Marko 7:34 “akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka. Mara masikio yake yakafunguka, kifungo cha ulimi wake kikalegea, akasema vizuri. AKAWAONYA WASIMWAMBIE MTU; LAKINI KADIRI YA ALIVYOZIDI KUWAAGIZA, NDIVYO WALIVYOZIDI KUTANGAZA HABARI; wakashangaa mno kupita kiasi, wakinena, Ametenda mambo yote vema; viziwi awafanya wasikie, na bubu waseme”