SWALI: Yule tajiri alimaanisha nini kumwambia Lazaro, achovye ncha ya kidole chake majini uuburudishe ulimi wake?
Luka 16:24
[24]Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
JIBU:
Habari hiyo la Tajiri na Lazaro, Bwana Yesu aliieleza kufunua uhalisia wa jehanamu jinsi ulivyo… Na mambo ambayo mtu aliyeukataa wokovu atakutana nayo baada ya kifo.
Anaeleza jinsi yule tajiri alivyokufa katika hali ya dhambi..na hatimaye akajikuta mahali pale pa mateso, ambapo hakutana hata ndugu zake wafike, tunaona hata alipoomba mtu atokaye kwa wafu aende kuwahubiria ndugu zake akaambiwa hawatashawishwa…Ni kuonyesha kuwa mahali pale palikuwa pa mateso Sana, kiasi cha kutaka mwingine yeyote kufika.
Lakini tukio lingine tunaonyeshwa akimwomba Ibrahimu Amruhusu Lazaro achovye ncha ya kidole Chake majini amburudishe ulimi wake, nalo pia akaambiwa haiwezekaia kwasababu kuna kizuizi kikubwa Sana katikati yao.
Sasa swali linakuja tukio lile linamaana gani Je kiu kile ni halisi au ni ufunuo?.
Bwana Yesu alipokuja duniani.. aliona Dunia nzima ina Kiu kikubwa sana.. na hivyo inahitaji maji ya kuweza iponya.
Sasa maji inayohitaji sio haya ya mtoni..bali maji ya rohoni ambayo ni ya uzima, na mtu pekee awezayo kutoa hayo ni yeye mwenyewe..hakuwahi kutokea mtu aliyeweza kuyatoa.
Kama tunavyojua mwili ukikosa maji, mwishowe utakufa..Ndivyo ilivyokuwa sisi sote, hapo mwanzo kabla ya Kristo, Wote tulikuwa wafu kiroho..
Utauliza vipi kwa watakatifu wa kale kama akina Musa na Eliya?…Wale walikuwa wanaishi kwa ahadi ya Kristo, Hivyo walitii madhihirisho yake aliyokuwa akijifunua kwao kwa namna mbalimbali huku wakiiongejea ahadi kamili ya ukombozi ambayo alikuja kuikamilisha yeye mwenyewe (Yesu Kristo) alipofufuka Katika wafu..(waebrania 11)
Yeye mwenyewe Alisema..
Yohana 7:37-39
[37]Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
[38]Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
[39]Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.
Sasa kiu hii ni ya nini?
Ya maisha….
Tangu zamani mwanadamu amekuwa akitafuta ‘maisha’ ambayo hata sasa hajayapata…ndio maana wengi wanakimbilia kutafuta elimu, fedha na utajiri wakidhani kuwa ndio wamepata maisha, lakini hivyo vipo mbali sana na maisha …vitakufanya ule vizuri tu, unywe vizuri, ulale vizuri kama maandalizi ya heri ya kifo chako baadaye..kwasababu Haviwezi kukudumishia maisha.. vinapooza tu kiu..lakini haviondoi kiu.
Yesu amekuja kuondoa kiu.
Sasa watu Ambao watapuuzia kuyapokea maji hayo ambayo Yesu anatupa…wakifa Katika hali hiyo hiyo huko waendapo ni majuto makubwa.
Kwasababu watataka hata tone dogo la maji hawatapata…yaani kiwango kidogo tu cha neema ya uzima hawatapata…
Leo Yesu hatupi maji tu, kwa kipimo fulani bali anapanda kabisa chemchemi za maji ndani yetu Ambazo zinabubujika uzima wa milele.
Yohana 4:14
[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
Madhara ya kukosa maji ya uzima si tu baada ya kufa…hata hapa Hapa duniani.. mtu ambaye hana Kristo rohoni anajulikana kama nchi kamena matokeo yake ni kuwa makao ya mapepo yanakuwa Ndani yake hata kama hujui..
Angalia Yesu alichokisema juu ya hilo.
Mathayo 12:43-45
[43]Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.
[44]Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.
[45]Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.
Yanakwenda mahali pasipo na maji…yaani moyo ambao hauna Kristo ndani yake.
Ndugu…umeona hatari waliyonao wenye dhambi, hapa duniani na baada ya kifo?
Shetani asikupumbaze, tubu leo kwa kumpokea Bwana Yesu katika maisha yako ili upate ondoleo la dhambi zako haraka sana.
Hizi ni siku za mwisho, dunia hii inakwisha…vilevile hujui ni siku Gani utakufa…Acha kuchezea maisha yako, ukafanana na yule tajiri aliyekosa maji ya uzima angali akiwa hai.
Okoka leo..
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SWALI: Bwana Yesu alikuwa na maana gani kusema ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’.
Luka 13:33
[33]Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu.
JIBU: Bwana Yesu alikuwa anaeleza asili ya mji wa Yerusalemu nyakati zote ulivyokuwa wa mauaji, mji ambao ungepaswa uwe wa kupokea manabii wa Mungu, lakini kinyume chake uligeuka mji wa kuwaua Manabii…
Sasa kusema maneno yale ni kutokana na taarifa aliyoletewa na wale mafarisayo kuwa Herode anataka kumwangamiza, hivyo aondoke pale aende mji mwingine…ndipo Bwana Yesu akawaambia ‘haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu’ yaani haipaswi nabii afe nje ya Yerusalemu…
Manabii wengi wa Mungu, waliuliwa pale pale Yerusalemu hivyo hata na yeye kuangamia hapo si jambo geni, …
Na ndivyo ilivyokuwa
Mfano wa hao katika maandiko alikuwa;
Zekaria mwana wa Yehoyada (2Nyakati 24:20-21). Ambaye aliuliwa hekaluni
Mwingine ni Uria nabii (Yeremia 26:20 – 24)
Na manabii wengine wengi ambao hawajatajwa, moja kwa moja katika maandiko waliuawa Yerusalemu…ndio sababu ya Yesu kusema maneno Haya;
Mathayo 23:37-39
[37]Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
[38]Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.
[39]Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.
Jambo hili hujirudi sasa rohoni..
Watu wote ambao wanaipinga injili mioyoni mwao leo, hata kama hawajashiriki moja kwa moja kuwarushia mawe watu wa Mungu, ni shirika moja tu na wale waliokuwa wanawaua manabii wa Bwana zamani.
Ndivyo walivyodhani mafarisayo kwamba wenyewe hawahusiki na mauaji ya manabii wa Bwana, angali wanampinga yeye waziwazi, kwa unafiki wao aliwaambia maneno haya..
Mathayo 23:29-36
[29]Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki,
[30]na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii.
[31]Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii.
[32]Kijazeni basi kipimo cha baba zenu.
[33]Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?
[34]Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji;
[35]hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.
[36]Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
Hii ni hatari kubwa sana kwa walio nje ya Kristo.
Mwamini Yesu leo uoshwe dhambi zako. Upokee uzima wa milele. Kwingineko si salama.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yesu alikuwa na maana gani aliposema ‘tena siku ile hamtaniuliza neno lolote (Yohana 16:23)
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
SWALI: Nini maana ya Yeremia 31:30 “Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi”.
JIBU: Zamani za agano la kale katika taifa la Israeli, kulikuwa na usemi maarufu, unaosema “Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi”.
Kikawaida zabibu au matunda mengine yenye asidi nyingi mtu alapo , huwa meno yanatia ganzi, lakini kamwe haiwezekani mtu mwingine akatiwa ganzi kwa ulaji wa mwingine.
Hapa Waisraeli wakiwa wanamaanisha kuwa adhabu za Mungu huwa zinatembea hata kwa kizazi cha watu, Lakini Mungu kwa kinywa cha Yeremia anawasahihisha kuwa hilo si jambo lake..Anawaambia kila mtu ataadhibiwa sawasawa na uovu wake, wala watoto hawatauchukua uovu wa wazazi wao..Jambo ambalo alilirudia pia kwa kinywa cha Nabii Ezekieli (Ezekieli 18:20).
Lakini pia ukisoma muktadha wa vifungu hivyo, utaona anatoa unabii wa agano jipya ambalo atalifanya na watu wake kupitia Yesu Kristo, akimaanisha kuwa wokovu wake pia , utakuwa ni wa mtu binafsi, mmoja mmoja. Tusome habari yote tokea juu.
Yeremia 31: 27 Tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapoipanda nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda, mbegu ya mwanadamu na mbegu ya mnyama.
28 Tena itakuwa, kwa kadiri nilivyowaangalia, ili kung’oa, na kubomoa, na kuangusha, na kuangamiza, na kutesa; kwa kadiri iyo hiyo nitawaangalia, ili kujenga, na kupanda, asema Bwana.
29 Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi.
30 Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe; kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi.
31 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda.
32 Si kwa mfano wa agano lile nililolifanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri; ambalo agano langu hilo walilivunja, ingawa nalikuwa mume kwao, asema Bwana.
33 Bali agano hili ndilo nitakalofanya na nyumba ya Israeli, baada ya siku zile, asema Bwana; Nitatia sheria yangu ndani yao, na katika mioyo yao nitaiandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Hivyo vifungu hivi, vinatupa kutambua kuwa wajibu wa kulitunza agano la Mungu ni la mtu binafsi, sawasawa na alivyokuja kulifunua katika agano jipya kupitia Yesu Kristo, kwamba ijapokuwa wokovu umeachiliwa kwa wote, lakini haupokelewi kijumuiya, kifamilia, au kikabila, bali kibinafsi.
Kila mtu atalibeba furushi lake mwenyewe. (Wagalatia 6:5)
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Yeremia 29:12 Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba, nami nitawasikiliza.
Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote”
1 Petro 5:10
[10]Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.
Tafsiri ya Neema ni kukubaliwa kusikostahili.. au upendeleo usio na sababu. Kwamfano pale mtu anapomwajiri mtu asiye na ujuzi kisha akampa nafasi au mshahara mkubwa wa kiwango cha sawasawa na yule mwenye elimu nyingi na uzoefu..hiyo tunaiita neema.
Hivyo katika ukristo msingi mkuu wa wokovu wetu unategemea neema ambayo ililetwa na Bwana wetu Yesu Kristo(Yohana 1:17).
Yaani Tunakubaliwa na Mungu kuwa sisi tumestahili kuingia katika ufalme wa Mungu na kuwa watoto wake, kwa kumwamini tu Yesu Kristo bila kutegemea matendo yetu wenyewe kama kigezo cha sisi kufikia kiwango hicho.
Neema hiyo hujulikana kama neema ya wokovu. Ambayo ndio neema kuu, iliyomfanya Kristo aje duniani kufa kwa ajili yetu kama fidia ya dhambi ili sisi tuitwe waliostahili. (Waefeso 2:8-9)
Lakini pamoja na hayo Mungu hana mipaka kwamba anatoa neema ya aina moja tu yaani ya wokovu peke yake…hapana anazo Neema nyingi, ambazo zinaingia katika nyanja mbalimbali za maisha ya mwanadamu.
Sehemu nyingine katika biblia huitwa. Neema juu ya neema..
Yohana 1:16
[16]Kwa kuwa katika utimilifu wake sisi sote tulipokea, na neema juu ya neema.
Neema hii unamwezesha mtu, kuwa na matokeo katika Huduma na ustahimilivu wote. Ndiyo ambayo Paulo na Barnaba walipewa, iliyowafanya waweze kukichukua kijiti cha injili na kufanikiwa kukipeleka kwa mataifa.
Matendo ya Mitume 13:2
[2]Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.
Mbeleni utaona maandiko yanasema..
Matendo ya Mitume 14:26
[26]Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza.
Hivyo wewe kama mtakatifu ukitaka mafanikio katika huduma au karama yako. Kujifunza kuomba neema ya Mungu katika huduma ni liwe ni sehemu ya maisha yako. Kwasababu hiyo Ipo kukusaidia…Na utapata matokeo ambayo hayategemei zaidi nguvu zako. Ndicho walichokuwa wanakiomba sana mitume.
Matendo ya Mitume 15:40
[40]Lakini Paulo akamchagua Sila, akaondoka, akiombewa na wale ndugu apewe neema ya Bwana. Neema ya kupokea vitu.
2 Wakorintho 9:8
[8]Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema;
Kumbukumbu la Torati 8:18
[18]Bali utamkumbuka BWANA, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.
Hata kupata vitu kiwepesi, hasaa hutegemea neema ya Mungu, kama mkristo ni lazima ujifunze kumwomba Mungu neema ya kufanikishwa, katika mambo yako yote ya kimaisha, isizitegemee tu nguvu zako au akili zako, hata kama jambo ni jepesi vipi, ikiwa ni kazi Omba Mungu akupe neema ya mafanikio, ikiwa ni biashara omba Akupe neema ya kupata Faida Zaidi, ikiwa ni elimu omba Mungu akuongezee akili zaidi.
Zaburi 68:9
[9]Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
Ni sifa ya Mungu kauchilia neema yake kwa watu wake pale wanapochoka huwatia nguvu mpya, wao wenyewe wanashangaa wanainuka tena na kuendelea mbele.. Ndio maana tunasema Mtu anayedumu katika wokovu maisha yake yote, hata anapopitia katika tufani, Pepo na mawimbi, bado hatetereki.. Ni neema ya Kristo inakuwa imehusika hapo kumvusha, si nguvu Zake.
Jifunze kuiomba hii namna ya neema.
Matendo ya Mitume 6:8
[8]Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu.
Karama za Roho, mfano miujiza, uponyaji, lugha, unabii, utume, uchungaji, n.k, ni vipawa ambavyo hutolewa bure na Roho Mtakatifu, Hakuna jitihada Yoyote ambayo mtu atafanya aweze kukunua nguvu za kumfufua mfu, au kuona mambo ya mbeleni Ayatolee unabii, au kuundoa Ukimwi kwenye damu Ya mtu, isipokuwa kwa neema za Mungu, kutembea na yeye.
Ni neema ambayo tunapaswa tuiombe, ambayo inamfanya Mungu aachilie mafuta mengi ndani yako ya kutembea katika vipawa hivyo, ili kulijenga kanisa.
1 Petro 4:10
[10]kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu.
2 Wakorintho 1:12
[12]Kwa maana kujisifu kwetu ni huku, ushuhuda wa dhamiri yetu, ya kwamba kwa utakatifu na weupe wa moyo utokao kwa Mungu; si kwa hekima ya mwili, bali kwa neema ya Mungu; tulienenda katika dunia, na hasa kwenu ninyi.
Inategemea nguvu ya Mungu (neema), kutembea katika hali ya kutimiza mapenzi yote ya Mungu katika utakatifu… maana yake ni kuwa mwanadamu Akijifunza kumpa Nafasi Roho Mtakatifu ndani yake. Atajaliwa kuishi Maisha yote yampendezayo Mungu, sawasawa na Wagalatia 5:16
2 Wakorintho 8:1-3
[1]Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia;
[2]maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.
[3]Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;
Hii ni uwezo wa kutoa vitu/ maisha/ chochote kwa wengine bila kujali nafsi yako mwenyewe.
Jifunze kumwomba Mungu neema ya utoaji. inafaida kubwa sana kwa wengine, kwa binafsi lakini pia katika kukua kwa ufalme wa Mungu.
2 Wakorintho 8:9
[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.
1 Petro 1:13
[13]Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.
Yapo mambo Mengi mema tusiyoyajua, ambayo tutapewa tukifika kule ng’ambo Kristo atakaporudi.. ni mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, biblia imehitimisha kwa kuyaita “neema”
Je Umepokea neema zote? Lakini zaidi ya yote neema ya wokovu?. Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari leo Yesu akusamehe dhambi zako, basi tawasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya chapisho hili upate msaada huo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NI MAJIRA YAPI YA NEEMA WEWE UPO?
TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.
UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?
Waefeso 6:16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu
Waefeso sura ya 6, inaeleza mapambano ambayo yapo rohoni kati ya sisi na ufalme wa giza, na namna ambavyo tunapaswa tusimame kushinda vita hivyo, kwa kuvaa zile silaha zote za haki zinazotajwa pale. Kama vile chapeo ya wokovu, dirii ya haki, kweli kiunoni, upanga wa Roho, na ngao ya Imani,.
Lakini pia katika vifungu hivyo tunaelezwa mojawapo ya silaha ya adui, nayo ni “mishale ya moto”. Swali Je hii mishale ya moto ni ipi?
Mishale ni silaha zilizotumika zamani, za kumshambulia adui kwa mbali, na hivyo ili kuziboresha waliweka moto kwa mbele ili zitakapomfikia adui basi zilete madhara zaidi ya yale tu ya kutoboa, bali kuunguza kama sio kumuharibu kabisa adui.
Tofauti na silaha kama rungu, au upanga ambavyo vinahitaji uso kwa uso kutumika. Kwa mbali havina matokeo.
Tukirudi katika ulimwengu wa sasa mishale ya vita ni makombora, Kwanini hapo shetani anaonekana akirusha mishale kutokea mbali? Ni kwasababu kwa karibu hamwezi mwamini, kwani nguvu zilizo ndani yake ni nyingi kuliko alizonazo.
Shetani hutumia sana ulimi kuleta, aidha udanganyifu, mafarakano, vita n.k. Ndio maana maandiko yanasema;
Yakobo 3:5 Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.
6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum.
7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu.
8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.
10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo.
Hawa alidanganywa na Nyoka kwa ulimi, Mafundisho ya uongo, huanzia katika maneno. Hivyo sisi kama watoto wa Mungu ni lazima tuijue silaha hii na kuidhibiti kwanza sisi wenyewe ndani yetu, kuhakikisha hatutumiki kama warusha mishale, kwa kusema yasiyopasa, lakini pia kusimama kwa imani kuhakikisha, tunakuwa thabiti kiimani, kwa kupuuzia, au kutokuweka moyoni kila Neno linalosemwa kinyume chetu, sambamba na kuwa makini kwa kupima kila neno tunaloambiwa kama kweli ni la Mungu au la!.
Mkristo usipojua silaha hii ya adui, utajikuta kila kukicha unaishi kwa machungu ya maneno ya watu, huna raha, una mashindano, au utajikuta unaanguka katika mikono ya manabii wa uongo, na hatimaye shetani anakuwa amekupata.
1Petro 4:12 Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.
13 Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.
14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia
Majaribu yote hutoka kwa Yule mwovu, lengo lake ni kumwangusha mwamini ili amwasi Mungu, hata wakati ule Bwana Yesu anakaribia kusulubiwa, alimwombea Petro ili imani yake isitindike, kwasababu alijua wataingia kwenye majaribu makubwa, kwa upungufu wa maombi yao. Vivyo na sisi yatupaswa tuwe waombaji ili tuizime mishale ya majaribu mbalimbali ya adui tusiyojua pembe ipi yanatokea. Na pia tunapojikuta ndani ya hayo majaribu, yatupasa kuishikilia imani yetu hasaa, kwa kuamini kuwa Bwana yupo pamoja nasi kutengeneza njia ya kutokea.
Shetani akijua kuwa hana nguvu ya kumshinda mwamini moja kwa moja, hivyo hupenda kuinua ujasiri wake kama silaha, na akiwa mbali anajua akirusha mishale yake kisha Yule mtu akiiogopa basi anamwangusha. Ndio hapo huleta vitisho, mfano wa kipindi kile cha wana wa Israeli walipopewa agizo la kwenda kumjengea Mungu nyumba Yerusalemu, tunasoma baada ya kipindi kifupi maadui zao wakainuka, na kuwasemelea kwa mfalme, hatimaye marufuku ikatoka, wasiendeleze ujenzi, hivyo mahali pa Mungu pakabaki gofu tu la msingi kwa muda mrefu, kisa hofu ya utalawa mpya. Lakini baada ya muda mwingi sana, tunaona Mungu akawaamsha mioyo Hagai pamoja na Zekaria, na kuwaambia Israeli kwanini wameacha kuijenga nyumba ya Bwana. (Hagai 1:1-9), walipogundua makosa yao, kwa kuruhusu hofu, Ndipo walipoamka kwa ujasiri tena na kuijenga, Mungu akawafanikisha sana.
Vivyo hivyo na sisi, tumepewa agizo la kuhubiri injili, ikiwa itapingwa, au tutatishiwa kuuawa au kufungwa, ikiwa tutapitishwa kwenye miiba au miamba hatupaswi kuogopa mishale hiyo, bali tusimame kwa imani kama akina Shedraki na Danieli, wakiwa katika matanuru ya moto, na matundu ya simba hawakutetereka. Bali walimtumaini Mungu anayewaokoa, na hatimaye kweli ikawa vile.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba ipo kweli mishale mingi ya moto, ya adui lakini hiyo mitatu ndio mikuu. Na tukiweza kusimama kwa imani basi shetani pande zote anakuwa ameshindwa kabisa kabisa, (Akiwa karibu na vilevile akiwa mbali) linda kinywa chako /puuzia/ pima maneno unayoyasikia, vilevile kuwa mwombaji ili usiingie majaribuni/ uyashinde majaribu, Lakini zaidi sana kamwe usiogope vitisho vya adui, kwasababu hawezi kufanya lolote kwa ihari yake mwenyewe.
Mungu akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi
Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?
Dini ni mfumo au utaratibu wa kumwabudu Mungu. Kwamfano ukienda mahali ukaona watu wamekusanyika na kukubaliana kuabudu kitu Fulani, ni lazima utaona tu utaratibu, au mwongozo au miiko wamejiwekea ya kuifuata na kuishika, ili ibada yao iwe na matokeo. Sasa huo utaratibu ndio unaitwa dini.
Hata imani yetu ndani ya Kristo, inasukumwa na dini. Hatumwabudu tu Mungu kama tunavyotaka bali Mungu aliweka utaratibu na njia ya kuifuata.
Lakini Dhehebu, ni “aina ya dini”. Ambayo huzalika ndani ya imani ile ile moja. Kwamfano utaona wakristo imani yao ni moja kwa Kristo Yesu, na msingi wa kuegemea ni biblia ile ile moja takatifu. Lakini ndani yao kuna michipuko mingi tofauti tofauti ya kitaratibu na ufanyaji ibada, kulingana na walivyoielewa biblia. Ndio hapo utaona wengine wanajiita wapentekesto, wengine wakatoliki, wengine wasabato, n.k. Sasa hii yote ni michupuko, ambayo mengine inakaribiana sana na uhalisia, na mengine inakwenda mbali na kweli ya Mungu.
Lakini cha kumshukuru Mungu ni kuwa biblia imeshaeleza asili ya dini ya kweli inapaswa iweje….
Yakobo 1:26 Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai. 27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.
Kwamba ni lazima itakuwa ya kimatendo zaidi. Yaani utafunzwa utakatifu, na kujitoa.
Hapana, kwasababu Yesu hakuja kuleta dhehebu jipya duniani. Kwani alipokuja alikuta tayari yapo madhehebu mengi yamesha-zaliwa kama tu ilivyo sasa, mfano Mafarisayo, na masadukayo. Lakini hakuwahi kutetea lolote kati yao. Bali alisisitiza watu kumwamini yeye, kama ndio njia ya kweli na uzima mtu asipofanya hivyo hawezi kumwona Baba (Yohana 14:6).
Ikiwa na maana haijalishi una dhehebu zuri kiasi gani. Ukikosa shabaha ya Ukristo, bado mbinguni huendi. Waamini wengi wanashikilia zaidi dini, jambo ambalo ni jema, lakini dini ni kisaidizi cha imani. Sio imani yenyewe, ni sawa na shule na elimu, tunaweza kusema shule ni kisaidizi cha elimu, lakini sio elimu yenyewe.
Hivyo ni busara kuchukua tahadhari ya dhehebu unalotaka kumwabudia Mungu, kwasababu ukweli ni kwamba madhehebu mengine hayana ubora wa kumfanya mtu awe mkristo kamili.
Kwamfano dhehebu lisilo, patana na imani katika Kristo Yesu tu, au lisilofundisha utakatifu, au lisilo amini juu ya vipawa vya Roho Mtakatifu, au linalochanganya ibada ya Mungu na sanamu, bali linasisitiza mambo ya mwilini tu, hilo halikujengi, bali linakupoteza.
Lifananishe kwanza na biblia yako, huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, kisha ndio ufanye maamuzi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini kuna tafsiri nyingi za Biblia, na tafsiri ipi ni sahihi?
Jibu: Turejee..
Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya FALME na MAMLAKA, juu ya WAKUU WA GIZA HILI, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”.
Hapa kuna vitu vinne, vilivyogawanyika katika sehemu mbili.. Kundi la kwanza ni “FALME na MAMLAKA” na kundi la pili ni “WAKUU WA GIZA na JESHI LA MAPEPO” jumla mambo manne (4)
Sasa hebu tuanze na kundi la kwanza la FALME na MAMLAKA.
Mwandishi (ambaye ni Paulo, Mtume wa Bwana YESU) alitumia mfumo wa Tawala za dunia, kutoa picha ya tawala za ufalme wa giza.
Katika Dunia tunajua kunakuwa na Falme za wanadamu… Kwamfano kuna Falme za kiafrika, falme za kiarabu, Falme za kiasia n.k,
Sasa kwa vizazi vyetu nyakati hizi mfano wa Falme ni hizi SERIKALI tulizonazo (ambapo kila nchi inayo serikali yake), lakini zamani za kale Falme zilibaki kuitwa falme..Kwamfano kwenye Biblia utaona kulikuwa na Ufalme wa Umedi na Uajemi, Ufalme wa Babeli, Ufalme wa Uyunani, Ufalme wa Rumi n.k.. Hizi zote zilikuwa ni falme na ziliongozwa na Wafalme.. kwahiyo katika ulimwengu kulikuwepo na Falme Nyingi, zenye wafalme wengi, lakini dunia ni moja.
Tusogee mbele zaidi..
Chini ya kila Falme (au serikali) kunakuwa na Mamlaka, kwamfano katika Serikali ya nchi ya Tanzania, kuna Mamlaka mbalimbali, kuna Mamlaka ya mapato (TRA), Mamlaka ya Maji safi na maji taka, Mamlaka ya mawasiliano, Mamlala ya Hali ya hewa, Mamlaka ya Elimu, Mamlaka ya bandari n.k, hivi vyote ni viungo vya Serikali kwaajili ya kuwahudumu walio chini ya Serikali/Ufalme.
Kwahiyo tunaweza kurahisisha kwa kusema mfano huu, “Vyanzo vya maji vyote vilivyopo katika UFALME wa Tanzania vipo chini ya MAMLAKA ya maji ya maji ya nchi hiyo”… au Ukusanyaji wa kodi za wananchi katika Ufalme/serikali ya Tanzania upo chini ya MAMLAKA ya Ukusanyaji mapato (TRA)….Au jukumu la Ulinzi wa raia na mali zao la Ufalme wa Tanzania lipo chini ya Mamlaka ya ulinzi na usalama kupitia chombo chake maalumu kiitwacho Polisi….Umeona huo muunganiko wa Ufalme na Mamlaka?.
Na kawaida kila Mamlaka inayo Wakuu wake na jeshi.. Ndio hapo utasikia “Mkuu wa mamlaka ya mapato” au Mkuu wa mamlaka ya mawasiliano, na jeshi zima la mamlaka hiyo ni wafanya kazi wote waliopo chini ya mamlaka hiyo..
Na katika ULIMWENGU wa giza ni hivyo hivyo, kuna FALME na pia kuna MAMLAKA mbalimbali… Zipo mamlaka za uuaji na utekaji (mfano wa hizo ni zile zilizoruhusiwa kumkamata Bwana YESU (Soma Luka 22:53),
zipo mamlaka za uharibifu wa ndoa, zipo mamlaka za uharibifu wa huduma, zipo mamlaka za uharibifu wa familia, kazi n.k n.k,
Na kila mamlaka ya giza inayo Mkuu wake/Kiongozi ambaye ni Pepo (hao Ndio wanaoitwa wakuu wa giza).. Hapa ndipo tunapofika katika kundi la Pili la WAKUU WA GIZA na MAJESHI YA MAPEPO.
Sasa kama kuna kiongozi au mkuu, ni wazi kuwa kuna Jeshi chini yake, (hakuna kiongozi/mkuu asiye na jeshi la watu chini yake la kuliongoza)
hivyo mapepo yote yaliyosalia yanayofanya kazi chini ya Wakuu wa giza ndio wanatengeneza kundi la majeshi ya mapepo wabaya.
Kwahiyo Biblia inaposema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama bali juu ya FALME NA MAMLAKA NA WAKUU WA GIZA NA MAJESHI YA PEPO WABAYA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, imemaanisha kuwa tunapambana na wakuu wa giza (Wakuu wa mapepo) na majeshi yao ambayo yanatumia Mamlaka na Ufalme wa giza kupambana nasi.
Kwahiyo ufalme wa giza, imesimama katika ngazi zake, kuonyesha kuwa vita vyetu si virahisi kama tunavyovichukulia, kupambana na falme si kazi ndogo! Inahitaji msuli wa kutosha wa kiroho, maana yake ni lazima mtu uwe umesimama kwelikweli, umezama kweli kweli kwenye ufalme wenye nguvu kuliko huo wa giza.
Na hakuna ufalme mwingine wenye nguvu kuuzidi ufalme wa giza, zaidi ya UFALME WA MBINGUNI, ambao Mkuu wa Ufalme huo ni YESU KRISTO (Mwamba Mgumu). Huyo ndiye mwenye nguvu za kuuvunja nguvu zote za falme za giza, na hana namba mbili yake!..
Je unaye YESU moyoni na maishani?.. Kama hujaokoka fahamu kuwa upo chini ya ufalme wa giza na mamlaka za giza hata kama ni tajiri, au una afya au una mafanikio mengine yote, bado upo chini ya utawala wa giza, wanaweza kukufanya chochote kwa wakati wowote, na wanaweza kukutumia vyovyote watakavyo, Mgeukie YESU leo na uhame kutoka katika huo ufalme wa giza.
Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;
15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.
17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.
18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote”.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je mkristo anaweza akawa na mapepo?
Je! tunaweza kuwaamuru Malaika kama tunavyoyaamuru mapepo?
Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?
Wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe. Akawapa ruhusa.
SWALI: Naomba kufahamu Warumi 7:25 ina maana gani?
Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.
JIBU: Katika sura yote ya saba, mtume Paulo, anaeleza kwa kina mapambano yaliyo ndani ya mwamini. Kwamba nia yake kutoka ndani ni kuitii sheria ya Mungu, lakini mwili wake kwa nje ni kikwazo kikubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kabisa kutimiza maadhimio yake.
Warumi 7:19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu
Na ni kweli huo ndio uhalisia wa kila mtu. Na ndio maana mwishoni mwa sura hiyo anahitimisha kwa kueleza hali hiyo, Lakini katika vifungu hivyo, wengi wanatafsiri vibaya wakidhani Paulo anatetea udhaifu wa mwili hapana.. Kinyume chake alianza kwanza kueleza uhalisia wa kibinadamu, ili atoe suluhisho halisi la namna ya kushinda, ambalo ndio tunalisoma katika sura inayofuata ya nane (8)
Ambapo sasa kwenye sura ya nane(8) inayofuata, anaeleza namna ambayo Kristo anatusaidia kuishinda hiyo hali, kwa sheria nyingine mpya ya Roho ambayo anaiweka ndani yetu.
Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.
2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. Maana yake ni kuwa, Roho Mtakatifu, anatuweka huru katika huo utumwa wa mwili unaotupelekesha.
Inahitaji tu kutii, kwa kumfuata Roho Mtakatifu, kisha yeye mwenyewe atatupa nguvu ya kushinda mambo yote ya mwilini. Lakini sio kwa kutegemea nguvu zetu tu wenyewe.
Warumi 8: 5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.
7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. 8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.
10 Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.
Hivyo ukiishi kwa kumtii Roho Mtakatifu, basi huwezi tumikishwa tena na mwili,
Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.
17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
Warumi 7:25, Paulo analenga hasaa sababu ya sisi kushindwa kutimiza sheria ya Mungu, Ni kwasababu ipo sheria nyingine (ya dhambi iliyojificha ndani yetu) ambayo ni ngumu kutoka kwa namna ya kibinadamu, hivyo anataka hilo tulijue ili tufahamu kuwa kwa nguvu zetu wenyewe hatuwezi kuishinda, Lakini kwa Yesu Kristo atupaye Roho wake ndani yetu, tukienenda kwa kumtii huyo, basi sheria hiyo ya dhambi tutaishinda kabisa kabisa.
Ni wito wa kila mwamini kujifunza kutembea katika Roho.
Je! Unafahamu namna ya kutembea katika Roho kama sio. Basi tutumie ujumbe kwa namba uzionazo chini ya somo hili tukutumie.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Nyaraka za Paulo tunaona ni barua kwenda kwa makanisa yaliyokuwepo wakati huo, kama Korintho, Efeso, Kolosai na Galatia na nyingine kwenda kwa watu waliokuwepo wakati huo, kama Timotheo, Tito na Filemoni sasa iweje nyaraka hizo zituhusu na sisi na hata ziwe ni neno la MUNGU?, na kuzitumia hizo kufundishia sasa?
Jibu: Swali zuri lakini ili tuweze kupata majibu yaliyojitosheleza, hetu tutafakari mifano ya kawaida iliyopo,
Alikuwepo mwanasayansi mmoja wa kijerumani maarufu ambaye sasa ni marehemu ajulikanaye kama Albert Einstein (Mgunduzi wa kanuni ya kutengeneza bomu la Nyuklia), huyu wakati wa vita vya pili vya dunia alimwandikia waraka Raisi wa Marekani aitwaye Roosevelt, kwamba atengeneze silaha ya Nyuklia, kabla Adolf Hitler hajaitengeneza, na katika waraka huo alimpa pia hiyo fomula/kanuni ya kutengeneza silaha hiyo. (Waraka huo uliandikwa mwaka Agosti 2,1939).
Na matokeo ya waraka huo ni Raisi Roosevelt kuunda bomu la Nyuklia, na kwenda kulifanyia majaribio katika miji miwili ya nchi ya Japani (Mji wa Heroshima na Nagasaki).
Lakini ajabu ni kwamba baada ya wakati huo, sehemu za waraka huo zilizobeba kanuni za utengenezaji wa nyuklia zilivuja na kufikia mataifa mengine, na mataifa hayo kama Urusi hayakulaza damu bali nayo pia yakaunda mabomu ya nyuklia yenye kanuni ile ile, zilizokuwepo ndani ya ule waraka.
Na cha ajabu zaidi ni kwamba miaka mingine mingi mbele mataifa mengine kama Ufaransa, Pakistani,India, na mengine machache yakaichukua kanuni hiyo hiyo ya kuunda bomu la Nyuklia na kutengeneza mabomu yao,
Na cha kushangaza zaidi na zaidi ni kwamba mataifa mengine mengi leo yanafanya jitihada kuunda mabomu yao kupita kanuni ile ile ya mwanasayansi huyo Albert Einstein aliyetokea miaka mingi huko nyuma kupitia waraka wake aliomwandikia Raisi wa Marekani.
Sasa swali la kujiuliza, ni hili; kulikuwa kuna haja gani ya Mataifa kama Urusi, Ufaransa, na mengineyo kufuatilia waraka Einstein aliomwandikia Raisi Roosevelt na hata kuzitumia kanuni/fomula alizoziandika ndani yake kutengeneza mabomu yao??..
Tulitegemea waraka wa Einstein kwenda kwa Raisi huyo, uishe matumizi baada ya kusomwa na kutumika na Raisi huyo wa Marekani, lakini ajabu ni kwamba mpaka sasa una matokeo katika ulimwengu wetu, ingawa uliandikwa miaka mingi iliyopita.
Kwahiyo Utaona kwamba sababu pekee ya mataifa mpaka leo hii kuitumia kanuni ya mwanasayansi huyo aliyetokea miaka mingi huko nyuma ni kwasababu alichokigundua Albert Einstein ni kitu cha Kweli chenye manufaa na tija si tu kwa wakati wake tu, au Taifa lake tu bali hata kwa mataifa mengine na kwa vizazi vingi vijavyo.
Na ni hivyo hivyo Nyaraka za Mtume Paulo na za Mitume wengine… kwa jicho la nje zitaonekana kama zimeandikwa kwaajili ya makanisa yale ya wakati ule, au kwaajili ya watu wa wakati ule, lakini kwa jicho la rohoni ni ujumbe kwetu zaidi hata ya watu wa wakati ule.
Kwasababu yaliyoandikwa katika nyaraka za Mitume wa kwenye Biblia ni maneno ya kweli yanayoishi katika vizazi vyote, na tena kwa jinsi muda unavyozidi kwenda ndivyo yanavyohitajika zaidi kwasababu yaliyokuwa yanatendeka zamani, sasa hivi yamezidi mara nyingi sana.
Vita vya kiroho walivyokuwa wanapigana watu wa kanisa la Korintho, Galatia, na mengineyo nyakati hizo ndizo tunazopambana sasa, tena wakati huu zimezidi zaidi, kwahiyo tunahitaji fomula na kanuni za wanasayansi wetu wa kiroho (Mitume na manabii wa kwenye Biblia) kutengeneza silaha zetu za kiroho sasa, na kupambana hivi vita mpaka tushinde.
Lakini tukibaki na kusema zile nyaraka zilikuwa ni za wakorintho tu peke yao na wagalatia tu peke yao, na kwamba sisi hazituhusu tutamalizwa vizuri na shetani, ni sawa na Taifa la Urusi liseme ule waraka wa Einstein aliomwandikia Raisi wa Marekani, kuhusu utengenezaji wa Nyuklia uliwahusu Wamarekani peke yao, wangekuwa na akili hiyo, leo wangeisha, au wangetawaliwa!.
Na sisi ni lazima tuiamini Biblia, kuwa ni Neno la MUNGU linaloishi kwa nyakati zote na vizazi vyote, hakuna wakati litaisha matumizi, au litapitwa na wakati, Mafunuo yaliyokuwemo ndani ya Biblia yana nguvu na Uwezo, kwani waliofunuliwa wamefunuliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu na si kwa akili zao.
Mwisho; Je umempokea YESU kwelikweli au kidini?.. kama maisha unayoishi ni ya uvuguvugu bado hunaye YESU, unamhitaji YESU aingie maishani mwako, unahitaji kujikana nafsi na kubeba msalaba na kumfuata YESU, Fanya mageuzi na acha kuishi maisha ya uvuguvugu, kwani tunaishi nyakati za hatari na muda umeenda sana, na parapanda inalia muda wowote, na mambo yote yatapita.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?
Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?
NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)
Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.
Kibiblia, hekima, ni uwezo wa kupambanua , kuhukumu na kufanya maamuzi yenye matokeo makamilifu ya Ki-Mungu duniani.
Kwamfano, biblia inatuambia kwa hekima Mungu aliziumba mbingu na nchi (Mithali 8:22-31)
Sulemani alimwomba Mungu hekima ya kuchunga na kufanya hukumu kwa watu wake Israeli, na Mungu akampa, Danieli alipewa hekima ya upambanuzi wa ndoto na maono yote ya siri,
Kwa ufupi hekima ya ki-Mungu ni zaidi ya maarifa, elimu, au akili, ni uwezo wa juu sana ambao unazidi upeo wa ki-binadamu.
Kumbuka Biblia inaitaja hekima pia kuwa ni mtu. Na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.
1Wakorintho 1:24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.
Na kama Ndio hekima mwenyewe..Basi ndani yake matunda yote ya hekima yapo.
Wakolosaia 2:3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.
Hivyo ili mtu kuiona hekima tafsiri yake ni kuwa anapaswa amwone YESU. Na kumwona Yesu ni kumpokea kama Bwana na mwokozi wa maisha yako (Warumi 10:9), pamoja na kumtii kutembea katika njia zake.
Katika mahubiri, Mahubiri yanapatikana wapi? Kila mahali, kwenye njia kuu, viwanja, kwenye mikutaniko ya watu, mastendi, masokoni, mitandaoni n.k.
Anapazaje sauti?
Anapaza sauti kupitia watumishi wake mbalimbali Aliowatuma kumuhubiri.
Hivyo, hilo andiko linalosema,
Mithali 1:20 Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, Hutoa sauti yake katika viwanja; 21 Hulia penye mikutano mikubwa ya watu, Mahali pa kuyaingilia malango, Ndani ya mji hutamka maneno yake.
Unaweza kuelewa sasa analenga injili, inayohubiriwa kila mahali duniani kote. Ukweli ni kwamba hakuna mtu anayeweza kusema hajawahi kuisikia injili, kwasababu kila mahali inahubiriwa kwa nguvu. Kuonyesha kuwa hekima haijajificha ipo sikuzote, bali ni watu ndio wanaikwepa.
Mtu yeyote anayemwamini Kristo basi tayari amefungua mlango wa ufahamu mkubwa sana unaoweza kufungua mambo yote katika hii dunia.
Bwana akubariki.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine: