Title August 2019

Kwanini pale Bwana Yesu alichukua hatua ya kumsamehe dhambi kwanza kabla ya kumponya yule mtu mwenye kupooza?(Marko 2).

JIBU: Ubarikiwe dada tuisome kwanza habari yenyewe.. 

Marko 2: 1 “Akaingia Kapernaumu tena, baada ya siku kadha wa kadha, ikasikiwa ya kwamba yumo nyumbani.

2 Wakakusanyika watu wengi, isibaki nafasi hata mlangoni; akawa akisema nao neno lake.

3 Wakaja watu wakimletea mtu mwenye kupooza, anachukuliwa na watu wanne.

4 Na walipokuwa hawawezi kumkaribia kwa sababu ya makutano, waliitoboa dari pale alipokuwapo; na wakiisha kuivunja wakalitelemsha godoro alilolilalia yule mwenye kupooza.

5 Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.

6 Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao,

7 Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu?

8 Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu?

9 Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?

10 Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza),

11 Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako.

12 Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastaajabu wote,wakamtukuza Mungu, wakisema, Namna hii hatujapata kuiona kamwe” …

Kama ukichunguza utaona kuwa jambo la kwanza Bwana aliloliona ni ile Imani yao kwake, aliona ndani yao walikuwa na kitu cha ziada zaidi ya imani ya kuponywa, nayo ni Imani kwa Yesu Kristo…..Na tunajua kitu cha kwanza kilichomleta Bwana Yesu duniani ni kuokoa dhambi za watu, na vitu vingine baadaye…

Ukisoma Yohana 8:24 Bwana aliwaambia makutano ..“Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu”….

Unaona hapo?…Inakupasa uamini kwanza. Na ndio maana jambo la kwanza alilolitamka yeye kama mkuu wa uzima wa roho za watu mara baada ya kuona Imani yao kwake, akamwambia yule aliyekuwa amepooza..UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO…..Ni Neno zuri na la neema kiasi gani!!! Lakini wale wengine mawazo yao yalikuwa tofauti, wao walitazamia tu, Bwana amponye yule mtu kisha amwambie nenda zako, halafu yule mtu akaendelee kuishi maisha ya dhambi kisha mwisho wa siku afe aishie kupata hasara ya nafsi yake!..na uponyaji wake wa mwili usimfaidie kitu baada ya maisha ya hapa. 

Sasa Ukiendelea kusoma pale utaona Bwana anawauliza tena wale watu, Marko 2:9 “Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?, Sasa kwa namna ya kawaida kwa mtu mwenye akili za rohoni atagundua kuwa ni afadhali usipone ugonjwa wako, lakini dhambi zako ziwe zimesamehewa…kuliko kuponywa halafu dhambi zako ziendeleee kubaki! Na ndio maana Bwana alimchagulia fungu lililo jema la kusamehewa dhambi zake kwanza, kisha baadaye amponye… 

Na ndivyo tunavyopaswa na sisi kama wakristo kufanya sasahivi, tunakimbilia kuwaombea watu magonjwa ,wapokee miujiza, na mafanikio na huku tunasahamu kuwafundisha watu habari za msamaha wa dhambi ambao ndio msingi wa Imani ya kikristo.. vyepesi ni vipi??? Ni heri tukamuhubirie mtu habari za msamaha na toba, aokolewe roho yake hata kama hatapokea uponyaji kuliko kuhubiri kila siku mimbarani miujiza na uponyaji na huku bado watu wanakufa katika dhambi zao.

Au ni afadhali kufanya vyote kuliko kutupilia mbali habari za msamaha wa dhambi, na kushikamana na miujiza tu. 

Ubarikiwe .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

HOME

Print this post

Manabii walisema “Neno la Mungu likanijia” ..Maana ya hili neno ni nini?.

JIBU: Kujiliwa na Neno la Mungu ni sawa sawa na kufunuliwa ujumbe unaomuhusu mtu au jamii fulani, na ujumbe huu Mungu anamshushia mtu aidha kwa njia ya ndoto, au maono, au sauti, au kutembelewa na malaika, au njia nyingine yoyote ya ki-Mungu. 

Kwahiyo unaposoma mahali popote kwenye biblia,unakutana na sehemu inasema Neno la Mungu lilimjia Isaya, au Yeremia au Yona, hap ni sawa na kusema, ujumbe utokao kwa Mungu umemfikia Isaya, au Yeremia au Yona awapelekee watu. Kadhalika hata sasa hivi Neno la Mungu, huwa linawajilia watu kwa njia mbalimbali, mt anapofunuliwa Neno lolote kwa njia ya ndoto, au maono au kuzuriwa na malaika, au katika biblia, na Neno hilo limebeba ujumbe wa kwenda kuwapelekea watu wengine, hiyo ni sawa tu na Neno la Mungu limemjia mtu huyo. Kadhalika unaposikia ndani wito wa kwenda kuwashuhudia wengine habari njema, hapo ni sawa na lile Neno linalosema

Marko 16:15 “Enendeni ulimwenguni kote mkahubiri injili kwa kila kiumbe”

limekujia, hivyo unapaswa ukauwasilishe huo ujumbe kwa wakati. Na kuna hatari za kutokutii Neno la Mungu linalokujia, na hatari zenyewe ndio kama zile zilizompata Nabii Yona na zile alizoonywa Nabii Ezekieli zikisema.. 

Ezekieli 3: 17 “Mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa nyumba ya Israeli; basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu, ukawape maonyo haya yatokayo kwangu.

18 Nimwambiapo mtu mbaya, Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.

19 Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye hauachi ubaya wake, wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako.

20 Tena mtu mwenye haki aiachapo haki yake, na kutenda uovu, nami nikiweka kikwazo mbele yake, atakufa; kwa sababu hukumwonya, atakufa katika uovu wake, wala matendo yake ya haki aliyoyatenda hayatakumbukwa; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako”.

 Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

BIBLIA INASEMA USIONGEZE WALA USIPUNGUZE NENO LA MUNGU, HUKO KUONGEZA NA KUPUNGUZA KUKOJE?

WANA WA MAJOKA.

JIWE LA KUKWAZA

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

MADHAIFU.

WITO WA MUNGU


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

JIBU: Kwanza sio sahihi kwa mtu aliyeamini kwenda kutwaa mke au mume asiye wa imani yake ya kikristo, kwasababu moja tu! nayo ni KUEPUKA KUGEUZWA MIOYO!..   Kumbuka jambo mojawapo ambalo Mungu aliwakanya sana wana wa Israeli hata kabla ya kufika nchi ya Ahadi ni suala la kuoa/kuolewa na watu wa jamii nyingine tofauti na wayahudi, na sio kwasababu labda ni wabaya, au hawavutii hapana, ni kwasababu moja tu! Watageuzwa mioyo yao wasiambatane na Mungu wa Israeli kinyume chake wataambata na miungu migeni. Na Mungu siku zote ni Mungu mwenye wivu!.   Tukisoma;

Nehemia 13:25 “………… nikawaapisha kwa Mungu, nikasema, Msiwaoze wana wao binti zenu, wala msiwatwae binti zao ili waolewe na wana wenu, wala na ninyi wenyewe.

26 Je! Sulemani, mwana wa Daudi, hakufanya dhambi kwa kutenda hayo? Lakini katika mataifa mengi hapakuwa na mfalme mwingine mfano wake. Tena alipendwa na Mungu wake, naye Mungu akamfanya mfalme juu ya Israeli; walakini WANAWAKE WAGENI WALIMKOSESHA HATA YEYE.

27 Basi, na sisi, je! Tuwasikilize ninyi kutenda neno hili baya, hata kumhalifu Mungu wetu kwa kuwaoa wanawake wageni?”  

Unaona hapo?. Mfalme Sulemani pamoja na hekima zake zote nyingi za kuweza kupambanua mambo lakini aligeuzwa moyo, na wale wanawake wa mataifa mpaka kufikia hatua ya kuivukizia uvumba miungu migeni, Unadhani itashindanaje kwa mkristo mwingine yeyote wa kawaida?. Unaweza ukasema aa! Mimi nitaweza kumtawala, lakini hilo haliwezekani Mungu sio mwongo, akisema atakugeuza, ni kweli atakugeuza,.Mwanzoni utaona kama inawezekana lakini mwisho wa siku utajikuta unaangukia katika shimo kama Sulemani.   Vivyo hivyo ukimsoma Mfalme Ahabu alikoseshwa na Yezebeli mchawi, Samsoni naye alikoseshwa na Delila. Wote hawa wake zao walikuwa ni wanawake wa kimataifa n.k.  

Kwahiyo unapokuwa mkristo unapaswa umtafute mtu mwenye imani moja na yako ya kikristo, au kama sio basi umgeuze kwanza amgeukie Kristo ndipo umuoe au uolewe naye, vinginevyo utakuwa unajiweka mwenyewe katika hali ya hatari kubwa ya kumkosea Mungu, na kuishia katika majuto…   Lakini kama ikitokea mlishaoana tayari huko nyuma na mtu mwingine kabla wewe hujawa mkristo, na wewe baadaye ukaja kuamini na Yule mpenzi wako hajaamini lakini bado anaona vema kuishi na wewe hapo biblia inasema haupaswi kumuacha, unatakiwa ukae naye katika hali yake hiyo hiyo pengine wakati ukifika kwa matendo yako mema ya kikristo yatambadilisha na yeye naye aamini…

Lakini kama akichukizwa na uamuzi wako wa wewe kuwa mkristo na anataka kuondoka…Hapo haufungiki, anaweza kwenda, na biblia inaruhusu kutwaa mke/mume mwingine ila katika Bwana tu ambaye ni mkristo mwenye imani moja na wewe.   Soma.

1Wakoritho 7: 12 “Lakini watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache.

13 Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe.

14 Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu.

15 Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani.

16 Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?”  

Kwahiyo hairuhusiwi kuoa mtu ambaye sio wa IMANI moja nawe kulingana na maandiko.  

Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

NDOA NA TALAKA:

JE! NI HALALI KUTOA CHETI KWA WAKRISTO WANAOOA?

NINI TOFAUTI KATI YA UZINZI NA UASHERATI ?

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?

NAPENDA KUJUA MAANA NA TOFAUTI KATI YA MYUNANI, MFARISAYO NA MSADUKAYO.

UKWELI UNAOPOTOSHA.

DUNIANI MNAYO DHIKI.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Wapendwa nini maana ya hili andiko “Ushuhuda wa YESU ndio ROHO YA UNABII” (ufunuo 19:10)?

JIBU: Biblia inaposema ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii…inamaanisha kuwa mtu yeyote ambaye anajiona kuwa anayo roho ya kinabii ndani yake au anayejiita nabii, kama maisha yake au mahubiri yake hayalengi katika kumshuhudia YESU KRISTO BWANA WETU..basi huyo ni nabii wa uongo ushuhuda wake ni wa uongo!..hata kama atakuwa anaona maono kiasi gani, au anatabiri na kutenda miujiza kiasi gani huyo bado sio nabii wa kweli, ni nabii wa uongo..

Biblia inasema katika..

1 Yohana 5:9-11“9 Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana USHUHUDA WA MUNGU NDIO HUU, KWAMBA AMEMSHUHUDIA MWANAWE.

10 Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu ANAO HUO USHUHUDA NDANI YAKE Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe.

11 Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe.” 

Hivyo ili tumtambue kama huyu ni nabii kutoka kwa Mungu au la! …hatupaswi kukimbilia kuangalia miujiza anayofanya, au maono anayoona, tutampima kwa ushuhuda anaouhubiri (Neno la Kristo) je! anaturudisha kwa YESU? Anamuhubiri Yesu yule wa Kalvari? Yesu yule aliyesema mtu akinifuata ajikane nafsi yake ajitwike msalaba wake anifuate, Yesu yule aliyesema “itamfaidia nini mtu kupata ulimwengu mzima na kupata hasara ya nafsi yake” kama atamhubiri Yesu huyu basi hata asipofanya muujiza hata mmoja, au kutabiri huyo ni nabii wa kweli kwasababu anao ushuhuda wa Yesu Kristo ambayo ndio Roho ya unabii. Unamkumbuka Yohana mbatizaji, yeye hakuwahi kufanya muujiza hata mmoja, wala ishara yoyote..lakini ushuhuda wake ulikuwa ni nini?..ulikuwa ni kuwapeleka watu kwa YESU, na si kingine..lakini Bwana alimwambiaje?…yeye ni zaidi ya NABII..na hakuna aliyetokea kama yeye hata Musa hakuwa mfano wake. 

Lakini kitu gani kilichopo sasahivi…watu wanajiita manabii wanatabiri lakini hawana ushuhuda wa Yesu Kristo ndani yao, mungu wao ni tumbo, wanahubiri tu mafanikio ya ulimwengu huu na kukwepa mafundisho ya kumpeleka mtu mbinguni na toba, kama biblia inavyosema katika

Wafilipi 3:18-21 “18 Maana wengi huenenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, KUWA NI ADUI ZA MSALABA WA KRISTO;

19 mwisho wao ni uharibifu, MUNGU WAO NI TUMBO, utukufu wao u katika fedheha yao, WANIAO MAMBO YA DUNIANI.

20 KWA MAANA SISI, WENYEJI WETU UKO MBINGUNI; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;

21 atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake.” 

Kwahiyo roho yoyote isiyoturudisha kwa YESU KRISTO na maneno yake, hiyo ni roho ya Yule mwovu, ikivaa kinyago cha roho ya kinabii, hivyo ili ile Roho ya kinabii iwe juu yako inakupasa kumshuhudia YESU KRISTO katika maisha yako na katika huduma yako.

 Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinaendana:

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

MJUE SANA YESU KRISTO.

VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.

CHAKULA CHA ROHONI.

SWALI LA KUJIULIZA!


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja KUITANGUA TORATI AU MANABII; La!, SIKUJA KUTANGUA, bali KUTIMILIZA.

18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie”.

JIBU: BWANA aliposema hakuja kuitangua torati wala manabii bali kuitimiliza…alikuwa ana maana kuwa yeye hakuja kuondoa neno lolote la torati lililosemwa bali alikuja kulifanya kuwa IMARA ZAIDI..kwa mfano torati iliposema usizini, haikuishia pale tu katika mwili…lakini Bwana Yesu alipokuja alisema amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye nafsini mwake…si umeona hapo.. hajaiondoa amri ile bali ndio ameikolezea..Ikiwa na maana sio tu kwenda kuchukua hatua ya kuzini ndio iwe kosa hapana bali kitendo cha kumtamani tu tayari ni kosa, hivyo haupaswi kutamani kabisa ili kuitimiliza torati… 

Kadhalika Torati pia ilisema usiue..lakini Yesu alisemaje? amchukiaye ndugu yake ni sawa na muuaji..umeona na hapo pia sio tu Kuua ndio iwe kosa, hapana! bali hata hilo wazo la kumchukia tu ndugu yako halitakiwi liwepo ndani ya mtu. Torati ilisema pia ikumbuke siku ya sabato uitakase, lakini Bwana Yesu alisema ..Yeye ndiye BWANA wa Sabato (Marko 2:28), ikimaanisha kuwa ukimpata Yesu umeishika sabato yako, kwasababu ndani ya moyo wako kila wakati unakuwa ndani ya pumziko lako na kila siku unakuwa katika ibada na sio tena siku moja maalumu. 

(Mathayo 11:28)…Unaona hapo? Hajaiondoa lakini ameifanya ieleweke zaidi. Na ndivyo ilivyo pia kwa maneno mengine yote yote ya torati Bwana hakuyaondoa bali aliyafanya kuwa imara zaidi. 

Ubarikiwe sana .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa njia ya maelezo unaweza kufungua video chini

[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=RxbUfwts4fg[/embedyt]


Mada zinazoendana:

UTIMILIFU WA TORATI.

JE! VITABU VYA BIBLIA VILIWEZAJE KUKUSANYWA PAMOJA?

UMEIZALIA MATUNDA MIAKA 4 YA NEEMA ULIYOPEWA?

USIMFANYIE JEURI ROHO WA NEEMA.

JE! UKRISTO UNAMPA MTU DHAMANA YA KUWA TAJIRI?

TAFUTA KUMJUA MUNGU ZAIDI YA SHETANI

NITASHINDAJE HALI YA KUUMIZWA NA MANENO YA WATU!


Rudi Nyumbani:

Print this post

Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?

Tukisoma

Luka 13:1 “Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichanganya DAMU YAO NA DHABIHU ZAO.

2 Akawajibu akawaambia, Je! Mwadhani ya kwamba Wagalilaya hao walikuwa wenye dhambi kuliko Wagalilaya wote, hata wakapatwa na mambo hayo?

3 Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.

4 Au wale kumi na wanane, walioangukiwa na mnara huko Siloamu, ukawaua, mwadhani ya kwamba wao walikuwa wakosaji kuliko watu wote waliokaa Yerusalemu?

5 Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.”  


JIBU: Kama ukiitazama kwa ukaribu habari hiyo picha utakayokujia hapo ni kwamba kwa wakati huo ambao Bwana aliokuwepo na hao watu, kulikuwa na habari iliyozagaa sana mjini kote, maeneo kadha wa kadha uko uyahudi,ni habari ya tukio ambalo sio la kawaida kutokea katikati ya jamii ya watu wa Israeli,nalo si lingine zaidi ya kuuawa kwa wayahudi kikatili tena kibaya zaidi na cha kushtusha ni kuchangwa damu zao na za wanyama.  

Tuchukulie kwamfano hapa Tanzania wakati ule tulivyosikia ajali ya wanafunzi wa Lucky Vincent kule Arusha, jambo lile liliwashutusha watu wengi sana, mpaka kupelekea tukio kama lile kuzungumziwa mara kwa mara katika vyombo vya habari Tanzania nzima, na tunajua habari za matukio kama hayo huwa kwa namna ya kawaida zinachua muda mrefu kidogo kuacha kuzungumziwa, Na ndio maana unaona hapo wale watu walimwendea Bwana Yesu kumuuliza ili waone kama na yeye anazo hizo taarifa au la! na kama anazo je! yeye naye analizungumziaje suala hilo? Ni kwanini Pilato aamue kufanya kitendo cha kikatili kama kile cha kuchanganya damu za wale wagalilaya na dhabihu zao wenyewe?. Hilo ni swali lililokuwa ndani ya vichwa vya watu wengi sana kwa wakati ule.

Lakini kama tunavyofahamu kwenye biblia Pilato alikuwa ni Liwali (Governor) wa Uyahudi,(Luka 3:1) chini ya utawala wa kikatili wa Rumi (Kumbuka kwa wakati ule Bwana akiwa duniani Dola ya Rumi ndio ilikuwa inatawala Dunia) Hivyo yeye kama Liwali aliyeteuliwa na Kaisari mkuu wake huko kutoka makao yao makuu Rumi, aiongoze Yudea, alikuwa na jukumu la kuhakikisha Maeneo aliyowekwa ayaongoze yanatulia kikamilifu chini ya utawala . kwahiyo jambo lolote ambalo lingeonekana kujitokeza aidha usaliti, au vurugu, au mapinduzi, au uvunjaji wa amani katika uyahudi lisingevumilika kwa namna yoyote chini ya utawala wa Pilato kwasababu naye pia alikuwa ni mkatili…tunamwona baadaye alikuja kuhusika hata na kifo cha Bwana Yesu.   Kwahiyo biblia haijaeleza sababu hasaa ya Herode kutaka kuwaua wale Wagalilaya waliokwenda kuabudu Yerusalemu wakati wa sikukuu. Inaeleza tu waliposhuka kutoka Galilaya kwenda kuabudu ghafla kikosi cha Pilato kiliwadondokea na kuwachinja na si mahali pengine zaidi ya Hekaluni kwasababu huko ndiko dhabihu zilikuwa zinatolewa , kisha kuchukua damu zao na kuzichanganya na damu za wanyama waliokuja nao kutolea dhabihu kwa Mungu wao..

Pengine Pilato alihisi kuna tukio la usaliti au uvunjaji amani lilipangwa na hao watu au vinginevyo hatujui lakini inaelekea itakuwa ni sababu ya kiusalama zaidi.   Na tunaona pia na wale{makutano} nao hakuwajua sababu hasaa ya Pilato kufanya vile, Wao WALIKISIA TU! mioyoni mwao, labda wale watu watakuwa na laana kutoka kwa Mungu na ndio maana wamekutwa na mambo kama yale, au walimkufuru Mungu katika mioyo yao,na ndio maana Mungu akaruhusu Pilato aje kuwaua, au walikuwa na dhambi sana zisizovumilika na ndio maana yakawapatwa mambo kama yale n.k.,  

Lakini Bwana akifahamu mawazo yao, akawaongezea kuwakumbusha kisa kingine cha kushtusha kinachofanana na hicho kilichowatokea pengine miezi michache tu! nyuma huko huko Israeli kabla ya tukio hilo, nacho ni kuhusu wale watu walioangukiwa na mnara kule Siloamu..,kwamba wasidhani na wale yaliwapatwa na yale mambo eti kwasababu walimuudhi Mungu kupita kiasi? jibu lake lilikuwa ni hapana.. … Na ndio maana ukiendelea kusoma utaona Bwana anawaambia sivyo kama wanavyofikiri..   Soma tena hapo hiyo habari utaona mawazo ya wale watu yalikuwa ni nini?…

Luka13:1 Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichanganya damu yao na dhabihu zao.

2 Akawajibu akawaambia, Je! Mwadhani ya kwamba Wagalilaya hao walikuwa wenye dhambi kuliko Wagalilaya wote, hata wakapatwa na mambo hayo?

3 Nawaambia, SIVYO; lakini MSIPOTUBU, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.  

Unaona hapo Bwana Yesu alijua mawazo yao kwamba wanadhani kuwa yale mambo yaliyowakuta wale watu ni kutokana na dhambi zao kuwa nyingi sana. Lakini yeye aliwambia sivyo kama wanavyofikiri.   Bwana aliwaambia hata wao pia wasipotubu yatawapatwa na mambo kama hayo hayo. Kadhalika, tetemeko la ardhi lililotokea Kagera, tunadhani wale watu walikuwa na laana sana kuliko sisi??..Ile mvua ya mawe iliyouwa makumi ya watu kule Geita tunadhani wale watu walimkosea sana Mungu kuliko sisi?? ajali ya MV BUKOBA wale watu walikuwa waovu zaidi yetu sisi?..hapana Hakika na sisi pia tusipotubu yatatukuta kama hayo hayo.. Tsunami iliyotokea 2004 huko Indonesia na kuua maelfu ya watu duniani, na sisi kunusurika, tunadhani zile nchi zilimkosea Mungu sana zaidi yetu sisi …Sivyo, tusipotubu na sisi yatatukuta kama hayo..   Huyo jirani yako aliyekufa na ajali wiki chache zilizopita unadhani alikuwa anayo bahati mbaya sana kuliko wewe?..Sivyo lakini usipotubu siku moja yatakukuta na wewe kwa ghafla na kujikuta umeenda kuzimu.  

Hivyo tujichunguze kwanza sisi mioyo yetu, kisha tujue kuwa uvumilivu wa Mungu ni kutuvuta sisi tufikie toba. Mungu amekupa uhai na pumzi, sio kwasababu wewe ni mwema sana zaidi ya yule aliyekufa jana hapana..lakini fahamu kama usipomzalia matunda ya uhai wako sasa, yatakukuta hata pengine makubwa zaidi ya hayo yaliyowakuta hao wengine. Je! Umeokolewa? Je! Una uhakika wa kwenda mbinguni ukifa leo kifo cha ghafla?… yahakiki maisha yako tena, na umgeukie Mungu maadamu muda upo.  

Ubarikiwe sana .jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

JINSI EDENI ILIVYOKUWA.

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!

MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya ELOHIMU?

JIBU: Kwanza kumbuka katika lugha ya kiswahili hilo neno ELOHIM, halionekani likitajwa katika biblia yetu kwasababu halipo katika lugha ya kiswahili. Hili ni neno la Kiebrania linalomaanisha Mungu, Kama tukisoma katika sura ya kwanza kabisa ya kitabu cha mwanzo biblia inasema “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi”..Hii ni katika lugha yetu ya kiswahili lakini kwa kiebrania inatafsiriwa hivi; Hapo mwanzo ELOHIM aliziumba mbingu na nchi.

Unaona tofauti hapo? na neno hili limetokea kwenye agano la kale mara 2500 katika biblia yao ya kiyahudi, lakini kwetu limetafsiriwa kama Mungu. Wakati mwingine hili neno ELOHIM limefupishwa kama “EL” ..Na ndio maana sehemu nyingine anajulikana kama EL’Shadai ikiwa na maana kuwa yeye ni “Mungu mwenyezi” kwa lugha yetu ya kiswahili (Mwanzo 17:1, kutoka 6:3 )..Sehemu nyingine anatajwa kama EL ROI, ikimaanisha “Mungu anayeona”(Mwanzo 16:13)..

Kadhalika sehemu nyingine anatajwa kama El Elyoni ikimaanisha “Mungu aliye juu”…Haya majina yote utayakuta katika nakala za biblia ya kiebrania. mahali pengine tuliomwona Bwana Yesu akilitamka hili jina kama lilivyo, pale alipokuwa msalabani tunaona alisema..EL’OI ELOI lama Sabakthani…tafsiri yake ni Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha?.. 

Kwahiyo jina Elohimu ni Mungu ikimaanisha kwamba ni Mungu asiyekuwa na mwanzo, wala mwisho, Mungu mwenyezi, muweza yote, muhukumu, muumba, n.k. kwa ufupi hilo jina Elohimu linabeba tabia zote za Mungu. 

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

JINA LA MUNGU NI LIPI?

USILITAJE BURE JINA LA BWANA!

ACHENI MJUE YA KUWA MIMI NI MUNGU.

MUNGU MWENYE HAKI.

DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.


 

Rudi Nyumbani

Print this post

Wale manabii 400 waliomtabiria mfalme Ahabu wakati wa Mikaya walikuwa ni manabii wa Mungu au?

JIBU: Ndio wale manabii 400 waliomtabiria Ahabu (tunaowasoma katika 1wafalme 22 ) walikuwa ni manabii wa Mungu, na hapo kabla walikuwa wanapokea unabii sahihi kutoka kwa Mungu kwasababu manabii zamani ilikuwa ni lazima wajaribiwe kwanza kabla ya kuitwa mbele za wafalme,. Ni lazima nabii huyo ashuhudiwe kutoa unabii na kutimia vinginevyo hawezi hata kumkaribia Mfalme. kwahiyo ni dhahiri walikuwa wanatoa unabii na unatimia kabisa, japo mioyo yao haikuwa mikamilifu mbele za Mungu kama ilivyokuwa kwa nabii Mikaya…

walikuwa wanapenda utukufu wa wanadamu kuliko utukufu wa Mungu na ndio maana walikuwa wanakaa katika majumba ya kifalme, wakipenda kuwatabiria watu mambo mazuri tu ya faraja hata kama wapo katika dhambi zao, Hivyo tabia hiyo ikawapelekea kupata sifa nyingi kutoka kwa wafalme, lakini hawakujua kuwa Mungu alikuwa amewaacha. Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake Luka 6: 26 ” Ole wenu ninyi watu wote watakapowasifu, kwa kuwa baba zao waliwatenda manabii wa uongo mambo kama hayo.”

 Mfano mwingine wa manabii kama hawa tunamwona nabii Balaamu (hesabu 22), aliyetaka kwenda kuwalaani Israeli kwa ujira wa udhalimu ili amridhishe tu mfalme Balaki.. 

Huu ni mfano pia wa manabii wengi tulionao sasa wanapenda kusifia pesa,umaarufu,ukubwa, vyeo, wanawatolea watu unabii ili wapate pesa, na kupendwa, sasa manabii kama hao ni rahisi kuingiwa na roho zidanganyazo, hivyo kuwafanya leo wasikie kutoka kwa Mungu kesho wasikie kutoka kwa shetani..lakini manabii kama Mikaya ambao ni wachache sana wao husimama katika Neno, huishi maisha matakatifu na kusema kile Mungu anachotaka tu waseme pasipo kujali cheo cha mtu,utajiri wa mtu, au hali ya mtu, hivyo Mungu anawaepusha na roho zidanganyazo na unabii wao unakuwa thabiti na hakika siku zote, lakini kwa hao wengine wanafungua milango kwa roho zidanganyazo kama ilivyowatokea wale manabii 400.(Mapepo yalivyowaingia wote na kutabiri uongo mbele za Mfalme) 

Hivyo ndugu ni kuwa makini na aina ya manabii waliopo leo hii. Mtu yeyote anayejiita nabii akija na kukutolea unabii ni vizuri kabla ya kuupokea huo unabii, uupime kwanza kwenye NENO, kisha ukilandana nalo ndipo uuchukue, kama haulandani hata kama alishakutolea unabii hapo kabla na ukatimia, usipokee. Kwamfano mtu alikutabiria na kukwambia Bwana kamwonyesha baada ya mwezi mmoja utabeba mimba ya mapacha na wewe wakati huo ni mgumba, na kweli huo wakati ulipofika ukapata mimba na kujifungua mapacha kama alivyokutabiria, lakini leo hii anakuja tena na kukwambia Bwana kamuonyesha umuache huyo mume uliyefunga naye ndoa uliye naye leo ukaolewe na mwingine Bwana aliyekukusudia..Sasa kiharakaharaka ni rahisi kumwamini kwasababu alishakutabiria mara ya kwanza na ikatimia lakini wewe hujui mahusiano yake na Mungu wake yalishaharibika hivyo kumfanya apokee maono mengine kutoka kwa shetani akidhani ni ya Mungu, kwasababu ulinzi ndani yake haupo, dhambi imemtawala amekuwa lango la shetani …Ndivyo walivyofanya wale manabii 400 wa Ahabu. 

Sasa unapokutana na unabii kama huo unakumbuka lile neno linalosema “mtu atakayemwacha mume/mume wake isipokuwa kwa habari ya uasherati na kwenda kuolewa na mwingine azini na anamfanya yule aliyemwacha kuwa mzinzi”…Hivyo hapo unauacha huo unabii na kulishikilia Neno. Soma mstari huu. 

Kumbukumbu 13: 1 “Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu,

2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo;

3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote.

4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye.

5 Na yule nabii, au yule mwotaji wa ndoto, na auawe, kwa kuwa amesema yaliyopotoka juu ya Bwana, Mungu wenu, aliyewatoa katika nchi ya Misri, akakukomboa katika nyumba ya utumwa, apate yule mtu kukupotoa katika njia aliyokuamuru Bwana, Mungu wako, uiendee. Ndivyo utakavyouondoa uovu utoke katikati yako”. 

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

NITAMJUAJE NABII WA UONGO?

TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.

MPINGA-KRISTO

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

KUCHEZA KARATA NI SAHIHI KWA MTU ALIYE MKRITO?

SEHEMU ISIYO NA MAJI.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Bwana Yesu alikuwa anamaanisha nini kusema Marko 2:19″walioalikwa harusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao?”

Marko2:18 “Nao wanafunzi wake Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga; basi walikuja, wakamwambia, Kwani wanafunzi wa Yohana na wanafunzi wa Mafarisayo hufunga, bali wanafunzi wako hawafungi?
19 Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao? Muda wote walipo na bwana-arusi pamoja nao hawawezi kufunga.
20 Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana-arusi, ndipo watakapofunga siku ile.   

JIBU: shalom! Mfano huo sawa tu, na mwanafunzi aliye na mwalimu wake, pindi anapokuwa naye anao uwezo wa kumuuliza swali lolote na likajibiwa, au akampelekea mwalimu wake maswali yote magumu yanayomsumbua na yakatatuliwa pindi wakati yupo naye, lakini kikifika kipindi cha mitihani, labda mtihani wa NECTA, pale ambapo anawajibika kuketi mwenyewe kwenye chumba cha mtihani mahali ambapo mwalimu wake hawezi kuwepo tena hapo ndipo itampasa atumie nguvu na jitihada ya ziada kutatua maswali yote peke yake anayokutana nayo kwa maarifa aliyopewa na mwalimu wake, lakini hapo mwanzo angeweza kumpelekea tu kila swali linalokuja mbele yake na akasaidiwa pasipo hata kujishughulisha…  

Na ndivyo ilivyokuwa kwa mitume wa BWANA wetu YESU KRISTO wao walipewa neema ya kipekee kutembea na Mungu( BWANA YESU) duniani tofauti na wanafunzi wa Yohana au masadukayo, sasa unategemea vipi watu kama hao wafunge, au kujisumbua kwa lolote, wakati wanayemwomba wapo naye hapo hapo…wakiwa wanahitaji ufunuo wa jambo fulani si wanamkimbilia BWANA na kumuuliza kwasababu yupo nao hapo?!!!…

Na ndio maana akasema wakati utafika Bwana arusi atakapoondolewa…hapo ndipo watalazimika kufunga kama wenzao. Wakitaka ufunuo wa jambo fulani sasa itawapasa wafunge, wakitaka kutatua au kujua jambo fulani itawapasa wafunge kwanza na kuomba,Kwahiyo kile kitendo cha wao kutembea, kula, kuishi na kufundishwa na BWANA ndio kualikwa kwenyewe Harusini.   Kuna kipindi Bwana alimwamsha Petro na wenzake wasali, lakini walilemewa na usingizi wakalala, lakini baada ya Bwana kuondoka unamwona Petro anakuwa wa kwanza kusali na kufunga mpaka anazimia kwa njaa (Matendo 10:9).  

Kadhalika na sisi tunapompokea Kristo kwa mara ya kwanza kunakuwa na neema fulani ya kipekee inakuwa juu yetu, kila tuombalo tunalipokea haraka sana, kwasababu bado hatujajua umuhimu wa kuomba, hatujajua umuhimu wa kufunga, hivyo neema ya Mungu inakuwa juu yetu kubwa kama watoto wachanga, lakini unafika wakati Bwana anaipunguza ile neema, (Bwana arusi anaondolewa )unakuwa ili upate jambo fulani inakupasa uombe kwa bidii, wakati mwingine kwa kufunga, ili upate ufunuo wa Roho inakupasa kujifunza sana maandiko kwa muda mrefu n.k, kwasababu unakuwa sio mtoto tena, Bwana anakutoa hatua moja kwenda nyingine.  

Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

MUNGU NDIYE ANAYEISHAWISHI MIOYO.

JIKANE NAFSI MTEULE WA MUNGU.

NINI MAANA YA HILI ANDIKO “USHUHUDA WA YESU NDIO ROHO YA UNABII” (UFUNUO 19:10)?

NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO:


Rudi Nyumbani:

Print this post

Paulo alimwambia Timotheo atumie mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lake, Je! tunaruhusiwa na sisi pia kutumia pombe?

Tukisoma hilo andiko Biblia inatuambia

1Timotheo5:23″ TOKEA SASA USINYWE MAJI TU LAKINI TUMIA MVINYO KIDOGO,KWA AJILI YA TUMBO LAKO,NA MAGONJWA YAKUPATAYO MARA KWA MARA.  

JIBU: Mtume Paulo alivyosema hivyo hakuwa na maana ya kuhalalisha pombe hapana!! kumbuka divai nyakati za zamani ilikuwa na matumizi mengi, ilikuwa inatumika kama dawa kutibia vidonda,n.k. Kwamfano unamwona yule Msamaria ambaye tunasoma habari zake

Luka 10: 33 “Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,

34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia MAFUTA NA DIVAI; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza”.

Unaona hapo?   Na ilikuwa pia ina matumizi mengine mengi, sasa zamani za kanisa la kwanza wakristo wengi walikuwa wanafunga muda mrefu, na kusafiri umbali mrefu kwenda kuhubiri injili, kwasababu kulikuwa hakuna magari wakati ule, au ndege kama tulizonazo sasa , kwahiyo kutokana na hari za jua na majangwa, na kufunga juu yake, wakati mwingine utumbo unakuwa unajisokota, au kunakuwa na udhaifu fulani katika mwili,   Sasa Mtume Paulo kwa kulijua hilo kutokana na uzoefu wa muda mrefu aliokuwa nao wa kusafiri masafa marefu kuhubiri injili, alimshauri Timotheo asitumie maji tu bali na mvinyo(divai) kidogo kwa ajili ya tumbo, na sio kwaajili ya kujifurahisha au kujiburudisha wanavyofanya watu sasahivi,

kwahiyo unaona hapo? anamshauri atumie kama DAWA, ni sio kama kiburudisho, ni sawa na mimi nikushauri wewe unaposafiri mahali palipo na ukame kidogo wa chakula kwa ajili ya injili usinywe maji matupu peke yake, bali unywe kinywaji chenye nguvu kidogo (mfano Energy drink),ili mwili usipungukiwe nguvu njiani. unaona hapo nia yangu sio kukwambia unywe energy drink kila wakati, kujiburudisha hapana bali nia yangu ni kukuzuilia mwili usidhoofike njiani kwa muda ule utakapokuwepo safarini, kutokana na uzoefu nilio nao kusafiri mda mrefu.  

Hivyo mtu yoyote anayeshikilia hilo andiko kiuhalalisha atajua kabisa pombe ni makosa, kwasababu hakuna mtu yoyote anayekunywa pombe kama dawa katika mwili wake,.wote wanakunywa kwa ajili ya tamaa za mwili na ulevi, ambayo ni dhambi na hata hivyo ukiangalia kwa makini utaona pombe zote tulizonazo sasahivi hazina matumizi mengine zaidi ya ULEVI tu, basi zimetengenezwa mahususi kwa ajili ya kazi hiyo na si vinginevyo…Hivyo mkristo yoyote anayekunywa pombe anafanya makosa mbele za Mungu kwa kisingizio cha huo mstari.  

Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada zinazoendana:

MATUMIZI YA DIVAI.

JE! MABALASI BWANA YESU ALIYOYATUMIA KUGEUZIA MAJI KUWA DIVAI, YALITUMIKA TU KWA KAZI HIYO?

JE NI SAWA KWA MKRISTO KUUZA MAZAO YA KUTENGENEZEA POMBE KAMA VILE MTAMA?

RABONI!

KWA MUNGU ASIYEJULIKANA.


Rudi Nyumbani:

Print this post