Hapo anasema NA KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, ikiwa na maana kuwa, kuna uwezekano tukamfahamu kidogo, hivyo inahitajika kumfahamu sana MWANA WA MUNGU (YESU KRISTO) Na kusudi lenyewe la kumfahamu sana Yesu Kristo, sababu zimeshatolewa hapo mbele nazo ni “ili tusiwe tena watoto wachanga tukichukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja,na kuzifuata njia za udanganyifu”.
Moja ya jukumu la muhimu sana kwa mkristo yoyote aliyezaliwa mara ya pili ni KUJIFUNZA KUMJUA YESU KRISTO NI NANI??…Kwa maana neno lenyewe Mkristo, limetokana na neno KRISTO yaani yeye aliyetiwa mafuta na Mungu, kwa hiyo kama Yesu ndiye Kristo moja kwa moja wafuasi wake wataitwa Wakristo. Taifa la Tanzania lina watu wake wanaoitwa watanzania, kadhalika na taifa la Marekani, watu wake wanajulikana kama wamarekani, vivyo hivyo Taifa la Yesu Kristo, watu wake wataitwa Wakristo..