Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?

Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?

JIBU: Ubarikiwe ndugu…Mlozi ni mti fulani, unaositawi sana sana huko mashariki ya kati (Lebanoni, Israeli, Palestina n.k.).Jina lake kwa kiyahudi unaitwa “SHAKEI” na tafsiri yake ni KUTAZAMA/KUANGALIA...Kwahiyo Yeremia kuonyeshwa pale Mti wa Mlozi ni lugha tu ya picha anayoonyesha kwamba Bwana ANATAZAMA, na je! anatazama nini?..Anatazama NENO lake ili alitimize alilolinena juu ya Israeli..na ndio maana ukisoma hapo anasema..

Yeremia 1: 11 Tena neno la Bwana likanijia, kusema, Yeremia, waona nini? Nikasema, Naona ufito wa mlozi. 12 Ndipo Bwana akaniambia, Umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize…

Kumbuka pia Mungu huwa anatazama Neno lake ili alitimize kwa namna zote, Hivyo kama ni jema, ni lazima alitimize, na kama ni baya juu ya watu wake ni lazima alitimize pia!.Kote kote. Lakini tunaona Israeli walikuwa waasi kwa Mungu tangu zamani, ukisoma katika habari za wafalme utaona jambo hilo, jinsi walivyokuwa wanamuasi Mungu mpaka akawaapia kuwa wataenda utumwani tena Babeli, kwa vinywa vya manabii wake waliotangulia kabla ya Yeremia mfano Isaya n.k. Na ndio maana hapo Yeremia anaonyeshwa kama UFITO(FIMBO) tu, ya mlozi, Ikimaanisha kuwa Mungu analitazama NENO lake, na kulitimiza juu yao kama ADHABU na sio BARAKA...

kwasababu FIMBO ni kwaajili ya kuadhibu siku zote tunajua hilo. Hivyo Ukizidi kuendelea mistari inayofuata ndio utaona mabaya yote Mungu aliyoyanena juu ya yao yalikuja kutimia ikiwemo kuchukuliwa utamwani Babeli.

ubarikiwe


Mada Nyinginezo:

FIMBO YA HARUNI!

UFUNUO: MLANGO WA 1

SANDUKU LA AGANO LILIKUWA LINAWAKILISHA NINI KATIKA AGANO JIPYA?

NI RAHISI KWA NGAMIA KUPENYA KATIKA TUNDU LA SINDANO, JE! NI SINDANO IPI HIYO INAYOZUNGUMZIWA?

SWALI LA KUJIULIZA!

RACA

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Anonymous
Anonymous
3 years ago

kwanini isaya anaaminiwa sana na watu kuliko yeremia?