huo ubatizo sahihi lakini bado ni waovu? je! wewe unamkosoa Bwana wako aliyekupa hayo maagizo kwamba alichokisema hakina umuhimu sana katika kazi ya ukombozi?..Mbona husemi hivyo kwa mitume waliobatizwa kwa njia hiyo?.. Nakushauri usiwaangalie wanadamu kama ni kipimo cha wokovu wako, hujui mtu huyo aliuendea ubatizo kwa kidini tu, au kuwaridhisha wanadamu, au kwa faida zake mwenyewe..Lakini fahamu kuwa Ubatizo sahihi wafaa sana kwa wokovu wako mwenyewe. 

Ubarikiwe.


Mada nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?

NINI MAANA YA KUTOKA KATIKA MADHEHEBU?

ROHO ZILIZO CHINI YA MADHABAHU:

MKATAE SHETANI NA MAWAZO YAKE YA KIBINADAMU.

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments