Ni kweli mtu anaweza akafa lakini roho yake ikawa inatumika kama msukule (kumilikiwa na mtu fulani kwa wakati) mahali pengine?

Ni kweli mtu anaweza akafa lakini roho yake ikawa inatumika kama msukule (kumilikiwa na mtu fulani kwa wakati) mahali pengine?

JIBU: Biblia inasema mtu ameandikiwa kufa mara moja na baada ya kifo ni hukumu, (waebrania 9:27). Hivyo mtu akishakufa, amekufa hawezi kurudi tena. Lakini hiyo unayosemea kwamba mtu kafa halafu anatumika mahali fulani, kiuhalisia ni kwamba mtu huyo bado hajafa, Kwasababu mtu akishaenda kuzimu au peponi kurudi tena huku haiwezekani . bali mtu huyo anakuwa amehamishwa tu, roho yake bado ipo hapa hapa duniani pamoja na mwili wake sehemu fulani.. Huo ni uchawi tu wa shetani(watu wengine wanaita kiini macho) na mambo kama hayo yapo tu, Hivyo watu wa namna hiyo jinsi ya kuwatambua inahitaji macho ya rohoni, au kama sio hivyo basi ni kuomba kwa imani kwa jina la YESU KRISTO na mtu huyo atarudi (sasa hapo ni kulingana na imani yako mwenyewe).

Kwasababu biblia inasema yote yawezekana kwake yeye aaminiye. Kumbuka pia hayo mambo sio ya kuyahofia kana kwamba shetani anayomamlaka ya kujiamulia kumteka kila mtu kwa jinsi apendavyo. Hapana bali watu wanaokutwa na mambo kama hayo sehemu kubwa wanakuwa ni watu waliombali sana na Mungu, au walishajihusisha na uchawi hapo kabla katika maisha yao Ndiyo inapelekea wigo mwepesi zaidi kwa shetani kuwachezea jinsi apendavyo. Lakini sio kwa kila mtu anayemwona. Na pia kuna vifo vingine vinatokea, ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu, ili baadaye Bwana aje kudhihirisha uweza wake, na mfano huo tunauona kwa Lazaro. Na watu kama hao nao hawawi wamekufa kabisa(yaani kwenda sehemu za wafu) hapana bali wanakuwa wamelala (japo hata hilo linawezekana kwa Mungu). Hivyo nao pia kwa jina la YESU wanaarudishwa na kuwa hai tena. 

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

JE!MUNGU ANAWEZA KULETA MAJIBU KUPITIA NGUVU ZA GIZA KAMA ALIVYOFANYA KWA MFALME SAULI?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO.(MATHAYO 8:21)?

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

KUNA UFUFUO WA AINA NGAPI?

NGUVU YA UPOTEVU.

JINSI EDENI ILIVYOKUWA.


Rudi Nyumbani:

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments