Title May 2020

سؤال: ماذا كانت الشوكة في لحم بولس؟

سؤال: ماذا كانت الشوكة في لحم بولس؟

الجواب: دعنا نقرأ ،

2 كورنثوس 12: 7 “لئلا يرفعني فوق القياس من خلال وفرة الوحي ، أعطيت لي شوكة في الجسد ، رسول الشيطان ليعطفني ، لئلا أرفع من فوق القياس.

8 من اجل هذا طلبت من الرب ثلاث مرات ليخرج عني.

9 فقال لي تكفيك نعمتي لان قوتي في الضعف تكمل. لذلك ، بكل سرور ، سأفضل المجد في عيوبي ، حتى تتوقف قوة المسيح علي “

كان هناك الكثير من التكهنات حول الشوكة في جسد بول ، لا يزال البعض يعتقد أنها كانت شوكة حقيقية موضوعة على جانبه ، أنه في كل مرة يحاول التباهي بها فإنه يخترقها.

يقول آخرون أنها ذكرى للأشياء السيئة التي فعلها في الماضي ، لذلك كان الله يجلب له الأفكار التي كانت تحركه ، والتي اتضح أنها شوكة له وتوقف عن التفاخر / التفاخر.

ولكن ، في كل هذا ، إذا نظرنا عن كثب إلى الآية 7 ، فإنها تقول أن الله كان لديه شوكة في جسده “رسول الشيطان”.

تلك الكلمة ، “رسول” ، هي كلمة تعني شخصًا وليس فكرة أو فكرة أو شيء ما. حتى بالمعنى السليم ، ما علاقة شجيرة الشوك بالتفاخر؟

لذلك لم يكن بول يتحدث عن شجيرة شوكة أو بعض الأمراض في جسده ، لكنه كان يتحدث عن شخص كان مثل شوكة له.

الآن سؤال آخر ستطرحه هو لماذا يقول أنه في الجسد وليس في الروح؟

الجواب هو أن كلمة الجسد يمكن أن تعني حياة شخص أو شعب …

دعونا نقرأ الآيات التالية التي قالها الرب لبني إسرائيل وسوف نفهم المزيد.

Numbers 33:55 ولكن ان لم تطردوا سكان الارض من امامكم. فيكون ان الذين تركتهم يبقون في عينيك وشوك في جانبكم ويغشونكم في الارض التي تسكنون فيها.

56 علاوة على ذلك ، سأفعل بك ، كما ظننت أن أفعل بهم “.

Judges 2: 3 3 لذلك قلت ايضا لا اطردهم من امامك. بل يكونون كجواهر في جنبكم وتكون آلهتهم فخا لكم.

هل رأيت أن؟ .. يمكن مقارنة حياة المرء بجسد ، ويمكن تشبيه الشخص الذي يزعجك ويعذبك في حياتك بشوكة في جسمك.

ولكن إذا عدنا إلى الرسول بولس ، فمن كان هذا الشوكة؟

عندما نقرأ .. 2 تيموثاوس 4:14 تقول ..

“الإسكندر النحاسي جعلني شرًا كثيرًا: يكافئه الرب حسب أعماله:

15 منهم تكون ايضا. لأنه صمد كثيرا في كلماتنا “

لم يقدم الكتاب المقدس الكثير من المعلومات عن هذا الإسكندر ، وهو صانع نحاسي. لكنه يخبرنا أنه كان أكبر عقبة لبولس في حياته وخدمته. لم يستخدم كلمة “شرير” فحسب ، بل استخدم أيضًا كلمة “شرير كثير” ، لإظهار أن العديد من الأعمال الشريرة التي أظهرها الإسكندر لبولس.

ربما كان يسيء تمثيل بولس طوال الوقت ، كان يتحدث فقط عن أوجه القصور الخاصة به ، وكيف كان قاتلاً في الماضي (قتل واضطهاد المسيحيين) ، يشهد تصريحات كاذبة أمام الناس الذين آمنوا بولس.

وهذا جعل بول ، الذي اشتهر بالكثير من الوحي ، والكثير من المعجزات ، والخدامات العظيمة ، يبدو أنه لا يوجد في وسط بعض الذين آمنوا به.

ليس من غير المعتاد رؤيتها اليوم ، يمكنك رؤيتها للعديد من قادة العالم ، الله يرفع خصومهم كشوكة لهم ، للتحدث فقط عن شرهم ، أو عيوبهم ، بغض النظر عن عدد الأشياء الجيدة التي قام بها القائد. سمح الله بذلك حتى لا يتفاخر القائد كثيراً.

كان هذا هو الحال مع بولس بالنسبة للإسكندر الحداثي البرونزي. كان شوكة عظيمة ، حتى توسل الله أن يأخذه ، (ليقتل)

اقرأ ، ١ تيموثاوس ١: ٢٠ “منهم هميناوس والاسكندر. الذي سلمته للشيطان ، لكي لا يتعلموا التجديف “

لكن الله أخبره أن نعمته كانت كافية. لذلك بقي معها حتى وقته قد انتهى.

وبالمثل ، إذا كنا متغطرسين ، فإننا نعتقد أننا شيء ما ، فقد قمنا بشيء أفضل من الآخرين ، أو لدينا شيء أكبر من الآخرين.

لنتذكر أن الرب يستطيع أن يرفع لنا الشوك.

شالوم مران عطا!

يرجى مشاركة هذه الأخبار الجيدة مع الآخرين ، وكذلك إذا كنت ترغب في أن نرسل إليك هذه الدروس عبر بريدك الإلكتروني أو WhatsApp أرسل لنا رسالة في مربع التعليق أدناه أو اتصل عل+255 789001312(tanzania country code)


من أين حصل قايين على زوجته؟

ما هو كتاب الحياة؟

من هو الجشورون في الكتاب المقدس؟

التنين القديم

Print this post

What was the thorn in Paul’s flesh?

QUESTION: What  was the thorn in Paul’s flesh?

Ans: Let’s read,

2 Corinthians 12:7 “ And lest I should be exalted above measure through the abundance of the revelations, there was given to me a thorn in the flesh, the messenger of Satan to buffet me, lest I should be exalted above measure.

8 For this thing I besought the Lord thrice, that it might depart from me.

9 And he said unto me, My grace is sufficient for thee: for my strength is made perfect in weakness. Most gladly therefore will I rather glory in my infirmities, that the power of Christ may rest upon me”

There has been a lot of speculation about the thorn in Paul’s body, some still think it was a real thorn placed on his side, that every time he tries to brag then it pierces him.

others say it is a memory of the bad things he did in the past so God was bringing him thoughts that were stirring him up, and that turns out to be like a thorn to him and he stops bragging/boasting.

But, in all of this, if we look closely at verse 7, it says that God had a thorn in his body a “messenger of the devil”.

That Word, “messenger”, is a Word that means a person and not some idea or some thoughts or something. Even in the common sense what does the thorn bush have to do with bragging?

So Paul wasn’t talking about a thorn bush or some disease in his body, but he was talking about someone, who was like a thorn to him.

Now another question you will ask is why does it say it is in the body and not in the spirit?

The answer is that the word body can mean the life of a person or people…

Let’s read the following verses that the Lord was telling the children of Israel and we will understand more.

Numbers 33:55 “ But if ye will not drive out the inhabitants of the land from before you; then it shall come to pass, that those which ye let remain of them shall be pricks in your eyes, and thorns in your sides, and shall vex you in the land wherein ye dwell.

56 Moreover it shall come to pass, that I shall do unto you, as I thought to do unto them”.

Judges 2: 3 “Wherefore I also said, I will not drive them out from before you; but they shall be as thorns in your sides, and their gods shall be a snare unto you”

Have you seen that? .. one’s life can be compared to a body, and the person who is disturbing and torturing you in your life can be likened to a thorn in your body.

But if we return to the Apostle Paul, Who was this thorn?

When we read .. 2Timothy 4:14 says ..

“Alexander the coppersmith did me much evil: the Lord reward him according to his works:

15 Of whom be thou ware also; for he hath greatly withstood our words”

The Bible has not given much information about this Alexander, a coppersmith. But it tells us he was Paul’s greatest obstacle, in his life and ministry. He used not only the word “evil” but the word “much evil”, to show that many evil deeds this Alexander showed Paul.

Probably, he was just misrepresenting Paul all the time, he was only talking about his own shortcomings, how he had been a killer in the past (killing and persecuting Christians), witnessing false statements before people who believed in Paul.

And that made that Paul, who is famous for so many revelations, and many miracles, and great ministries, seemed to be nothing in the midst of some who believed in him.

It is not unusual to see it today, you can see it for many world leaders, God raises up opponents as a thorn for them, to speak only of their evil, or their shortcomings, no matter how many good things that leader has done. God permits this so that the leader does not boast too much.

Such was the case with Paul for the bronze-smithing Alexander. He was a great thorn, until he begged God to take him away, (to be killed)

Read, 1 Timothy 1:20 “Of whom is Hymenaeus and Alexander; whom I have delivered unto Satan, that they may learn not to blaspheme”

but God told him His grace was sufficient. So he remained with it until his time was over.

Likewise with us, if we are arrogant, we think we are something, we have done something better than others, or we have something bigger than others.

Let us remember that the Lord can lift up the thorns for us.

Shalom, Maran atha!

Please share this good news with others, and also if you would like us to send you these lessons via your email or WhatsApp send us a message in the comment box below or call +255 789001312


OTHER TOPICS:
NEHUSHTAN (THE BRONZE SERPENT).
THE SPIRIT INDEED IS WILLING,BUT THE FLESH IS WEAK
What did God mean to say deny yourself?

Home:

Print this post

Tofauti kati ya kuungama na kutubu ni ipi?

Kuungama kunakwenda sambamba na kutubu.

Kuungama ni kitendo cha kukiri, au kukubali makosa yako kuwa wewe ni mwenye dhambi au ulikosa na hivyo unahitaji kusamehewa.

Mathayo 3:5 “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;
6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao”.

 

Matendo 19:17 “Habari hii ikajulikana na Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawaingia wote, na jina la Bwana Yesu likatukuzwa.
18 Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao”.

 

1Yohana 1:8 “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.
9 Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

Lakini kutubu ni kitendo chenyewe cha kujutia  yale uliyoyaungama tayari (yaani makosa yako)..Ili usamehewe. Na hii inaambatana na kukusidia kuyaacha kivitendo yale uliyokuwa unayafanya kwa kuomba msamaha .

Mathayo 12:41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona”.

 

Mathayo 21:28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu.

29 Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende.

30 Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda.

31 Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Basi Yesu akawaambia, Amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu.

32 Kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini, nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.”

Na ndio maana mtu hawezi kusema nimetubu kama hajaungama dhambi zake, Yaani hajakubali kuwa amekosa mbele za Mungu, kwamba yeye ni mwenye dhambi na hivyo anahitaji rehema.

Mithali 28:13 “Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema”.

Hivyo kutubu kunaambatana na kuungama, kama ukienda mbele za Mungu halafu huoni kosa lako nini, basi hapo hakuna toba yoyote.

Ubarikiwe.

 

Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

 

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

Rudi Nyumbani:

Print this post

KILA KIUNGO LAZIMA KISHUGHULIKE.

Kanisa la Kristo limefananishwa na mwili wa binadamu. Kama vile mwili ulivyo na viungo mbalimbali, mfano mikono, miguu, macho, masikio, mdomo n.k. vikiongozwa na kitu kimoja cha muhimu kiitwacho kichwa. Vivyo hivyo na kanisa la Kristo. Biblia inasema sisi tu viungo mbalimbali na kichwa chetu ni Kristo.

Sasa kama vile katika mwili tunajua hakuna kiungo hata kimoja kisichokuwa na shughuli yoyote vivyo hivyo sisi kama viungo hakuna hata mmoja anayesema ameokoka akawa hana shughuli yoyote ya  kufanya katika mwili wa Kristo. Tena sifa nyingine ya viungo ni  kwamba vyote huwa vina vinashirikiana kwa umoja usiokuwa wa kawaida.

Waefeso 4:16 “Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo”.

Umeona huwezi kusema umeokoka, miezi inapita, miaka inapita, hakionekani chochote unachokichangia katika mwili wa Kristo,..Ukiona hivyo basi ujue ulishakufa kutoka katika mwili wa Kristo, na hivyo ulishakatwa na kutupwa nje siku nyingi. Hutambuliki, ukijiona ni wa kuhubiriwa tu daima, lakini wewe hakionekani chochote unachomfanyia Kristo,ni lazima ujitathimini tena mara mbili wokovu wako.

Tabia ya viungo vilivyo hai vya Kristo ni hizi.

1.Kwanza kiungo kinakuwa kinalihudumia kanisa la Kristo kwa mali zake: Ni jukumu la kila mkristo kumtolea Mungu ili kazi ya injili izidi kuenda mbele, na hii sio tu kwamba inawahusu wanaopelekewa injili tu, bali pia kwa Yule anayeipeleka injili, yeye pia anao wajibu wa kumtolea Mungu, sehemu ya alivyo navyo kwa kadiri alivyokirimiwa neema.. Kwasababu jukumu hilo ni la kila kiungo.

2. Pili ni wajibu wa kila kiungo kuliombea kanisa: Maombi ni sehemu ya maisha ya mkristo yoyote, ni lazima aliombe kanisa lote la Mungu kwa ujumla duniani kote, Si rahisi kukutana viungo vyote kwa wakati mmoja, lakini maombi yanawakutanisha katika roho..Hata viungo katika mwili si vyote vinavyokutana, lakini vinajuana, na kusaidiana kwa kuchukuliana udhaifu, vivyo hivyo na sisi, kuliombea kanisa la Kristo ni wajibu wetu kila siku kama wakristo. Macho hayawezi kujiosha yenyewe ni lazima mikono iisaidie, na kadhalika hata mkono mmoja unauhitaji mkono mwingine..

3. Tatu; Kiungo ni lazima kifanye kazi ya kupeleka habari njema kwa wengine: Jukumu ambalo tulipewa wote na Bwana wetu ambaye ni Kichwa, ni kwamba tuenende ulimwenguni mwote, tukawafanye mataifa kuwa wanafunzi (Mathayo 28:19).. Hivyo kila mmoja wetu kwa jinsi alivyopewa karama, anayowajibu wa kuifanya kazi ya kuwahubiria wengine kwa jinsi awezavyo. Ikiwa ni muhubiri, unawajibu wa kuhubiri kwa bidii, ikiwa ni mwinjilisti, mwalimu, mtume, nabii, mwimbaji, mwandishi, n.k. Unafanya vyote kwa bidii, na katika Roho na kweli..Na hiyo inathibitisha kuwa wewe ni kiungo kilicho hai.

Hizo ni ndizo dalili zinazothibitisha uhai wa viungo vya Kristo.  Lakini ni kwanini watu wengi wanaosema ni wakristo wamekosa vigezo hivyo  vitatu kwa pamoja?

Ni kwasababu hawataki kukaa ndani ya Kristo kumtii yeye, ambaye ndiye anayewajalia watu uhai huo. Ndugu usipokitii kichwa, kamwe huwezi kufanya lolote mwilini. Bwana Yesu mwenyewe alisema.

Yohana 15:4 “Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.

15 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

6 Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea”.

Umeona,..Ukiwa hutakubali kumaanisha kuyasalimisha maisha yako moja kwa moja kwa Kristo, yaani kukataa maisha ya mguu mmoja ndani mwingine nje, kamwe hutaweza kuwa kiungo hai, hata iweje. Wewe utakuwa ni sawa na tawi lililokatwa linangojea tu kutupwa motoni. Na pia kumbuka huwezi kuwa na karama zote, hata viungo vya mwili vinatufundisha, lakini utakuwa na karama yako ya kipekee ambayo itakuwa ya muhimu katika kanisa la Kristo.

Huu ni wakati wa wewe, kufanyika kiungo hai Kristo..Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi tubu makosa yako, mrudie Kristo, nenda kabatizwe kama ulikuwa hujabatizwa ipasavyo hapo kabla, kwa ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji tele sawasawa na (Yohana 3:23 na Matendo 2;38). Kisha kuanzia huo wakati anza kuishi maisha yanayouhakisi wokovu.

Na kuanzia huo wakati  wewe mwenyewe utaona tu, Kristo anavyoanza kukutumia kwa ile karama atakayoishusha ndani yako..Na wewe pia utakuwa kiungo chenye kazi yake maalimu ndani ya mwili wa Kristo. Siku ile ya mwisho kikisubiriwa kupewa heshima yake ya kipekee.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

Jina la Bwana Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze maneno ya uzima.

Biblia inasema..

Ufunuo 14:14 “Kisha nikaona, na tazama, wingu jeupe, na juu ya wingu hilo ameketi mmoja, mfano wa Mwanadamu, mwenye taji ya dhahabu juu ya kichwa chake, na katika mkono wake mundu mkali.

15 Na malaika mwingine akatoka katika hekalu, akimlilia kwa sauti kuu yeye aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu, Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa.

16 Na yeye aliyeketi juu ya wingu akautupa mundu wake juu ya nchi, nchi ikavunwa”.

Ndugu saa ya mavuno, ipo karibu sana..tena Sanaa.. Utauliza tunajuaje kuwa ipo karibu? Tunajua kutokana na jinsi tunavyoona magugu na ngano yanavyojitenga kwa kasi katika kanisa la Mungu, na katika dunia kwa ujumla. Baadhi ambao walikuwa wanasema huyo Yesu mbona hahukumu dunia, nataka niwaambie wapo kwenye uwezekano mkubwa sana wa kukumbana na hukumu hiyo wakiwa bado hai, kama hawatageuka..

Hawajui kuwa Siri ya Mungu ya kutowahukumu waovu tangu zamani, imejificha ndani ya ule mfano wa magugu na ngano ambao Bwana Yesu aliutoa kwa makutano, embu tusome kidogo..

Mathayo 13:24 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;

25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.

27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?

28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?

29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.

30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

Na tafsiri yake ilikuwa ni hii..

37 Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni Mwana wa Adamu;

38 lile konde ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme; na yale magugu ni wana wa yule mwovu;

39 yule adui aliyeyapanda ni Ibilisi; mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika.

40 Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia.

41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,

42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Hakuyang’oa magugu, kwasababu magugu yakiwa machanga ni ngumu kuyatambua, yanafanana sana na ngano.

Vivyo hivyo Zamani ilikuwa ni ngumu sana kuwatambua watu ambao ni mashoga katika kanisa la Kristo, Lakini leo hii tunawaona tena wana vyama vyao na viongozi wao katika hayo wanayoyaita makanisa yao. Zamani, ilikuwa ngumu kuona mtu anayejiita mkristo halafu ni mzinzi, lakini leo hii utawaona tena kwa mavazi yao ya kikahaba , utaona waasherati wazi wazi katika nyumba ya Mungu, na wengine wanajiita wachungaji na manabii…Wahuni ilikuwa ni ngumu kuwajua ndani ya kanisa, lakini leo utawaona wazi wazi..n.k

Mambo hayo kama ukifuatilia historia utaona Kuanzia karne ya 19 kushuka chini, hayakuwepo kabisa,..Vilevile dunia nzima ilikuwa inaamini walau kuna kitu kinachoitwa Mungu..Lakini leo hii, utaona wimbi kubwa la watu ulimwenguni lisiloamini Mungu kabisa..Hiyo ni ishara kuwa ngano na magugu tayari yameshajitenga, na kukomaa..Ulikuwa huwezi kuona mkristo anajihusisha na miziki ya kidunia, lakini leo hii utawaona kwa staili za uimbaji wao..

Utajiuliza ujasiri wote huo wameutolea wapi?.. Sio ujasiri, bali ni magugu yamekomaa sasa, yanajitofautisha na ngano halisi za Mungu. Haziwezi kuishi Maisha matakatifu kwasababu zenyewe hazikuwa ngano tangu awali, mwanzoni zilijifanya tu kama wakristo ili zipate hifadhi ya mvua ya neema, lakini sasa zimeshakua hazihitaji tena kujificha..

Na hiyo ndio inayokwenda kupelekea wavunaji (malaika) wa Bwana, waje kuuvuna ulimwengu huu wakati sio mwingi.

Wawafunge matita matita, kabla ya kwenda kuwateketeza kwenye lile ziwa la moto. Na hiyo inakuja pale mtu anapohubiriwa njia ya kweli lakini anashupaza shingo yake, wale malaika wanachofanya ni kumtia muhuri, ambayo ndio Kamba yenyewe. Sasa Hilo likishakutokea basi mtu huyo ni ngumu kumgeukia Mungu, ataendelea kuwa hivyo hivyo mkaidi, mpaka mwisho…

anachosubiria ni hukumu tu ya mwisho. (Na hiyo ni kulingana na maandiko na sio kumhukumu Mtu). Wokovu hauna uvuguvugu..

Hichi si kipindi tena cha kuishi Maisha ya kutokujali, si wakati wa kufurahia maovu kanisani, si wakati wa kuiga kila staili ya Maisha inayozuka ulimwenguni, si wakati wa kupokea kila aina ya elimu za uongo zinazohubiriwa na manabii wa uongo, Huu si wakati wa kushikilia dini, Bali Ni wakati wa kuujenga uhusiano wako wewe na Mungu. Kabla ya nyakati za hatari hazijafika..

Kumbuka..Yule malaika alimbiwa..

Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa.

Kipindi chenyewe ndio hichi.. Je! Unasubiria uwekwe kwenye kundi la magugu? Kama sivyo basi yasalimishe Maisha yako kwa Kristo na yeye atakuponya. Kimbilia msalabani upate wokovu wa kweli, ambao sasa unapatikana bure, utafika wakati hautapatikana kabisa.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

SWALI: Je ni sahihi kualikwa kwenye karamu za watu wasio wakristo (mfano waislamu kwenye sikukuu zao za eid au futari) na kula nao ni dhambi?


JIBU: Swali hili jibu lake lipo katika kitabu cha 1Wakorintho 8, Mtume Paulo kwa uweza wa Roho alifafanua jambo hili, akasema chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu (Maana yake hakitusogezi mbele za Mungu)..tukila hatuonekani watakatifu mbele za Mungu na wala tusipokula hatujipunguzii kitu kutoka kwa Mungu…(1Wakorintho 8:8).

Tunajua Mungu ni mmoja na ndiye aliyeumba vitu vyote, Naye ni Yehova, sababu hiyo basi hakuna mchele wowote ulioumbwa na shetani, wala muhogo ulioumbwa na mungu fulani mwenye jina fulani aliyeko Asia, wala hakuna pilipili iliyoumbwa na mungu fulani aliyopo mashariki ya kati tofauti na Yehova, n.k. vyote hivyo vinatoka kwake.

Hiyo ikiwa na maana kwamba chakula chochote kilichopikwa kwa mimea au viungo vyovyote vinavyopatikana katika dunia tunayoiishi vimetengenezwa na Mungu mmoja na ni halali kuliwa. Ukipita njiani na kukuta mpera na una njaa usiogope kula! Hakuna chochote kitakachokupata, ukitumiwa zawadi ya chakula fulani na baada ya kumshukuru Mungu kile kwa Imani, utakuwa hujafanya kosa lolote mbele za Mungu.

Ukifika mahali umekaribishwa chakula usianze kuuliza uliza kimetoka wapi, au kimepitia wapi au kimetengenezwa na nini…wewe baada ya kumshukuru Mungu kula!, lakini wenyewe wakikwambia chakula hichi ni wakfu kwaajili ya miungu yetu hapo usile kwasababu ukila utawafanya na wao waamini kwamba miungu yao ipo sawa…na kama kuna mkristo aliyemchanga kiroho karibu yako akikuona umekula chakula hicho atashawishika kuamini kwamba ni sahihi kuabudu hiyo miungu na hivyo utamsababisha aanguke kitu ambacho hakimpendezi Mungu mtu yoyote apotee..Kwahiyo kwaajili ya dhamira za hao watu ili wasitie muhuri ibada hizo, hapo tu ndio biblia imetukataza tusile…

Na kuna tofauti ya “chakula cha sherehe” na “chakula cha sadaka”…Chakula kinachopikwa kwenye sherehe ya mtu asiyeamini sio chakula kinachotolewa sadaka, hata Bwana alialikwa mara nyingi na watu wenye dhambi na wasioamini na alikula …chakula kinachotolewa sadaka ni kwa mfano unakuta labda kuna msiba umetokea, na wahusika wananjinja kuku fulani maalumu wa kimatambiko na damu yake imemwagwa sehemu fulani na nyama ya yule kuku inapaswa iliwe na watu fulani maalumu..sasa nyama ya yule kuku aliyefanyiwa matambiko ndio mfano wa chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, hicho ndio tunapaswa kuwa nacho makini…Lakini pilau iliyopikwa au chakula kingine chochote kilichopikwa kwenye huo msiba kisichohusisha matambiko sio chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu….Na sherehe ni hivyo hivyo.

1Wakorintho 10:25 “Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri; 26 maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo.

27 Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.

28 Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri.

29 Nasema, dhamiri, lakini si yako, bali ya yule mwingine. Maana kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?

30 Ikiwa mimi natumia sehemu yangu kwa shukrani, kwa nini nitukanwe, kwa ajili ya kitu nikishukuriacho?

31 Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.

32 Msiwakoseshe Wayahudi wala Wayunani wala kanisa la Mungu,

33 vile vile kama mimi niwapendezavyo watu wote katika mambo yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila faida yao walio wengi, wapate kuokolewa.”

Kwahiyo ikiwa ni ndugu yako au jirani yako (labda ni muislamu au mhindu ), na amekualika kwake au kwenye sherehe yao na amekuandalia chakula kwajinsi anavyojua yeye…kula bila kuhojihoji hufanyi dhambi kwa Mungu….isipokuwa tu amekupa chakula kilichotolewa sadaka na amekueleza

Mada Nyinginezo:

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

 

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

Kwanini Bwana aliongea na Abramu baada ya kutengeana na Lutu?

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Zile mbao mbili za mawe Musa alizoambiwa achonge zilikuwaje?

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

RABI, UNAKAA WAPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

Habari ya uumbaji ina mafunzo mengi sana. Biblia inatuambia Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke kwa mfano wake(Mwanzo 1:27). Lakini katika siku sita za uumbaji, Tunaona kulikuwa na uumbaji mmoja muhimu ulikosekana., Embu tengeneza picha mpaka Mungu anastarehe siku ya saba, mwanamke hakuwepo,..Ni kama vile Mungu alijifanya amemsahau hivi..Lakini kulikuwa na sababu kubwa mno ya yeye kufanya hivyo.

Alimwacha Adamu awepo peke yake duniani kwa kipindi fulani kirefu, aone uumbaji wake wote, aushangae huo, aseme ama kweli Mungu ameumba..kila kitu kweli ni kizuri, tazama jua, tazama, nyota, tazama twiga, tazama nyangumi, tazama hiki tazama kile, vyote ni vikamilifu, vimejitosheleza kweli kweli, sihitaji kingine…

Lakini hakujua kuwa Mungu alikuwa hajaukamilisha uumbaji wake bado (hiyo siri alikuwa nayo mwenyewe), ameihifadhi mpaka wakati mtimilifu utakapofika.

Sasa baada ya Mungu kumuacha Adamu kwa kipindi chote hicho kirefu, pengine miezi, miaka inapita aendelee kufikiria hivyo hivyo kuwa kila kitu ndio tayari, mpango wote umekamilika, Mungu kamaliza uumbaji wake, , shughuli zinaendelea kama kawaida bustanini.. Lakini wakati ulipofika wa Mungu kuikamilisha kazi yake alishuka bustanini tena kama muumbaji yule yule wa zamani..

Tungeweza kudhani labda angeshuka ardhini amtoe mwanadamu mwingine kwenye udongo mwekundu, lakini mambo yalikuwa ni tofuati, alimkabili Adamu moja kwa moja..Na mara moja Akamletea usingizi mzito sana. Wakati Adamu akiwa ndotoni, mkono wa Mungu ulianza kupita sehemu ya ubavu wake, pengine mfano wa kisu kikali(hatujui), tunachojua ni kuwa aliundoa ubavu wake mmoja, jaribu kutengeneza picha operasheni iliyokuwa inafanyika pale ni ya namna gani..Si ajabu hata Mungu alimletea usingizi mzito..

Hatushangai hata madaktari wa leo wameiga mbinu hiyo ya Mungu ya kufanya operasheni, yaani kumpiga kwanza mtu nusu-kaputi ili apotelee usingizini kabla ya kumfanyia matibabu makubwa..Wanafanya hivyo Si kwamba hawapendi mtu aone operasheni ile hapana, kwanza ni ili kuepuka usumbufu, chukulia mfano ikiwa mtu yule ataona tumbo linakatwa na utumbo unatolewa nje au anaona kichwa chake kinapasuliwa, anaweza asikubali, au akaogopa kupitiliza na mwisho wa siku akasababisha operesheni isiende vizuri au hata kifo kabisa..Na ndivyo ilivyokuwa kwa Mungu..Alikuwa anamfanyia Adamu operasheni yenye umakini sana, ya kuumba kitu bora kuliko vyote alivyovifanya ndani ya siku zile 6.. Hivyo ikamgharimu atafute njia itakayomfanya awe na utulivu, na ndio akatumia njia ya usingizi mzito, kwasababu kinachokwenda kuumbwa ni bora sana.

Sasa Mungu alipomaliza kuutoa ubavu wake mmoja, akarudishia nyama eneo lile, ndipo akauchukua ule ubavu akamuumbia Hawa. Na kazi ilipomalizika, bwana Adamu akazinduka usingizini, kujitazama anajiona kama vile mwili umepungua, na kuangalia pembeni anamwona mgeni, ambaye si wa pale bustanini. Na kumtazama vizuri anaona hafanani na swala, hafanani ni mbuzi bali anafanana na yeye, anazungumza kama yeye, anaumbile linalokaribia kufanana na la kwake.. Hapo ndipo alipogundua kuwa ni ile sehemu ya mwili wake ameumbwa yule mtu.

Na Adamu alipomwangalia tena hakuona wa kulinganishwa naye katikati ya uumbaji wote ambao Mungu alishawahi kufanya.

Sasa Ni jambo gani Mungu alikuwa anamwonyesha Adamu?

Alikuwa anamwonyesha kuwa uumbaji wake bora unatoka ndani ya mtu, na si penginepo.. Hakuna mwanaume asiyejua katika uumbaji wote wa Mungu hakuna hata kimoja kinachoweza kufananishwa na mwanamke.

Vivyo hivyo somo hilo Mungu hakumfundisha Adamu tu peke yake,..Bali na Hawa pia, pale alipomwekea uwezo wa kubeba mimba, ambapo aliruhusu kiumbe kikae ndani ya tumbo lake kwa miezi 9, lakini baada ya ya hapo, ghafla anatokea tena mwanamume..

Na vivyo hivyo hakuna mwanamke asiyejua kuwa katika uumbaji wote wa Mungu, hakuna kilichoumbwa bora kama mwanamume…Lakini mwanamume huyo anatoka katika tumbo lake na sio mbinguni au ardhini tena. Na kwa kupitia mzunguko huo huo duni leo imejaa watu.

Mambo hayo hayo yanaendelea rohoni hata sasa, Uumbaji mkamilifu wa Mungu unatimia ndani ya Maisha ya wanadamu..ikiwa tu tutamruhusu aifanye kazi yake mwenyewe ndani yetu bila kusumbuliwa..Mungu anataka kufanya makubwa kupitia sisi, kuliko angefanya yeye mwenyewe. Lakini ni sisi hatuwi watulivu kufanyiwa operasheni.

Tunashindana na Mungu, kwa mambo mengi maovu,anapotuambia tuache Maisha ya dhambi, hatuwi tayari kufanya hivyo, tunapoambiwa tusivae nguo zisizompa Mungu utukufu hatuwi tayari, tunapoambiwa tuombe, hatutaki, tunapoambiwa tuikimbie zinaa sisi tunairidhia, biblia inapotuonya tuache hiki au kile hatutaki kutii, tunachosema ni Mungu haangalii mwili anaangalia mavazi, tunapoambiwa tujitenge na mambo ya ulimwengu, tunamwona kama anatunyima uhuru wetu, kila siku tunashindana na mkono wake.. na wakati huo huo tunataka Mungu aumbe mambo makubwa maishani mwetu..Ataumbaje katika hali hiyo ya masumbufu?

Mungu anahitaji utulivu wa roho, tukiukosa huo tusitazamie uumbaji wowote. Tusitazamie Mungu kufanya miujiza maishani mwetu. Ikiwa wewe ni mwenye dhambi, huu ni wakati wako sasa wa kumrudia Mungu, Anza kujenga uhusiano wako vizuri na Mungu, ndipo Mungu naye achukue nafasi ya kuumba mambo mazuri ndani yako.

Tubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, na pia nenda kabatizwe kulingana na matendo 2:38, na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu atakayekuongoza na kukutia katika kweli yote na kukupa utulivu wa roho.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

MJUMBE WA AGANO.

Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

KUWA WEWE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

Jibu la swali hili linahitaji unakini mkubwa kwasababu lisipoeleweka vizuri ni rahisi kusema biblia ina ubaguzi wa kijinsia au biblia haimaanishi hivyo inavyomaanisha.

Hebu tusome mistari michache ifuatayo..

1Wakorintho 11:3 “Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.

4 Kila mwanamume, asalipo, au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaaibisha kichwa chake.

5 Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa.

6 Maana mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele. Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa, na afunikwe.

7 Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.

8 Maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke katika mwanamume.

9 Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume.

10 Kwa hiyo imempasa mwanamke awe na DALILI YA KUMILIKIWA KICHWANI, kwa ajili ya malaika”.

Katika mistari hii Mtume Paulo aliindika kwa uongozo wa Roho Mtakatifu ili kufikisha ujumbe kwa kanisa lote la Mungu kwa wote watakaosoma waraka huo, na waraka huo haukuwahusu wakorintho tu kama wengi wanavyotafsiri..bali ililihusu kanisa la Kristo kwa ujumla, ikiwemo na sisi watu wa nyakati hizi za mwisho.

Sasa kama ukisoma mistari hiyo utaona, Imejikita sana katika Eneo la KICHWA…Na imezungumzia vichwa vitatu…1) kichwa cha Kristo, 2) Kichwa cha Mwanamume 3) Kichwa cha mwanamke…

Tukianza na kichwa cha Kwanza, ambacho ni cha Kristo, biblia imekitaja kuwa ni Mungu mwenyewe…maana yake aliyekuwa na mamlaka juu ya Kristo ni Mungu peke yake, ambaye ndiye Baba yake..

Na pili kichwa cha Mwanamume ni Kristo..maana yake ni kwamba..Kristo ndiye mwenye mamlaka juu ya kila mwanamume…

Na tatu kichwa cha kila mwanamke ni mwanamume…Maana yake ni kwamba mwenye mamlaka juu ya mwanamke ni mwanamume…Na mamlaka hayo mwanamume alipewa na Mungu pale Edeni (Mwanzo 3:16)

Sasa kwasababu mwanamume ndiye kichwa cha Mwanamke…basi mwanamke ni lazima aonyeshe dalili au ishara ya kumilikiwa katika kichwa chake…na ishara hiyo sio nyingine zaidi ya kufunika kichwa…Ni kama vile ulivyo utaratibu wa mwanamke kuvishwa shela linalofunika mpaka kichwa wakati wa harusi au anapovishwa pete, ni kuonyesha ishara ya kumilikiwa na mwingine…Ndivyo hivyo hivyo kila mwanamke anapaswa afunike kichwa anapokuwa kanisani kuonyesha ishara ya unyenyekevu, na ya kumilikiwa na wanaume ambao ndio vichwa vyao.

Sasa wengi wakisikia hili neno kutawaliwa/kumilikiwa wanachukia na linawakwaza!..wanadhani wameambiwa waabudu wanaume, (kumbuka anayestahili kuabudiwa ni Bwana wetu mmoja tu Yesu Kristo)!..Lakini katikati yetu wanadamu Mungu katuweka chini ya milki ya watu wengine,ili kufikisha ujumbe Fulani wa rohoni. Kwamfano Mtoto yoyote yule awe wa kiume au wakike anapokuwa mdogo anakuwa yupo chini ya milki ya wazazi wake, kwa faida yake huyo mtoto…Sasa mtoto akichukia kumilikiwa na wazazi wake atakuwa ni mgonjwa, kwasababu Mungu akitaka kumlisha au kumbariki ni lazima atumie wazazi wake/walezi wake kumbariki huyo mtoto. Na ndio hivyo hivyo, katika roho wanawake wote ni milki ya wanaume, ndivyo Mungu alivyopenda iwe hivyo, hakuna awezaye kubadilisha, na hiyo pia ni kwa faida ya wanawake..

Mwanamke yoyote anayekataa kutawaliwa au kumilikiwa na mwanamume akidhani atakuwa anamwabudu, anajimaliza mwenyewe!…ukitaka mambo yako yaende sawa kubali kumilikiwa, lakini ukitaka laana kataa kumilikiwa!…Vivyo hivyo unapokuwa kanisani mwanamke ukitaka ufaidike na ibada yako FUNIKA KICHWA CHAKO!, kama ishara ya kumilikiwa!…na tena biblia hapo kwenye mstari wa 10 inasema wazi kabisa kwamba “kwaajili ya malaika funika kichwa chako”….Maana yake ni kwamba malaika wa Bwana wanaopita kanisani kwaajili ya kuwahudumia watakatifu kulingana na Waebrania 1:14, wanapopita na kukuta kichwa chako kipo wazi, na tena umeweka wigi, au rasta hawawezi kukuhudumia…

Na ndio kazi ya shetani kuyafanya yale mambo madogo yaonekane sio maana sana, ili watu wasipate Baraka kutoka kwa Mungu..

Funika kichwa mwanamke wa kikristo uwapo ibadani, hilo ni Neno la Mungu na lipo katika agano jipya na si la kale, Usilidharau Neno la Mungu kwa kiburi cha kupandikiziwa na shetani, usikubali shetani akichezee kichwa chako..kumbuka ndio utukufu wako upo hapo, biblia inasema hivyo.

Kama maneno haya unafikiri ni ya uongo, hebu fanya utafiti siku moja, kisafishe kichwa chako, vaa vizuri, funika kichwa chako kwa kitambaa/kilemba, halafu nenda kanisani..utaona utofauti wa siku hiyo na siku nyingine, ndipo utakapojua kuwa Neno la Mungu sio uwongo…Utaona hata maneno yanayotoka katika kichwa chako yanakuwa na nguvu na uweza, hata uombaji wako utakuwa tofauti,,utatembea na jeshi la malaika wa mbinguni. Vilevile jambo hilo linaambatana na kujisitiri, ukiwa ni mwanamke wa kuvaa ovyo ovyo tu kila mahali, kamwe hutakaa uuone utukufu wa Mungu haijalishi utasema wewe umeokoka kiasi gani.

Hilo ni Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

NI NANI ALIYEWALOGA?

USIMZIMISHE ROHO.

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu aliitaja Tiro na Sidoni, kwamba kama ingeliona miujiza ile aliyoifanya kule Bethsaida ingalitubu kwa kuvaa magunia na majivu. Kwani miji hii ilikuwa ni ya namna gani, na ilifanya kosa gani?


JIBU: Tusome..

Mathayo 11:21 “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.

22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.

23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo”.

Ukitazama kwa karibu utaona Bwana Yesu aliiona miji hiyo miwili (yaani Tiro na Sidoni), ilifanana na Sodoma na Gomora kwa tabia zake.

Kumbuka Sodoma na Gomora iliangamizwa kwa maovu yaliyopindukia, Vivyo hivyo Tiro na Sidoni ziliangamizwa, lakini wengi wetu hatufahamu iliangamizwaje? Na Kwa kosa gani..Na hiyo ni kutokana na kwamba habari zao hazipo wazi sana katika biblia kama vile zilivyokuwa za Sodoma na Gomora.

Jaribu kufikiria mpaka biblia inamfananisha mfalme wa Tiro na Shetani mwenyewe..Ujue kuwa ilikuwa inamwangaza shetani mwenyewe duniani kwa tabia zake..Tutakuja kuona huko mbele..

Sasa ukisoma agano la kale, utagundua kuwa mji huu ulikuwa ni mkubwa sana kibiashara hususani ule wa TIRO, Ujenzi wa Hekalu la Mfalme Sulemani kwa sehemu kubwa ulitegemea njenzo na vifaa kutoka katika nchi hizi mbili (Soma 1Nyakati 22:4)..

Hivyo enzi zile za wafalme, mataifa haya mawili yalitajirika kwa haraka sana, japokuwa mataifa kama Babeli na Ashuru yalikuwa bado yapo juu yao, lakini mataifa haya mawili yalikuwa na nguvu kubwa sana kiuchumi, ni sawa leo tuyaite CHINA, huku Babeli na Ashuru yabakie kuwa , Marekani na Urusi. Jinsi leo hii China ilivyochangamka kibiashara ndivyo ilivyokuwa miji hiyo miwili.

Sasa ukipata muda unaweza kusoma kitabu cha Ezekieli kuanzia sura ya 26 mpaka ya 28, Ujione jinsi mataifa haya yalivyosifiwa na Mungu kuwa imara kibiashara na kiuchumi, Na jinsi Mungu alivyoyatamkia maangamizo yao, siku moja, ambayo yatatelekezwa na mfalme wa Babeli Nebukadreza..

Ukisoma pale utaona inasema..

nchi hiyo kwa jinsi ilivyokuwa nzuri mpaka ikajiita “Ukamilifu wa Uzuri” hakuna wa kufananishwa nayo. Jinsi Ilivyokuwa kiini cha biashara cha mataifa yote, mpaka Nchi ya Tarshishi ile Yona aliyoikimbilia, ilitegemea kufanya biashara na Tiro, watu wasomi na wenye akili walikuwa wanaishi humo (TIRO).. kila aina ya biashara ya madini na mawe, biashara ya wanyama, na vifaa vya kivita zilifanyika humo. Biashara za nguo na urembo wa kila namna, biashara ya vyakula na matunda. walikuwa na jeshi kubwa la kutosha, mpaka wakawa wanawauzia silaha mataifa mengine.

Hiyo ndio ikampa kiburi mkuu wao mpaka afikie hatua ya kujilinganisha na Mungu, kutokana na Hekima na utajiri aliokuwa nao na fedha nyingi..Na Yezebeli Yule tunayemsoma kwenye biblia alitokea huko(Ndiye aliyemwingiza mungu baali Israeli)..Hivyo Mungu akapanga siku ya maangamizo yao..(Ezekieli 28:1-10)

Biblia inasema Wafalme wa kila mahali watatetemeza kwa jinsi anguko lake litakavyokuwa(Tiro), wakisema wewe uliyekuwa mwenye nguvu imekuaje umeanguka ghafla hivi, kirahisi,

Ezekieli 27:32 “Na katika kulia kwao watakufanyia maombolezo, na kukuombolezea, wakisema, Ni nani aliye kama Tiro, kama yeye aliyenyamazishwa kati ya bahari?

33 Bidhaa zako zilipotoka katika bahari, uliwajaza watu wa kabila nyingi; uliwatajirisha wafalme wa dunia, kwa wingi wa mali zako, na kwa utajiri wako”.

 

Ezekieli 26: 1 “Ikawa katika mwaka wa kumi na mmoja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,

2 Mwanadamu, Kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemu, Aha! Yeye amevunjika aliyekuwa lango la kabila za watu; amenigeukia; nitajazwa kwa kuwa sasa ameharibika;

3 basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi kupigana nawe, kama bahari iinuavyo mawimbi yake.

4 Nao wataziharibu kuta za Tiro, na kuibomoa minara yake; tena nitakwangua hata mavumbi yake yamtoke, na kumfanya kuwa jabali tupu”.

Ukiendelea sasa kusema Ezekieli 28:11-19 utaona Mungu akitoa unabii wa shetani, na jinsi anguko lake lilivyokuwa kule mbinguni kwa kivuli hichi hichi cha mfalme wa Tiro.

Vivyo hivyo na Sidoni naye alikuwa pacha wake, soma habari iliyosalia utaona hilo. Kama vile tu Gomora alivyokuwa pacha wa Sodoma.

Sasa watu wa miji hiyo walitiwa kiburi kwa mali na fedha, wakamsahau Mungu muumba wa mbingu na nchi, wakawa wanaishi maisha ya dhambi, wanawaza tu mambo ya kidunia hadi siku moja Mungu alipoleta uharibifu wao kwa mkono wa Nebukadneza.

Lakini tunaona pale Bwana Yesu anasema.. Laiti ingeliona miujiza iliyokuwa inafanywa na yeye, basi miji hiyo miwili ambayo imefananishwa na utawala wa shetani kwa kujiinua..Watu hao wangalitubu tena kwa kuvaa nguo za magunia na majivu. Mpaka na mfalme wao angetubu.

Tengeneza picha, ni sawa na leo hii, kila mahali tunasikia shuhuda nyingi, tunaona miujiza mingi Kristo akiifanya, mpaka wafu wanafufuliwa mbele ya macho yetu lakini bado tunaupuuzia wokovu, tunaona kama ni habari za kale.

Tujiulize Je siku ile tutastahimili vipi adhabu ya hukumu?.

Ni wazi kuwa kama ziwa la moto litakuwa kali sana, basi kwa vizazi vyetu litakuwa limechochewa mara 7 zaidi,.Bwana atusaidie tusiupuuzie wokovu, Kristo alilipa gharama kubwa sana kwa ajili yetu..kwahiyo tusiudharau wokovu hata kidogo.

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

MTANGO WA YONA.

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIABUDU SANAMU.

Sanamu ni kitu chochote kile kinachotengenezwa chenye umbile aidha la malaika wa mbinguni, mwanadamu, mnyama, au mimea…Mwanadamu yoyote anayetengeneza kitu chochote chenye mifano ya hivyo vitu tayari kashatengeneza sanamu.

Sasa sio dhambi kutengeneza sanamu…ikiwa ina lengo lisilo la kiibada…kwamfano sanamu zilizopo makumbusho, hizo lengo lake ni la kumbukumbu, pia sanamu za Wanyama kama tembo, samaki,swala,watu n.k zilizopo sehemu za makumbusho au sehemu za maonyesho, au ambazo zinawekwa mahali kama nembo ya nchi au urembo wa mji sio dhambi…

Tatizo kubwa ni pale zinapotengenezwa kwa lengo la Ibada!…kwamba inapofikia hatua ya mtu kuamini kwamba sanamu ile ya tembo ina UUNGU ndani yake na hivyo inahitajika kuogopwa au kusujudiwa, kwamba Sanamu ya mtu yule ambaye alikuwa shujaa wa Taifa letu ina Uungu ndani yake, sanamu ile ya Mtakatifu aliyewahi kuishi Ina Uungu ndani yake, na hivyo inastahili kusujudiwa, na kupewa heshima fulani na hata kutukuzwa..Hilo ndio tatizo.

Sasa kuzitumikia na kuzisujudia sanamu kwa namna hiyo ndiko kunakoitwa IBADA ZA SANAMU. Na hizi ibada za sanamu zilianzia kwa wapagani, na shetani ameziingiza mpaka kwenye kanisa..na amewapofusha watu macho na kuwafanya wasione kabisa ukweli kuwa wanaabudu sanamu..

Kwamfano utaona sanamu ya mtakatifu fulani wa kwenye biblia labda tuseme Petro, au Paulo au Hana…imewekwa pale na inapewa heshima kana kwamba ni Paulo mwenyewe yupo ndani ya ile sanamu, inapewa heshima kana kama ni Petro mwenyewe yupo ndani ya ile sanamu kiasi kwamba mtu anaogopa hata kuikanyaga kwa bahati mbaya..kwasababu anahisi kabisa yule pale ni Petro, au Paulo amesimama…

Unakuta imewekwa sanamu ya Bwana Yesu pale, mtu anaogopa hata kuitazama usoni akihisi ni Bwana Yesu Mwenyewe yupo pale anamtazama,…hivyo inamfanya aende kwa adabu na staha na moyo wa ibada mbele ya ile sanamu, hatimaye kujinyenyekeza chini yake na hata kutaka kubarikiwa chini ya ile sanamu…HAYO NDIYO MACHUKIZO MBELE ZA MUNGU…Hiyo ndiyo sababu Bwana amesema Kwamba tusizichonge kabisa kama zitatupeleka katika kuzisujudia na kuzitumikia kwasababu zinamtia Mungu WIVU…Maana yake ni kwamba badala moyo wako uwe mbinguni Mungu aliko, na akili yako uipeleke mbinguni, na mawazo yako uyapeleke mbinguni mahali alipo…wewe unayapeleka kwenye ile sanamu iliyopo mbele yako, unayapeleka katika picha iliyopo mbele yako, hicho ndicho kinachomtia Mungu wivu.

Na inafika mbali Zaidi hadi wengine wanaziundia sala maalumu za kuombea, yaani wanafanya sanamu hizo kama nyezo au daraja la kuwasiliana na Mungu.

Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.

Mungu wetu anataka tumwabudu katika roho na kweli…na si katika sanamu…

Yohana 4:20 “Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia

21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli”

Umeona Mungu aabudiwi kupitia sanamu fulani, wala kilima fulani wala mtu fulani wala malaika fulani..yeye anaabudiwa katika roho na kweli…Laiti kama angekuwa anapenda tumwabudu kwa kumuuona…asingekuwa kama alivyo leo…angejidhihirisha duniani kote na wote tungeijua sura yake, na picha yake ingezagaa kila mahali, tungeiabudu na kuisujudia na wote tungekuwa na nakala ya picha hiyo…tungeiweka mpaka kama nembo ya Hela yetu..lakini hajayaruhusu hayo kwasababu anataka sisi tusimwabudu kupitia picha yake..anataka tumwabudu katika ROHO NA KWELI.

Hatumwoni lakini tunaamini yupo…Na hiyo Imani ya kwamba hatumwoni lakini tunaamini yupo, ndiyo ya thamani kwake…na ndiyo anayotaka tumwabudu nayo…

Kama ni picha ya Bwana Yesu au mtakatifu yoyote iwepo tu kama “lugha ya picha” na si chombo cha ibada wala kichukuacho sehemu ya hisia za mtu kana kwamba ndio kitu chenyewe halisi….Bwana anataka tukiweka sanamu/picha ya mtakatifu fulani tuichukulie ile picha kama vile tunavyoichukulia picha/sanamu ya mnyama iliyopo makumbusho…Hakuna mtu anayeweza kwenda mbele ya sanamu tembo na kuiogopa na kuipa heshima kana kwamba ni tembo halisi yupo pale, hakuna mtu anayeweza kuona sanamu ya simba akatetemeka na kukimbia, hakuna mtu anaweza kuona sanamu ya ng’ombe akaenda kukamua maziwa chini yake…Na sisi hatupaswi kwenda kukamua baraka kutoka kwenye sanamu ya mtakatifu Mariamu tulioitengeneza sisi au ya Bwana mwenyewe.

Shetani ameshalijua hilo, Hivyo alichokifanya ni kwenda kujipachika nyuma ya sanamu hizo, ili mumwabudu kisirisiri. Hivyo unapojihusisha na mojawapo ya ibada hizo ujue kabisa unamwabudu shetani.

2Wakorintho 6:16 “Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.

18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,

Bwana atubariki na kutusaidia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO YA MASHETANI

DANIELI: Mlango wa 3

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post