Kigutu ni nani? (Marko 9:43)

by Admin | 27 March 2024 08:46 am03

Swali: “Kigutu” ni mtu wa namna gani kama tunavyosoma katika Marko 9:43?


Jibu: Turejee,

Marko 9:43  “Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima U KIGUTU, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;

44  ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.]”

“Kigutu” ni mtu aliyekatwa mkono au aliyekatika mkono, tazama picha juu.

Biblia inatufundisha kuwa kiungo chetu kimoja kikitukosesha tukiondoa ili kisitupeleke katika jehanamu ya moto.

Sasa ni kweli kiungo kinaweza kuwa tabia, au marafiki, au vitu vya kimwili ambavyo vimejiungamanisha na mtu kiasi kwamba vinamkosesha katika Imani. Lakini pia biblia iliposema kiungo, imemaanisha pia kiungo kama kiungo, ikiwa na maana kwamba kama ni mkono ndio unakukosesha basi uondoe!, kama mkono wako umezoea kuiba, baada ya kutubu!, basi uondoe! Na hautaiba tena.

Kama ni jicho pia liondoe, na viungo vingine vyote… Na sababu ya Bwana kusema hivyo ni ili mtu aokoke na ziwa la moto, ambao kule kuna funza wasiokufa!, na moto wa kule hauzimiki, na wote wanaoshuka huko moshi wa maumivu yao unapanda juu milele na milele.

Ufunuo 14:10 “yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; NAYE ATATESWA KWA MOTO NA KIBERITI MBELE YA MALAIKA WATAKATIFU, NA MBELE ZA MWANA-KONDOO

11 Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake”.

Kwa upana juu ya viungo vinavyokosesha fungua hapa >>YESU alimaanisha nini aliposema “mkono wako ukikukosesha ukate?

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mafundisho mengine:

Nini tofauti kati ya moyo na roho?

Bwana alimaanisha nini kusema “kila mtu atatiwa chumvi kwa moto”

MADHARA YA KUKOSA MAJI YA UZIMA BAADA YA KIFO.

Kulingana na 1Wakorintho 3:10-15, kama inavyosema..ni kwa namna gani kazi ya mtu itateketea, na kupimwa kwa moto?”

IFAHAMU FAIDA YA KUMKIRI KRISTO UKIWA HAPA DUNIANI.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2024/03/27/kigutu-ni-nani-marko-943/