Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

JIBU: Mtu yeyote aliyejiingiza katika mahusiano na Yesu Kristo, mtu huyo katika roho anajulikana kama ni Mpenzi wa Yesu Kristo, Na mtu anajiingiza katika mahusiano hayo kwanza kwa kumwamini YESU KRISTO, kwamba alikuja kufa kwaajili ya dhambi zake, na kwamba yeye ndiye mwokozi wa ulimwengu, Na kumwamini huko kunatokana na kuisikia Injili ya Kweli inayohubiriwa na watumishi wake (Soma 2Wakorintho 11:2)..na baada ya kumwamini anatubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zake na kwenda kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu, sasa mtu aliyepitia hatua hizo zote katika ulimwengu wa roho anajulikana kama mpenzi wa YESU KRISTO au kwa jina lingine anaitwa Bibi arusi wa Kristo.

Yeremia 3:14 “Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; MAANA MIMI NI MUME WENU; nami nitatwaa mtu mmoja wa mji mmoja, na wawili wa jamaa moja, nami nitawaleta hata Sayuni;”

Sasa ikitokea Mtu wa namna hii akiacha mahusiano yake haya na Kristo na kurudia tena kuishi maisha ya dhambi, na kumdharau Roho Mtakatifu, akaenda kuzini, au kuabudu sanamu, akaenda kwa waganga wa kienyeji…kibiblia mtu kama huyo ni anafanya uasherati wa kiroho, ambao ndio unaomtia Mungu wivu, ambao unaweza kupelekea hata kifo cha ghafla kwa huyo Mtu.

Waebrania 10:28 “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?

30 Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.

31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.”

Unaweza kupitia binafsi mistari hii inaeleza zaidi juu ya uasherati huu wa kiroho (Soma 1Nyakati 5:25-26, Zaburi 106:39, Yeremia 13:27, Ezekieli 6:9, Walawi 17:7, Ezekieli 16:27,)

Waamuzi 2:16 “Kisha Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara.

17 Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana bali wao hawakufanya hivyo”.

Hivyo uasherati wa kiroho sio ndoto za kufanya mapenzi usiku na mtu au viumbe visivyojulikana, kama zinavyotafsiriwa na wengi leo, bali ni kufanya kitendo chochote kilicho kinyume na Imani yako ya kikristo, ambacho ni machukizo mbele za Mungu, na Mungu alisema yeye ni Mungu mwenye wivu,(Soma Nahumu 1:2 na Kutoka 20:4).

Wivu huo ni wivu anauona pale mtu anapokwenda kufanya vitu kinyume na ile Imani aliyokuwa nayo.

Bwana atusaidie sana.

Ubarikiwe.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 13

UFUNUO: Mlango wa 17

UFUNUO: Mlango wa 18

TIMAZI NI NINI

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments