Tuchulie Mfano ulio hai ni sawa na leo hii unataka kuwasiliana na mimi bila kutegemea hicho kioo kilichopachikwa mbele ya simu yako, ni kweli kabisa Simu sio hicho kioo ambacho unakipangusa,na kuandika namba juu yake, …Simu ni ni kitu kingine cha ndani kilichojawa na Commands tofauti tofauti ili kufanya kifaa hicho kiweze kutumika kwa mawasiliano, sasa ikiwa utaondoa hicho kioo cha juu na ukataka kuwasiliana nami, basi jiandae kukukutana huko nambo ambayo hujayazoea maneno huko kama Galllery, au Contacts, au SMS, usitazamie utayakuta huko wala kidole hakitahitajika huko kufanya mawasiliano yaende.., ni wazi kuwa utakutana na vitu kama chips, cards,modems,processors,circuit board, na vinginevyo ambavyo hata kwa lugha ya Kiswahili havina tafsiri, ambavyo wewe kwa akili yako ya kawaida hutaelewa chochote isipokuwa yule mtaalamu wa hivyo vitu, yeye pekee ndiye anayeweza kupiga simu pasipo kioo kile, kwa vifaa na ujuzi alionao ..