Title March 2024

Shukrani ni nini kibiblia?

Shukrani au kushukuru ni ile hali ya kurudisha hisia chanya kwa mema au mabaya yaliyokufikia.

Kwa tafsiri ya kidunia, shukrani inatolewa pale mtu anapopokea mambo mema.. Kwamfano mtu atarudisha shukrani aidha ya maneno au matendo pale anapozawadiwa kitu, au anapofanyiwa jambo Fulani jema.

Lakini kibiblia, Shukrani inatolewa si tu baada ya kupokea mambo mazuri/mema bali pia kwa mambo yote (hata kwa yale mabaya).. Ndivyo biblia inavyotufundisha..

1Wathesalonike 5:18 “SHUKURUNI KWA KILA JAMBO; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu”.

Soma pia Ayubu 2:10,

Maana yake ni lazima kumshukuru Mungu hata katika yale mambo ambayo tunaona hayajaenda kama tulivyotarajia, (Ikiwemo misiba, na hata wakati mwingine hasara)… kwasababu tunajua yote ni mapenzi ya Mungu kwetu maadamu tupo ndani ya KRISTO.

Lakini Zaidi sana ni vizuri kumshukuru MUNGU kwa mema anayokufanyia.

Moyo wa shukrani ni moyo unaompendeza MUNGU, na moyo usio na shukrani huondoa/hukausha mema yote na Baraka zote kwetu kutoka kwa Mungu.

Wengi wanajifungia milango yao ya Baraka baada ya kukaa kimya pale wanapotendewa jambo fulani na MUNGU, lakini wengine wanaendeleza milango ya Barakabaada ya kumshukuru Mungu kwa mambo waliyotendewa.

Shukrani ni jambo linalompendeza Mungu na linaloendeleza Baraka juu yetu.

Luka 17:12  “Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,

13  wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

14  Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.

15  Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;

16  akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

17  Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?

18  Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?

19  Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa”.

JE SHUKRANI IPI NI BORA?..

Shukrani iliyo bora ni ile inayoambatana na Sadaka.. Hii ni shukrani bora na yenye nguvu sana zaidi ya ile ya midomo mitupu tu!.

Ifuatayo ni baadhi ya mistari ya shukrani katika biblia.

1Nyakati 16:8 “Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; Wajulisheni watu matendo yake”.

Ezra 13:11 “Wakaimbiana, wakimhimidi Bwana, na kumshukuru, wakasema, Kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake kwa Israeli ni za milele. Kisha watu wote wakapaza sauti zao, na kupiga kelele, walipomhimidi Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana umekwisha kuwekwa”.

Zaburi 7:17 “Nitamshukuru Bwana kwa kadiri ya haki yake; Nitaliimbia jina la Bwana aliye juu”

Mistari mingine ni pamoja na Zaburi 9:1, Zaburi 28:7, Zaburi 33:2, Zaburi 92:1, Zaburi 136:1-3 na Isaya 12:4.

NI MAJIRA GANI SAHIHI YA KUMSHUKURU MUNGU.

Majira sahihi ya kumshukuru Mungu ni pale siku inapoanza, na inapoisha.. Inapoamka asubuhi na kuianza siku ni lazima kumshukuru Mungu kwa ulinzi wa usiku kucha na kwa kukupa siku mpya, vile vile unapoimaliza siku ni lazima umshukuru kwa kuimaliza salama na kwa ulinzi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mistari ya biblia kuhusu shukrani.

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

SI KWA MATENDO BALI NEEMA.

AMEFANYIKA BORA KUPITA MALAIKA!

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya Ayubu 31:10, “Mke wangu na asage kwa mwingine”?

Swali: Kusaga kunakozungumziwa katika Ayubu 31:10 ni kupi?..na maandiko hayo kwa ujumla yana maana gani?


Jibu: Turejee kuanzia mstari ule wa 9.

Ayubu 31:9 “Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke, Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu;

10 Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine, Na wengine na wainame juu yake.

11 Kwani hilo lingekuwa kosa kuu; Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi”

Maneno haya ni ya Ayubu kwa rafiki zake watatu, ambapo alikuwa anajaribu kuwaambia ukamilifu wake kuwa hajawahi hata kumtazama mwanamke kwa kumtamani (Ayubu 31:1) wala hajawahi kumchukua mke wa jirani yake… Hivyo majaribu yaliyompata si kwasababu ya dhambi au makossa.

Na hapo mstari wa 9 anazidi kujithibitisha kuwa kama “moyo wake ulishawishwa kwa mwanamke, Na ameotea mlangoni pa jirani yake;  Ndipo hapo mke wake na asage kwa mwingine, Na wengine na wainame juu yake”.

Akimaanisha kuwa kama yeye aliotea mlango kwa jirani yake, maana yake alisubiri mume wa mke wa jirani yake aondoke kisha aingia na kulala na mwanamke huyo.. basi na yeye pia mke wake na achukuliwe na akasage kwa nyumba ya mwanaume mwingine.

Sasa kusaga kunakozungumziwa hapo ni “kule kusaga nafaka”.. Kumbuka shughuli maarufu ya wanawake wa zamani katika nyumba zao zilikuwa ni kusaga nafaka kama ngano au mtama..

Ndio maana utaona katika lile tukio la unyakuo limefananishwa na wanawake wawili kukutwa wakisaga, na si wanaume..

Luka 17:34 “Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

35  Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.

36  Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.]

Kwahiyo kusagan ilikuwa ni shughuli ya siku zote ya wanawake wa nyumbani, Na walikuwa wanasaga kwa kutumia mawe maalumu yajulikanayo kama “Mawe ya kusagia”

Kwa maelezo ziadi kuhusiana na Jiwe/mawe ya kusagia fungua hapa >>>JIWE LA KUSAGIA

Kwahiyo Ayubu alimaanisha kama aliiba mke wa mtu mwingine, basi wake pia achukuliwe na kutumikia nyumba nyingine, (kwa shughuli hizo za kusaga na nyingine kama za mama wa nyumbani).. na si tu asage, bali pia na wengine wainame juu yake, (maana yake walale naye).

Lakini hayo yote Ayubu hayakumpata kwasababu alikuwa mkamilifu katika njia zake, na wala hakuwahi kulala na mke wa jirani yake, wala kudhulumu, wala kumnyima maskini mkate..njia zake zote zilikuwa ni kamilifu kama Bwana Mungu alivyomshuhudia..

Ayubu 1:1 “Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu”

Ni mambo gani tunajifunza kwa maisha ya Ayubu?

Jambo la kwanza: ni roho ya kumcha Mungu na kuepukana na Uovu.. Watu wanaomcha Mungu na kuepukana na uovu ndio wanaosifiwa naye..

pili: ni Uvumilivu wa Ayubu…Pamoja na majaribu yote yale, alimngoja BWANA, wala hakumwazia Mungu kwa upumbavu (Ayubu 1:22), na mwisho wa siku Bwana alimwokoa na majaribu yale yote.

Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.”

Je umempokea YESU?..kama bado unasubiri nini?.. Fahamu kuwa mlango wa wokovu hautakuwa wazi siku zote, ipo siku utafungwa, na siku hiyo imekaribia sana, huwenda ikawa leo?..Je parapanda ikilia na ikikukuta ukiwa katika hali hiyo, utakuwa mgeni wa nani?..au ukifa katika hali hiyo kule uendako utakuwa mgeni wa nani?.. Tafakari sana na ufanye maamuzi, kama bado hujaokoka.

Bwana YESU ANARUDI.

Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.

Maran atha!.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

Biblia inamaana gani inaposema “Wewe uchukiaye sanamu, wateka mahekalu?”

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Kuba ni nini (Ayubu 22:14)?

Rudi Nyumbani

Print this post

NI NJIA GANI MTU AITUMIE AWEZE KUSHINDA TAMAA NA VISHAWISHI?

Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu,

Ni swali ambalo linaulizwa na wengi, je ni kweli mtu anaweza kuzishinda tamaa za mwili? Au vishawishi vyake?  Anaweza kweli kuacha dhambi ya uzinzi, au kujichua,au kutazama picha za ngono, au ulevi, au miziki, n.k.?

Jibu la kibinadamu ni hapana! Na ndivyo ilivyo.. Lakini jibu la Mungu ni ndio, kwasababu alisema kwake yote yanawezakana.(Mathayo 19:26).

Akili yako itakuambia haiwezekani, kwasababu hujajua kanuni ya kuwezekana. Mimi niliwahi pia kufikiri hivyo hapo nyuma. Lakini nikathibitisha kile maandiko yanasema, kuwa hilo jambo linawezakana, Mungu hasemi uongo. Sasa utauliza ni kwa namna gani?

Awali ya yote ni vema ukafahamu kuwa hakuna mwanadamu yoyote aliyeumbwa na uwezo wa kuzishinda tamaa za mwili.  Hayupo. Vilevile anayejaribu kufanya hivyo kwa akili zake, na kwa nguvu zake peke yake, pia anajidanganya mwenyewe kwasababu, utafika wakati atayarudia yaleyale tu. Ikiwa wewe ni mmojawapo unayejaribu kupambana kwa nguvu zako, utavunjika moyo ni heri leo ujue kanuni sahihi ya kuitumia.

Sasa ni kwa namna gani tutaweza kushinda hali hizo za mwili?

Kanuni imetolewa kwenye mistari huu.

Wagalatia 5:16  BASI NASEMA, ENENDENI KWA ROHO, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. 17  Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

Anasema “Enendeni kwa Roho”, biblia ya kiingereza inatumia neno “Walk in spirit” akiwa na maana “Tembeeni katika Roho”

Wakristo wengi, wanampokea kweli Roho Mtakatifu, wanajazwa Roho kabisa, lakini ni wachache sana “wanaotembea katika Roho Mtakatifu”.

Ni sawa, na mgeni unayemkaribisha nyumbani mwako. Halafu unapokwenda kazini, au matembezini unamwacha nyumbani, hajui kingine chochote kuhusu wewe zaidi ya maisha ya palepale unayokutana naye nyumbani. Ndivyo anavyofanywa Roho Mtakatifu na waamini wengi.

Tunamtambua Roho tu, pale tunapokuwa ibadani, lakini maisha nje ya ibada, sisi ni watu wengine kabisa. Na hapo ndipo linapokuja tatizo kwanini vishawishi na tamaa zinatushinda. Kwasababu hatutembei na  Roho Mtakatifu.

Ukweli ni kwamba Roho Mtakatifu ndiye anayekusaidia wewe kuua nguvu ya tamaa ndani yako. Na hivyo anahitaji uwepo wake uwe nawe wakati wote, ili hilo liwezekane.  Ni sawa na GANZI, anayopigwa mgonjwa, wakati ganzi, ipo mwilini hawezi kusikia maumivu, lakini inapoisha maumivu yanamrudia kwa kasi, hivyo anahitaji kuongezewa ganzi nyingine, ili aendelee tena kukaa bila maumivu.

Ndivyo alivyo Roho Mtakatifu, huna budi kufahamu ni namna gani atakupiga ganzi, ili uweze kuishi maisha ya ushindi hapa duniani. Na kanuni si nyingine zaidi ya Kuenenda katika Roho. Kuanzia leo acha kupambana na hizo tamaa kivyako, hutazishinda, pambania kujawa na Roho lakini pia kutembea naye maishani mwako.

Sasa Tunatembeaje katika Roho?

Kwa kuzingatia mambo makuu matatu.

1). KWA KUWA WAOMBAJI WA DAIMA:

Watu wengi wanapofikiria maombi akili zao zinakwenda moja kwa moja kudhani ni wasaa kwa  kuwasilisha mahitaji yao. Lakini maombi si mahali tu pa mahitaji, bali ni mahali pa kujazwa Roho. Hivyo kama mtoto wa Mungu uingiapo kwenye maombi yako kila siku tumia nafasi ya kuomba ujazwe Roho Mtakatifu, akuongoze, akupe nguvu, akujenge nafsi yako, uimarike. Hivyo yakupasa uingie katika maombi ya ndani kabisa sio juu juu ya kutimiza ratiba, bali ya kuweka mawazo yako yote kwa Roho Mtakatifu, akujawe ndani yako, hili ni muhimu sana, kwasababu yeye ndio atakayekusaidia.

Sasa kwa jinsi unavyoomba kwa muda mrefu, na kwa mara kwa mara, ndivyo unavyozidi kumpa nafasi Roho wa Mungu kukujaza nguvu, na mwisho unaona vitu kama tamaa ni vidogo sana, kwasababu ganzi imeshaingia vya kutosha ndani yako.

Jambo hili linatakiwa liwe ni la kila siku(Waefeso 6:18). Kama wewe sio mwombaji, kiwango cha Roho kitakuwa kidogo ndani yako, mwili utakulemea tu, haijalishi upo kwenye wokovu kwa miaka 50, utasumbuliwa tu na tabia za mwilini, Ndio maana tunasisitizwa tuombe kila wakati. Maombi ni kila wakati, kila saa, omba kwa akili, pia omba wa kunena kwa lugha kwa jinsi Bwana atakavyokujalia. Lakini elekeza mawazo yako katika kujazwa na yeye, ukiwa ni mwombaji wa wiki mara moja uendapo kanisani jumapili, au mwezi mara moja, hapo unapoteza muda, hutembei katika Roho. Uthibitisho wa anayetembea kwa Roho ni Yule ambaye ni mwombaji wa kila siku.

2) LIWEKE NENO LA MUNGU AKILINI MWAKO WAKATI WOTE.

Neno la Mungu, husisimua roho zetu wakati wote. Na adui anachohakikisha ni kutufanya sisi tulisahau, hivyo mambo mengine yatawale akili zetu. Anajua akili yako ikiwa inatafakari habari na maonyo katika biblia, itakaa mbali na njia mbovu.

Pale adui anapotaka kukujaribu ukifiria wema Mungu aliomtendea Yusufu, kwa kuukimbia uzinzi, anajua utapata nguvu, pale Mungu alipomtukuza Ayubu kwa kukaa mbali na maovu, utapata nguvu, jinsi Danieli alivyokuwa mwaminifu, Mungu akamwinua anajua utaendelea katika uaminifu wako . Hivyo hapendi, wewe utawaliwe na Neno kichwani, anataka utawaliwe, na movie, utawaliwe na mipira, utawaliwe na siasa, na  mambo ya mitaani, basi. Akili yako izunguke hapo, lakini isizunguke kwenye BIBLIA.

Ukijizoesha kilizungusha Neno la Mungu, na ahadi za Mungu kichwani mwako. Tafsiri yake ni kuwa unamzungusha Roho Mtakatifu, katika ulimwengu wako wa maisha. Na ni nini atakachokifanya kwako kama sio kukusimua roho yako, kwa Neno lile. Hivyo unayashinda yote kirahisi. Watu hawajui Neno la Mungu ndio Roho Mtakatifu mwenyewe wanasema nao.

Yohana 6:63  Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; MANENO HAYO NILIYOWAAMBIA NI ROHO, TENA NI UZIMA.

Soma sana Neno, lakini zaidi, lidumu kichwani pako, kutwa nzima. Huu ni ulinzi kamili, na silaha madhubuti ya mambo yote ya mwilini.

3) FANYA MAAMUZI YA GEUKO LA KWELI.

Maamuzi ni kutii. Ukiwa mtu wa nia nia mbili, unataka kumfuata Yesu, na wakati huo huo hutaki ulimwengu ukuache nyuma. Hapo napo unamzuia Roho wa Mungu kufanya kazi yake vema ndani yako. Unaweza ukawa ni mwombaji kweli lakini kama moyoni mwako hujaamua kufanya maamuzi, bado ni kazi bure.

1Yohana 2:15  Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16  Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17  Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele

Ukiamua kumfuata Yesu, fahamu kuwa hii dunia sio fungu lako tena, anasa sio rafiki tena kwako. sio tu na ulimwengu lakini pia na nafsi yako.Ndipo hapo unachukua hatua za dhahiri kabisa katika  imani yako, kama ulikuwa na vichocheo vyote vinavyokusababishia utende dhambi, ndio hapo Yesu anakuambia ukate, usione huruma kutupa hizo nguo za kizinzi ulizozoea kuzivaa, kuachana na huyo girlfriend, kuacha hizo muvi za kizinzi, unazoangalia, usione shida kuacha kampani zako za walevu, usijihurumie hata kidogo, huku ukiwa na mawazo kuwa unafanya hivyo kwasababu ya Kristo ndiye atakayekupa neema ya kushinda.

Ijapokuwa mwanzoni utaona shida kwasababu unafanya kimwili, kwa utiifu wako huo baadaye Roho wa Mungu atakunasa, kwasababu umempa umiliki wote wa maisha yako. Ganzi kubwa sana itaingia ndani yako,.

Ukizingatia mambo hayo matatu, kila siku katika maisha yako. Basi wewe unaenenda kwa Roho. Hakuna litakalokuwa gumu kwako. Kwasababu si kwa nguvu zako bali kwa nguvu za aliye ndani yako, unayashinda hayo.

Wagalatia 5:25  Tukiishi kwa Roho, na tuenende kwa Roho.26  Tusijisifu bure, tukichokozana na kuhusudiana

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI JAMBO GANI LINALOMTAMANISHA SANA BWANA TUMWOMBE BILA KUKATA TAMAA?

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

KWANINI MUNGU HAJIBU MAOMBI?

Roho Mtakatifu ni nani?.

Rudi Nyumbani

Print this post

MSINGI WA NYUMBA YA MUNGU, NI JINA LA MUNGU.

Kamwe hatuwezi kuitenganisha nyumba ya MUNGU na JINA LAKE.. Vitu hivi viwili vinakwenda pamoja DAIMA!!!..

Lakini nyumba ya Mungu inapogeuzwa na kuwa  nyumba ya Jina la Mchungaji, au jina la Nabii, au inakuwa nyumba ya Maji ya Upako, au mafuta ya Upako, au chumvi ya Upako..nyumba  hiyo inakuwa si nyumba tena ya Mungu bali inakuwa ni pango la wanyang’anyi kulingana na biblia.

Yeremia 7:11 “Je! Nyumba hii, IITWAYO KWA JINA LANGU, imekuwa pango la wanyang’anyi machoni penu? Angalieni, mimi, naam, mimi, nimeliona jambo hili, asema Bwana”.

Tunapoacha kulinyanyua jina la BWANA YESU ndani ya nyumba yake, na badala yake tunalinyanyua jina la Nabii, au Mchungaji, au Mtume, au mtu Fulani ndani ya kanisa, hapo MUNGU tunayemtamani hayupo!.

Tunapoliondoa jina la BWANA YESU ndani ya Kanisa, na kuanza kutumia mafuta ya upako kila wakati kama njia mbadala!…hapo tumemwondoa MUNGU kabisa na tumemweka mungu mwingine ambaye ni shetani..tunapoliondoa jina la YESU na kutumia chumvi au udongo kama mbadala wake, kwa kila changamoto inayouja mbele yetu…hapo MUNGU hayupo, bali tupo wenyewe!!.

Tunapoacha kuomba kwa jina la BWANA YESU na kuanza kuziomba sanamu..hayo ni machukizo makubwa..

Yeremia 7:30 “Maana wana wa Yuda wametenda yaliyo maovu machoni pangu, asema Bwana; wameweka machukizo yao NDANI YA NYUMBA HIYO, IITWAYO KWA JINA LANGU, hata kuitia unajisi”.

Kama Mkristo au Mhubiri kamwe usilitenganishe jina la BWANA YESU na NYUMBA YAKE!.. Nyumba yake imekusudiwa kukaa jina lake humo MILELE.. Hakuna wakati ambapo JINA LA YESU, Litaisha muda wa matumizi yake ndani ya KANISA.. Hicho kipindi hakipo!.

Zama hizi za siku za mwisho shetani amenyanyua uongo mkubwa sana, kuwa ZAMA ZA JINA LA YESU ZIMEPITA! Hivyo sasa jina la YESU halina nguvu tena wala hatulitumii tena.. Ndugu fahamu kuwa huo ni uongo wa adui asilimia zote, jina la YESU limekusudiwa kutajwa na kutumika ndani ya NYUMBA YAKE DAIMA..

2Nyakati 7:16 “Maana sasa nimeichagua nyumba hii na kuitakasa, ILI KWAMBA JINA LANGU LIPATE KUWAKO HUKO MILELE; yatakuwako na macho yangu, na moyo wangu daima”

Na tena Macho ya Mungu na Moyo wake upo katika Nyumba ile ambayo ndani yake LINAKAA JINA LAKE na si jina la Mtu au kitu. Na tena maandiko yanasema hakuna jina lingine tulilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo isipokuwa hilo jina la YESU.

Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”.

Na zaidi sana yanasema,  lolote lile tufanyalo liwe kwa tendo au kwa Neno tufanye yote kwa jina la BWANA YESU.

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye”.

Hivyo kwa hitimisho ni kuwa JINA LA YESU ndio MSINGI WA KANISA la kweli la MUNGU.. Mahali pasipotajwa wala kutumika jina hilo, mahali hapo hapana MUNGU wa mbingu na nchi bali pana roho nyingine, ambayo ni ya Adui shetani.

Mistari mingine inayozidi kuthibitisha kuwa nyumba ya MUNGU imekusudiwa kuwekwa jina lake milele ni kama ifuatayo.. 2Samweli 7:13, 1Wafalme 5:5, 1Wafalme 8:18-19, 1Wafalme 9:7, Yeremia 7:10-14, Yeremia 32:34 na Yeremia 34:15.

Je! Umempokea YESU kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako?..fahamu kuwa tunaishi siku za mwisho za kurudi kwake mwana wa Adamu, na hukumu ya mwisho ipo karibu.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx1

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

ORODHA YA MITUME.

Je Mungu anaketi katika giza? (1Wafalme 8:12)

Nitamjuaje nabii wa Uongo?

Rudi Nyumbani

Print this post

Kigutu ni nani? (Marko 9:43)

Swali: “Kigutu” ni mtu wa namna gani kama tunavyosoma katika Marko 9:43?


Jibu: Turejee,

Marko 9:43  “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima U KIGUTU, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;

44  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]”

“Kigutu” ni mtu aliyekatwa mkono au aliyekatika mkono, tazama picha juu.

Biblia inatufundisha kuwa kiungo chetu kimoja kikitukosesha tukiondoa ili kisitupeleke katika jehanamu ya moto.

Sasa ni kweli kiungo kinaweza kuwa tabia, au marafiki, au vitu vya kimwili ambavyo vimejiungamanisha na mtu kiasi kwamba vinamkosesha katika Imani. Lakini pia biblia iliposema kiungo, imemaanisha pia kiungo kama kiungo, ikiwa na maana kwamba kama ni mkono ndio unakukosesha basi uondoe!, kama mkono wako umezoea kuiba, baada ya kutubu!, basi uondoe! Na hautaiba tena.

Kama ni jicho pia liondoe, na viungo vingine vyote… Na sababu ya Bwana kusema hivyo ni ili mtu aokoke na ziwa la moto, ambao kule kuna funza wasiokufa!, na moto wa kule hauzimiki, na wote wanaoshuka huko moshi wa maumivu yao unapanda juu milele na milele.

Ufunuo 14:10 “yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; NAYE ATATESWA KWA MOTO NA KIBERITI MBELE YA MALAIKA WATAKATIFU, NA MBELE ZA MWANA-KONDOO

11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake”.

Kwa upana juu ya viungo vinavyokosesha fungua hapa >>YESU alimaanisha nini aliposema “mkono wako ukikukosesha ukate?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Nini tofauti kati ya moyo na roho?

Bwana alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto”

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

Kulingana na 1Wakorintho 3:10-15, kama inavyosema..ni kwa namna gani kazi ya mtu itateketea, na kupimwa kwa moto?”

IFAHAMU FAIDA YA KUMKIRI KRISTO UKIWA HAPA DUNIANI.

Rudi nyumbani

Print this post

Kwanini tarehe ya pasaka inabadilika kila mwaka?

(Maswali yahusuyo pasaka)

Swali: Je kwanini tarehe ya pasaka inabadilika kila mwaka, kwamfano mwaka 2023 pasaka ilikuwa ni Aprili 13, lakini mwaka huu 2024 ni Marchi 31, na inategemewa kubadilika tena katika mwaka ujao na miaka yote inayokuja, kwanini iwe hivyo, wakati Krismasi ni tarehe ile ile 25 miaka yote?


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kujua kuwa pasaka ni moja ya sikukuu 7 za wayahudi, na inasheherekewa na wayahudi katika kila terehe 14 ya mwezi wao wa Kwanza, ambapo mwezi wao wa kwanza unaangukia katikati ya mwezi Machi na Aprili kwa kalenda tunayoitumia sisi.

Lakini kuhusiana na kwanini tarehe za pasaka zinabadilika kila mwaka kwa upande wa wakristo, ni kutokana na MWONEKANO WA MWEZI.

Mwezi unapozuka mzima (yaani angavu/full moon) basi jumapili inayofuata ndiyo inayosherekewa na wakristo wengi kama jumapili ya pasaka.

Kuna miaka ambapo “mwezi mwangavu” unawahi kuchomoza na kuna miaka unachelewa. Ikiwa na maana kuwa kama mwezi mwangavu  utaonekana jumatano basi jumapili inayofuata itakuwa jumapili ya pasaka, ambayo itakuwa ni baada ya siku nne,  Kwamfano kwa mwaka 2023 mwezi mwangavu ulionekana jumatano ya Tarehe 5 Aprili, hivyo jumapili iliyofuata ya tarehe 9 ndio ikawa jumapili ya pasaka.

Lakini kwa mwaka 2024, Mwezi mwangavu umewahi kuonekana, kwani umeonekana Jumatatu ya tarehe 25 Machi, hivyo jumapili inayofuata ya tarehe 31 Machi, ndio itakayokuwa jumapili ya pasaka.

Lakini pia kwa mwaka 2025, Mwezi mwangavu unatarajiwa kuonekana jumapili ya tarehe 13 Aprili, hivyo jumapili itakayofuata ya tarehe 20 Aprili ndio itakayokuwa jumapili ya pasaka.

Kwahiyo hiyo ndio sababu kwanini tarehe hizo zinabadilika badilika kila mwaka, (ni kutokana na mwonekano wa mwezi).

Sasa kujua pasaka ni nini na kama wakristo ni halali kuiadhimisha fungua hapa >>PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA?

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana?

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

KRISIMASI (CHRISTMAS) NI NINI? JE IPO KATIKA BIBLIA?

Rudi nyumbani

Print this post

MIMI NIKO AMBAYE NIKO

Musa alipomwuliza Mungu kuhusu jina lake, alitarajia kuwa atapewa jina Fulani maalumu kama vile jina la miungu mingine yoyote ijulikanayo mfano wa Baali, au arishtoreth, n.k.

Lakini tunaona Mungu alimjibu kwa ujumla na kumwambia, wakikuuliza jina langu waambie kuwa MIMI NIKO AMBAYE NIKO

Kutoka 3:14 Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO;akasema,Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli;MIMI NIKO amenituma kwenu.

Sasa kama ukitazama biblia yako kwa chini utaona imeeleza kwa tafsiri nzuri zaidi hiyo sentensi. Akiwa na maana kuwa NITAKUWA KAMA NITAKAVYOKUWA.

Yaani mimi sina jina moja maalumu, lenye sifa Fulani. Bali nitatambulika pindi niwapo katika hilo tukio, au tatizo au haja hiyo jina langu. Na kweli ndivyo ilivyokuwa baada ya pale. Tunaona Farao alipogoma tu, kuwaruhusu wana Israeli kutoka Misri tena kwa adhabu ya kuwaongezea kazi, ndipo hapo Mungu akaanza kujifunua kwa majina yake. Akamwambia Musa, kwa jina langu Yehova nilikuwa sijajifunua, sasa nitakwenda kujifunua, kwa jina hilo,

Kutoka 6:1 Bwana akamwambia Musa, Sasa utaona nitakavyomtenda Farao; maana kwa mkono hodari atawapa ruhusa kwenda zao, na kwa mkono hodari atawafukuza katika nchi yake. 

2 Kisha Mungu akasema na Musa, akamwambia, Mimi ni YEHOVA; 

3 nami nilimtokea Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao. 

4 Tena nimelithibitisha agano langu nao, la kuwapa nchi ya Kanaani; nchi ya kukaa kwao hali ya ugeni. 

5 Na zaidi ya hayo, nimesikia kuugua kwao wana wa Israeli, ambao Wamisri wanawatumikisha, nami nimelikumbuka agano langu. 

6 Basi waambie wana wa Israeli, Mimi ni YEHOVA, nami nitawatoa ninyi mtoke chini ya mizigo ya Wamisri, nami nitawaokoa na utumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyoshwa, na kwa hukumu kubwa; 

7 nami nitawatwaeni kuwa watu wangu, nitakuwa Mungu kwenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ni YEHOVA, Mungu wenu, niwatoaye mtoke chini ya mizigo ya Wamisri. 

8 Nami nitawaleta hata nchi ile ambayo naliinua mkono wangu, niwape Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo; nitawapa iwe urithi wenu; Mimi ni YEHOVA

Umeona? Jina la Mungu lililowatoa wana wa Israeli Misri ni jina la Yehova. Na baada ya hapo tunaona sehemu mbalimbali akijifunua kwa majina mengine mengi, kama Yehova yire, Yehova Nisi, Yehova shama, Yehova shalom, Ebenezeri, n.k. nyakati za vita, za mahitaji, za huzuni n.k. Kulingana na jinsi alivyowasaidia watu wake, walipomlilia.

Na mwisho kabisa akajifunua kwa jina kuu la UKOMBOZI, ambalo ni YESU, lenye maana ya Yehova-mwokozi.  

Hii ni kufunua nini?

Yatupasa tumwelewe Mungu wetu sikuzote kama “NITAKUWA KAMA NITAKAVYOKUWA”. Hana mipaka ya kujifunua kwake kwetu, nyakati za mahitaji atajifunua, nyakati za raha atajifunua, nyakati za magumu atajifunua, mabondeni atajifunua tu kwako, milimani ataonekana tu, yeye ni vyote katika yote. Uwapo visiwani, uwapo jangwani, uendapo mbinguni, ushukapo mahali pa wafu utamwona tu Mungu wako. Hakuna mahali hatajidhihirisha kwako. Pindi tu umwaminipo. Huhitaji kuwa na hofu na wasiwasi na kumwekea mipaka kwamba kwenye jambo hili au hili hataweza kuwepo au kujidhihirisha.

Swali ni je! Umemwamini Mungu aliyejifunua kwako kama mwokozi? Yaani Kristo? Kumbuka, kabla hujasaidiwa kwingine kote na yeye , unahitaji kwanza uokolewe, kwasababu umepotea katika dhambi, na mshahara wa dhambi ni mauti. Leo hii ukimwamini Yesu atakupa ondoleo la dhambi zako, utakuwa na uzima wa milele. Na utaufurahia wokovu kwasababu utakuwa tayari umevukishwa kutoka mautini kwenda  uzimani. Kumbuka hizi ni siku za mwisho. Itakufaidia nini uachwe katika UNYAKUO, angali nafasi unayo leo.Geuka umfuate Kristo.

Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu maishani mwako, basi wasiliana na namba zetu chini kwa msaada bure wa kuokoka.

Ubarikiwe.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

JE! MUNGU NI NANI?

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

Rudi nyumbani

Print this post

Kulaumu/ Lawama ni nini kibiblia?

Je! wakristo tunalaumiwa?

JIBU: Ni mashtaka au maneno  Fulani yanayotolewa dhidi yako, yanayolenga kutoridhishwa na mwenendo, au maneno au tabia yako.

Tunaweza tukawa watoto wa Mungu, na bado siku ile ya mwisho tukalaumiwa na Mungu.  Utauliza ni kwa namna gani?

Ni kweli deni letu la mashtaka limeondolewa pale msalabani kwa Kifo cha Yesu Kristo. Na kwamba mtu anapomwamini tu Yesu Kristo haukumiwi, bali anaingia uzimani. Tafsiri yake ni kuwa hana lawama la hukumu ya jehanamu (Wakolosai 1:21-22)

Lakini, kumbuka wewe “unahesabiwa” kuwa mwenye haki. Lakini kiuhalisia “huna haki ndani yako”. Yaani kwa asili wewe huna kitu chochote kizuri ndani yako mbele za Mungu, na kimsingi huo sio mpango Mungu aliokusudia kwa mwamini. Mungu anataka amwokoe mtu wake, na wakati huo huo awe mkamilifu kama yeye.

Ndio hapo hatupaswi kuichukulia NEEMA ya Mungu kama fursa ya sisi kupumzika katika dhambi, au kupuuzia matendo ya haki. Au kutokuonyesha bidii yoyote ya Kufanana na Kristo.

Maandiko yanasema watu wengi wataonekana kuwa na lawama, mbele za Kristo, kwa kushindwa tu kurekebisha baadha ya mienendo yao, walipokuwa hapa duniani.

Kwa mfano maandiko haya yanaeleza baadhi ya mienendo, hiyo; moja wapo ni  kukaa katika  Mashindano, au manung’uniko ndani ya wokovu hupelekea utumishi wako,kulaumiwa .

Wafilipi 2:14  “Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,  mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu”

Vilevile kutofikia upendo  na  Utakatifu, ni zao la lawama.

1Wathesalonike 3:12  Bwana na awaongeze na KUWAZIDISHA KATIKA UPENDO, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;

13  apate kuifanya imara mioyo YENU IWE BILA LAWAMA KATIKA UTAKATIFU mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.

Tufanye nini ili tuweze kuepuka lawama, na tuwe na ujasiri, mbele za Kristo siku ile?

Ni kuitendea kazi neema ya Kristo maishani mwetu. Kwa kumtii yeye, na kumfuata kwa mioyo yetu yote, nguvu zetu zote, akili zetu zote na roho zetu zote, Ambayo inafuatana pia na bidii katika kujitenga na maovu, Ndipo itakuwa rahisi sisi kuyashinda,kwasababu ataiachilia nguvu yake ya ushindi itende kazi ndani yetu, na hivyo tutajikuta tunakaa mbali na mambo ya kulaumu.

1Wathesalonike 5:22  jitengeni na ubaya wa kila namna.

23  Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu MHIFADHIWE MWE KAMILI, BILA LAWAMA, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.

Hivyo ndugu uliyeokoka, tambua kuwa kila mmojawetu atatoa hesabu yake mbele za Mungu, siku ile. Hatuna budi sasa kuishi kama watu wanaotarajia TAJI bora, na sio watu wasio na mwelekeo wowote. Bwana asije akaona “neno ndani yetu”, mfano wa yale makanisa 7  tunayoyasoma katika Ufunuo 2&3, ambayo Yesu aliyapima akaona mapungufu. Hivyo tuishi kama watu wenye malengo, sio tu wa kukombolewa, bali pia wa kukamilishwa.

2Wakorintho 6:3  TUSIWE KWAZO LA NAMNA YO YOTE KATIKA JAMBO LO LOTE, ILI UTUMISHI WETU USILAUMIWE; 4  bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida;

5  katika mapigo, katika vifungo, katika fitina, katika taabu, katika kukesha, katika kufunga;

6  katika kuwa safi, katika elimu, katika uvumilivu, katika utu wema, katika Roho Mtakatifu, katika upendo usio unafiki;

7  katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu; kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto;

8  kwa utukufu na aibu; kwa kunenwa vibaya na kunenwa vema; kama wadanganyao, bali tu watu wa kweli.

Bwana akubariki.

Hivi ni baadhi ya vifungu vingine utakavyokutana na Neno hilo pia (1Timotheo 3:1-7, Luka 1:5-6)

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

Mtakatifu ni Nani?

HUDUMA YA MALAIKA WATAKATIFU.

MUNGU MWENYE HAKI.

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya mmoja alikufa kwaajili ya wote hivyo walikufa wote? (2Wakorintho 5:14)?

Swali: Biblia ina maana gani inaposema, Kristo alikufa kwaajili ya wote hivyo wote walikufa?..Je na sisi tumekufa kwasababu Kristo alikufa?


Jibu: Turejee,

2Wakoritho 5:14 “Maana, upendo wa Kristo watubidisha; maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja alikufa kwa ajili ya wote, BASI WALIKUFA WOTE”.

Bila shaka yoyote kuwa huyu mmoja alikufa kwaajili ya wote si mwingine Zaidi ya YESU KRISTO, MFALME MKUU, BWANA wa mabwana na MWAMBA WA DAIMA!.

Lakini swali ni je!.. Kwanini afe na wengine wote wawe wamekufa?

Ni muhimu kujua kuwa wanaozungumziwa hapo kuwa “WOTE WAMEKUFA” Si watu wa ulimwengu mzima, bali ni “WALE WALIOMWAMINI YEYE”. Hao ndio waliokufa pamoja naye, maana yake mtu aliyemwamini Mwokozi YESU na kubatizwa anakuwa amekufa katika utu wa kale wa dhambi na amefufuka katika utu upya.

Wakolosai 3:3 “Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu”.

Warumi 6:8 “LAKINI TUKIWA TULIKUFA PAMOJA NA KRISTO, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye;

9  tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena.

10  Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu.

11  VIVYO HIVYO NINYI NANYI JIHESABUNI KUWA WAFU KWA DHAMBI NA WALIO HAI KWA MUNGU KATIKA KRISTO YESU”.

Na hatua yote hii kwa ujumla pamoja na ubatizo wa Roho Mtakatifu ndio inayoitwa KUZALIWA MARA YA PILI. Maana yake mtu anakufa katika utu wa wa dhambi na kuzaliwa katika utu upya. Na neno la Mungu linatuonya kuwa mtu asipozaliwa mara ya pili hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

Yohana 3:5“Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.

6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.

7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.

Je na wewe umekufa kwa habari ya dhambi kwa kuzaliwa mara ya pili?.. Kama bado basi neema ya YESU bado ipo na inakuita, ingawa haitakuwa hivyo siku zote, utafika wakati mlango wa Neema utafungwa na tumekaribia sana huo wakati, hivyo amua leo kumkabidhi YESU maisha yako kabla huo wakati haujafika, kwamaana utakapofika haitawezekana kumsogelea tena mwokozi kwaajili ya wokovu.

Luka 13:23  “Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia,

24  Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25  Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

26  ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27  Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu”.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?

Yesu ni Mungu?, Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?

Je Farao alikufa kwenye maji pamoja na jeshi lake au alipona?

Rudi nyumbani

Print this post

FAHAMU SEHEMU NNE (4)  APANDWAPO MWAMINI.

Shalom.

Sisi kama waamini tunafananishwa na mche, au zao Fulani linalopandwa. Kwamfano ukisoma

Zaburi 1:1-3 Inasema..

1 Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. 

2 Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.

3 NAYE ATAKUWA KAMA MTI ULIOPANDWA KANDOKANDO YA VIJITO VYA MAJI, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.

Hii ni kufunua kuwa mtu yeyote mwenye haki (Aliyeokoka), huwa anapandwa mahali Fulani rohoni.

Sasa ni vema kufahamu maeneo Mungu aliyoyaruhusu/ aliyoyakusudia sisi tupandwe, na hii ni muhimu kujua ili tuwe na amani, kwasababu wakristo wengi wanapoona kwanini baadhi ya mambo yapo hivi, huishia kurudi nyuma, au wengine kukata tamaa kabisa, au wengine kupoa, na wengine kulegea legea. Lakini kwa kufahamu haya, nguvu mpya itakuja ndani yako.

Hizi ni sehemu nne (4), Ambazo sisi kama waamini tunapandwa.

1) TUTAPANDWA PALIPO NA  MAGUGU

Mathayo 13:24  Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;

25  lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

26  Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.

27  Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?

28  Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?

29  Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.

30  Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

Ukiendelea mbele mstari wa 36-43, utaona Yesu anatolea ufafanuzi, wa mstari huo akisema hizo mbegu njema ni wana wa Ufalme, na konde hilo ni ulimwengu, na magugu ni wana wa ibilisi. Hivyo vyote viwili vimeruhusiwa vimee katika shamba hilo hilo moja la Mungu. Vishiriki neema sawa sawa, lakini mwisho, ndio vitofautishwe.

Kufunua kuwa tumewekwa pamoja na waovu, kamwe hatutakaa tuwe sisi kama sisi tu duniani, na hivyo basi tuwe tayari kusongwa na shughuli zao mbaya, kuudhiwa nao wakati mwingine, tuwapo kazini, majumbani, mashuleni, na wakati mwingine hata makanisani, watakuwepo. Na kibaya zaidi tuwe tayari kuona wakibarikiwa kama sisi tu tubarikiwavyo, watapokea mema yote kama tu wewe, kwasababu mvua ileile inyweshayo kwako itawapata na wao.

 Lakini Bwana anataka nini?

Anataka tuwapo katika mazingira hayo ya watu waovu tusifikirie kujitenga, na kutafuta mahali petu wenyewe tuishi, Yesu alisema Baba siombi uwatoe ulimwenguni, bali uwalinde na Yule mwovu, Bwana atakata tuwapo katikati yao tuzae matunda ya haki, kama Danieli alivyokuwa Babeli kwa wapagani, kama Yusufu kwa Farao, kama Kristo kwa ulimwengu. Vivyo hivyo na wewe kwa mume/mke wako asiyeamini, kwa majirani zako wachawi, kwa wafanyakazi wenzako walevi. Angaza nuru yako usijifananishe na wao, wala usingoje siku utengwe nao, jambo hilo linaweza lisitokee. Hivyo weka mawazo yako mengi katika kuangaza Nuru kuliko kutengwa na waovu. Kwasababu ni mapenzi ya Mungu tuwepo miongoni mwao.

2) TUTAPANDWA KATIKATI YA MITI MINGINE MEMA.

Bwana Yesu alisema tena, mfano huu;

Luka 13:6  Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate.

7  Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu?

8  Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi;

9  nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate.

Tafakari huo mfano, Mtu huyu alikuwa na shamba la mizabibu tu! Lakini akajisikia moyoni mwake apande na mti mmoja wa TINI katikati ya shamba lake. Matokeo yake ni kwamba ule mtini ukagoma kuzaa. Baadaye  akataka kuukata. Akitufananisha na sisi. Upo wakati utapandwa katikati ya jamii nyingine ya watu. Na Mungu atatarajia uzae matunda yaleyale ya wokovu wako uliopokea mwanzo. Je! Utafanya hivyo au utalala?

Hili ni jambo ambalo linawaathiri waamini wengi, pale panapohama na kwenda ugenini, mfano labda kasafiri kaenda mkoa mwingine, sasa kwasababu kule hakuna wapendwa wa namna yake, basi anaamua kuwa vuguvugu hamzalii Mungu matunda yoyote, kwasababu kule  hawapo wakristo. Mwingine amesafiri nje ya nchi. Mbali sana na watu wenye imani ya Kristo. Kwasababu yupo kule anasema mimi nipo peke yangu, siwezi kufanya lolote la Kristo. Ndugu usifikiri hivyo, Bwana anakutaka uzae matunda sawasawa, bila kuangalia ni wewe tu peke yako upo hapo. Kama ni kuwashuhudia wengine habari njema, wewe fanya. Timiza wajibu wako, usiangalie kundi au dhehebu, au jamii nyingine ya waamini waonaokuzunguka. Wewe timiza wajibu wako hivyo hivyo. Bwana akuone unazaa. Kwasababu kwa namna moja au nyingine hatuwezi kuyaepuka mazingira mapya, ambayo tutajikuta tupo sisi tu wenyewe. Tufanye nini? Kumbuka tu mtini ulio katikati ya mizeituni. Usiwe mlegevu.

3) TUNAPANDWA  JUU YA MITI MINGINE.

Tofauti na sehemu mbili za kwanza, ambazo ni katikati ya magugu, na katikati ya miti mingine. Lakini pia tunapandwa juu ya miti mingine. Hii ikiwa na maana, “tunapachikwa” juu ya mti uliokatwa. Wana wa Israeli, walifananishwa na mzeituni halisi, na sisi mataifa mizeituni mwitu. Hivyo wao walipoikataa neema, basi wakakatwa,tukapachikwa sisi, neema ikatufikia pia.

Warumi 11:17  Lakini iwapo matawi mengine yamekatwa, na wewe mzeituni mwitu ulipandikizwa kati yao, ukawa mshirika wa shina la mzeituni na unono wake,

18  usijisifu juu ya matawi yale; au ikiwa wajisifu, si wewe ulichukuaye shina, bali ni shina likuchukualo wewe

Na hivyo hapa tulipo tumepachikwa juu ya shina lingine. Na hivyo yatupasa tuwe makini, na kuuchukulia wokovu wetu kwa kumaanisha  sana, kwasababu na sisi tusiposimaa tutakatwa. Mhubiri mmoja wa Injili wa kimataifa aliyejulikana kwa jina la Reignhard Bonnkey, mwanzoni mwa huduma yake, Mungu alimwambia nenda kanitumikie, yeye akawa anasua-sua, Mungu akamwambia neema hii niliyokupa alipewa mwingine akaikataa, na hivyo itaondoka kwako na kwenda kwa mwingine usipotii. Aliposikia vile alikubali kutii kwa moyo wote, akaenda kuhubiri injili. Kuonyesha kuwa sisi ni wa kupachikwa, sio shina. Tuipokee neema kwa kuogopa na kutetemeka (Wafilipi 2:12). Usiwe mkristo vuguvugu, tumia muda wako vema, mzalie Mungu matunda. Kwasababu ulipachikwa tu, kwa kosa la mwingine.

4) TUNAPANDWA KWENYE UDONGO ULIORUTUBISHWA SANA.

Fuatilia habari hii,

Marko 11:12  “Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa.

13  Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.

14  Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia”

Kama tunavyoifahamu hiyo habari asubuhi yake Bwana Yesu alipopita karibu na njia hiyo, ule mti ulionekana umekauka kabisa kabisa. Lakini swali la kujiuliza ni kwanini aulaani, wakati haukuwa msimu wake wa kutoa matunda? Mbona ni kama ameuonea tu?

Ukweli ni kwamba Yesu aliona mti ule kwa mazingira uliokuwepo ulistahili kuwa na matunda hata kabla ya msimu. Kwa namna gani, chukulia mfano wa mazao ambayo yanastawishwa  kwa kilimo cha kisasa, mfano “banda kitalu”(green house), kulingana na matunzo yake, huwa yanastawi kwa haraka na kuzaa ndani ya muda mfupi. Kwasababu yamerutubishwa sana, kwa madawa na mbolea na kuwekewa mazingira rafiki mbali na wadudu waharibifu, mfano wa kuku wa kisasa, ndani ya wiki 6 wamekomaa, lakini matunzo yao hayawezi kama ya wale kuku wa kienyeji ambao wanaachwa wakajitafutie.

Sasa fikiri kama muda wote huo unapita halafu hawazai/hawakui, wanafanana na wale wa kienyeje, ni nini watarajie? Kama sio kuondolewa.

Ndivyo ilivyo kwetu sisi, tunapookoka, muda huo huo tunapokea ROHO MTAKATIFU. Huyu ndiye anayetupa uwezo na nguvu, ya kumshuhudia, na kuzaa matunda ya haki. Hivyo hatuhitaji tena kusubiri mpaka miaka Fulani ipite kama watu wa zamani, ambao walikuwa bado hawajakaliwa na Roho. Bali wakati huo huo tunapookoka na sisi tunawafanya wengine kuwa wanafunzi.

Hatupaswi kujiona sisi ni wachanga kiroho, au watoto, Bwana atakuja ghafla akikosa matunda atatuondoa, na sisi tutabakia kudhani wakati ulikuwa bado.

Hivyo ndugu, fahamu kabisa tayari tumesharutubishwa, usingoje wakati Fulani ufike, hapo hapo fanya jambo kwa Bwana, waeleze wengine habari ya wokovu wamjue Mungu. Wataokoka, usihofu kiwango chako cha kujua maandiko, anayewashawishi watu ni Mungu na sio wewe. Hivyo hubiri kwa ujasiri na Mungu atakuwa na wewe.

Bwana akubariki.

Kwa kufahamu sehemu hizo kuu nne (4), itoshe kutukumbusha mwenendo wetu hapa duniani, uzidi kuwa katika uvumilivu, hofu, wajibu na bidii. Ili tusijikwae, au kufa moyo.

Maran Atha.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU

SIRI YA KUASI KATIKA KANISA LA MUNGU.

JE! WEWE NI MBEGU HALISI YA KRISTO?

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

Rudi nyumbani

Print this post