Huyu FUNZA ni KUMBUKUMBU ZENYE MAJUTO. Hizi kumbukumbu kila mmoja atakayekuwepo kuzimu, zitamla, kila mmoja atakuwa anajutia maisha yake aliyoishi duniani, atakumbuka kuanzia siku ile alipokuwa mdogo anahubiriwa injili na kuipuuzia, atakumbuka siku aliyokuwa anadhihaki kazi ya Mungu, atakumbuka siku alizokuwa anafanya uasherati huku Roho wa Mungu akimwonya kwamba hicho kitu anachokifanya ni dhambi lakini hakutaka kusikia, atakumbuka siku aliyokuwa anasoma mahubirini na kuyapuuzia,
Atakumbuka muda aliokuwa anakawia kutubu mpaka kifo kilipomkuta kwa ghafla, atasema imekuwaje kuwaje nimefika hapa muda ambao bado?, yale majivuno yangu yananisaidia nini hapa?, ule uzuri wangu uko wapi tena?, zile pesa zangu mbona haziji kunitetea huku,.wale rafiki zangu niliokuwa nafanya nao anasa kumbe walinidanganya,..Ni majuto yasiyoelezeka utakapogundua kuwa wewe ni UZAO wa NYOKA, na ulidanganywa na shetani roho yako inakwenda kuteketezwa. UTALIWA NA HAYO MAWAZO kama vile FUNZA atafunavyo mzoga.