Je! Mungu anasababisha ajali au Majanga?

Je! Mungu anasababisha ajali au Majanga?

SWALI: Je! Mungu anasababisha ajali au majanga, kwamfano ajali ya kivuko cha MV Nyerere kuzama?


JIBU: Mungu hasababishi ajali yoyote ile, japo Mungu anaweza akamwadhibu mtu kwa makosa yake. Shetani ndiye mwenye lengo siku zote la kuangamiza hata wakati ambapo mtu hana makosa, kama alivyofanya kwa Ayubu, kwasababu biblia inasema yeye alikuwa ni muuaji tangu mwanzo.(Yohana 8:44).

Asilimia kubwa ya ajali na majanga yanaletwa na shetani. Na pia biblia inasema yapo majanga mengine yanaletwa na Mungu mwenyewe, na mpaka imefikia hivyo ujue ni adhabu kutokana na makosa ya watu wenyewe, na pia Bwana anasema huwa hafanyi jambo lolote bila kuwafunuliwa hao watumishi wake manabii, kuwaonya kama tunavyoona alivyofanya kwa watu wa Ninawi.

Leo hii mtu anamuudhi Mungu labda ni muuaji, lakini kabla Mungu hajamwadhibu atamwonya pengine kwa kumtumia Mtumishi wa Mungu au kwa kusikia mahubiri, na akajua kabisa Mungu anamwonya atubu utakuta pengine alisikia Neno likisema “Uaye kwa upanga, atauawa kwa upanga”..

Lakini yeye akapuuzia na kuendelea na tabia yake ya kuuiba na kuua watu pasipo hatia.. Sasa mtu kama huyo inatokea mazingira labda siku moja amekutana na kundi la wanyang’anyi usiku, na kwa bahati mbaya wakamvamia na kumchoma kisu, kisha na kufa..Sasa kwa nje unaweza ukasema ni shetani lakini sio shetani bali ni Mungu mwenyewe kamlipizia kisasi juu yake.

Hivyo zipo ajali zinazotoka kwa Mungu mwenyewe. Kadhalika zipo pia zinazotengenezwa na shetani, ambazo hizo ndio nyingi kuliko zile zinazotoka kwa Mungu.

Ubarikiwe.

Ikiwa utahitaji msaada zaidi ya mafundisho ya kila siku/maombezi/ubatizo/ushauri basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi +255693036618/+2557890001312

Au jiunge na makundi yetu ya mafundisho ya kila siku kwa kwa njia ya Whatsapp kwa kubofya hapa >>>> WHATSAPP GROUP


Mada zinazoendana:

NI NANI ANAYETAWALA DUNIA KATI YA MUNGU NA SHETANI?

KWANINI MUNGU ANARUHUSU WATU WAPITIE SHIDA?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

MPENDEZE MUNGU ZAIDI.

Jehanamu ni nini?

RAHABU.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments