Title May 2020

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Tukishaokoka tu hatujiishii tu kwenye kujitenga na dhambi, kama vile kuzini, kuvaa nguo za uchi uchi, kuiba, kula rushwa, kutoa mimba, n.k..Sio tu hapo bali pia tunapaswa tuishi maisha ya kujizuia na mambo mengine mengi… Yapo mambo mengi ambayo tunaweza kuyafanya lakini hatujui kuwa yanaweza kuzisonga imani zetu na wakati mwingine tushindwe kuzaa matunda..

Kwamfano rafiki yako wa kidunia anaweza kukwambia naomba nisindikize kwenye birthday ya rafiki yangu, jambo hilo linaweza lisiwe ni dhambi, lakini kabla ya kufikiria kufanya hivyo jiulize?, Je! Ni faida gani na hasara gani utapata kwenye shughuli kama hizo?..Faida inaweza ikawa ni kula na kucheka, lakini tusijidanganye, hasara rohoni zitakuwa ni nyingi kuliko faida? Ukitoka pale ndio utajua.

Au Kuna tamthilia fulani kwenye Tv, halafu unasema haina shida, ni burudani, lakini ukweli ni kwamba, akili yako yote itahamia kule, kitu kitakachokupa furaha ni pale unapoikumbuka ile tamthilia ilipoishia..Na hivyo unakuwa mtumwa wa hiyo.

Au Unaunga urafiki na kila mtu wa mtaani kwako, hata wale waovu, wewe kila mtu tu ni rafiki Kwanini usichague kuishi nao kama majirani, wa kusalimia na kujuliana hali, mpaka ijiingize ndani muwe marafiki, mkutane kila siku mjadili mambo mengine ambayo hata sio ya maana?.

Una magroup kama 50 ya kuchat whatsapp, kuanzia ya shule ya chekechea, mpaka chuo, magroup mpaka ya marafiki wa mtaani, mpaka ya michezo na ya vichekesho vya kila namna..Hayo yote yanakusaidia nini, rohoni? Lakini group la kujifunza biblia unalo moja tu..Akili yako inaposongwa na mambo mengi inaisonga ile mbegu ya Mungu iliyopandwa au inayopandwa ndani yako isikue (sawa na ule mfano Bwana Yesu alioutoa wa mbegu zilizopandwa kwenye miiba, ambazo zilisongwa na shughuli na hazikuzaa)

Kabla ya kwenda kuzurura huku na huko vijiweni ulishawahi kujiuliza kuna umuhimu gani wa kwenda huko?

Tukiishi maisha ya namna hiyo ya kutojizuia biblia inatuambia.. hatutaipokea tuzo kamwe tuliyowekewa mbele yetu.

1Wakorintho 9:24 “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

25 Na kila ashindanaye katika michezo HUJIZUIA KATIKA YOTE; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika”.

Unaona Mtume Paulo anaendelea kusema…

“26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Si kila kitu cha kuvutia tunapaswa tukijaribu, ni lazima tujifunze kujizuia, kama vile wanamichezo, na kuchagua vipi vya kuchukua na vipi vya kuacha.. ili kusudi kwamba tupate muda mwingi wa kutumia kumtafakari Mungu, na kusali, na kufanya ibada..Vinginevyo wakati wote tutaona ratiba imesonga, muda ni kidogo wa kujihusisha na mambo ya msingi ya wokovu wetu.

Ndio hapo Utashangaa unapojaribu kwenda mlimani au sehemu yako faragha kusali mara marafiki wanakupigia simu, wanakuuliza upo wapi, tunataka tuje? Mara muda wa tamthilia umefika unawaza umalize ibada haraka haraka uende ukaangalie(mawazo yako yote yapo kule), mara unafungua whatsap ili ukaangalie ni nini kinaendelea huko, na kwenye lile group lako moja la Neno ulilojiunga, hapo hapo message kama 200 zinaingia kutoka magroup mengine tofauti tofauti, yanakuvutia usome hizo message jiulize utapata wapi muda wa kulitafakari vizuri Neno la Mungu?.

Hivyo muda wako utakuwa ni wasongwa songwa tu hivyo daima.

Chagua marafiki tu wachache wa karibu, hao wengine kama wanaulazima wabakie kuwa marafiki wa mbali ambao hawawezi kujishikamanisha na wewe muda mwingi..Pia Acha kufuatilia movie na thamthilia za Kikorea na nyinginezo kwenye TV, ziache zipite,dunia hii inapita ndugu (na hayo ma-movie na matamthilia karibia yote yana maudhui ya kipepo, kuyafuatilia ni kujiongezea idadi ya mapepo tu maishani mwako.)… Left magroup yote yasiyo na maana, bakiwa na yale ya kujifunza Neno la Mungu,.na ya familia…Group la watu wa shule ya msingi ulilosoma miaka 10 au 20 huko nyuma linakusaidia nini kwasasa?..labda lingekuwa na maana kwako kama ungekuwa huna jukumu lingine la kuutafuta uso wa Mungu, lakini kwasababu umepewa jukumu lingine na mamlaka iliyo juu…hilo group la shule ya msingi ondoka, kwasababu linakuchukulia muda wako na ilihali huo muda ungeutumia kusoma biblia…Mbona kabla ya hii mitandao ulikuwa unaweza kuishi na ulikuwa na furaha tu..kwanini sasahivi ushindwe?

Futa mazoea na baadhi ya watu unaoishi nao mtaani, abakie kuwa jirani mwema kwako basi, lakini kuingiliana maisha futa uhusiano huo, sio lazima ujiunge vijiweni mwao..wala usiogope kwamba siku ukipata matatizo hawatakusaidia…(Bwana ndiye ngome yetu na kimbilio letu hatuna hofu na wanadamu, Waebrania 13:6), tunapomtii Mungu na yeye anakuwa upande wetu na si upande wa Adui.

Na baada ya kufanya hayo…utakuwa umeuokoa muda mwingi sana sasa utumie huo muda wako ulioupata, kuomba, kusoma biblia, kujifunza Neno la Mungu kwa bidii, kufanya ibada, nakuambia ukijijenga utamaduni huo licha tu ya kuwa utapata amani Fulani moyoni lakini pia utamwona Mungu maishani mwako kwa namna isiyokuwa ya kawaida. Atajifunua kwako.. Matokeo yake Utakuwa kiroho kwa haraka sana na kwa kasi, mpaka kumzalia Mungu matunda ndani ya kipindi kifupi sana..Lakini tukiyaendekeza maisha ya kutojizuia, miezi, itaenda, miaka itaenda, tutakuwa wale wale wachanga, ambao ni rahisi kuchukuliwa tena na ibilisi.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

KWANINI USIICHAGUE TUZO ISIYOHARIBIKA?

NI NANI ALIYEWALOGA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

RAFIKI WA KWELI NI YUPI?

Rafiki wa kweli ni mmoja tu naye ni YESU..Leo tutatazama ni kwanini!.

Ni rahisi kujitoa kwa ndugu yako wa damu, kujitoa kwa mali na hali….hata wakati mwingine kujitoa hata uhai kwaajili ya ndugu yako wa damu, hilo linawezekana pia…Ndio, wengi wapo radhi wafe ili watoto wao waishi, wapo radhi wao wapitie shida nyingi na dhiki lakini wadogo zao, au wazazi wao wasipitie hizo dhiki. hilo kundi la watu lipo, tena idadi yake ni kubwa sana…

Lakini kuwapata watu ambao wanaweza kuutoa uhai wao kwaajili ya “rafiki zao”, ni wachache sana, kama sio hawapo kabisa..

Kwanini ni ngumu?..kwasababu Ndugu ni bora mara nyingi kuliko rafiki, Baba ni bora kuliko rafiki, mtoto ni bora kuliko jirani rafiki, mama ni bora kuliko rafiki n.k..kwasababu rafiki haaminiki leo anaweza kuwa rafiki yako mzuri kesho akawa adui yako tena mbaya sana…Sifa hiyo ya rafiki ndiyo inayoficha thamani ya urafiki usiwe na nguvu kuliko cha ndugu wa damu.

Lakini endapo akitokea mtu ambaye atakuwa tayari kuutoa uhai kwake kwaajili ya rafiki zake…Yaani yeye yupo tayari kufa ili tu rafiki zake wasife!…bila shaka huyo mtu atakuwa ni wakipekee sana..Kwasababu japokuwa anaujua unafiki wa marafiki lakini yupo tayari kuutoa uhai wake hivyo hivyo, hata kama anajua hao marafiki wanaweza kuja kumsaliti au kumkana baadaye.. Hakika huyo atakuwa zaidi ya rafiki…Upendo wake utakuwa umepita upendo wa ndugu..

Na huyo si mwingine zaidi ya Yesu..ambaye alikubali kuutoa uhai wake kwa sisi rafiki zake, ambao ni vigeugeu..Ndio!..alijua Petro atakwenda kumkana masaa machache tu mbeleni lakini alikubali kuutoa uhai wake kwaajili yake hivyo hivyo…Alijua Yuda anakwenda kumsaliti masaa machache tu mbele lakini alimwita rafiki..(kasome Mathayo 26:48-50).

Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.

14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.

15 Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu”.

Je bado tu hujamwona rafiki wa kweli?..Yeye mwenyewe anasema HAKUNA ALIYE NA UPENDO MWINGI KULIKO HUU, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake…(Kuutoa kwa Ndugu ni rahisi lakini si rafiki).

Mimi siwezi kuwa rafiki yako wa kweli, wala yule rafiki yako wa karibu sana hawezi kuwa rafiki yako kwa kiwango hicho cha kufikia kuutoa uhai wake kwaajili yako…Je! huyo rafiki yako ukijua kwamba kesho atakusaliti ufe, je utaendelea kumpenda leo?..bado utaendelea kumwita rafiki??…

Au je rafiki yako akijua kwamba kesho utamrusha ataendelea kukuita leo rafiki? Si atakuchukia na kukuita mnafiki..je! yupo tayari kufa kwa ajili yako?..kama haweza basi sio rafiki wa kweli..ni rafiki tu! Lakini si rafiki wa kweli.

Rafiki wa kweli yupo mmoja tu…ambaye hata sasa japokuwa upo mbali naye bado anakupenda, na alishakufa kwaajili yako..

Mithali 18:24 “…. Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu”.

Hivyo msogelee huyu rafiki aitwaye YESU, yeye si mnafiki, haweki kinyongo, wala hasitisiti..amekupenda amekupenda!!..hana kusitasita..Na anamaanisha kuhitaji kuyaokoa Maisha yako.

Usimdharau, Mpe maisha yako leo kama hujampa…na utapata mema, na siku ya mwisho atakufufua na atatufufua wote tuliomwamini na kumpokea…Maana alisema mahali atakapokuwepo ndipo na sisi tutakapokuwepo.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JIRANI YANGU NI NANI?

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UZAO WA NYOKA.

WALIPO WAWILI AU WATATU KWA JINA LANGU

BASI, JIANGALIENI MIOYO YENU ISIJE IKALEMEWA NA ULAFI, NA ULEVI.

MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MIJI YA MAKIMBILIO.

Wana wa Israeli walipoingia katika nchi ya Ahadi, Na kuigawanya ile nchi, Makabila yote yalipewa Urithi wa ardhi isipokuwa kabila la Lawi, Wao waliganywa katikati ya makabila mengine yote 11 yaliyosalia..  Kati ya makabila hayo ilitengwa miji 48, sehemu tofauti tofauti kwa ajili ya Wana hawa wa Lawi.

Lakini kati ya miji hiyo 48, Ilitengwa miji 6 maalumu, ambayo iliitwa “miji ya makimbilio”…Miji hiyo haikuwa sehemu moja bali  ilikuwa imezagaa karibia  taifa zima. Miji hiyo ilitengwa mahususi kwa ajili ya wale watu ambao walifanya makosa ya uuaji yasiyokuwa ya makusudi, kwa wageni wa wenyeji..(Soma Hesabu 35:1-8)

Ikumbukwe kuwa katika torati ya Musa, ilikuwa ni kosa linalostahili kifo, ikiwa utamua mtu mwenzako, (Kutoka 21:14), hata moja ya zile amri 10 ilikataza tendo hilo.. Sasa mtu yeyote ambaye alipatikana na kosa la mauaji, ilikuwa ni lazima auawe kulingana na sheria au,auawe na mlipiza kisasi.

Lakini pamoja na hayo yapo makosa ambayo yalijulikana sio ya makusudi kwamfano, wakati mwingine labda wanakata magogo maporini na kwa bahati mbaya shoka likamponyoka mmojawao na kwenda kumpiga mtu mwingine ikampelekea mauti, sasa kosa kama hilo ni la bahati mbaya, kwasababu huyo hakukusudia kuua ni bahati mbaya tu (Soma Kumbukumbu 19:5)..Hivyo sheria inaweza isimuhukumu lakini “mlipiza kisasi” labda ndugu yake yule aliyeuliwa anaweza akalipiza kisasi kwa tendo hilo na isiwe ni dhambi. Sasa mtu kama huyu nusura yake ili apone..Ilikuwa ni sharti akimbilie kwenye mojawapo wa miji hiyo sita iliyotengwa.

Miji hiyo iliwekwa karibu na miji yote, kiasi kwamba mkimbizi, atatumia mwendo wa siku moja tu au chini ya hapo, kuufikia mmojawapo wa miji hiyo.. Vitabu vya kihistoria vya kiyahudi vinasema  njia za kuelekea miji hiyo zilikuwa ni pana, zilizochongwa vizuri, bila mabonde, au miinuko yoyote, ili kumsaidia mtu huyo afikie miji hiyo kwa haraka bila kipingamizi chochote, na pembeleni kunakuwa na kibao kimeandikwa ‘Miklat’ yaani “Makimbilio”

Sasa anapofika malangoni mwa miji hiyo, anakutana na wazee wa mji pale,(Ambao ni walawi). Anawaeleza tatizo lake, (kwamba ameua pasipo kukusudia), ndipo wale wazee wanampa hifadhi. Na wale washitaki wake watakapokuja na kuwaomba wazee  wamtoe wamuue wale wazee hawatawaruhusu..kulingana na torati.

Mtu huyo ataendelea kubaki huko mjini mpaka kuhani mkuu atakapokufa (kasome Yoshua 20:6) ndipo atakapokuwa huru kurudi katika nchi yake mwenyewe. Lakini akiondoka ndani ya mji ule kabla ya kuhani mkuu kufa, wale walipiza kisasi wakimwona wakamvizia na kumuua, wale watu waliomuua hawatashitakiwa kwa mauaji yale.(watakuwa hawana hatia kwa watakachokifanya)..Kwahiyo huyo mtu hataruhusiwa hata kwenda kuwasalimia ndugu zake nje ya mji, wala kwenda kununua chochote, wala kutalii..atabaki humohumo…mpaka kuhani mkuu atakapokufa ndio atakuwa huru kutoka.

Yoshua 20:1 “Kisha Bwana akanena na Yoshua, na kumwambia,

2 Nena wewe na wana wa Israeli, uwaambie, Haya, toeni hiyo miji ya makimbilio, ambayo niliwaambia habari zake kwa mkono wa Musa;

3 ili kwamba mwenye kuua mtu, aliyemwua mtu awaye yote pasipo kukusudia, na pasipo kujua, apate kukimbilia kuko; nayo itakuwa ni mahali pa kukimbilia kwenu, kumkimbia huyo ajilipizaye kisasi cha damu.

4 Naye ataikimbilia miji hiyo mmojawapo, naye atasimama hapo penye maingilio ya lango la huo mji, kisha atanena neno lake masikioni mwa wazee wa mji; nao watamtia kwao ndani ya mji, na kumpa mahali, ili apate kukaa kati yao.

Hivyo ndivyo watu waliofanya makosa ya uuaji usio wa makusudi walivyonusuka Israeli..

Je! Habari hiyo inafunua nini katika agano jipya?

Sisi tumepata neema iliyo kubwa zaidi ya hao, sio tu wanaofanya dhambi za bahati mbaya ndio wanaopata neema ya wokovu kama hao .Hapana, bali sasa hivi ni wote waliofanya dhambi..ziwe za bahati mbaya au makusudi, Mungu ametupa MJI WA KUKIMBILIA, nao ndio  huo “kuwa ndani ya KRISTO”..

Haijalishi umeua watu wengi kiasi gani kwa makusudi, umetoa mimba nyingi namna gani, umeloga watu wengi vipi, umezini nje ya ndoa mara nyingi kiasi gani, umejibadilisha maumbile yako, umekuwa shoga, umekuwa msagaji, anaiba, unatapeli.. Mambo ambayo unajua kabisa unastahili ziwa la moto leo hii, unastahili kuuliwa na Mungu, unastahili hukumu wakati huu..

Lakini Bwana anakupa nafasi nyingine, ambayo itakuwa ni salama yako..Nayo ni msalabani.

Hakuna sehemu nyingine yoyote utakayoweza kuepuka hukumu isipokuwa kwa Yesu ndugu yangu. Hizo dhambi zako huwezi kuzificha ili usihukumiwe, kama leo hii hutayasalimisha maisha yako kwa Bwana Yesu.

Nje yake, ni HUKUMU tu  wala hakuna kingine..Ukifa leo katika hali uliyopo, fahamu kuwa hakuna msamaha milele, Vilevile ukiendelea kuishi katika maisha hayo ya dhambi fahamu kuwa ibilisi mshitaki wako anakuwinda usiku na mchana akuangamize.. Anakupangia mipango mingi kwasababu anajua unastahili hukumu kwa hizo dhambi zako nyingi..Hawezi kukuacha kukufuatilia maadamu anakuona bado upo nje ya Kristo. Biblia inasema shetani ni mshtaki…maana yake anafananishwa na huyo mlipiza kisasi Habari zake tulizozisoma hapo juu.

Kimbilia kwa YESU, ndiye Kuhani mkuu leo..

Vilevile na wewe ambaye upo tayari ndani ya wokovu, baki huko huko usifikirie hata kidogo kurudi kwenye ulimwengu..Kama vile tunaona wale ambao walitoroka kabla kuhani mkuu hajafa, walijiweka wenyewe hatarini kuuliwa na walipiza kisasi wao..Nawe pia usijaribu kufanya hivyo, dhambi ulizomfanyia Mungu huko nyuma zinatosha,.Usitoke nje ya mji wa Yesu wa makimbilio.

Na katika Habari hiyo makuhani wakuu walikuwa wanakufa ndipo mtu yule aliyeua bila kukusudia awe huru kurudi kwenye mji wake wa zamani…Lakini sasa hivi kuhani mkuu wetu YESU HAFI MILELE!!…Yupo…na maadamu yupo hai, hatupaswi kutoka nje ya uzio wake tusije tukafa.

Na kitu kingine cha kipekee ni kwamba….Ndani ya hiyo miji sita ya makimbilio…ilikuwa ni miji ya raha, haikuwa ni miji ya shida, kwasababu ilikuwa ni miji makuhani wa Bwana wanaishi..hivyo hakukukauka chakula, zaka zote na baraka zote wana wa Israeli walizokuwa wanamtolea Mungu, za mashambani na katika shughuli zao zote walikuwa wanazipeleka kwenye hii miji..Hivyo ilikuwa ni miji ya baraka, neema na rehema…aliyekimbilia kule aliishi Maisha yake yote bila shida!..kwani ni miji iliyobarikiwa, mtu huyo hawezi kamwe kupungukiwa na chochote kile iwe mavazi, chakula wala mahitaji mengine yoyote..lakini pia ilikuwa ni miji mitakatifu sio ya anasa, kwasababu ndio watumishi wa Mungu (makuhani wa Bwana) walikuwa wanakaa huko.

Kadhalika na leo ndani ya milki ya Yesu ambaye ndie Kuhani mkuu wetu, ni mji mtakatifu, wote wanaomkimbilia yeye wanakaa salama, wanatunzwa na kuhifadhiwa Maisha yao yote. Huoni hizo ni baraka za ajabu?

Ikiwa hujatubu na leo upo tayari kumkabidhi Kristo maisha yako kwa Bwana. Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

JE KUJIUA NI DHAMBI?

TUZIJARIBU HIZI ROHO.

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.

Bwana Yesu sehemu nyingi aliifananisha baadhi ya mifumo ya maisha yetu na ufalme wa mbinguni…Kwamfano utaona alisema ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara, mwenye kutafuta lulu nzuri; naye alipoona lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua (Mathayo 13:45).

Maana yake ni kwamba injili au Neno la Mungu pia limeandikwa katikati ya maisha yetu…

Yupo mtu mmoja aliufananisha ufalme wa mbinguni na sayari iliyo mbali sana….ambayo kwa mbali inaonekana ndogo sana kama nyota…lakini isogelewapo na kukaribiwa zaidi ni kubwa mno yenye uwezo wa kubeba viumbe vyote vya ulimwengu….Au kama ndege iliyo mbali sana angali, ambapo tukiwa huku chini tunaweza kuiona ni ndogo sana kuliko kalamu…lakini ishukapo chini ni kubwa yenye uwezo wa kubeba watu wengi na mizigo yao..

Hali kadhalika ufalme wa mbinguni unaonekana ni mdogo sana ukiwa mbali na mtu au watu…lakini ushukapo chini au ukaribiwapo ni mkubwa san ana wenye uwezo wa kubeba watu wengi na mizigo yao.. Hiyo yote ni mifano ya maisha ambayo imebeba injili ya Mungu ndani yake.

Upo mfano mwingine wa kimaisha ambao tunaweza kuutafakari kwa pamoja….ambao huo utaweza kutusaidia kumjua Mungu zaidi na ulinzi wake kwetu…

Hebu tafakari zile hifadhi za taifa kule porini, ndani yake kuna wanyama wengi, wanaishi…lakini wote wanalindwa na mamlaka kuu ya serikali pasipo wao kujijua, ushwari wa wao kuishi bila kuuawa na majangili inatokana na kazi ngumu askari wanazozifanya usiku na mchana kuzizunguka hifadhi hizo…ipo mipaka ambayo wananchi hawaruhusiwi kuisogelea kabisa licha ya kuiingia.

Na watoto wa Mungu wanakuwa wapo kwenye hifadhi ya Mungu…wanalindwa na serikali ya mbinguni…Malaika wanahakikisha kwamba hakuna pepo lolote linaloingia ndani ya mipaka hiyo na kuwadhuru…tunaweza tusiwaone malaika kwa macho siku zote za maisha yetu, lakini wapo wanatulinda..

Lakini kama tunavyojua mnyama yoyote akitoka nje ya ile hifadhi, usalama wake unapotea kwasababu huko nje majangili wapo na maadui wengi…hali kadhalika wanyama wanaoishi katikati ya wanadamu kifo chao hakithaminiki…mbwa wa kawaida halindwi na akifa anaonekana kama uchafu tu…lakini mbwa mwitu mmoja akifa ni hasara kubwa kwa Taifa. Wana thamani kubwa sana kwa taifa..na hakuna nchi inaweka nembo yake ya taifa mnyama wa kufugwa, utaona mara nyingi ni wanyama waliopo kwenye hifadhi za Taifa.

Hivyo na sisi tukitaka tusiishi maisha ya mashaka, maisha ambayo hayana usumbufu, yaliyokusudiwa kuishi mwanadamu…maisha ya ulinzi, maisha ya kuthaminika na mamlaka ya mbinguni, hatuna budi kuingia ndani ya “hifadhi ya Mungu (yaani ya mbinguni)”…Malaika kazi yao ni kuwahudumia tu wateule wa Mungu kasome waebrania 1:14, hakuna askari wa hifadhi anashughulika na mbwa wa kufuga (sehemu yao ni ndogo sana)…lakini wanakesha kwa wanyama wa hifadhini…Na malaika wa Mungu ni hivyo hivyo, wanakesha kuwalinda na kuwahudumia watakatifu.

Hakuna malaika anayetumwa kwenda kumlinda mwasherati asife, hakuna malaika anayetumwa kwenda kumlinda muuaji asikamatwe, au mtukanaji asiwindwe na wachawi n.k

Kwahiyo tunapokaa chini ya hifadhi ya Kristo ndio tunajipandisha thamani..Na hifadhi ya Mungu inazungukwa na mipaka ya Neno la Mungu…unapomwamini Yesu Kristo na kutubu dhambi zote na kubatizwa tayari unakuwa chini ya mamlaka ya mbinguni…shetani hawezi kukusogelea tena….na unapozidi kutoikaribia na kutoivuka ile mipaka ndivyo unavyozidi kuwa salama…Neno la Mungu linasema usiibe, usizini, usiue, usile rushwa n.k. Hiyo ndiyo mipaka.

Kama hujamwamini Yesu unasubiri nini?..mlango wa neema upo wazi, lakini hautakuwa hivyo siku zote…Tubu leo mgeukie Yesu, hizi ni siku za mwisho, na Yesu anakaribia kurudi. Fanya bidii ili uingie katika hifadhi ya Mungu.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

Tofauti kati ya kuungama na kutubu ni ipi?

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

Rudi Nyumbani:

Print this post

BIBLIA TAKATIFU.

Biblia takatifu ni kitabu kilichobeba maneno ya Mungu katika mfumo wa maandishi..Kitabu hichi kimebeba taarifa muhimu zote zinazomhusu mwanadamu…biolojia ya mwili wake, mwanzo na mwisho wa milki yake..Biblia takatifu ndio kitabu pekee kinachompa mwanadamu kalenda yake ya miaka inayokuja mbele yake.

Biblia ni kitabu kitakatifu…ndio maana inaitwa “biblia takatifu”… sasa sio karatasi yaliyokiandikia ndio matakatifu, au wino uliotumika kuandikia ndio mtakatifu wala jalada lililotumika…hapana, bali kilicho kitakatifu ni maneno yaliyoandikwa mule ndani.. Kwahiyo kitabu hicho kikitumika kwa akili ya damu na nyama..ya kuamini kwamba makaratasi yale na wino ndio matakatifu hakina manufaa yoyote kwa mwanadamu.

Tukiitumia biblia na kuiweka kifuani mwetu tukiamini kuwa itaondoa matatizo yetu hatutanufaika na chochote, tukiichukua biblia na kwenda kutolea nayo pepo hatutanufaika chochote, tukiichukua biblia na kuiweka kichwani usiku kama mto ili wachawi au mambo mabaya yasitupate hatutaambulia chochote. Ni sawa na mgonjwa anayeumwa kichwa na kuichukua dawa ya panadol na kuiweka kifuani, au kichwani kama mto akiamini itamtibu ugonjwa wake.

Au ni sawa na mtu anayechukua kitabu cha upishi (kinachoelezea hatua ya upishi)..na kukipeleka hicho kitabu jikoni mbele ya masufuria na majiko kimpikie…Unaona kitabu hakiwezi kupika haijalishi kimehakikiwa na mtaala wa nchi, na kupewa daraja la kwanza. Ili kitabu hicho kiwe na manufaa ni sharti aliyenacho akisome, ile elimu iingie kichwani mwake, kwa ile elimu ndipo aitumie kupika.

Vivyo hivyo na biblia takatifu ili iwe na manufaa kwetu, ni lazima tuyasome yale yaliyoandikwa mule ndani, tupate elimu ya kutosha..ndipo ile elimu tuitumie katika kumpendeza Mungu, kumshinda adui, kupata Baraka na mafanikio.

Biblia takatifu ni kitabu cha maarifa, hekima, na mashauri. Hakuna kitabu chochote chenye mashauri bora na hekima zilizo kuu kuliko biblia.

Kwamfano hebu itafakari hii hekima..

Luka 12:23 “Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.

24 Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana ghala wala uchaga, na Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege!

25 Na yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

26 Basi, ikiwa hamwezi hata neno lililo dogo, kwa nini kujisumbua kwa ajili ya yale mengine?

27 Yatafakarini maua jinsi yameavyo; hayatendi kazi wala hayasokoti; nami nawaambia ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

28 Basi, ikiwa Mungu huvika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatawatendea ninyi zaidi, enyi wa imani haba?”

Biblia takatifu ndio katiba ya wanadamu. Kwa kutumia katiba mtu anaweza kuhukumiwa na anaweza kupatiwa haki yake. Na kama vile jinsi ilivyo kwamba hakuna mtu aliye juu ya katiba ya nchi..Hata Raisi wa nchi hawezi kuivunja katiba…kadhalika Biblia ni katiba ya wanadamu..hakuna mwanadamu yoyote wala malaika anayeweza kuvuka mipaka ya maneno yaliyoandikwa ndani ya kitabu hicho (yaani biblia takatifu)..Zaidi ya yote hata Mungu mwenyewe hawezi kulivunja Neno lake…Kwamfano alisema hataiangamiza tena dunia kwa maji…haiwezekani hata siku moja akalivunja hilo neno na kuiangamiza dunia kwa gharika…Naam dunia itaadhibiwa kwa kitu kingine kama maandiko yanavyosema katika kitabu cha Petro lakini si kwa maji tena…Na hiyo ni kwasababu analishika Neno lake alilolisema.

Alisema pia yoyote amwaminiye mwanawe mpendwa YESU KRISTO, Ataokoka na hukumu ya milele, na asiyemwamini atahukumiwa…Hilo Neno hawezi kamwe kulibadilisha kwamba..baadaye ageuke na kusema “hapana wote watakaomwamini hawatapata uzima wa milele” wala hawezi kulitangua neno lake alilosema kwamba “wote wasiomwamini watahukumiwa”..Neno lake litabaki palepale..mbingu na nchi zitapita lakini maneno yake yatabaki yale yale.

Biblia takatifu ni maneno ya Mungu yenye ujumbe pia wa maonyo na ahadi. Hakuna kitabu kingine chochote chenye ahadi, kitabu cha fizikia hakina ahadi yoyote, kitabu cha saikolojia hakina ahadi yoyote ndani yake, kitabu cha hisabati hakina ahadi yoyote ile, lakini biblia takatifu imejaa ahadi zilizo thabiti mpaka za vizazi vijavyo vya watoto wetu, mifugo yetu, mali zetu na hata maisha ya ulimwengu ujao.

Bwana atusaidie kulishika Neno lake na kuliheshimu, kwa faida yetu wenyewe hapa duniani na kwa maisha yanayokuja baada ya haya.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

KITABU CHA UZIMA

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

Shalom,

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima. Karibu tena tujifunze maneno ya uzima wa milele.

Yohana 1:35-39 inasema..

“Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake. 36 Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!

37 Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.

38 Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?

39 Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI”.

Unaweza ukajiuliza kulikuwa na umuhimu gani kwenye Habari hii kutoa muda ambao Yesu aligeuka na kuzungumza na wale wanafunzi wawili..?Ambao muda wenyewe ulikuwa ni saa kumi?..Ulishawahi kujiuliza umuhimu wa huo muda kuwekwa pale?. Wakati mwingi tunaweza kuona ni kawaida tu lakini, kila jambo lina sababu yake,.

Tukiitafakari tangu juu Habari hiyo utaona wanafunzi hao ambao mmojawapo alikuwa ni Andrea, walipoonyeshwa tu Yesu na Yohana mbatizaji , mara moja waliacha kumsikiliza Yohana na kuanza kumfuata Bwana kwa nyuma tena kimya kimya…

Hawakusubiri apotelee mbali kwasababu kumbuka wakati huo Yesu alikuwa anakatiza njiani, pengine alikuwa anatembea kwa mwendo wa kasi kidogo hatujui, lakini hawakumwacha apotee mbele ya macho yao.. waliendelea kumfuatilia hivyo hivyo mpaka wajue anapokaa, japo biblia haijaandika ni kwa muda gani waliutumia kumfuatilia , pengine jambo hilo lilianza majira ya asubuhi labda kwenye saa nne nne hivi , au saa 6, au saa 7 hatujui.. Lakini walimfuatilia kwa muda tu.

Hawakujua kuwa Bwana alishagundua kuwa kuna watu wawili wanamfuatailia kwa nyuma tangu mbali..wao hawakuligundua hilo, walidhani Bwana bado hajui chochote..

Ghafla tu majira fulani yalipofika kwenye saa kumi alasiri wakashangaa Bwana amewageukia, na kuwauliza.. ,

Mnatafuta nini? Pengine kwa hofu kidogo hawakuwa na cha kusema.. wakajibu Rabi unakaa wapi?.. Ndipo Bwana akawachukua na kwenda kuwaonyesha anapokaa, wakakaa naye siku ile yote..

Hiyo ilikuwa ni saa kumi alasiri Kabla jua halijazama walimpata Yesu.

Ndugu mpendwa,

Biblia inatuhimiza kuwa tutafute nasi tutaona kwasababu kila atafutaye ataona..

Leo hii unaweza ukawa unamtafuta Kristo, unaonyesha bidii kujifunza Neno lake, unafuata nyendo zake, nakwambia haijalishi itakugharimu muda mrefu kiasi gani kumtafuta, lakini ni uhakika kuwa kabla jua lako halijazama utamwona Kristo. Kristo hawezi kuruhusu mpaka giza liingie bado upo tu katika hali hiyo hiyo ya kumtafuta yeye. Hayupo hivyo..alisema kila atafutaye ni lazima apate.

Siku moja moja atajidhihirisha kwako, atajifunua kwako, kwa namna ambayo hakuifanya hapo mwanzo.

Watu wengi leo hii wamekata tamaa, kumtafuta Bwana, kisa miezi imepita, miaka kadhaa imepita, hawaoni Mungu akichua hatua yoyote maishani mwao? Hawajui kuwa, Bwana alishaona bidii yako ya kumtafuta Kristo tangu zamani, Lakini muda wako wa saa kumi ulikuwa haujafika..

Mtazame, Simeoni, yeye alikuwa ni mtu mwenye haki, lakini Mungu alimwambia kabla hujafa, utamwona Masihi.. Kati ya mabilioni ya watu waliokuwa duniani wakati ule, yeye ni mmoja kati ya watu wachache sana waliomtambua Kristo kuzaliwa kwake(Luka 2:25).

Hakuna mtu anayemtafuta Mungu, Mungu akamwacha, asijifunue kwake.

Lakini Saa kumi yako itafika tu, siku fulani, wakati fulani, majira fulani..Atakugeukia, na kujifunua kwako kwa namna isiyo ya kawaida, Na atakufahamisha mengi sana.

Usikate tamaa.

Luka 11:9 “Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; TAFUTENI, NANYI MTAONA; bisheni, nanyi mtafunguliwa.

10 Kwa kuwa kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.

11 Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka?

12 Au akimwomba yai, atampa nge?

13 Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni HATAZIDI SANA KUWAPA ROHO MTAKATIFU HAO WAMWOMBAO?”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

ALIYE MKUU KATIKA UFALME WA MBINGUNI.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

MTANGO WA YONA.

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

KUWA WEWE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

Biblia inasema kila jambo na majira yake (Mhubiri 3)…maana yake ni kwamba hata mti una majira yake ya kuzaa matunda…sio kila wakati, tutakwenda kukuta maembe katika mti wa muembe…Inahitajika uwe ni msimu wa maembe ndipo mti uzae…Haijalishi huo mti utaumwagilia maji kiasi gani, au utauwekea mbolea kiasi gani…Kama sio msimu wake wa kuzaa hautazaa….Hiyo yote ni kwasababu gani?..Ni kwasababu kila jambo lina majira yake.

Vivyo hivyo katika roho, tangu Bwana wetu Mkuu Yesu Kristo, apae juu mbinguni kwenda kutuandalia makao..majira yalibadilika…kabla ya hapo hakukuwa na mlango wowote wa sisi kumzalia Mungu matunda anayoyataka…ikiwa na maana waliokuwa na fursa ya kumjua Mungu kwa undani na kunufaika sana walikuwa ni manabii wa Mungu wachache waliochaguliwa..na si watu wote, Roho Mtakatifu alikuwa anashuka juu ya watu wa Mungu wachache aliowachagua…kasome vizuri habari ile ya Musa katika..

Hesabu 11:24 “Musa akatoka, akawaambia watu maneno ya Bwana; akawakutanisha watu sabini miongoni mwa wazee wa watu, akawaweka kuizunguka Hema.

25 Ndipo Bwana akashuka ndani ya wingu, akanena naye, akatwaa sehemu ya roho iliyokuwa juu ya Musa, akaitia juu ya wale wazee sabini; ikawa, roho hiyo ilipowashukia, wakatabiri, lakini hawakufanya hivyo tena.

26 Lakini watu wawili walisalia kambini, jina la mmoja aliitwa Eldadi, na jina la wa pili aliitwa Medadi; na roho ile ikawashukia; nao walikuwa miongoni mwao walioandikwa, lakini walikuwa hawakutoka kwenda hemani; nao wakatabiri kambini.

27 Mtu mmoja kijana akapiga mbio, akaenda akamwambia Musa, akasema, Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.

28 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa tangu ujana wake, akajibu akasema, Ee bwana wangu Musa, uwakataze.

29 Musa akamwambia, Je! Umekuwa na wivu kwa ajili yangu; INGEKUWA HERI KAMA WATU WOTE WA BWANA WANGEKUWA MANABII NA KAMA BWANA ANGEWATIA ROHO YAKE.

30 Kisha Musa akaenda akaingia kambini, yeye na wale wazee wa Israeli”.

Umeona hapo mstari wa 29?.. Musa anasema ingekuwa heri kama watu wote wa Bwana, Bwana angewatia roho yake…Ikiwa na maana kuwa ni wachache tu waliochaguliwa kwa Neema ndio waliokuwa wananufaika na kipawa cha Roho Mtakatifu. Wengine wote walitamani lakini hawakukipata. Kwanini?..ni kwasababu haukuwa wakati wala majira ya kitu hicho, kushuka kwa watu wote.

Lakini Bwana Mungu wetu, ambaye ni alitabiri kwamba utafika wakati Roho huyu atamwagwa kwa wote wenye mwili…huo utakuwa ni msimu wa kuzaa matunda…Kwahiyo watakaozaliwa msimu huo watakuwa na bahati sana..Na wakati huo si mwingine zaidi ya tangu ule wakati Bwana wetu alipopaa mbinguni mpaka wakati huu wa sasa tunaouishi sisi.. Bwana alisema…

Yoeli 2:27 “Nanyi mtajua ya kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu hawatatahayari kamwe.

28 Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono”

Hii ni neema ya ajabu sana, ambayo hatupaswi tuipuuzie…Huu ndio wakati uliokubalika wa Bwana kutumwagia kipawa chake cha Roho Mtakatifu pasipo ubaguzi…Ndio maana biblia inasema katika…

2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.

2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati ULIOKUBALIKA NDIYO SASA; tazama siku ya wokovu ni sasa)”

Ndugu huu ndio wakati uliokubalika…biblia inasema watu wa zamani walikitamani hichi kipindi tunachoishi sisi…wafalme walikitamani, wakuu walitamani waonje kipawa cha Roho Mtakatifu, waliomba na kusubiri, lakini walikufa bila kuifikia hii saa tuliyopo sasa..Lakini sisi ndio tupo hiyo saa, ambayo yule Roho aliyeshuka juu ya Musa, ndiye huyo huyo ambaye tunamiminiwa sisi wengine ambao hata hatustahili…Ni neema ya namna gani?..Tukose kila kitu lakini tusimkose Roho Mtakatifu kwasababu huyo ndiye Muhuri wa Mungu (Waefeso 4:30)..

Je umempokea huyu Roho Mtakatifu?..kama bado fahamu kuwa anapatikana bure kwa yeyote ambaye atamuhitaji, lakini hatumuhitaji kwa mdomo bali kwa vitendo..maana yake ni hii: Ili ashuke juu yako ni lazima utubu kwa kumaanisha kuacha dhambi kweli kweli…kwasababu yeye ni Roho Takatifu ya Mungu, na hivyo haichangamani na uchafu wa aina yoyote,

kwahiyo unatubu kwa dhati kabisa na kwa vitendo..kama ulikuwa unaiba unaacha wizi na kuwarudishia uliowaibia mali zao kama bado unazimiliki, kama ulikuwa unajiuza, unaacha na kufuta namba za wote uliokuwa unajishughulisha nao katika kazi hiyo, kama ulikuwa unafanya uchafu wowote ule kama kujichua, unatazama picha chafu, ulikuwa mfiraji, msagaji, mlaji rushwa, muuaji n.k unaviacha vyote hivyo…kisha unakwenda kwa Yesu, na kumwomba rehema…Na Bwana wetu mwenye huruma akiona umegeuka kwa vitendo namna hiyo…tayari Yule Roho wake Mtakatifu atakuwa ameshakukaribia sana, utaanza kuona ni kama vile ulikuwa unatembea na kuchoka na ghafla nguvu mpya imekuingia…

Na kukamilisha muhuri huo wa Roho Mtakatifu ndani yako, nenda katafute ubatizo sahihi haraka sana, na ubatizo sahihi kulingana na maandiko ni ule wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO…Kumbuka jina la Bwana Yesu ndio Jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu…Hakuna jina lingine tulilopewa sisi wanadamu litupasalo kuokolewa kwalo isipokuwa jina la Yesu.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.

40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

USIMWOGOPE YEZEBELI.

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

JIRANI YANGU NI NANI?

KILA KIUNGO LAZIMA KISHUGHULIKE.

MPINGA-KRISTO

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Kristo hakuitwa Imanueli badala yake akaitwa Yesu?

SWALI: Unabii uliotolewa na Isaya kumuhusu Kristo unasema angekuja kuitwa Imanueli (Isaya 7:14), lakini badala yake tunaona alikuja kuitwa Yesu? Ni kwanini?


JIBU: Tukisoma pale katika Mathayo 1:19-23 Inasema..

Mathayo 1:19 “Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.

20 Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.

22 Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema,

23 Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; NAO WATAMWITA JINA LAKE IMANUELI; YAANI, MUNGU PAMOJA NASI”.

Jiulize ni kwanini biblia haijaishia tu pale kwenye jina Imanueli, badala yake ikamalizia kuandika mpaka tafsiri yake, yaani “Mungu Pamoja nasi”?..Ni Kwasababu msisitizo upo hapo kwenye hiyo tafsiri na sio jina tu..

Ukiangalia tena utaona Malaika anasema “Nao watamwita” Ikimaanisha “sisi” ndio tutakaomwita yeye kuwa ni Mungu ambaye yupo Pamoja nasi..Lakini yeye jina lake hasaa sio hilo bali ni YESU ..ambayo tafsiri yake ni (YEHOVA-MWOKOZI).

Jambo hilo limekuja kutumia kama lilivyo kwasababu sisi ndio tunaojua Yesu kwetu sisi si mwokozi tu, bali ni Zaidi ya mwokozi,..Ni Mungu kwetu, aliyeutwaa mwili akaishi Pamoja nasi..Kama maandiko yanavyosema..

Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu”…..

14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.”

“Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”(Wakolosai 2:9) .

“tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;(Tito 2:13)

Hivyo tunao ujasiri wote wa kusema kuwa YESU ni MUNGU WETU..

Yaani IMANUELI.

Haleluya.

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

nini maana ya haya maneno aliyosema Bwana ; Tuliwapiga filimbi wala hamkucheza; Tuliomboleza wala hamkulia?

 

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

BWANA HUWAJUA HAO WAMKIMBILIAO.

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

Je! kuna ubaya wowote kuwaombea ndugu zetu waliokufa katika dhambi, Mungu awakumbuke katika ufalme wa mbinguni?.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hakuna mtu anenaye katika Roho,kusema Yesu amelaaniwa

SWALI: Mstari huu una maana gani?

1 wakorinto 12:3 “Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

JIBU: Maana yake ni kwamba hakuna mtu aliyejazwa Roho Mtakatifu anayeweza kusema Yesu amelaaniwa, hilo haliwezekani kwasababu mpaka ameshaingia ndani katika Roho hawezi kumwona Yesu kwa namna hiyo….Na vile vile hakuna mtu ambaye hajajazwa Roho Mtakatifu anayeweza kusema Yesu ni Bwana…Ni lazima yeye naye awe katika Roho Mtakatifu kwanza ndio awe na ufunuo huo wa kusema Yesu Ni Bwana,

Vinginevyo atakuwa anatamka kwa mdomo tu, kwamba Yesu ni mwokozi wangu, au Yesu ni Bwana wangu, au Yesu ni njia lakini isiwe imetoka ndani ya moyo wake…akawa anasema kishabiki tu!..au kidini tu au kwa kuiga tu!…wakati ndani ya moyo wake hajapata ufunuo kamili au hajamwelewa Yesu kabisa!…ambao ufunuo huo wa kumwelewa Yesu, unatoka kwa Roho Mtakatifu mwenyewe. Ndio maana hapo anasema pasipo Roho Mtakatifu mtu hawezi kusema Yesu ni Bwana, kutoka ndani ya vilindi vya moyo wake!!…

Na sio hilo tu!…Pia mtu ambaye hana Roho Mtakatifu biblia inasema huyo sio wa Mungu..

Warumi 8:9 “…Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.”

Kwanini sio wake?…Kwasababu huwezi kusema unamjua Mungu wakati kile kinachokufanya wewe umjue yeye hakipo ndani yako….(na hicho kinachotufanya tumjue yeye, na kutufunulia maandiko ni Roho Mtakatifu)…Kamwe hatuwezi sisi kumjua Mungu wala kumwelewa wala kumfuata yeye kwa nguvu zetu, tunamhitaji Roho Mtakatifu huyo ndiye anayetuvuta na kutusogeza kwa Mungu na kutufunulia Yesu ni nani..(Yohana 6:44, Yohana 15:16).

Hivyo ni muhimu sana kuwa na Roho Mtakatifu kwasababu huyo ndio MUHURI wa Mungu kwa mtu, Kama vile alama ya mnyama ilivyo(666), vivyo hivyo alama ya Mungu au muhuri wa Mungu ni Roho Mtakatifu ndani ya mtu (soma Waefeso 1:13, Waefeso 4:30 na 2Wakorintho 1:22).

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?

Wewe u nabii yule akajibu la!..swali huyu ‘nabii yule’ ni nani?

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

IF GOD IS IMPROVING HIS WORKS,WHY DON’T YOU IMPROVE YOURS?

Shalom.

The Bible says: Man shall not live by bread alone, but by every word that proceedeth out of the mouth of God.That means if we diligently study the Word of God we can be sure that our souls are enriched and thus extend our earthly lives.(1Kings 3:14)

As we read the book o Genesis the first chapter we see how the Lord did His work of creating the world in 6 days, and on the seventh day He ended all His works and rest, and blessed that day to show that everything was completely done,

Also, if you read again the second chapter you will see how the Lord gives Adam the instructions of how to live in the garden, he also brought him  all the animals to name them, and he did so, Therefore the life of Adam and all of his creatures went on that way for quite a while.Until one day God looked at Adam and said to himself ‘it is not good this man to live alone’

We read it from..

Genesis 2:18 (KJV)

18 And the Lord God said, It is not good that the man should be alone; I will make him an help meet for him.

Just  imagine someone saying  “It is not good“, what does it signify?, it is clear that he had noticed some shortcomings, and  need to make some improvement so that  to get things going well as he wants.

So it was with God, though he had already created a woman in his mind for a long time, Genesis 1: 27-28 confirms it, the woman was already created before the creation itself begun, but God allowed her not to be there as if he forgot her., So that he could pass this message titled “ IT IS NOT GOOD”, to us to teach us something.

Notice, A woman came to creation later,After Life has been going on for a  space of time probably  1 or 10 or 100 years later.

Now Why did God do it?  He did it because he was teaching us that he is much interested with improvements, Yes his improvements which are of great benefit to us today, try to imagine how this world would be without women, how would it be without the  loving of sister, where would you taste the love of a wife today, what kind of man would you be?., No animal, no bird, no sea creature would give you a sweet confort as a woman could today?..Life would be boring as any other planet up there.

That is why we thank God for giving us this great gift, but that is all due to some improvements he made, if God said I had finished my creation, and on the 7th day I was relaxed, what we see today would not be into existance.

In the same way  God expects us to make changes in our Christian lives, in our ministry of building the kingdom of heaven, not to be contented by saying everything is okay … If God who cannot be wrong improved his works, how much more are we supposed to be improve ourselves..Why be content with the same christian life that you had lived 10 years ago.?

The work of God is falling asleep, the church’s daily structures are collapsing, why not say this Is not right let me donate my money, or my energy to fix them, or my mental experience to the builders to accomplish that structure of the church … God wants us to think that way. Who knows by doing that act you would bring thousands of soul to Christ?

If you feel you have been saved and still you are living in the same situation  for a long time without showing no signs of improving in your prayer line, or ability to  share the gospel with others, you don’t fast, Know that you are out of the purpose of God which you were supposed to be., if we always see  everything  is just well around us,  then we are deceiving ourselves.

It is my prayer that you and I,will begin to learn to say this word IT IS NOT GOOD, in almost every aspect of our Christian lives, Iam sure we will certainly make big changes not only in our lives but also in our ministries.

Please share this message with others.

Blessings.

Related articles:

What was the thorn in Paul’s flesh?

THE BOOK OF LIFE.

WHO HATH BEWITCHED YOU?

THE SPIRIT INDEED IS WILLING,BUT THE FLESH IS WEAK

DON’T BE AFRAID WHEN YOU GO DOWN.

WHERE IS THE POWER OF GOD MANIFESTED? 

Home:

Print this post