DUNIANI MNAYO DHIKI.

DUNIANI MNAYO DHIKI.

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

Maneno hayo yalitoka kinywani mwa Bwana wetu YESU KRISTO mwenyewe ambaye yeye hakuwa na dhambi hata moja. Ni mtu aliyependwa na Baba kuliko mtu mwingine yeyote ambaye alishawahi kutokea hapa duniani kwa jinsi tu ule mwenendo wake ulivyokuwa mkamilifu..Mtu ambaye alikuwa  akimwomba Mungu jambo lolote anafanyiwa haraka sana, angetaka utajiri wote duniani angepewa, angetaka kuabudiwa angeabudiwa, alikuwa hana shida ya jambo lolote, lakini bado hapa tunaona anawaambia wanafunzi wake “Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”…

Hivyo dhiki haijalishi wewe ni mtakatifu kiasi gani, maadamu upo tu duniani utakumbana nazo kwa namna moja au nyingine, dhiki zinazokuja kutokana na Imani yako, kuchukiwa kutengwa, kudharauliwa, kupigwa, kufungwa, kuwindwa, kupungukiwa, kufiwa na ndugu wa karibu, magonjwa n.k.

Lakini pamoja na hayo alituahidi kuwa atakuwa nasi sikuzote hadi ukamilifu wa dahari (Mathayo 28:20)na kwamba hatutajikwaa hata tukitembea katika majaribu mazito namna gani atatembea na sisi kuhakikisha hatuanguki, kama tu bado tutakuwa katika wokovu.

Zaburi 34:7 “Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa”.

Zaburi 91:11 “Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.

12 Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe”.

Na ndio maana akatuambia hapo TUJIPE MOYO. Kama yeye ameyashinda, basi tuwe na uhakika kuwa na sisi tutayashinda kwasababu yeye yupo pamoja na sisi kutusaidia..Kwahiyo ndugu yangu mkristo, uliyeokoka ambaye upo katika tumaini la kumngojea Bwana, nataka nikuambie usifadhaishwe na dhiki ya aina yoyote mbele yako wewe JIPE MOYO, aliye ndani yako hawezi kukuacha. Hakumwacha Danieli katika tundu la Simba, hawezi kukuacha na wewe, kukutana na simba haikumaanisha ndio mwisho wa kila kitu, wewe kukutana na dhiki haimaanishi ndio mwisho wako umefika, jipe moyo tu, hakuwaacha akina Shedraka, Meshaki na Abadnego katika tanuru la moto mkali namna ile hatoweza kukuacha na wewe..Hakumwacha Yusufu katika dhiki zile kule gerezani milele ulifika wakati akamfariji hatakuacha na wewe. Ikiwa bado unaishikilia imani yako, na kudhamiria kweli kweli kumfuata Kristo bila kigugumizi.

Wakati wako utafika mawimbi yote yatakwisha, lakini maadamu upo sasahivi katika hali hiyo liweke hili Neno moyoni, JIPE MOYO, JIPE MOYO, JIPE MOYO…Bwana yu pamoja nawe..USHINDI NI LAZIMA. Kama yeye alivyoshinda hivyo SONGA MBELE..

Maran Atha!

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JIPE MOYO.

BADO KITAMBO KIDOGO HAMNIONI

VIUNO VYENU VIWE VIMEFUNGWA NA TAA ZENU ZIWE ZINAWAKA.

WACHUNGAJI WA BWANA MAKONDENI.

VITA BADO VINAENDELEA.

TUKAZE MWENDO ILI TUUFIKILIE UTIMILIFU.


 

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Adamu Kimu
Adamu Kimu
1 year ago

Ni mafundisho mazuri sana sijawahi kukutana nayo. Yamenijenga kiimani, nimeyapenda sana niendelee kujifunza katika siku za usoni ,
Bwana Yesu awabariki kwa kazi hii njema