Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

SWALI: Mstari huu una maana gani?…

Mithali 26:4 “Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Usije ukafanana naye.
5 Umjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Asije akawa mwenye hekima machoni pake”.


JIBU: Katika huo mstari hilo neno “sawasawa” jinsi lilivyojirudia mara mbili..ndilo linalochanganya..lakini tukitafakari kwa kina tutagundua kuwa hilo Neno halijichanganyi, lipo sawasawa.

Sasa kabla ya kuendelea mbele hebu tujifunze mtu mpumbavu ni mtu wa namna gani,

Mpumbavu ni mtu asiyeweza kupambanua mambo vizuri hususani ya ki-Mungu. Mtu ambaye bado anafuata mambo ya ulimwengu au ambaye haamini kuhusu Mungu ni mpumbavu kulingana na biblia, kwasababu bado hajaweza kupambanua vizuri elimu ya maisha, ambayo ni kumjua muumba wake, na kuepukana na uovu….Hiyo ndiyo elimu ya kwanza ambayo kila mwanadamu anapaswa awe nayo..kwasababu hata wanyama na ndege kwa sehemu fulani wanayo. Wanajua kuwa kuna muumba..

Zaburi 14:1 “Mpumbavu amesema moyoni Hakuna Mungu”..

Na neno “upumbavu au mpumbavu” kama linavyotumika kwenye biblia sio tusi….bali ni hali mtu aliyonayo ya kushindwa “kupambanua mambo” kama tulivyotangulia kujifunza.

Sasa mtu asiyemjua Kristo anapokutana na wewe unayemjua Kristo na kukutukana matusi, na wewe unapomjibu kwa kurudisha matusi…hapo wewe na yeye hamna tofauti..wote wawili mmefanana na ni wapumbavu…hiyo ndio maana biblia inasema usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake ili usije ukafanana naye.

Lakini kama amekutukana…na wewe uliye ndani ya Kristo, ukatambua Yule mtu tatizo lake ni dhambi ndani ya moyo wake, na hivyo kulingana na biblia ni mpumbavu, na anamhitaji Yesu ili upumbavu wake uondoke…na hivyo kwa hekima ukaanza kumjibu kwa na kumuelekeza njia iliyo sahihi kwa upole na utaratibu..hapo atakapoona wewe umemzidi hekima, hujamrudishia tusi kama yeye alivyokutukana, yeye atajiona hana hekima..na hivyo atachomwa dhamira yake na kushawishika kugeuka kuacha njia yake mbaya.

Au pale mpumbavu anapotoa maneno ya kukulaani, lakini wewe ukambariki hapo ni sawa na umemjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake,
Ambapo kwa tendo hicho kitamfanya ajione hana hekima machoni pake mwenyewe.

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

Hapa ana maana gani kusema hivi? ” Usiseme moyoni mwako,Ni nani atakayepanda kwenda Mbinguni? (yaani ni kumleta Kristo chini), “au,Ni nani Atakayeshuka kwenda Kuzimu? (yaani, ni kumleta Kristo juu,kutoka kwa wafu.). {Warumi10:6-7.}

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

Paulo alimwambia Timotheo atumie mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lake, Je! tunaruhusiwa na sisi pia kutumia pombe?

USIINGIE MKATABA NA DHAMBI.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments