Umeona ndugu?, hakuna nafasi ya pili kama ukimkataa Kristo kwa makusudi sasa, unapohubiriwa injili yake kwa Roho wake, anaondoka na kwenda kwa mwingine? Na kwako inabakia kuwa hukumu. Biblia inasema waasherati wote, wasengenyaji, walafi, walawiti, walevi,wachafu,watukanaji, wala rushwa, waabudu, sanamu sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti, HAIDANGANYI!! Ni kweli itakuwa hivyo, mtu yeyote anayekuambia kwamba walevi wataokolewa anakudanganya, yeyote anayekuambia kwamba wanaopaka wanja na lipstiki na kuvaa wigi na suruali na herein wataokolewa kwamba Mungu haangalii Roho anaangalia mwili, nataka nikuambia jambo hili moja Roho Mtakatifu anasema sehemu yao itakuwa ni KATIKA LILE ZIWA LA MOTO!!. Anayekuambia kwamba kuwa kuishi na mwanamume au mwanamke ambaye hamjafunga ndoa au ambaye ameachana na mke/mume wake sio dhambi, anakudanganya Yesu Kristo anazungumza na wewe leo kwa namna ya Roho, kwamba “AMWACHAYE MKE WAKE NA KUOA MWINGINE AZINI, NAYE ALIYEMUOA YULE ALIYEACHWA AZINI” Mtii Yesu Kristo leo na maneno yake, Usiusikilize uongo wa shetani ambao baadaye utakufanya ujute milele.