Title October 2019

Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani?

Huu ni mfululizo wa maswali machache yamhusuyo Bwana Yesu, ambayo yamekuwa yakiulizwa na watu wengi hususani wale wasio Wakristo, ambao hawamjui Bwana Yesu kwa mapana, na Baadhi ya maswali hayo ni pamoja na 1)Bwana Yesu alizaliwa wapi? 2) Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani? 3) Bwana Yesu alikuwa dini gani  4) Yesu alizikwa wapi? 5) Je Yesu aliteswa msalabani au juu ya mti ? n.k 

Maswali yote na mengine mengi tutayapata majibu yake hapa, hivyo karibu!

Tukianza na swali la kwanza linalouliza

1) Bwana Yesu alizaliwa wapi?

Swali la Yesu alizaliwa wapi..Jibu lake lipo wazi katika Biblia kwamba alizaliwa huko Bethlehemu ya Uyahudi…Bethlehemu ulikuwa ni mji aliozaliwa Mfalme Daudi, uliokuwepo maili chache sana kutoka mji wa Yerusalemu…Hivyo Kutokana na Daudi kuupendeza sana moyo wa Mungu, Mungu aliubariki mji wake aliozaliwa na kuufanya kuwa mji atakaokuja kuzaliwa Masihi yaani Yesu Kristo.

Mathayo 2:1 ‘Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu’

Sasa ingawa Bwana Yesu alizaliwa Bethlehemu lakini maisha yake yote hakuishi huko Bethlehemu bali aliishi mji mwingine uliokuwepo mbali sana unaoitwa Nazareti, hivyo alijulikana sana kama Yesu Mnazareti kuliko Mbethlehemu.

2) Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani?

Biblia haijaeleza Bwana Yesu alizaliwa mwaka gani, lakini tukisoma hiyo Mathayo 2:1 hapo juu inasema…Yesu alizaliwa zamani za Mfalme Herode..Hivyo inaaminika na wanathelojia wengi kuwa Kristo alizaliwa kati ya mwaka 4-6 KK. Lakini katika Kalenda yetu tunafahamu kuwa umeshapita zaidi ya Miaka elfu 2 tangu Kristo awepo duniani…Hivyo ni kusema kwamba Kristo alizaliwa miaka 2019 iliyopita, kama leo hii ni mwaka 2019..

3) Bwana Yesu alikuwa dini gani 

Ahadi ya kuzaliwa Mwokozi walipewa wayahudi (yaani Waisraeli) Lakini ahadi hiyo haikuishia kuwa Baraka kwa Waisraeli tu peke yao, bali kwa watu wote hata wa Mataifa kwasababu maandiko yanasema..Mataifa yote ulimwenguni yatamtumainia, na yeye atakuwa wokovu kwa mataifa yote…Lakini sharti kwanza Wokovu huo uanze kwa Wayahudi ambao ndio walioahidiwa kwanza na kisha uje kwa watu wa mataifa mengine.

Hivyo wayahudi walikuwa na Dini yao ya kiyahudi ambayo ndio ile waliyopewa na Musa, ya kushika sheria na Torati..Lakini Ahadi ya ujio wa Masihi ni kurekebisha pale palipopunguka..Hivyo alipozaliwa alizaliwa katika dini ya kiyahudi, lakini kwa uweza wa Roho aliitimiliza torati pale palipopunguka na pale palipoeleweka vibaya…Ndio maana akasema katika 

Mathayo 5:17 ‘Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza’. 

Hivyo dini ya kiyahudi Bwana Yesu alikuja kuitimiliza kwa kuwaambia amchukiaye ndugu yake ni sawa na muuaji, hivyo chuki haitakiwi kabisa, amtazamaye mwanamke kwa kumtamani tayari kashazini naye hivyo kutamani hakutakiwi kabisa licha tu ya kuua,..Hiyo ndiyo ilikuwa dini  Bwana Yesu aliyokuwa nayo na ndio aliyokuwa anahubiri watu wawe nayo…Hakuhibiri Dini ya kiyahudi kwamba watu wawe wayahudi au wajina fulani…Bali alihubiri watu wabadilike na kuwa wema, watakatifu wenye upendo n.k…hiyo ndio Dini ya Bwana Yesu..

Yakobo 1:26 ‘Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai.

27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa’.

Kwahiyo dini ni matendo sio Jina! au  kikundi fulani cha waabudio fulani..

4) Yesu alizikwa wapi?

Bwana Yesu alizikwa wapi? Jibu: alizikwa Yerusalemu, mji uliokuwepo karibu sana na mji aliozaliwa Bethlehemu…soma Luka 13:33 na Mathayo 27:60

5) Je Yesu aliteswa msalabani au juu ya mti?

Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa Msalaba unatengenezwa kwa mti, hivyo mahali popote kwenye biblia panaposema Bwana aliangikwa juu ya mti kama kwenye Wagalatia 3:13, basi fahamu kuwa inazungumzia msalaba kwasababu msalaba unatengenezwa kwa mti. Na msalaba ulikuwa unatengenezwa kwa vipande viwili vilivyokatana kama alama ya kujumlisha…na sio kipande kimoja kilichosimama wima kama inavyoaminika na ‘mashahidi wa Yehova’

Utamaduni wa kuwatundika Watu msalabani haukuanzia kwa Bwana Yesu bali ulikuwepo kabla yake, kwamba wahalifu waliokosa sana walikuwa wanauawa kwa kutundikwa msalabani vile vile kama Bwana Yesu alivyotundikwa, ndio maana utaona siku ile aliposulibiwa kulikuwepo pia kuna wengine wawili waliosulibiwa pamoja  naye..Kwahiyo Bwana Yesu aliteswa msalabani wenye mfano wa alama ya kujumlisha.

Kumbuka Bwana YESU alikufa kwaajili ya dhambi zako na zangu, alisulubiwa na kuteswa na alikufa na siku ya tatu akafufuka, naye hatakufa tena..sasa hivi tunavyozungumza yupo hai, na anakutazama wewe na mimi, ametuma Neno lake kutuponya..Hivyo kama hujampa maisha yako ni vyema ukafanya hivyo sasa kama unatamani kuishi milele..

Yeye atakupokea na kukusafisha dhambi zako zote bure! alisema 

Mathayo 11:28 ‘Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi’.

Je mzigo wako ni mzito? unasubiri nini usiende kuutua kwa Yesu sasa?

Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

Rudi Nyumbani

Print this post

KUVUNJA MAAGANO YA UKOO.

Unatafuta kujua namna ya kuvunja maagano ya ukoo?. Upo sehemu sahihi fuatilia somo hili hadi mwisho kabisa utafahamu njia rahisi ya kuondokana na hizo laana milele zisikurudie tena.

Biblia inasema:

Yohana 8:36  “Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”

Unaweza ukajiuliza ni kwanini pale msalabani Bwana Yesu alisema neno moja tu IMEKWISHA!!(Yohana 19:30), Na sio YAMEKWISHA?…Ukilifahamu hilo utajua ndio sababu kwanini huwezi kuona maneno kama laana za ukoo, laana za kifamilia, laana za mababu, laana za mapepo, kifungo vya kikabila n.k katika biblia..kwasababu hayo yote yamejumuishwa katika hicho kitu kimoja kilichokwisha pale msalabani  nacho si kingine Zaidi ya DHAMBI.

Dhambi ndio mzizi wa matatizo imefananishwa na  ugonjwa wa ukimwi, Ambao vijidudu vyake vinafanya kazi  moja tu nayo ni kwenda kushambulia kinga ya mwili  basi, havileti madhara mengine yoyote mwilini, havisababishi kutokwa na vidondo, havisababishi kutapika, havisababisha kuugua, havisababishi kukohoa La!..Lakini vinaua kinga ya mwili, sasa ile kinga ikishakufa, ina maana kuwa mwili hauna ulinzi tena, hapo ndipo kila aina ya ugonjwa unapata nafasi ya kuingia, mara malaria, mara Tb, mara mkanda wa jeshi, mara homa ya ini n.k. n.k. Na hivyo ndivyo mwisho wa siku vinakwenda kummaliza mtu…

Ogopa sana ugonjwa  mmoja  unaokwenda kushambulia kinga ya mwili kuliko magonjwa 99 yanayokwenda kushambulia sehemu nyingine zote mwilini.

Sasa dhambi na yenyewe ndio inafanya kazi hiyo hiyo, Adamu na Hawa walipoasi pale Edeni, dhambi iliingia ndani yao, ikamaliza kinga yao yote ya ulinzi Mungu aliokuwa amewawekea pale Edeni, Na ghafla uuaji ukaingia, dhuluma ikaingia, magonjwa yakaanza, uchawi ukaanza, laana zikaingia, vita vikaingia, matabaka na matambiko yakajitokeza ndio maagano zote za ukoo zikatokea huko huko n.k. Na hili likawa ni tatizo lisilokuwa na tiba kwa vizazi na vizazi, kwa karne na karne..Dawa ya dhambi haikupatika kama vile dawa ya ukimwi usivyopatikana leo, kwa Zaidi ya maelfu ya miaka.

Lakini Bwana Yesu alipokuja miaka karibia 2000 iliyopita hakuja kushughulika na tawi Moja la dhambi labda tuseme maagano ya ukoo, au laana za kifamilia, hapana angefanya hivyo basi tatizo lote lisingeondoka, lakini alikuja kuung’oa mzizi wote wa DHAMBI, kiasi kwamba mfano mtu aking’olewa mzizi huo ndani yake basi hakuna vimelea vyovyote vya laana yoyote ile itakayomwandama.

Jambo ambalo watu wengi hawafahamu, ni kuwa wanadhani kwenda kuombewa au kufanyiwa maombi fulani ya muda mrefu labda tuseme ya kufunga, na kukaa milimani na kutumia masaa mengi kuomba na kukemea ndio kunaondoa laana na maagano ya ukoo au maagano ya kifamilia, wengine wanadhani kutoa sadaka fulani maalumu ndio kunaondoa maagano ya kiukoo hapana, mtu anaweza akafanya hivyo na bado hayo mambo yasiondoke ndani yake, kama ikiwa bado yupo nje ya wokovu.

Kama mtu hajakusudia kweli kuokoka, mambo hayo hayawezi kuondoka hata iweje, yataendelea kumfuata tu, lakini kama leo hii ukasema mimi na dhambi basi, nimeamua kujitwika msalaba wangu na kumfuata YESU popote atakapotaka mimi niende, sirudi nyuma tena, ukatubu kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako zote, kisha ukatii agizo la Ubatizo, ukaenda kubatizwa katika ubatizo wa kuzamishwa kwenye maji mengi, na Kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38, ili upate ondoleo la dhambi zako, na kuanzia huo wakati ukawa unaishi Maisha ya kama mkristo aliyeokoka, nataka nikuambie, sio tu maagano ya ukoo yatafutwa juu yako, bali pia hata na yale maagano mengine usiyoyajua ya kipepo yaliyokuwa juu yako yote hayo yatafutwa..

Usihangaike kwenda kuombewa huku na kule, ukifika kule kila mmoja atakuambia hichi, mwingine kile. Kumbuka Wokovu ni muujiza mkubwa sana ambao unatokana na neema ya Kristo tunaoupata bure bila kujisumbua wala kugharamia chochote, wewe ni kutii tu, hivyo pale ulipotubu basi jua vyote vimefutika,..Lakini kitu shetani anachokifanya ni kukutisha, kukufanya ujione kuwa bado upo chini ya maagano hayo, atakuletea hichi na kile, hapo unapaswa usimsikilize wewe sema tu maneno haya..

Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”

Atafanya hivyo kwa muda tu, lakini kwa jinsi unavyozidi kujifunza maneno ya Mungu na biblia, kwa bidii Zaidi ndivyo utakavyomfanya aende mbali na wewe Zaidi na mwishoni asikusumbue kabisa, kwasababu shetani huwa anamsumbua mtu na kumletea vitisho kutokana na ujinga wake, kutokana na uzembe wake wa kutokuzingatia kujifunza maandiko,..hivyo unapaswa ujifunze sana maandiko ili uweze kumshinda atakapokuletea majaribu yake.. Na ndio maana biblia inasema.

Yohana 8:32  “tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru”.

Na “KWELI” ni Neno la Mungu biblia inasema hivyo katika (Yohana 17:17)..Hivyo ukiwa ni mtu wa kujifunza na kuyatafakari Maneno ya Mungu kwa bidii shetani atakaa mbali na wewe sikuzote. Hiyo ndio njia pekee ya kuvunja maagano ya ukoo, ukiipata hiyo huhitaji kwenda kuombewa, wala kufanyiwa maombi yoyote ya ukombozi, lakini kama Maisha yako ya wokovu yapo mbali na Kristo halafu unatafuta njia mbadala ya kuondoa tatizo hilo, kumbuka hayo mambo yalishafanyika zamani sana, na yakashindikana..Hivyo na wewe pia usijaribu kuyarudia hayo..bali Mkaribishe leo YESU maishani mwako, awezaye kuondoa mzizi wote wa dhambi na laana zake zote. Na kukufanya kuwa kiumbe kipya. Na hakika atayavunja maagano yote ya ukoo, babu zako, na mababu zako waliyoingia na kuapa iwe ni katika afya, au mafanikio, au furaha vyovyote vile vitakwisha ndani yako.

Ubarikiwe sana.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Kwanini kuna watu wanafanyiwa deliverance (Maombi ya kufunguliwa), lakini baada ya muda wanarudiwa tena na hali ile ile sababu ni nini?

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

IPO NGUVU ITUVUTAYO KWA KRISTO, ITHAMINI!.

KWANINI MOTO NA UPEPO VINAWAKILISHA TABIA ZA MUNGU?

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! MUNGU NI NANI?

Je Mungu ni nani?

Neno “Mungu” linatokana na neno “Muumbaji” au “mtengenezaji”…Kwahiyo hata mtu akiumba gari yeye ni mungu wa hilo gari..

Hivyo kama gari limeumbwa na mtu, kadhalika kuna kitu kilichomuumba huyo mtu ambaye ni mungu kwa gari…na kitu hicho kilichomuumba mwanadamu ndio kinachoitwa “Mungu wa miungu”…Hakiwezi kuelezewa kwa undani kwasababu hata gari haliwezi kumwelewa mtu kazaliwa wapi, mwaka gani, na anaishije… hata lingefanyaje.

Kwahiyo huyo aliyemuumba mwanadamu ndiye anayeitwa Mungu, (zingatia ‘M’ inaanza kwa herufi kubwa na si ndogo). Huyo anakaa mahali pa kiroho mbali sana panapoitwa mbinguni. Anafanana na mwanadamu lakini si mwanadamu, anatabia kama za mwanadamu lakini si mwanadamu.

Kwasababu sisi wanadamu tunaishi kwa pumzi, kwa chakula, tunahitaji mwanga ili tuone, tunahitaji maji ili tuishi, lakini huyo Mungu yeye ana pua lakini hategemei pumzi, yeye ana macho lakini hategemei mwanga kuona, yeye anaishi lakini hategemei kula, kwasababu kila kitu kimeumbwa na yeye.

Kwahiyo hatuwezi kumwelezea Mungu kwa undani kwasababu ni kitu kilichotutengeneza sisi. Kama vile ilivyo ngumu roboti nililolitengeneza mimi kwa mfano wangu na sura yangu liwe na uwezo wa kujua asili yangu au mwanzo wangu au kunichambua kwa undani mimi ni nani? hata tu huo ufahamu haliwezi kuwa nao…Vivyo hivyo Mungu tukitafuta kumchambua tutakuwa tunapoteza muda, na ndio tutakuwa tunakwenda mbali naye na kuishia aidha kupotea au kukosa majibu kwasababu upeo wake ni wa mbali sana

Lakini pamoja na hayo hajatuumba sisi kama maroboti, sisi katuumba kama wanawe, ambao anatupenda na kutujali kwa namna isiyoelezeka. Na anataka tuishi katika haya maisha kwa kufuata sheria zake ili tupate faida na kufanikiwa, kwa kulitekeleza hilo alimtuma mwanawe wa pekee duniani ili kila amwaminiye asipotee bali apate uzima wa milele. Na huyo mwanawe ndiye Yesu Kristo tunayemfahamu…

Huyu Yesu Kristo pekee ndiye aliyekabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na duniani, hakuna mtu yeyote atakayeweza kumfikia Mungu Baba mbinguni pasipo kupitia kwa yeye (Yesu Kristo)

Yohana 6:44 “14.6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.”

Je unataka kwenda kumwona Baba mbinguni?. Kama ndio je umemwamini mwanawe mpendwa Yesu Kristo, na kutubu dhambi zako na kuoshwa kwa damu yake? kama ndio basi unalo tumaini la kumwona Mungu siku moja lakini kama hutamwamini na kuwa mtakatifu hutamwona kamwe.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”;

Bwana akubariki sana.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba 

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

YEZEBELI ALIKUWA NANI

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

Luka 12:47b“………Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.

Kila siku tunapolisikia Neno la Mungu tujue kabisa tunajiongezea deni mbele zake, kama vile biblia inavyosema Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu (Waebrania 4:12), inamaanisha kuwa pindi tu Neno la Mungu linapoingia ndani yetu linatazamiwa litoe matunda ya uhai, yaani lionyeshe mabadiliko ndani ya mtu, na pili watu wengine wabadilishwe kupitie Neno hilo hilo lililoingia ndani yetu.

Sasa kama inatokea leo hii tunalisikia Neno la Mungu, kisha hatulitendei kazi, tunasikia tu au tunasoma tu kama habari fulani ya kusisimua, tukitoka hapo, tunafikiria mambo mengine, tunaendelea na shughuli zetu kama kawaida, Kesho tena tunasoma vile vile kama habari fulani iliyojiri mpya, kisha baada ya hapo tunaendelea kuwa kama tulivyokuwa, Kesho kutwa nayo vivyo hivyo, tunasoma tunaondoka, siku zinakwenda, miezi inakwenda, miaka inakwenda, ukiangalia jumla ya mahubiri au mafundisho uliyosoma au kuyasikia hayahesabiki, na bado hakuna badiliko lolote ndani yako, leo hii tunaangalia kichwa cha somo ni kipi, tunasoma, tunapita, tunachukulia ni kawaida tu, tukidhani Mungu naye anachukulia hivyo kama sisi…..Ndugu Mungu anahesabu kila Neno lake linaloingia katika masikio yetu, kwasababu yeye mwenyewe anasema hakuna Neno lake linalokwenda bure bure (Isaya 55:11), ni lazima limrudishie majibu, na majibu hayo yatamrudia siku ile tutakaposimama katika kiti cha hukumu.

Biblia inasema kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi…

Mungu anatazamia hicho unachokisikia na mwingine akisikie kupitia wewe kwa ile karama Mungu aliyoiweka ndani yako, lakini unakihifadhi tu, ni sawa na mtu anayetupa chakula wakati wengine wanakufa na njaa, ni sawa na kufuru, hujui kuwa mahali fulani kuna mama ambaye ni mwabudu sanamu, na anafanya vile kwa kutokujua laiti angefahamu ukweli huo kutoka kwako angebadilika na kuwa shujaa wa Bwana, lakini kwa kuwa hana wa kumwelezea habari hizo anakufa katika sanamu na kwenda kuzimu..

Mahali fulani yupo kijana ambaye anadhani kwa kushika dini yake fulani tu ndio tiketi ya kwenda mbinguni, lakini hajui kuwa hata pamoja na dini yake aliyonayo anaweza kwenda kuzimu kwasababu njia pekee ya kufika mbinguni ni kwa YESU tu, lakini kwasababu hakuna wa kumuhubiria yeye anaendelea kujitahidi na dini yake na mwisho wa siku anakufa na kwenda kuzimu na mtu wa kumweleza ulikuwepo..

Sehemu nyingine mtu fulani amekata tamaa ya Maisha, pengine kwa magonjwa anataka kujinyonga, anasema hakuna tumaini tena la kuishi, lakini hajui kuwa tumaini pekee lipo kwa YESU kwake huyo hakuna mzigo wowote usiotua, lakini anaenda kuishia kujinyonga kwasababu hakukuwa mtu wa kumsaidia…Vivyo hivyo wapo wengi wanateswa katika hali nyingi kama hizo na shetani..ambao wanahitaji maneno machache tu yahusuyo habari za YESU, ili wabadilike, lakini sisi ambao tumeshiba tukiachilia mbali ya kuwahubiria na wengine, sisi wenyewe hatulitendei kazi hilo tunalolisikia kila siku..

Hebu leo mwambie mtu amhubirie mwingine anayepotea kuhusu habari za Yesu, utasikia anakwambia hana karama ya kuhubiri au hana karama ya kichungaji, lakini hebu aone mtoto wake anazama kwenye matumizi ya madawa ya kulevya uone kama hatamhubiria kila siku kwa masaa mengi kwa uchungu na kwa kuhuzunika..

Siku ile tutaficha wapi nyuso zetu..wakati wale wengine ambao wamekuwa waaminifu wanapoambiwa Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.(Mathayo 25:21)

Sisi tutaambiwa..

Mathayo 25:26 “Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;

27 basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.

28 Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi.

29 Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, na kuongezewa tele; lakini asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa.

30 Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.

Tunapaswa tusilizoelee Neno la Mungu,..Pale tunapolisikia tulitendee kazi, kwasababu utafika wakati ambao Bwana akitazama na asipoona matunda yoyote, basi tutakatwa na tukishakatwa ndio milele hivyo hakuna tumaini tena baada ya hapo…

Ndio maana biblia inatuambia..utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.

Wafilipi 2:13 “………utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.

13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.”

Kila siku tunapaswa tujitathimini, na tupige hatua moja mbele..

Maran Atha!.

Bwana akubariki sana.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali aua Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba 

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KITABU CHA UZIMA

https://wingulamashahidi.org/2018/07/04/5-swali-je-kuna-dhambi-kubwa-na-ndogo-na-kama-hakuna-je-mtu-aliyeua-na-aliyetukana-je-watapata-adhabu-sawa/

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

YONA: Mlango 1

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

Ukiona Mungu kakuahidi mambo mazuri huko mbeleni, fahamu kuwa kuna uwezekano wa kupitia mabaya kabla ya hayo mazuri kuja…Na ukiona Mungu kakuahidia kuwa atakufunika na kukulinda na kukuokoa ujue kuwa unaweza ukapitia kwanza hali ngumu karibia na kupotea…Wengi tunazipenda faraja, hususani zinazotoka kwa Mungu lakini hatujui kuwa “huwezi kufarijiwa kama hujapitia kukatishwa tamaa au msiba fulani”..Hiyo ndio nguvu ya faraja iliyopo…Kadhalika Mungu anapotupa maneno ya faraja tufahamu kuwa kuna kukatishwa tamaa kutakuja kabla ya hiyo faraja.

Kwamfano Bwana anaweza kumwambia mtu “nitakuwa na wewe, na nitakubariki na kukuokoa na kukuweka juu”…na wakati anakwambia hayo pengine haupo kwenye shida sana, au tabu sana…Sentensi hiyo ni nzuri na ya faraja, lakini pia kwa upande wa pili ni ya Huzuni…Kwasababu kabla ya Mungu kuwa na wewe ni lazima utapitia hali Fulani ya kuona kama umeachwa, kabla ya kupata hiyo raha aliyokuahidia ni lazima upitie shida kwanza ili raha iwe na maana, kabla ya kukuinua juu sana ni lazima atakushusha kwanza chini sana, na kabla ya kukuokoa ni lazima ataruhusu upotee au uingie kwanza matatizoni..vinginevyo wokovu hautakuwa wokovu kama hakuna kilichopotea.

Kwasababu hakuna kuokolewa bila kupotea kwanza, wala kufarijiwa bila huzuni, wala kuinuliwa juu bila kushushwa chini kwanza. Ndivyo ilivyokuwa kwa Ibrahimu, Ili apewe Taifa lake mwenyewe ilimpasa anyanganywe Taila la Asili yake…ilimpasa aiache nchi yake, na aondoke aende mahali hata asipopajua…Biblia inasema hivyo katika..

Waebrania 11:8 “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako.

9 Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile”

Hizo ndio gharama za kuambiwa “Nitakufanya kuwa Taifa kubwa”… Unafikiri ni jambo jepesi kutoka nchi uliyozaliwa na kuacha ndugu zako wote, na mashamba yako na mali zako na kwenda nchi nyingine maelfu ya maili mbali na kwenu ambayo hata huijui?…Hivyo Baraka za Ibrahimu kufanywa Taifa kubwa hazikuwa ni nyepesi nyepesi kama zinavyodhaniwa…Alinyanganywa urai wa Taifa lake na Mungu ili apewe urai wa Taifa lake binafsi na Mungu.

Yusufu naye baada ya Mungu kumwonesha maono makubwa kama yale kwamba ndugu zake watakuja kumsujudia, alifurahi na kujua ni jambo la kesho na kesho kutwa, kwamba hatapitia lolote, mambo yatakuwa mteremko, mpaka atakapokuwa mtu mzima Mungu atakuwa kamnyanyua tu lakini badala yake miaka michache baadaye alifungwa kwenye Taifa lingine, katika gereza la kifalme kwa kosa la uzalilishaji wa kijinsia na jaribio la ubakaji..Ilimpasa achafuliwe kwanza kabla ya kusafishika..hauwezi kunyanyuliwa bila kushushwa kwanza.

Kadhalika Musa naye kabla hajawa mungu kwa Farao kama biblia inavyosema katika (Kutoka 7:1) ilimbidi aache ufalme wote, na enzi yote na mali zake zote aondoke aende jangwani kukaa huko miaka 40 akishushwa na kunyenyekezwa na Mungu, mpaka kufikia kiwango cha kuwa mtu mpole kuliko watu wote duniani waliokuwa kipindi kile..Na baada ya kushushwa hivyo ndipo ukaja wakati wa kunyanyuliwa kwake ambapo Mungu alimweka juu ya Taifa zima la Israeli. Biblia inasema Musa alipewa wana wa Israeli wote wawe wake.

Waebrania 11:24 “Kwa imani Musa alipokuwa mtu mzima, akakataa kuitwa mwana wa binti Farao;

25 akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo;

26 akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.

27 Kwa imani akatoka Misri, asiogope ghadhabu ya mfalme; maana alistahimili kama amwonaye yeye asiyeonekana”.

Kwa mifano hiyo michache kati ya mingi, unaweza kuona kuwa ili unyanyuliwe huwezi kukwepa kushushwa chini..Kadhalika hata tunapomfuata Kristo, wengi wetu tumeweka shabaha na matumaini asilimia 100 katika Baraka za Mungu, kwasababu tu Mungu kaahidi kutubariki mashambani na mijini pindi tunapomfuata…..tunadhani pindi tu tunapomfuata Kristo basi mambo yetu hapo hapo tu yanaanza kukunyookea..Lakini tunapojikuta tunashuka chini katika hatua za awali ndio tunaanza kurudi nyuma na kulaani na kukufuru na kumwona Mungu ni mwongo.

Mambo hayaendi hivyo ndugu! Ulikuwa unafanya kazi za pombe haramu au kujiuza mwili wako na ulikuwa unapata pengine laki moja kwa siku kutokana na kazi hiyo, leo hii umeokoka na umeamua kuacha hiyo kazi, unategemea vipi uendelee kupata hiyo laki kwa siku kama ulivyokuwa unaipata?..Ni wazi kuwa huwezi kuipata hiyo tena kwasababu hiyo kazi umeacha,…hivyo kiuhalisia utapitia dhiki kwa kitambo Fulani kutokana na kwamba fedha uliyokuwa unaizalisha huipati tena, lakini pendo Kristo atakalokuwa amelimimina ndani yako litaifunika hiyo dhiki, hata kuona sio kitu….

Kitendo hicho cha kuacha hayo yote ndio KUJIKANA kwenyewe huko! na hivyo Mungu atakutengenezea chaneli nyingine ya kazi ambayo utaipata faida zaidi ya hizo kazi haramu ulizokuwa unazifanya, lakini hiyo inaweza isiwe leo au kesho, inaweza ikapita kipindi Fulani cha muda..kwasababu ni lazima Mungu akuweke chini ya madarasa yake ili Baraka za baadaye zisije zikakuharibu kama kwanza. Ndicho kilichomtokea Musa, ndicho kilichowatokea wana wa Israeli, ndicho kilichomtokea Yusufu na wengine wengi…

Bwana Yesu aliwaambia Mitume wake maneno yafuatayo..

Mathayo 19:27 “Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?

28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele”.

Unataka kubarikiwa na Kristo leo unahitaji kupata mara mia? Kama ni ndio basi unahitaji kuingia gharama!..kwasababu Baraka hiyo haiji bila kuingia gharama..

Na gharama yenyewe ni kuacha vyote vilivyo viovu? unaacha ulevi wako, uasherati wako, upo kwenye mahusiano ambayo ni ya kizinzi unaachana na huyo uliye naye sasa, ulikuwa na bar! Unaifunga bila kujishauri shauri, umemtapeli mtu mali yake unamrudishia yote bila kujali umebakiwa na shilingi ngapi, ulikuwa unajiuza funga hiyo biashara na choma nguo zote za kikahaba, haijalishi zilikuwa zinakupa faida kiasi gani…tambua kuwa faida hiyo uliyokuwa unaipata sio kutoka kwa Mungu bali ni shetani ndiye aliyekuwa anakupa ili mwisho wa siku akupeleke kuzimu, kwahiyo mwachie shetani vilivyo vyake wewe tafuta vya Mungu, yeye anasema atakupa mara mia, na pamoja na hayo Uzima wa Milele?..Sasa ipi bora?…kupata pungufu pamoja na ziwa la moto au kupata mara mia pamoja na uzima wa milele?.

Na kumbuka unapoamua kuacha vyote leo na kumfuata Kristo, hatujapewa guarantee ya kupata mara mia kufumba na kufumbua, kwasababu lengo kuu na la kwanza la Mungu wetu ni kuziponya nafsi zetu zinazokwenda kuzimu sio kutufanya mabilionea!, hivyo katika hatua ya kututengeneza na kutupa mara mia..muda uliopo hapo katikati yeye ndio anayeujua mwenyewe….wengine miezi, wengine miaka, wengine miaka hata 30 au 40 ijayo, anajua yeye..kulingana na wito wa Mtu..Hivyo usiweke shabaha yako sana katika kupewa mara mia bali uweke katika kufanywa kiumbe kipya na kuyafanya mapenzi ya Mungu.

Mungu akubariki.

Maran atha!

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali, au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba 

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

DANIELI: Mlango wa 1

HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE ! BWANA YESU ALIKUJA DUNIANI KUAMUA NINI?

Siku moja nilimsikia mtumishi mmoja redioni akifundisha na kusema asilimia 60 ya mafundisho ya YESU yaliegemea katika fedha, na hivyo YESU alikuja hapa duniani ili sisi tujue kanuni za kufanikiwa kiuchumi..na ndio maana mimi hapa ninahubiri pesa.. alizungumza maneno hayo huku watu waliokuwa naye katika meza ya mazungumzo wakimsapoti kwa furaha kabisa..

Ni kweli, mifano mingi Bwana Yesu aliyokuwa anawafundisha makutano na wanafunzi wake, ni mifano aliyoitoa katika Maisha yetu ya kawaida tunayoishi kila siku, na mingine alitumia mifano ya fedha na wafanyabiasha pia, kwa mfano utaona ule mfano wa mfanyabiashara aliyekuwa anatafuta Lulu nzuri, baadaye alipoipata akaenda kuuza vyote alivyo navyo ili ainunue, mfano wa wale watu waliopewa talanta 10 wakaambiwa wafanyie biashara wazalishe, wengine wakazalisha wengine hawakuzalisha n.k.. Lakini ukiangalia mifano hiyo ilikuwa haimuelekezi mtu akawe bilionea au milionea, bali Bwana YESU aliitumia ile mifano ili kuwafundisha watu juu ya ufalme wa mbinguni..Kwamba kila mtu anapaswa akakizalie matunda kile anachopewa katika roho n.k.

Lakini Bwana YESU hakuja kwa lengo la sisi kuzijua kanuni za kuwa utajiri hapa duniani, hilo halikuwa lengo lake la msingi tangu mwanzo, kinyume chake wakati fulani maelfu kwa maelfu ya watu walipokusanyika ili kumsikiliza mpaka wakawa wanakanyagana, ukisoma Luka 12 pale utaona katikati ya mahubiri alitokea mtu mmoja ili kumwomba amsaidie kumwambia ndugu yake ampe sehemu ya urithi aliochiwa na baba yake.. Lakini saa hiyo hiyo Bwana alimjibu maneno haya.. “ Mtu wewe, ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au mgawanyi juu yenu”?..

Unaona maneno hayo?, hakuishia hapo akaendelea na kusema..

“Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo”..

Kama wewe ni mtu wa kusoma maandiko kwa kuyatafakari vizuri, utaelewa hapo BWANA, alikuwa anamaanisha kuwa yeye amekuja ili kuwa mwamuzi wa uzima wa mtu, au mpatanishi wa dhambi za mtu, lakini yeye anataka kumfanya kuwa mwamuzi wa mali za ulimwengu huu..

Ndio sababu ya kuwambia maneno hayo “Mtu wewe, ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au mgawanyi juu yenu”..Yeye kawekwa kuwa mwamuzi wa dhambi, sio mwamuzi wa mali.

Sasa ukiendelea kusoma utaona anawapa mfano huu..

Luka 12:16 “Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;

17 akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu.

18 Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.

19 Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.

20 Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?

21 Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu”.

Ndugu yangu, dunia ya sasa ya masumbufu imewafanya watu wengi wamkimbilie Mungu kwa lengo la kupata suluhisho la mali zao, na urithi wao, na biashara zao lakini hawataki kuambiwa habari za UZIMA wao, biblia inasema shina moja la mabaya ya kila namna ni kumpenda fedha (soma 1Timotheo 6:10), haimaanishi kuwa tusiwe na fedha au tusitafute fedha hapana, bali kuwa na tamaa ya fedha inatufanya tuangukie katika mambo mengi maovu, wengine wanawaua ndugu zao kikatili , kisa urithi tu, wengine wanakwenda kwa waganga, kisa urithi, wengine wanagombana mpaka kuwekeana visasi na vinyongo kisa mali tu, wengine wanatoa kafara za ndugu zao kisa mali, wengine wanawasaliti ndugu zao kisa mali na kuwatenga kisa fedha n.k..wengine wanaua watoto na watu wengine wasio na hatia kisa mali..

Hivyo kama wewe ni mkristo, pokea ushauri wa YESU anaotuambia jilindeni na choyo…usigombane na mtu kisa amekudhulumu, mtu akiichukua kanzu yako mwachie na joho pia, wala usimnyime mtu haki yake kwa tamaa ya mali..

Bwana akubariki sana. 

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba hizi

+225693036618/ + 225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Mada Nyinginezo:

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

FIMBO YA HARUNI!

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!

PEPETO LA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UMEPATANISHWA NA MAADUI ZAKO?

Je unawajua Wasamaria walikuwa ni watu gani?…Wasamari ni watu wanaotokea mahali panapoitwa SAMARIA, ulikuwa ni mji uliokuwepo katikati ya Taifa la Israeli. Zamani za wafalme Israeli ilipogawanyika sehemu mbili, yaani kaskazini na kusini, Eneo la Samaria lilibaki sehemu ya Kaskazini mwa Israeli na Yerusalemu ilibaki sehemu ya Kusini… kukawa na mataifa mawili ndani ya Taifa moja, sehemu ya kaskazini ikabakia na jina lile lile Israeli, ambayo mji wake mkuu ulikuwa ndio huo Samaria na sehemu ya kusini ikaitwa Yuda ambayo mji wake mkuu ndio uliokuwa Yerusalemu…

Lakini Israeli ilipokuja kuchukuliwa tena utumwani, wale waliokuwa kaskazini walipelekwa Ashuru wakabaki watu wachache sana ambao waliwekwa ili kuyatunza mashamba, na wale waliokuwa upande wa kusini walipelekwa Babeli, lakini baada ya miaka 70 Mungu aliwarudisha tena baadhi yao katika nchi yao ya ahadi, lakini wale waliopelekwa Ashuru hawakurudi tena, walidumu huko huko kwenye mataifa mengine, lakini Yule mfalme wa Ashuru alitoa watu baadhi kutoka katika taifa lake, na kuwaleta Israeli ili wakae Samaria, Hivyo kwa jinsi siku zilivyokuwa zinazidi kwenda hawa Wasamaria wakawa ni watu waliochanganyika, nusu wapagani nusu wanaishika sheria ya MUSA.

Sasa Wasamaria wao hawakuamini katika kuabudu katika lile Hekalu la Mfalme Sulemani kama wale wayahudi waliokuwepo Yerusalemu wakati huo….Hivyo ikasababisha kuwepo na matengano na kutokuelewana kwa muda mrefu…Waliokuwa wanaishi Yerusalemu yaani Yuda, waliwaona wasamari ni kama watu wa mataifa na hawajui sana dini. Na walikuwa hawachangamani, wakati mwingine hata kuzungumza walikuwa hawazungumzi. Waliendelea kuwa hivyo hadi wakati wa kutokea kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Bwana Yesu alikuwa yeye ni kutoka Uzao wa Daudi…Hivyo alikuwa ni myahudi ambaye ni wa upande wa Yerusalemu, yaani Yuda, na si msamaria. Siku moja alikuwa anapita kwenda Yerusalemu kutoka Galilaya na katika njia yake ilikuwa ni lazima akatize Samaria ili afike, kulikuwa hakuna njia nyingine, lakini alipofika Samaria wenyeji wakagundua kuwa anakwenda Yerusalemu kwa watu ambao hawaelewani kiimani..hivyo kwa jambo hilo tu, wakakataa asikae kwao wakamfukuza! Kwasababu walikuwa hawapatani.

Luka 9:52 “akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.

53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.

54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?

55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]

56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.

Je! Ingekuwa ni wewe ungejisikiaje labda unakwenda mahali fulani unazuiliwa kwasababu tu ya Imani yako?..labda unakwenda nchi fulani tuseme ya kiislamu, na kitendo cha kufika tu pale wenyeji wanagundua kuwa wewe ni mfuasi wa Imani ya kikristo, na wakakuzuilia hata kulala kwenye hoteli zao na kukwambia uondoke?..ungejisikiaje? bila shaka ungehuzunika sana, na kama si mkristo uliyesimama vizuri ungeweza hata kulaani..Ndicho kilichotokea kwa hawa wanafunzi waliwalaani Wasamaria, wakaona ni heri hata waangamizwe, hawana maana, wala roho nzuri…

Lakini Bwana Yesu alikuwa na moyo mwingine…akawaambia hamjui ni roho ya namna gani mliyonayo, Mwana wa Adamu hakuja kuangamiza roho bali kuokoa! Haleluya!..Tafsiri yake ni kwamba “yeye bado anawapenda hata kama wao wanamchukia”

Na kama ni msomaji wa Biblia ulishawahi kukutana na hili Neno..

“Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye (Mithali 16:7)”.

Sasa Bwana Yesu bila shaka njia zake zilimpendeza sana Mungu, na kama ni hivyo basi ni lazima maadui zake wangekuja kupatanishwa naye tu!..Na maadui wake wa kwanza ni hawa Wasamaria, hebu tuone ni wapi walikuja kupatanishwa naye…

Baada ya Wasamaria kumkataa Bwana hata kukataa alale nchini mwao, tunaona kipindi kifupi tu baadaye baada ya wao kumkataa labda miezi miachache tu mbeleni au wiki chache tu mbele, alikuwa anarudi tena Galilaya, na ikambidi apite tena pale pale Samaria walipomkataa kwanza…na kuna tukio la Ajabu sana liliotokea pale ambalo liliubadilisha mji wote wa Samaria kumpenda Bwana.

Tunasoma katika:

Yohana 4:3 “ aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya.

4 Naye alikuwa hana budi kupita katikati ya Samaria.

5 Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.

6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.

7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.

8 Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.

9 Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)

10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai.

11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai?

12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?

13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.

16 Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa.

17 Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume; 18 kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli.

19 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, naona ya kuwa u nabii!

20 Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia.

21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

25 Yule mwanamke akamwambia, Najua ya kuwa yuaja Masihi, (aitwaye Kristo); naye atakapokuja, yeye atatufunulia mambo yote.

26 Yesu akamwambia, Mimi ninayesema nawe, ndiye……………..

28 Basi yule mwanamke akauacha mtungi wake, akaenda zake mjini, akawaambia watu,

29 Njoni, mtazame mtu aliyeniambia mambo yote niliyoyatenda. Je! Haimkini huyu kuwa ndiye Kristo?

30 Basi wakatoka mjini, wakamwendea………………39 Na katika mji ule Wasamaria wengi walimwamini kwa sababu ya neno la yule mwanamke, aliyeshuhudia kwamba, Aliniambia mambo yote niliyoyatenda.

40 Basi wale Wasamaria walipomwendea, walimsihi akae kwao; naye akakaa huko siku mbili.

41 Watu wengi zaidi wakaamini kwa sababu ya neno lake.

42 Wakamwambia yule mwanamke, Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu; maana sisi tumesikia wenyewe, tena twajua ya kuwa hakika huyu ndiye Mwokozi wa ulimwengu”

Watu waliomkataa akae kwao sasa wanamwomba kwa kumsihi sana akae kwao angalau siku mbili…Hili Neno likatimia: Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye (Mithali 16: 7)” Mji mzima Samaria ulimgeukia Bwana…Na utaona hata baadaye walitaka kuja kumfanya kuwa mfalme wao, lakini Bwana akakataa.

Hakuna mahali ambapo Bwana Yesu alipokelewa vizuri kama kwa wasamaria ambao hapo kabla walimkataa.

Bwana wetu Yesu Kristo ni mfano kamili wa sisi kujifunza?..Alikuwa na maadui lakini waligeuzwa wote kuwa Rafiki zake, Hata wale waliomsulubisha msalabani aliwaombea msamaha na kwa kupitia damu yake kwa yeye ulimwengu umepatanishwa na yeye…Ndio maana mpaka leo Rafiki wa kweli amebakia kuwa Yesu tu!

Lakini maandiko yanatuambia katika:

Wafilipi 2:5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu”

Je! Waislamu ni maadui zako?”

Jifunze kwa Bwana Yesu hapo juu, je! Majirani zako ni maadui zako kiasi cha kutaka hata moto ushuke uwateketeze? Kama ndivyo basi Bwana Yesu anakuambia “hamjui ni roho ya namna gani mliyonayo!..Jifunze kwa Bwana Yesu hapo juu Paulo anasema Iweni na nia iyo hiyo …Je! Wafanyakazi wenzako ni maadui zako kiasi kwamba hawataki hata kukuona upo karibu nao?..Jifunze kwa Bwana Yesu hapo juu…Na likumbuke hili neno : Njia za mtu zikimpendeza Bwana hata adui zake hupatanishwa naye!…Tafuta kupatanishwa na maadui zako na si kugombanishwa nao. Kwasababu hiyo ndio Nia ya Kristo kwetu.

Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu

Kwa Maombezi/Ushauri/Maswali/Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba hizi

+225693036618/+225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

UCHUNGU WA KUIBIWA.

ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

BARAGUMU NI NINI?

Baragumu ni nini/ Nini maana ya Baragumu.

Baragumu kwa lugha rahisi tunaweza kusema ni “Tarumbeta” au “Parapanda” au Mbiu!..Matarumbeta au Mabaragumu yalikuwepo ya aina nyingi kulingana na Nyakati.

Nyakati za zamani mabaragumu yalikuwa yanatengenezwa kwa pembe za wanyama, Tofauti na nyakati zetu hizi Mabaragumu yanatengenezwa kwa shaba na wakati mwingine chuma.

Katika nyakati za zamani Mabaragumu yalitumika katika nyimbo,  hata sasa yanatumika katika Nyimbo, Katika maandiko tunasoma Daudi alisema kwa uweza wa Roho..

Zaburi 150:3 “Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;”

Na Baragumu lilitumika pia kuashiria Mwanzo wa Jambo fulani au mwisho wa Jambo fulani..Kwamfano katika biblia Wana wa Israeli wana wa Israeli walipokwenda vitani, Baragumu ndio iliyokuwa inatambulisha mwanzo wa vita au mwisho wa vita.

Na katika kitabu cha Ufunuo pia Mlango wa 8, Tunaona malaika wakiwa na Baragumu saba, kutangaza mambo yatakayokwenda kutokea kipindi kifupi kijacho

Ufunuo 8:1 “Hata alipoifungua muhuri ya saba, kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa.

2 Nami nikawaona wale malaika saba wasimamao mbele za Mungu, nao wakapewa baragumu saba”.

Je! na kwetu sisi wakristo Baragumu ni nini?.

Kadhalika Pia sisi wakristo hivi karibuni Baragumu moja la Mwisho litapigwa kwetu, baragumu(tarumbeta) hilo ni parapanda ya mwisho ambayo watakatifu wote waliooshwa kwa damu ya Mwana kondoo watanyakuliwa juu na kwenda kuonana na Bwana juu mbinguni. Baragumu hilo halijatengenezwa kwa pembe za wanyama wala shaba! bali kwa malighafi ya kimbinguni. Sauti ya Baragumu hilo itapenya mpaka kwa wafu na wataisikia sauti yake na kutoka makaburini.

Siku hiyo itakuwa ni siku ya shangwe na furaha isiyo na kifani, lakini pia itakuwa ni huzuni kwa walioachwa. Ni wajibu wetu kujitahidi kuingia kwa kupitia mlango mwembamba..

Bwana akubariki.

Kwa Maombezi/Ushauri/Maswali/ Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

NI KWANINI MUNGU HAONEKANI?

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

BWANA ALIPOSEMA “SIKUJA KUTANGUA TORATI BALI KUITIMILIZA” ALIKUWA ANAMAANISHA NINI?

KATIKA 1YOHANA 5:6-9, (A) NI KWA NAMNA GANI YESU ALIKUJA KWA MAJI NA DAMU?

KATIKA MARKO 2:2-12, KWANINI BWANA YESU ALICHUKUA HATUA YA KUSAMEHE DHAMBI KWANZA KABLA YA KUMPONYA YULE KIWETE?


Rudi Nyumbani:

Print this post

NINI MAANA YA UCHAWI?

JIBU: Katika ukristo kitendo chochote cha kutafuta msaada wa rohoni au mwilini kwa kupitia nguvu nyingine mbali na nguvu za Mungu, biblia inakiita Uchawi,…Na ni wazi kuwa hakuna nguvu nyingine iliyo kinyume na Mungu zaidi ya nguvu za shetani, Na uchawi kwa ujumla umebeba mambo mengi, kuloga, kuagua, kutazama utabiri wa nyota, kubashiri, kusihiri, kuabudu sanamu, hata kuamini baadhi ya movie au magemu ambayo yanatoa maagizo fulani kukuaminisha kuwa unaweza kupata maelekezo ya maisha yako mbali na nguvu za Mungu ni uchawi n.k. vipo vingi, kwa ujumla vyote hivyo vinaitwa uchawi.

Kumbukumbu 18:10 “Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,

11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.’’

Hivyo katika biblia uchawi umekemewa sana, tangu kipindi cha wana wa Israeli kuingia nchi ya Kaanani Mungu aliwaonya sana, mtu yeyote miongoni mwao asionekane anafanya mojawapo ya mambo hayo, Ni jambo ambalo lilikuwa linamuudhi Mungu kiasi kwamba adhabu yake ilikuwa ni kifo tu (Walawi 20:27, Kutoka 22:18)

Vile vile Biblia katika agano jipya inatuaeleza pia mtu yeyote anayejihusisha na uchawi hawezi kuurithi ufalme wa mbinguni..

Ufunuo 22:14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.

15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.

Kama tulivyoona hapo juu kujihusisha na uchawi sio tu kupaa na ungo, lakini pia hata kwenda tu kwa mganga tayari wewe ni mchawi, hata tu kuamini kuwa ipo nguvu nyingine mbali na nguvu ya Mungu inayoweza kukuongoza, au kukutabiria mambo yako, au kukusaidia kuamua mambo fulani tayari ni uchawi, kuamini kama mti Fulani au ua Fulani au nguo Fulani au tarehe Fulani, au mwezi au jua vinaweza kukuletea bahati nzuri au mbaya, huo tayari ni uchawi ambao unaangukia katika lile kundi la kutazama nyakati mbaya (Kumb 18:10) sehemu yako siku ile itakuwa ni katika lile ziwa la moto. Wewe na Yule mchawi anayewanga usiku hamna tofauti.

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.”

Hivyo kama wewe upo huko, au ulishawahi kujihusisha na mojawapo ya mambo kama hayo, unachopaswa kufanya ni kuamua kuacha kufanya hivyo tena, na kisha unatubu kwa kudhamiria kuacha kabisa hayo mambo kisha nenda kachome vitu hivyo, au katupe, halafu mfuate mchungaji wako au mtumishi yeyote mwaminifu wa Mungu akuombee, ili Roho wa Mungu aje juu yako, Kisha nawe utakuwa mmojawapo wa wana wa NURU. Lakini ukiendelea na mambo hayo, fahamu kuwa ukifa leo ni moja kwa moja kuzimu. Kwasababu ufalme wa giza ni kinyume na ufalme wa Nuru.

Ubarikiwe.

Kwa Maombezi/Ushauri/Maswali/ Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba 

+25683036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


 

Mada Nyinginezo:

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

FREEMASONS NI NINI? NA MTU ATATOKAJE HUKO?

JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUCHUKULIWA MSUKULE?

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

NYOTA ZIPOTEAZO.

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Biblia inamaanisha nini kusema Yeye aliye na sikio, na asikie?

SWALI: Tukisoma Ufunuo 2:17 inasema “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”..Ningependa kufahamu Sentensi hiyo ina maana gani? kwanini liwe sikio?.


JIBU: Kwasababu kuna uwezekano kabisa mtu akawa na masikio lakini asisikie!

Bwana Yesu alisema…katika Marko 8: 18

“Mna macho, hamwoni; mna masikio, hamsikii? Wala hamkumbuki?”..

Hao si viziwi Bwana aliokuwa anazungumza nao, wala sio vipofu! Bali ni mitume wake ndio aliokuwa anawaambia maneno hayo.

Kwahiyo kusikia kunakozungumziwa hapo ni kusikia kwa masikio ya ndani na si ya nje! (Yaani kuwa na uwezo wa kukichambua na kukielewa kile kitu kwa undani wake kama kinavyotakiwa kieleweke).

Hivyo na sisi tunaposoma Biblia tunapaswa tuisikie sauti nyuma ya kile tunachokisoma sio tusome tu kama habari..hapana bali kwa ufunuo…

Tunapaswa tuisikie SAUTI ya NENO lake, na sio Neno lake tu peke yake, wengi tunaisoma biblia lakini hatuisikii sauti nyuma ya kile tunachokisoma..Angalia hapa..

Zaburi 103:20 Mhimidini Bwana, enyi malaika zake, Ninyi mlio hodari, mtendao neno lake, Mkiisikiliza sauti ya neno lake. 

Na ndio maana tunabakia  kuona kama ni hadithi fulani tu Zilezile zinazojirudia kila siku.

Kwamfano Bwana aliposema kimwingiacho mtu hakimtii unajisi bali kimtokacho, hatupaswi tuanze kutafakari juu ya vyakula fulani tunavyokula kama nguruwe, kambale na nyama nyingine, au kuanza kutafakari juu ya vitu vitutokavyo mwilini kama vile majasho na mikojo n.k..badala yake tunapaswa tuelewe kwa sikio la ndani kuwa vitu vitutokavyo ndani kama vile, tamaa, matusi wivu, uasherati n.k ndio vitutiavyo unajisi, kwa maana vinatoka moyoni…Na mambo mengine yote tunapaswa tuyasikie hivyo hivyo kwa masikio la ndani.

Ndio maana sehemu nyingi utamwona Bwana akisisitiza neno hili mwenye masikio na asikie.

Bwana akubariki.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

UFUNUO: Mlango wa 18

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

 

Rudi Nyumbani:

Print this post