Je! Kufanya masturbation (Punyeto) ni dhambi?

Je! Kufanya masturbation (Punyeto) ni dhambi?

Punyeto ni dhambi?..Na je! Kuoa ni suluhisho la kuzuia tamaa kama biblia inavyosema katika 1 Wakorintho 7:9?.


JIBU: Bwana Yesu alisema amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye nafsini mwake. Sentensi hiyo inaonyesha kuwa dhambi haianzii nje ya mwili bali inaanzia moyoni, hivyo zinaa pia inaanzia moyoni, ikishafanyika moyoni ndipo inatoka nje, kwahiyo chochote kinachofanyika mwilini ni matokeo ya kitu kilichofanyika tayari rohoni, hivyo uasherati, masturbation (punyeto), utazamaji wa pornography hayo yote ni matokeo ya uasherati ambao tayari yalishafanyika ndani ya moyo wa mtu.  

Ndio masturbation ni dhambi. Na suluhisho pekee la kuikwepa hiyo dhambi ni kumkabidhisha Bwana Yesu maisha yako ki-kweli kweli, na kudhamiria kuanza maisha mapya katika Kristo, na kuamua KUACHA!! Wengi wanatafuta kuombewa waache kutazama pornography au kufanya masturbation lakini hawajadhamiria kuamua kuacha hivyo vitu,..wanasubiria miujiza ishuke wajikute wameacha na huku bado mioyo yao inaelekea kwenye zinaa…Nataka nikuambie ndugu yangu unayemtafuta Mungu,Hakuna maombi yoyote ya kuondoa hicho kitu ndani ya mtu, ili hivyo vitu viondoke ni kuamua kwanza kuchukua uamuzi wa kuacha hayo mambo ndipo Bwana anakuongezea UWEZO wa kushinda hayo mambo,. Kumbuka na Biblia inasema waasherati wote sehemu yao ni katika ziwa la moto.   Na pia kuhusu kuoa biblia imeweka wazi katika kitabu cha

1 Wakorintho7 :1 “Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke.2 Lakini kwa sababu ya ZINAA kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe”.

Ukisoma kwa makini huo mstari wa 2 anasema kwasababu ya ZINAA kila mtu mwanamume awe na mke wake mwenyewe…sio kwasababu ya KUEPUKA TAMAA…bali kwasababu ya ZINAA…na zinaa maana yake ni kufanya mapenzi nje ya ndoa au kabla ya ndoa, Hii ikiwa na maana kuwa, kuwa na mke hakumzuii mtu kulipuka tamaa…kama tabia ya mtu ni kutamani! Hiyo tabia hataiacha hata akioa au akiolewa..pengine ataepuka zinaa tu baada ya kuoa/kuolewa kwasababu atakuwa na mke/mume wake ndani!…. Lakini tama ya kutazama wanawake wengine itakuwa palepale kama atakuwa hajabadilishwa.  

Kwahiyo suluhisho pekee la kuzuia tamaa kwa aliyeoa au asiyeoa, ni kumkabidhi Kristo maisha kwanza, na kukusudia kuacha dhambi, (kumbuka Mungu hawezi kumsaidia mtu ambaye hajakusudia kwa dhati kuacha kile kitu kibaya anachokifanya)..mtu akishakusudia kuacha kwa vitendo tabia ya kutamani, kujitenga na vichochezi vyote vya uasherati, muvi zenye vimelea vya ngono ndani yake, pornography, matusi, maneno ya mizaha yasiyokuwa na maana, ndipo Roho Mtakatifu anakuja juu yake na kumsaidia na hivyo anajikuta vile vitu havimsumbui tena maishani mwake. Tofauti na yule anayetamani tu kuacha lakini haonyeshi jitihada yoyote ya kutaka hivyo vitu viondoke ndani yake.  

Ubarikiwe!


 

Mada Nyinginezo:

JE! KUSHIRIKI AU KUJIHUSISHA KWENYE MICHEZO NI DHAMBI?

JE! KUBET NI DHAMBI?

JE! ULEVI NI DHAMBI?.

NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.

MADHARA YA DHAMBI YA UASHERATI.

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments