SWALI: Naomba kufahamu Warumi 7:25 ina maana gani?
Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.
JIBU: Katika sura yote ya saba, mtume Paulo, anaeleza kwa kina mapambano yaliyo ndani ya mwamini. Kwamba nia yake kutoka ndani ni kuitii sheria ya Mungu, lakini mwili wake kwa nje ni kikwazo kikubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kabisa kutimiza maadhimio yake.
Warumi 7:19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu
Na ni kweli huo ndio uhalisia wa kila mtu. Na ndio maana mwishoni mwa sura hiyo anahitimisha kwa kueleza hali hiyo, Lakini katika vifungu hivyo, wengi wanatafsiri vibaya wakidhani Paulo anatetea udhaifu wa mwili hapana.. Kinyume chake alianza kwanza kueleza uhalisia wa kibinadamu, ili atoe suluhisho halisi la namna ya kushinda, ambalo ndio tunalisoma katika sura inayofuata ya nane (8)
Ambapo sasa kwenye sura ya nane(8) inayofuata, anaeleza namna ambayo Kristo anatusaidia kuishinda hiyo hali, kwa sheria nyingine mpya ya Roho ambayo anaiweka ndani yetu.
Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. Maana yake ni kuwa, Roho Mtakatifu, anatuweka huru katika huo utumwa wa mwili unaotupelekesha.
Inahitaji tu kutii, kwa kumfuata Roho Mtakatifu, kisha yeye mwenyewe atatupa nguvu ya kushinda mambo yote ya mwilini. Lakini sio kwa kutegemea nguvu zetu tu wenyewe.
Warumi 8: 5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.
7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. 8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.
10 Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.
Hivyo ukiishi kwa kumtii Roho Mtakatifu, basi huwezi tumikishwa tena na mwili,
Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
Warumi 7:25, Paulo analenga hasaa sababu ya sisi kushindwa kutimiza sheria ya Mungu, Ni kwasababu ipo sheria nyingine (ya dhambi iliyojificha ndani yetu) ambayo ni ngumu kutoka kwa namna ya kibinadamu, hivyo anataka hilo tulijue ili tufahamu kuwa kwa nguvu zetu wenyewe hatuwezi kuishinda, Lakini kwa Yesu Kristo atupaye Roho wake ndani yetu, tukienenda kwa kumtii huyo, basi sheria hiyo ya dhambi tutaishinda kabisa kabisa.
Ni wito wa kila mwamini kujifunza kutembea katika Roho.
Je! Unafahamu namna ya kutembea katika Roho kama sio. Basi tutumie ujumbe kwa namba uzionazo chini ya somo hili tukutumie.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Nyaraka za Paulo tunaona ni barua kwenda kwa makanisa yaliyokuwepo wakati huo, kama Korintho, Efeso, Kolosai na Galatia na nyingine kwenda kwa watu waliokuwepo wakati huo, kama Timotheo, Tito na Filemoni sasa iweje nyaraka hizo zituhusu na sisi na hata ziwe ni neno la MUNGU?, na kuzitumia hizo kufundishia sasa?
Jibu: Swali zuri lakini ili tuweze kupata majibu yaliyojitosheleza, hetu tutafakari mifano ya kawaida iliyopo,
Alikuwepo mwanasayansi mmoja wa kijerumani maarufu ambaye sasa ni marehemu ajulikanaye kama Albert Einstein (Mgunduzi wa kanuni ya kutengeneza bomu la Nyuklia), huyu wakati wa vita vya pili vya dunia alimwandikia waraka Raisi wa Marekani aitwaye Roosevelt, kwamba atengeneze silaha ya Nyuklia, kabla Adolf Hitler hajaitengeneza, na katika waraka huo alimpa pia hiyo fomula/kanuni ya kutengeneza silaha hiyo. (Waraka huo uliandikwa mwaka Agosti 2,1939).
Na matokeo ya waraka huo ni Raisi Roosevelt kuunda bomu la Nyuklia, na kwenda kulifanyia majaribio katika miji miwili ya nchi ya Japani (Mji wa Heroshima na Nagasaki).
Lakini ajabu ni kwamba baada ya wakati huo, sehemu za waraka huo zilizobeba kanuni za utengenezaji wa nyuklia zilivuja na kufikia mataifa mengine, na mataifa hayo kama Urusi hayakulaza damu bali nayo pia yakaunda mabomu ya nyuklia yenye kanuni ile ile, zilizokuwepo ndani ya ule waraka.
Na cha ajabu zaidi ni kwamba miaka mingine mingi mbele mataifa mengine kama Ufaransa, Pakistani,India, na mengine machache yakaichukua kanuni hiyo hiyo ya kuunda bomu la Nyuklia na kutengeneza mabomu yao,
Na cha kushangaza zaidi na zaidi ni kwamba mataifa mengine mengi leo yanafanya jitihada kuunda mabomu yao kupita kanuni ile ile ya mwanasayansi huyo Albert Einstein aliyetokea miaka mingi huko nyuma kupitia waraka wake aliomwandikia Raisi wa Marekani.
Sasa swali la kujiuliza, ni hili; kulikuwa kuna haja gani ya Mataifa kama Urusi, Ufaransa, na mengineyo kufuatilia waraka Einstein aliomwandikia Raisi Roosevelt na hata kuzitumia kanuni/fomula alizoziandika ndani yake kutengeneza mabomu yao??..
Tulitegemea waraka wa Einstein kwenda kwa Raisi huyo, uishe matumizi baada ya kusomwa na kutumika na Raisi huyo wa Marekani, lakini ajabu ni kwamba mpaka sasa una matokeo katika ulimwengu wetu, ingawa uliandikwa miaka mingi iliyopita.
Kwahiyo Utaona kwamba sababu pekee ya mataifa mpaka leo hii kuitumia kanuni ya mwanasayansi huyo aliyetokea miaka mingi huko nyuma ni kwasababu alichokigundua Albert Einstein ni kitu cha Kweli chenye manufaa na tija si tu kwa wakati wake tu, au Taifa lake tu bali hata kwa mataifa mengine na kwa vizazi vingi vijavyo.
Na ni hivyo hivyo Nyaraka za Mtume Paulo na za Mitume wengine… kwa jicho la nje zitaonekana kama zimeandikwa kwaajili ya makanisa yale ya wakati ule, au kwaajili ya watu wa wakati ule, lakini kwa jicho la rohoni ni ujumbe kwetu zaidi hata ya watu wa wakati ule.
Kwasababu yaliyoandikwa katika nyaraka za Mitume wa kwenye Biblia ni maneno ya kweli yanayoishi katika vizazi vyote, na tena kwa jinsi muda unavyozidi kwenda ndivyo yanavyohitajika zaidi kwasababu yaliyokuwa yanatendeka zamani, sasa hivi yamezidi mara nyingi sana.
Vita vya kiroho walivyokuwa wanapigana watu wa kanisa la Korintho, Galatia, na mengineyo nyakati hizo ndizo tunazopambana sasa, tena wakati huu zimezidi zaidi, kwahiyo tunahitaji fomula na kanuni za wanasayansi wetu wa kiroho (Mitume na manabii wa kwenye Biblia) kutengeneza silaha zetu za kiroho sasa, na kupambana hivi vita mpaka tushinde.
Lakini tukibaki na kusema zile nyaraka zilikuwa ni za wakorintho tu peke yao na wagalatia tu peke yao, na kwamba sisi hazituhusu tutamalizwa vizuri na shetani, ni sawa na Taifa la Urusi liseme ule waraka wa Einstein aliomwandikia Raisi wa Marekani, kuhusu utengenezaji wa Nyuklia uliwahusu Wamarekani peke yao, wangekuwa na akili hiyo, leo wangeisha, au wangetawaliwa!.
Na sisi ni lazima tuiamini Biblia, kuwa ni Neno la MUNGU linaloishi kwa nyakati zote na vizazi vyote, hakuna wakati litaisha matumizi, au litapitwa na wakati, Mafunuo yaliyokuwemo ndani ya Biblia yana nguvu na Uwezo, kwani waliofunuliwa wamefunuliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu na si kwa akili zao.
Mwisho; Je umempokea YESU kwelikweli au kidini?.. kama maisha unayoishi ni ya uvuguvugu bado hunaye YESU, unamhitaji YESU aingie maishani mwako, unahitaji kujikana nafsi na kubeba msalaba na kumfuata YESU, Fanya mageuzi na acha kuishi maisha ya uvuguvugu, kwani tunaishi nyakati za hatari na muda umeenda sana, na parapanda inalia muda wowote, na mambo yote yatapita.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?
Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?
NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)
Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.
Kibiblia, hekima, ni uwezo wa kupambanua , kuhukumu na kufanya maamuzi yenye matokeo makamilifu ya Ki-Mungu duniani.
Kwamfano, biblia inatuambia kwa hekima Mungu aliziumba mbingu na nchi (Mithali 8:22-31)
Sulemani alimwomba Mungu hekima ya kuchunga na kufanya hukumu kwa watu wake Israeli, na Mungu akampa, Danieli alipewa hekima ya upambanuzi wa ndoto na maono yote ya siri,
Kwa ufupi hekima ya ki-Mungu ni zaidi ya maarifa, elimu, au akili, ni uwezo wa juu sana ambao unazidi upeo wa ki-binadamu.
Kumbuka Biblia inaitaja hekima pia kuwa ni mtu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.
1Wakorintho 1:24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.
Na kama Ndio hekima mwenyewe..Basi ndani yake matunda yote ya hekima yapo.
Wakolosaia 2:3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.
Hivyo ili mtu kuiona hekima tafsiri yake ni kuwa anapaswa amwone YESU. Na kumwona Yesu ni kumpokea kama Bwana na mwokozi wa maisha yako (Warumi 10:9), pamoja na kumtii kutembea katika njia zake.
Katika mahubiri, Mahubiri yanapatikana wapi? Kila mahali, kwenye njia kuu, viwanja, kwenye mikutaniko ya watu, mastendi, masokoni, mitandaoni n.k.
Anapazaje sauti?
Anapaza sauti kupitia watumishi wake mbalimbali Aliowatuma kumuhubiri.
Hivyo, hilo andiko linalosema,
Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.
Unaweza kuelewa sasa analenga injili, inayohubiriwa kila mahali duniani kote. Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kusema hajawahi kuisikia injili, kwasababu kila mahali inahubiriwa kwa nguvu. Kuonyesha kuwa hekima haijajificha ipo sikuzote, bali ni watu ndio wanaikwepa.
Mtu yeyote anayemwamini Kristo basi tayari amefungua mlango wa ufahamu mkubwa sana unaoweza kufungua mambo yote katika hii dunia.
Bwana akubariki.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JIBU: Haya ni maneno ya kiyunani, yanayoeleza namna tofauti ya kutafsiri maandishi.
Ni namna ya kutafsiri maandiko kwa kuzingatia mtazamo wa awali uliokusudiwa na mwandishi, kwa kuzingatia muktadha, hali ya kihistoria, matamshi na matumizi ya lugha.
Ni namna ya kutafsiri Maandiko kwa namna ya mtazamo wa mtu mwenyewe, kwa kulileta andiko liendane Na wazo lake binafsi,. Namna hii haitilii maanani sana kusudio La kwanza la mwandishi, bali lile aliaminilio kuwa ni sahihi Kwake. (Mfano wa hii ni ile namna ya kusema nimefunuliwa)
Kwa ufupi eksejesisi ni Kuliruhusu andiko lijitafsiri lenyewe huku Eisojesisi ni lilete andiko litafsiri ninachokitaka au kiamini.
Ijapokuwa Eksejesisi,(tafsiri ya awali) ndio msingi hasaa wa kusimamia katika kuyaelewa maandiko lakini eisojesisi pia Mungu huitumia kusema na sisi katika nyakati Fulani.
La kuzingatia ni kwamba kabla hujaipokea namna nyingine.. Ifahamu kwanza asili ya kwanza ya andiko hilo, ilikuwa ni nini.
Kwamfano Bwana Yesu aliposema.
Mathayo 11:28
[28]Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
Katika Eksejesisi hiyo mizigo inayozungumziwa hapo na Bwana Yesu sio umaskini, Mateso, madeni, familia, majukumu,n.k. hapana, bali mizigo ya dhambi. Ndicho Bwana Yesu alichomaanisha na kusudi la kwanza lililomfanya kuja duniani lilikuwa ni hilo kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi zake.
Lakini pia Bwana anaweza tumia andiko hilo kulenga na mizigo mingine, kwasababu ni ukweli usiopingika alisema pia tumtwike yeye fadhaa zetu zote.
1 Petro 5:7
[7]huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.
Hivyo namna zote Mungu anaweza kutumia kutujenga. Kwasababu Neno lake ni pana na njia zake hazichunguziki, katika kuwajenga, kuwafariji na kuwaponya watu. Isipokuwa hatari inakuja mtu kukosa kulipambanua vizuri Neno na matokeo yake kutegemea zaidi mtazamo (alioupokea), na kuacha biblia yenyewe kujieleza.
Hii ndio Imekuwa chumbuko la mafundisho mengi ya uongo, na potofu, kwamfano mtu atasema chapa ya mnyama (ufunuo 13) Ni ugonjwa wa Korona (covid-19). Wakati si kweli.
Au mtu atasema Yesu alitengeneza matope kwa mate yake akampaka mtu machoni akaona,(Yohana 9:6-7) hivyo na sisi kufanya kwa namna hiyo si kosa. Kumbe lile lilikuwa ni “ingilio la Mungu” la wakati husika lakini sio agizo la kudumu. Kwani agizo la daima ni kutumia jina la Yesu kutenda/kuamuru jambo lolote.(Kol 3:17)
Hivyo ili kubaki katika upande sahihi ni vema ukajifunza eksejesisi, (kufahamu muktadha wa kimaandiko), na ndio pale esiojesisi inapokuja Basi unaeweza Kuligawanya vema Neno la Mungu. Bila kuleta uharibifu/ madhara yoyote, katika imani au kwa kile unachowafundisha wengine.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Swali: Katika kitabu cha Mathayo 17:4 Mtume Petro na wenzie waliwezaje kufahamu kuwa wale ni Musa na Eliya?
Jibu: Turejee habari hiyo kuanzia ule mstari wa kwanza..
Mathayo 17:1 “Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;
2 akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.
3 Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.
4 Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya”.
Biblia haijaeleza kama Musa na Eliya walijitambulisha katika maono yale, ikiwa na maana kuwa kuna njia nyingine iliyowafanya Petro na wenzie kujua kuwa wale ni manabii Musa na Eliya na si wengine.
Sasa njia Pekee iliyomfanya Petro na wenzie kufahamu kuwa wale walikuwa ni Musa na Eliya na si wengine, ni UFUNUO WA ROHO MTAKATIFU.
Kama vile ufunuo wa Roho Mtakatifu ulivyomjia Petro kumhusu YESU.
Mathayo 16.15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”.
Umeona hapo?, aliyemwambia Petro kuwa YESU ni KRISTO tena ni MWANA WA MUNGU aliye juu sio YESU mwenyewe!, bali ni ufunuo wa alioupokea kutoka kwa Baba.
Na hiyo sio ajabu kwani walikuwa wameenda mlimani kuomba.. ni kawaida kwa watumishi wa MUNGU kupokea mafunuo ya mambo yaliyopo, au yajayo wanapokuwa katika maombi, hususani kama hayo ya mlimani.
Kwahiyo Mtume Petro na wenzie walipata ufunuo wa ujio au uwepo wa manabii hao wawili wakiwa katika maombi, utaona jambo kama hilo lilishatokea tena kwa Petro wakati yupo kwa Yule Simoni mtengenezaji wa ngozi wa kule Yafa, wakati ambapo Roho Mtakatifu alimfunulia alipokuwa katika maombi kuwa kuna watu watatu wanamwulizia, hivyo aende nao asiogope!, na kweli ikawa hivyo..
Matendo 10:17 “Hata Petro alipokuwa akiona shaka ndani ya nafsi yake, maana yake ni nini maono hayo aliyoyaona, wale watu waliotumwa na Kornelio, wakiisha kuiulizia nyumba ya Simoni, wakasimama mbele ya mlango,
18 wakaita; wakauliza kwamba Simoni aitwaye Petro anakaa humo.
19 Na Petro alikuwa akiyafikiri yale maono. Roho akamwambia, Wako watu watatu wanakutafuta.
20 Basi ondoka ushuke ufuatane nao, usione tashwishi, kwa maana ni mimi niliyewatuma.
21 Petro akawashukia wale watu, akanena, Mimi ndiye mnayemtafuta. Mmekuja kwa sababu gani?”
Kwa namna hiyo hiyo, huenda Petro na wenzake walipokea ufunuo kuwa wale ni Musa na Eliya, labda walipokea ufunuo huo muda mchache kabla hawajawatokea, au wakati ule ule walipotokea.
Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kuwa tuwapo katika uwepo wa MUNGU kama katika maombi, ni rahisi kupokea ufunuo wa Roho Mtakatifu kwani tunakuwa tupo katika roho, na mtu anapokuwa katika roho anayatambua mambo yote ya rohoni pasipo kuambiwa!
Hivyo ni muhimu sana kuwa waombaji, na wasomaji wa Neno la MUNGU, endapo akina Petro wangekuwa si watu wa kusoma maandiko, ni dhahiri kuwa wasingemjua Musa wala Eliya na hiyo ingezuia Roho kuwafunulia watu hao, kwani Roho Mtakatifu anamfunulia mtu kitu ambacho kinahusiana na Neno la MUNGU.
Je na wewe ni mtu wa kudumu uweponi mwa MUNGU? Je KRISTO YESU?..Je unao uhakika kwamba akirudi unaenda naye?
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Eliya afunge Mbingu miaka mitatu na nusu? (1Wafalme 17:1)
TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?
Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?
Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?
Swali: Je huyu Yesu anayetwaja katika Wakolosia 4:11 alikuwa ni nani, na je ni kwanini aitwe hilo jina tukufu?
Jibu: Turejee..
Wakolosai 4:11 “Na YESU AITWAYE YUSTO; hao ni watu wa tohara. Tena hao peke yao ni watendaji wa kazi pamoja nami kwa ajili ya ufalme wa Mungu; nao walikuwa faraja kwangu”.
Katika Biblia Kristo mwokozi wetu hakuwa wa kwanza kuitwa jina YESU, bali walikuwepo watu wengine kadhaa kabla yake walioitwa kwa hilo jina, kwani lilikuwa ni jina linalojulikana Israeli yote,
Na tafsiri ya jina YESU ni (YEHOVA-MWOKOZI), kama vile ilivyokuwepo YEHOVA-YIRE ambayo tafsiri yake ni YEHOVA mpaji n.k
Kwahiyo YESU ni jina lililokuwepo hapo kabla, kama tu Simeoni aliyeitwa Petro, hakuwa wa kwanza kuitwa Simeoni, au Yuda aliyemsaliti Bwana YESU hakuwa wa kwanza kuitwa Yuda, kwani hata mtoto wa Yakobo, aliitwa Yuda, na ndio ukoo Bwana YESU aliotokea.
Sasa ni kitu gani kilichomtofuatisha YESU mwokozi wetu na maYesu wengine?.. si kitu kingine bali ni kiunganishi cha mwisho cha jina hilo,.. Aliyetufia anajulikana kama YESU KRISTO, maana yake YESU MTIWA MAFUTA na MUNGU…
Wengine wanaitwa “Yesu wa Yusto”, wengine “Bar-YESU” (soma Matendo 13:6) lakini ni mmoja tu anaitwa “YESU KRISTO”.. Huyu kwa jina lake hili ndio tunapata ondoleo la dhambi na wokovu (Matendo 4:12).
Na kwa jina la YESU KRISTO, Tunafunguliwa na kuponywa magonjwa yetu, na ziadi sana ndio kwa jina hili tunapaswa tuhubiri na kuhubiriwa ili tupate ukombozi.
Lakini katika hizi siku za mwisho shetani amewanyanyua maYesu wengi wa uongo, ambao na si Yule wa uzima.
2Wakorintho 11:3 “Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.
4 MAANA YEYE AJAYE AKIHUBIRI YESU MWINGINE AMBAYE SISI HATUKUMHUBIRI, au mkipokea roho nyingine msiyoipokea, au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye!”
Yesu mwingine, (asiye KRISTO) anahubiriwa sasa na manabii na watumishi wa uongo, ambaye yeye hahitaji utakatifu.. ukiona unahubiriwa kwa jina la YESU lakini injili hiyo haikupeleki kuwa msafi mwilini na rohoni, badala yake unazidi kuwa wa kidunia, fikiri mara mbili ni Yesu gani uliyempokea, kwahiyo hatuna budi kujipima.
Lakini tukirudi kwenye swali!, Je huyu Yesu aitwaye Yusto alikuwa ni nani?..
Huyu Yesu aitwaye Yusto, alikuwa ni mmoja wa wafuasi wa Bwana wetu YESU KRISTO, ambaye alishirikiana na akina Paulo (watumishi wa MUNGU) kuhubiri injili, na alikuwa ni Myahudi (ndio maana Biblia inasema hapo alikuwa ni mtu wa tohara, maana yake aliyetahiriwa).
Maana ya jina Yusto ni “mwenye haki”.. na aliitwa “Yesu aitwaye Yusto”, kumtofautisha na YESU KRISTO. Huyu hakusimama kutaka aabudiwe, bali kinyume chake alikuwa anamhubiri YESU KRISTO.
Je umempokea Bwana YESU KRISTO?. Kama bado unasubiri nini?
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE BWANA YESU ALIMTOKEA YUDA BAADA YA KUFUFUKA KWAKE?.
MANENO SABA YA YESU MSALABANI.
YESU MNAZARETI, ANWANI YA MSALABA.
Je shetani ana uwezo wa kujua mawazo ya mtu?
Swali: Je YESU alikuwa na dada na kaka (ndugu wa kike na kiume), kama watu wengine?
Jibu: Ndio! Bwana wetu YESU KRISTO alikuwa na ndugu wengine wa kike na kiume, waliozaliwa na Mariamu mamaye!, maandiko yanathibitisha hilo katika Mathayo 13:55-56 na Marko 6:3.
Mathayo 13:54 “Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii?
55 Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? NA NDUGUZE SI YAKOBO, NA YUSUFU, NA SIMONI, NA YUDA?
56 NA MAUMBU YAKE WOTE HAWAPO HAPA PETU? Basi huyu amepata wapi haya yote?”
Kulikuwa na sababu ya kuanza na “Mwana wa seremala (Yusufu) na kisha Mariamu mamaye na kumaliza na akina Yakobo, Yusufu, Simeoni na Yuda na maumbu (yaani wadada)”.. Ikimaanisha kuwa iliyokuwa inatajwa hapo ni familia, na si ukoo.
Ikimaanisha kuwa Marimu baada ya kumzaa Bwana YESU hakuendelea kuwa Bikira, bali alizaa watoto wengine pamoja na Yusufu mumewe, na watoto hao walikuwa wakike na kiume kama walivyotajwa hapo juu.
Ipo imani kuwa Mariamu hakuendelea kuzaa watoto wengine baada ya kumzaa Bwana YESU na kwamba watoto hao waliotajwa hawakuwa watoto waliozaliwa na Mariamu bali walikuwa ni ndugu wengine kama watoto wa mjomba, au baba mdogo ambao walikuwa karibu sana na Mariamu na Yusufu..
Hoja hii ni dhaifu na haina ukweli, kwani kusingekuwa na sababu ya MUNGU kuruhusu Mariamu achumbiwe na YUSUFU kama hawakuwa na mpango wowote wa kukutana na kuzaa watoto huko mbeleni,.. Malaika angeweza kumtokea Mariamu hata kabla hajachumbiwa, na hilo lingeweza labda kutufanya tuamini kuwa Mariamu aliendelea kuwa bikira mpaka anakufa!.
Lakini kitendo cha mpango wa MUNGU kuingilia kati wakati ambao tayari Mariamu kashachumbiwa, na kuonyesha kuwa hao tayari wamekusudiwa kuwa mume na mke na kuzaa watoto, na hata hivyo kipindi ambacho Yusufu amekusudia kumwacha Mariamu kwasababu ya ujauzito wake, bado kulikuwa na nafasi ya Malaika kumruhusu Yusufu amwache Mariamu, na kumruhusu akaoe mwanamke mwingine, ili Marimu abaki bikira maisha yake yote.
Lakini tunaona Yule Malaika hakumruhusu Yusufu amwache mkewe, ikifunua kuwa Yule ataendelea kuwa mke na ataendelea kutumika kama mwanamke mara baada ya kumzaa Bwana YESU.
Kwahiyo Bwana YESU alikuwa na ndugu wengine na Mariamu hakupaa, wala hakufa bikira, bali alikuwa na watoto wengine, na kati ya hao (yaani Yuda na Yakobo) ndio walioandika vitabu vya Yuda na Yakobo vya agano jipya katika Biblia.
Lakini pamoja na kuwa Bwana YESU alikuwa na ndugu wengine katika mwili, bado alisema kuwa ndugu zake hasa ni wale wayafanyayo mapenzi ya Baba yake.
Luka 8:19 “Wakamwendea mama yake na ndugu zake, wasiweze kumkaribia kwa sababu ya mkutano.
20 Akaletewa habari akiambiwa, Mama yako na ndugu zako wamesimama nje wakitaka kuonana nawe. 21 Akawajibu akasema, Mama yangu na ndugu zangu ndio hao walisikiao neno la Mungu na kulifanya”.
Je umempokea YESU?, Je Umefanyika kuwa ndugu yake Bwana kwa kulishika Neno lake na kulifanya?
YESU ANARUDI.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ni halali kubatiza watoto wadogo?
HUYU SI YULE SEREMALA, MWANA WA MARIAMU?
Je! Tutatambuana tukifika mbinguni?
Kwanini Mungu alichagua njia ya kifo cha msalaba kuwa njia ya ukombozi na si njia nyingine?, kwamba hakukuwa na njia nyingine ya ushindi? Amen.
Jibu: Ni kweli, MUNGU hakushindwa kutumia njia nyingine ya ukombozi wetu tofauti na hiyo ya kifo cha mwanawe wa pekee, kwani yeye ni MUNGU anayeweza mambo yote.
Lakini siri ya kwanini KIFO kitumike kama NJIA ya ukombozi wa dhambi ya mwanadamu ni matokeo ya dhambi za mwanadamu.
Bwana MUNGU alimwambia Adamu kabla ya kuasi kuwa pindi tu atakapokula matunda ya mti ule wa ujuzi wa mema na mabaya basi atakufa! (Mwanzo 2:17).. Hilo neno ATAKUFA!… Ndilo linalojibu swali letu, kwanini KRISTO afe ili kutukomboa sisi!.
Maandiko yanasema mshahara wa dhambi ni MAUTI! (Warumi 6:23).. Maana yake ili dhambi iweze kulipwa ni lazima MAUTI ihusike.. Kwahiyo KRISTO alipokuja ili aiondoe dhambi ya mwanadamu ilikuwa ni lazima alipe hilo deni!.
Hata mtu aliyepewa mkataba wa kazi, akiukatisha ule mkataba ni sharti alipe gharama za mkataba ule, na vivyo hivyo Kristo ili akatishe mkataba tuliongia sisi na dhambi, ni sharti alipe gharama za dhambi ambayo ni MAUTI.
Kwahiyo alikikubali kifo ili dhambi iondoke kwetu, na hakukuwa na njia nyingine ya mbadala ya kuondoa dhambi!.
Je umempokea YESU kama BWANA na MWOKOZI wa maisha yako?
Kama bado hufajanya hivyo, ni heri ukafanya hivyo sasa, kwa maana hizi ni siku na ule mlango wa rehema unakaribia kufungwa.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Fahamu maana ya 2 Wakorintho 8:9 alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.
MANENO SABA YA YESU MSALABANI.
YESU MNAZARETI, ANWANI YA MSALABA.
Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?
Theofania ni neno la kiyunani lenye muunganiko wa maneno ya mawili “theos (Mungu)” na “faino (kuonekana)”. Hivyo ukiunganisha linazalika neno “kuonekana kwa Mungu”
Theofania sio kuonekana kwa Mungu katika ule utimilifu wake wote, hapana, kwasababu maandiko yanasema hakuna mtu awezayo kumwona Mungu akaishi (Kutoka 33:20). Hivyo Theofania ni njia mbadala (isiyo ya moja kwa moja) ambayo Mungu aliitumia kujitokeza na kuongea na watu, kuthibitisha agano lake, au kuwapa maagizo.
Mfano wa njia hizo,
> Ni kijiti cha moto, alichotumia kuzungumza na Musa kule jangwani. (Kutoka 3)
> Mtu Yule aliyeshindana na Yakobo mweleka (Mwanzo 32:24-30)
> Melkizedeki (Mwanzo 14: 18-20)
> Yule mtu wanne aliyewatokea Shedraka, Meshaki na Abednego ndani ya moto (Danieli 3)
> Nguzo ya moto na wingu jangwani (Kutoka 13:21-22)
> Mungu kumtokea Samweli (1Samweli 3:10)
> Maono ya Ezekieli (Ezekieli 1)
Yesu Kristo alipozaliwa katika mwili, sio tena theofania, Bali ni utimilifu wote wa Mungu katika mwili.
Wakolosai 2:9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.
Hapo mwanzo watu hawakumwona Mungu katika utimilifu huo, kwasababu kama wangemwona Mungu wangekufa kwasababu ya dhambi. Lakini Kristo alipokuja kuondoa dhambi kwa damu yake, wanadamu wote tunamwona Mungu katika utilimilifu wote, kwa Roho Mtakatifu aliyemweka ndani yetu.
Tunakikaribia kiti cha rehema, na neema kwa ujasiri bila kufa kama kule mwanzo, kwasababu damu ya Yesu inanguvu ya kuzificha dhambi zetu zote. Ukimwona Kristo(moyoni) umemwona Mungu (Yohana 14:6-11)
Ndio maana ni kwanini leo hii mtu huwezi kumfikia Mungu bila Yesu Kristo.
Okoka leo upokee neema hii, ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wanethini ni kundi la watu ambao walitumika katika hekalu, ambao sio asili ya wayahudi. Wanatajwa sana kwenye kitabu cha Nehemia na Ezra. Maana ya neno ‘Nethini’ kwa kiyahudi linamaanisha “waliotolewa”. Wakimaanisha watu waliotelewa kuwasaidia walawi katika shughuli za hekaluni.
Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowataja;
Ezra 8:20 na katika Wanethini, ambao Daudi, na wakuu, walikuwa wamewaweka kwa ajili ya utumishi wa Walawi, Wanethini mia mbili na ishirini; wote wametajwa kwa majina yao.
Nehemia 7:73 Hivyo makuhani, na Walawi, na mabawabu, na waimbaji, na baadhi ya watu, na Wanethini, na Israeli wote, wakakaa mijini mwao. Hata ulipowadia mwezi wa saba, wana wa Israeli walikuwa wakikaa katika miji yao.
Soma pia, (Ezra 2:43, 2:58, 7:24)
Biblia haituonyeshi moja kwa moja asili yao ni wapi, lakini wanazuoni wengi huamini walitokea katika chimbuko la wale wagibeoni waliowadanganya Israeli wakati ule mpaka wakafanya nao maagano, Ambao Yoshua aliwapa kazi ya kupasua kuni, na kuteka maji.
Yoshua 9:27 Siku iyo hiyo Yoshua akawafanya kuwa ni wenye kupasua kuni, na wenye kuteka maji, kwa ajili ya mkutano, na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana, hata siku hii ya leo, katika mahali hapo atakapopachagua
Mbali na hawa wagibeoni wengine wanaweza wakawa ni wageni au mateka., ambao baadaye wakaja kuwekwa kwenye utumishi wa hekaluni.
Wanethini hawakufanya kazi zozote za kikuhani, ikumbukwe kuwa ilikuwa ni kosa, mtu ambaye sio myahudi tena wa kabila la Lawi kufanya shughuli zozote za kihekalu, Hawa walikuwa wanafanya kazi za usaidizi ule wa nje, kama vile kutweka maji, kukusanya kuni, usafi, na kazi nyingine zilizohitaji msaada wa pembeni.,Ili kuwaruhusu walawi wasilemewe wajikite zaidi katika kazi za hekaluni.
Maandiko yanaonyesha walikuwa na makao yao maalumu palipoitwa Ofeli kule Yerusalemu karibu na hekalu (Nehemia 3:26)
Hata Baadaya ya uhamisho wa Babeli, tunaona mabaki yaliyorudi Israeli kufanya shughuli za kihekalu, hawa wanethini pia walirejea
Kwa ufupi wanethini walikuwa ni la watu (wasio-wayahudi) waliowekwa kwa ajili ya kusaidia shughuli za hekaluni.
Licha ya kwamba Mungu ameliita kanisa lake na amelitenga, limtumikie lenyewe katika shughuli zote za kimadhabahu. Lakini Bado Bwana anaweza kunyanyua watu wengine nje ya kanisa, kusaidia kanisa kusonga mbele. Mfano wa hawa ni Yule akida wa kirumi ambaye alilipenda taifa la Israeli na kulijengea sinagogi (Luka 7:1-5). Hakuwa myahudi lakini aliwasaidia wayahudi.
Hata sasa wanethini wapo wengi, hawapaswi kuzuiliwa, endapo wanasaidia kanisa au kazi ya Mungu, kwasababu ni Bwana ndiye aliyewavuta.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: