UFUNUO: Mlango wa 18

UFUNUO: Mlango wa 18

Tukirejea kwenye ile sura ya 17 tunamwona yule mwanamke KAHABA aliyeketi juu ya yule mnyama mwekundu na kwenye paji la uso wake ana jina limeandikwa kwa “siri” BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI, na tulishaona huyu mwanamke si mwingine zaidi ya KANISA KATOLIKI, lenye makao yake makuu VATICAN, na ni kwanini hajulikani kwa wazi? ni kwasababu jina lake lipo katika SIRI, na pia BABELI hii ipo rohoni, kumbuka BABELI ya kwanza ilikuwa ya mwilini na ilishaanguka wakati ule wa utawala wa mfalme Nebukadneza(Tunasoma katika kitabu cha Danieli). Lakini katika Mlango huu wa 18, tunaona hukumu ya BABELI hii ya rohoni ambayo ndiyo inayotawala hata sasa.

Tusome.

Mlango 18:1 “Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake.

2 Akalia kwa sauti kuu, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye kuchukiza;

3 kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake.

4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.

5 Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake.

6 Mlipeni kama yeye alivyolipa, mkamlipe mara mbili kwa kadiri ya matendo yake. Katika kikombe kile alichokichanganyisha, mchanganyishieni maradufu.

7 Kwa kadiri alivyojitukuza na kufanya anasa, mpeni maumivu na huzuni kadiri iyo hiyo. Kwa kuwa husema moyoni mwake, Nimeketi malkia, wala si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.

8 Kwa sababu hiyo mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu.

9 Na hao wafalme wa nchi, waliozini naye na kufanya anasa pamoja naye, watalia na kumwombolezea; wauonapo moshi wa kuungua kwake;

10 wakisimama mbali kwa hofu ya maumivu yake, wakisema, Ole, ole, mji ule ulio mkuu, Babeli, mji ule ulio na nguvu! Kwa kuwa katika saa moja hukumu yako imekuja.

Kumbuka Babeli ya kwanza ambao ulikuwa (kwasasa ni maeneo ya Iraq) ngome pekee yenye nguvu iliyokuwa inatawala dunia nzima kwa wakati ule, ndio ilikuwa chimbuko la mambo yote maovu na dini zote za kipagani, ikiwemo kuabudu sanamu, na uchawi, zaidi ya yote ndiyo iliyohusika kuuhamisha hata uzao wa Mungu(Israeli) na kuupeleka utumwani na kuliteketeza HEKALU la Mungu, na kutumia vyombo vya madhabahuni vitakatifu kwa kufanyia anasa na uchafu kwa miungu yao, Kwasababu hiyo basi Babeli ulionekana kuwa ni mji wenye MACHAFUKO na MACHUKIZO makubwa sana mbele za Mungu.

Pamoja na hayo ulizidi kuwa kuendelea sana, miji yake ilikuwa imetengenezwa kwa utashi wa hali ya juu hata leo tunafahamu moja ya maajabu 7 ya dunia kwa wakati wote tukiachia mbali zile Piramidi za Misri nyingine ni “BUSTANI ZINAZOELEA ZA BABELI”. Mji huu ulitukuzwa sana, mpaka kufikia kiwango cha watu kuuita “BABELI MJI WA MILELE”, na ni kweli kwa jinsi ulivyokuwa na nguvu ilikuwa ni ngumu kutabiri kama kweli ungekuja kuanguka na kuwa makao ya mbuni na hayawani wa mwituni. Leo hii maeneo yaliyokuwa ni Babeli ni jagwa lisilokuwa na kitu.

Lakini Jambo hili tunaona Mungu alilitolea unabii kwa kinywa cha nabii Yeremia miaka 70 kabla ya Babeli kuanguka alisema…,

Yeremia 51:6 “Kimbieni kutoka kati ya Babeli, kila mtu na ajiokoe nafsi yake; msikatiliwe mbali katika uovu wake; maana ni wakati wa kisasi cha Bwana, atamlipa malipo.

7 Babeli umekuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Bwana; kilicholevya dunia yote; mataifa wamekunywa mvinyo wake; kwa sababu hiyo mataifa wameingiwa na wazimu.

8 Babeli umeanguka na kuangamia ghafula; mpigieni yowe; twaeni zeri kwa maumivu yake; ili labda apate kuponywa.

9 Tungependa kuuponya Babeli, Lakini haukuponyeka; Mwacheni, nasi twendeni zetu, Kila mtu hata nchi yake mwenyewe; Maana hukumu yake inafika hata mbinguni, Nayo imeinuliwa kufikilia mawinguni. “

Na pia tunamwona Nabii Isaya alishatabiri miaka 200 kabla ya Babeli kuanguka alisema…

Isaya 13:19 “Na Babeli, huo utukufu wa falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.

20 Hautakaliwa na watu tena kabisa, wala watu hawatakaa ndani yake tangu kizazi hata kizazi. Mwarabu hatapiga hema yake huko, wala wachungaji hawatalaza makundi yao huko.

21 Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini watacheza huko.

22 Na mbwa-mwitu watalia ndani ya ngome zake; na mbweha ndani ya majumba ya anasa; na wakati wake u karibu kufika, na siku zake hazitaongezeka.”

Kwahiyo unabii wote huu ulikuja kutimia kama ulivyo kwa wakati wake, pale wakuu wa Babeli walipokuwa wanafanya anasa tena kibaya zaidi wakiwa wanatumia vyombo vitakatifu vya Hekalu, kulitokea kile kiganja ukutani kikiandika MENE, MENE, TEKELI na PERESI, na usiku ule ule Waamedi wa waajemi waliuvamia mji kwa njia ambayo hawakuitegemea na ndio hapo ikawa mwisho wa BABELI na katika usiku mmoja tu! uliteketezwa, mji ule waliosemea UTAISHI MILELE ndio ulikuwa mwanzo wa kuwa makao ya mbuni, na wanyama wa mwituni,(Danieli 5). Hii ikithibitisha kuwa BWANA akisema jambo ni lazima litimie tu!.

Sasa hiyo iliyoangamizwa ilikuwa ni BABELI ya kwanza, lakini BABELI iliyopo sasa hivi ni ya ROHONI na ipo katika “SIRI”, Kumbuka ile ya kwanza iliwachukua wayahudi wa kimwili utumwani na kuchukua vyombo vya hekalu la Mungu kutumia kwa karamu zao za kipagani lakini hii ya sasa hivi inawachukua wayahudi wa rohoni(WAKRISTO) utumwani na kuchukua vyombo vitakatifu vya rohoni (Ibada Halisi ) na kuzitumia pamoja na ibada za masanamu, haya ni MACHUKIZO mbele za Mungu, na kama vile ile ya kwanza iliandikiwa MENE, MENE, TEKELI na PERESI vivyo hivyo na hii ya rohoni IMESHAHUKUMIWA na hivi karibuni tu itateketezwa na kuwa ukiwa.

Na ndio maana tukisoma kwenye hiyo mistari hapo juu tunaona;… “9 Na hao wafalme wa nchi, waliozini naye na kufanya anasa pamoja naye, watalia na kumwombolezea; wauonapo moshi wa kuungua kwake; wakisimama mbali kwa hofu ya maumivu yake, wakisema, Ole, ole, mji ule ulio mkuu, Babeli, mji ule ulio na nguvu! Kwa kuwa katika saa moja hukumu yako imekuja. “

Kanisa Katoliki makao yake makuu yakiwa VATICAN ni dini iliyojichanganya na SIASA, na ina utajiri mkubwa sana, kumbuka hazina kubwa ya dunia ipo VATICAN karibu kila taifa duniani lina mkono wa dola ya Rumi nyuma yake, kwamfano hata hapa Tanzania ukiangalia karibu miradi mikubwa mingi na mataasisi ya kijamii na mabiashara, mashule, mahospitali,n.k yanafadhiliwa au kuasisiwa na kanisa Katoliki na yapo karibu kila mkoa,limefanya hivi dhumuni lake kubwa ikiwa ni kueneza dini yake ya uongo na kutaka kutawala kama MALKIA.

Na kama maandiko yanavyosema “. Kwa kuwa husema moyoni mwake, Nimeketi malkia, wala si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.” Kanisa Katoliki limejiweka kama MALKIA, si ajabu hata ishara ya kanisa hili ni mwanamke (bikira Mariam) wakimfanya kama malkia wa mbinguni.

Na jambo hili lipo katika mataifa yote duniani, hivyo wafalme wote na mataifa yote duniani yamelewa kwa mvinyo wa uasherati wake na ndio maana tunaona hapo wataomboleza watakapoona uharibifu wake utakapokuja kwa ghafla ndani ya siku moja,

Kama vile Mungu alivyowatumia waamedi na waajemi kuiangusha ile BABELI YA KWANZA, vivyo hivyo Mungu ataenda kutumia zile PEMBE 10 zilizokuwa juu ya kichwa cha yule mnyama (ambayo ndiyo yale mataifa 10 ya ulaya) kuiangusha hii BABELI ya PILI ambaye ndio yule MAMA WA MAKAHABA aketiye juu ya yule mnyama(KANISA KATOLIKI), na KITI chake cha ENZI kikiwa VATICAN. Hivyo kwa siku moja VATICAN itateketezwa kwa moto pengine kwa bomu la ATOMIC. Na wale watu waliopata utajiri kupitia yeye biblia inasema watamwombolezea kwasababu watastaajabia imewezekanikaje ngome kubwa kama hiyo kuanguka ndani ya siku moja na pia utajiri waliokuwa wanaupata kwa kupitia yeye hawataupata tena..

 Tukiendelea mistari inayofuata.. UFUNUO 18:11-24 tunasoma..

“11 Nao wafanya biashara wa nchi walia na kumwombolezea, kwa sababu hapana mtu anunuaye bidhaa yao tena;

12 bidhaa ya dhahabu, na fedha, na kito chenye thamani, na lulu, na kitani nzuri, na nguo ya rangi ya zambarau, na hariri, na nguo nyekundu; na kila mti wa uudi, na kila chombo cha pembe, na kila chombo cha mti wa thamani nyingi, na cha shaba, na cha chuma, na cha marimari;

13 na mdalasini, na iliki, na uvumba, na marhamu, na ubani, na mvinyo, na mafuta ya mzeituni, na unga mzuri, na ngano, na ng’ombe, na kondoo, na farasi, na magari, na miili na roho za wanadamu.

14 Na matunda yaliyotamaniwa na roho yako yamekuondokea; na vitu vyote vilivyo laini na vitu vya fahari vimekupotea; wala watu hawataviona tena kamwe.

15 Na wafanya biashara ya vitu hivyo, waliopata mali kwake, watasimama mbali, kwa hofu ya maumivu yake; wakilia na kuomboleza,

16 wakisema, Ole, ole, mji ule mkuu! Uliovikwa kitani nzuri, na nguo ya rangi ya zambarau, na nguo nyekundu, na kupambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu;

17 kwa kuwa katika saa moja utajiri mwingi namna hii umekuwa ukiwa. Na kila nahodha na kila aendaye mahali popote kwa matanga, na mabaharia, nao wote watendao kazi baharini, wakasimama mbali;

18 wakalia sana, walipouona moshi wa kuungua kwake, wakisema, Ni mji upi ulio mfano wa mji huu mkubwa!

19 Wakatupa mavumbi juu ya vichwa vyao, wakalia, wakitokwa na machozi na kuomboleza, wakisema, Ole, ole, mji ule ulio mkuu! Ambao ndani yake wote wenye merikebu baharini walipata mali kwa utajiri wake; kwa kuwa katika saa moja umekuwa ukiwa.

20 Furahini juu yake, enyi mbingu, nanyi watakatifu na mitume na manabii; kwa maana Mungu amehukumu hukumu yenu juu yake.

21 Na malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe, kama jiwe kubwa la kusagia, akalitupa katika bahari, akisema, Kama hivi, kwa nguvu nyingi, utatupwa Babeli, mji ule mkuu, wala hautaonekana tena kabisa.

22 Wala sauti ya wapiga vinanda, na ya wapiga zomari, na ya wapiga filimbi, na ya wapiga baragumu, haitasikiwa ndani yako tena kabisa; wala fundi awaye yote wa kazi yo yote hataonekana ndani yako tena kabisa; wala sauti ya jiwe la kusagia haitasikiwa ndani yako tena kabisa;

23 wala nuru ya taa haitamulika ndani yako tena kabisa; wala sauti ya bwana-arusi na bibi-arusi haitasikiwa ndani yako tena kabisa; maana hao wafanya biashara wako walikuwa wakuu wa nchi, kwa kuwa mataifa yote walidanganywa kwa uchawi wako.

24 Na ndani yake ilionekana damu ya manabii, na ya watakatifu, na ya wale wote waliouawa juu ya nchi.”

Kama vile ile BABELI YA KWANZA ilivyoangamizwa kwa ishara Mungu aliyompa Seraya kwa mkono wa YEREMIA

 ukisoma….Yeremia 51:61-64″ Naye Yeremia akaandika katika kitabu habari ya mabaya yote yatakayoupata Babeli, maneno hayo yote yaliyoandikwa juu ya Babeli.

61 Naye Yeremia akamwambia Seraya, Utakapofika Babeli, basi angalia uyasome maneno haya yote.

62 ukaseme, Ee Bwana, umenena habari za mji huu kwamba utakatiliwa mbali, usikaliwe na awaye yote, wala wanadamu wala wanyama, lakini uwe ukiwa hata milele.

63 Tena itakuwa utakapokwisha kukisoma kitabu hicho, utakifungia jiwe, NA KUKITUPA KATIKA MTO FRATI;

64 nawe utasema,Hivyo ndivyo utakavyozama Babeli, wala hautazuka tena, kwa sababu ya mabaya yote nitakayoleta juu yake; nao watngachoka. Maneno ya Yeremia yamefika hata hapa.

Habari hiyo hiyo tunaona inajirudia tena kwa Babeli ya pili kama tunavyoona katika kitabu cha UFUNUO; 

Ukaisoma mstari wa 21 unasema ” Na malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe, kama jiwe kubwa la kusagia, akalitupa katika bahari, akisema, Kama hivi, kwa nguvu nyingi, UTATUPWA BABELI, mji ule mkuu, wala hautaonekana tena kabisa.” Hivyo Historia inajirudia tena..

Na pia mstari wa mwisho unasema.. 24 “Na ndani yake ilionekana damu ya manabii, na ya watakatifu, na ya wale wote waliouawa juu ya nchi.”

Ni dhahiri kuwa kuwa dini ya Katoliki ndio dini pekee iliyohusika na mauaji mengi ya wakristo historia inaonyesha zaidi ya wakristo milioni 68 waliuliwa kikatili na dini hii kwa kujaribu tu kwenda kinyume na desturi zao za kipagani, na isitoshe bado huko mbeleni katika kipindi cha dhiki kuu itamwaga damu nyingi za watu wote watakaokataa kumsujudia. kwa namna hiyo kwanini Mungu asiiteketeze?

Hivyo ndugu biblia inasema kwenye ule mstari wa 4 ” TOKENI KWAKE, ENYI WATU WANGU, MSISHIRIKI DHAMBI ZAKE, WALA MSIPOKEE MAPIGO YAKE.”

tena ni kwanini tuondoke??.. kwasababu biblia inasema pale kwenye Yeremia 51: 9 “Tungependa kuuponya Babeli, Lakini haukuponyeka; Mwacheni, nasi twendeni zetu, Kila mtu hata nchi yake mwenyewe; Maana hukumu yake inafika hata mbinguni, Nayo imeinuliwa kufikilia mawinguni. ” unaona hapo?

Kitabu cha Danieli 2:34 inasema jiwe lilichongwa pasipo kazi ya mikono ikalipiga miguu ya ile sanamu na kuteketea yote na tunajua lile jiwe si mwingine zaidi ya BWANA YESU KRISTO akiihukumu BABELI ya rohoni katika siku za mwisho inayowakilishwa na ule utawala wa chuma kilichochanganyikana na udongo ambayo ni RUMI ya kidini (UKATOLIKI).

Kwahiyo Huu ni wakati wa kutoka katika mifumo ya dini na madhehebu na kuligeukia NENO LA MUNGU ambalo ndio NURU yetu itakayotupeleka mbinguni, sio kutoka kwa miguu, bali ni kutoka kwa “ROHO”, kumbuka BABELI hii ipo rohoni, hatumfikii Mungu kwa mapokeo ya dini yoyote au dhehebu lolote, ibada za sanamu ni machukizo, kusali rozari ni machukizo, kwenda toharani ni uongo, ubatizo wa vichanga haupatani na maandiko,pamoja na ibada za wafu n.k..jambo pekee litakalokutoa huko ni kuifanya biblia kuwa KATIBA YAKO TU!

Mungu ni ROHO nao wamwabuduo biblia inasema imewapasa kumwabudu katika roho na kweli, kuwa mkristo halafu bado unakuwa mwasherati,unavaa vimini, suruali, msengenyaji, unapenda anasa, mtukanaji, mlevi unakula rushwa n.k. ni ishara kabisa kuwa na hapo bado hujatoka BABELI, Na kumbuka Tafsiri ya Neno BABELI ni MACHAFUKO, hivyo wafanyao haya machafuko yote wataharibiwa.

Mungu akubariki.

Kwa Mwendelezo >>UFUNUO: Mlango wa 19

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.


Mada Nyinginezo…


DANIELI: Mlango wa 2

MNARA WA BABELI

NINI MAANA YA KUISHI KWA NENO?

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Kinye Mkira
Kinye Mkira
6 months ago

Hakika Neno la Mungu halitapita hata yote yatimie.
Ahsante sana kwa ujumbe mzuri. Mungu azidi kukujalia kila kilicho chema kwako.
Amen

AYOUB MWAMPEPU
AYOUB MWAMPEPU
9 months ago

NINAOMBA KWAMBA niwe natumiwa MANENO YA MUNGU