Musa aliua lakini bado Mungu alimchangua kuwaongoza wana wa Israeli, je! Mungu anaruhusu mauaji?

Musa aliua lakini bado Mungu alimchangua kuwaongoza wana wa Israeli, je! Mungu anaruhusu mauaji?

JIBU: Kumbuka Musa alipokuwa Misri alikuwa bado hajamjua Mungu wa Yakobo, alikuwa ni mpagani tu akiabudu miungu ya kimisri kama wamisri wengine, hajasafishwa bado matendo yake ya kipagani,.Na siku alipojigundua kuwa yeye ni mwebrania, ndipo akajaribu kutaka kuwaokoa ndugu zake (wana wa israeli) kwa njia zake za kisiasa na kiburi cha ujuzi wa kimisri aliokuwa ameupata katika jumba la Farao, lakini Mungu hatendi kazi hivyo ndio maana tunaona Mungu alimpeleka kwanza jangwani kumnyenyekeza kwa muda wa miaka 40, Na aliporudi tunaona hakuua tena alikuwa mtu mwingine, biblia inasema Musa alikuja kuwa mtu MPOLE kuliko watu wote DUNIANI

Hesabu 13:3″ Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi”.

 Unaona Mungu hafanyi kazi na watu wenye kiburi na WAUAJI,Kwahiyo Mungu alianza kutembea na Musa baada ya ile miaka 40 lakini kabla ya hapo Musa alikuwa anajiamulia mambo yake mwenyewe alikuwa ni hodari katika maneno biblia inasema (matendo 7:22 “Musa akafundishwa hekima yote ya Wamisri, akawa hodari wa maneno na matendo”), lakini baada ya kunyenyekezwa tunaona akimwambia Mungu yeye sio mnenaji

Kutoka 4:10 ″Musa akamwambia Bwana Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.”

 Kadhalika na sisi pia Mungu hafanyi kazi na watu wenye kiburi tunaweza tukawa tumeitwa vizuri tu!, lakini ujuzi wetu, elimu zetu, uhodari wetu ukawa kikwazo kikubwa mbele za Mungu…Tunapaswa tutupe vyote tuende mbele zake sisi kama sisi, ndipo atutumie. 

Yakobo 4: 6 Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu. 

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


JE! MUNGU ANASABABISHA AJALI, KWAMFANO AJALI YA KIVUKO CHA MV NYERERE KUZAMA?

TOFAUTI KATI YA MYUNANI, MFARISAYO NA MSADUKAYO IPO WAPI?

UTAJI ULIOKUWA JUU YA USO WA MUSA.

KAMA MHUBIRI NI WOKOVU UPI UNAUPELEKA KWA WATU?

RACA


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments