Title March 2025

JE UTAKATIFU NI MATENDO YA SHERIA?

Ipo elimu kwamba kuishi maisha ya utakatifu ni kuishi kwa sheria, na biblia inafundisha kuwa “hatuishi chini ya sheria bali tunaishi chini ya Neema” na tunahesabiwa haki bure kwa imani si kwa matendo.

Dhana hii inazidi kwenda mbali  kwa kusisitiza kuwa maisha ya utakatifu ni ngumu kuishi, na ni vigumu kuishi maisha hayo kwasababu ni  sawa na kujifunga kwa sheria.

Ndugu kama na wewe ni mmoja ya watu wanaoamini hivi kwamba…“utakatifu ni kifungo kigumu cha sheria”…bali leo soma ujumbe huu mpaka mwisho, utapata kuelewa jambo.

Hebu tafakari mfano huu:

》 Upo jikoni unaandaa chakula kwa bahati mbaya ukagusa sufuria ya moto, bila shaka kitakachofuata baada ya hapo, ni wewe kutoa mkono wako sehemu hiyo ya moto kwa haraka sana..

》Au labda umeketi mahali na ghafla ukaona kuna kitu/uchafu unakaribia macho yako, ni wazi kuwa utafumba macho ghafla na kwa kasi.

》Au linapotokea jambo la kushtusha na mapigo ya moyo kuongezeka kasi na mwili kutetemeka

Sasa matendo hayo yote ya kuondoa mkono kwa kasi kutoka kwenye sufuria yenye moto na kufumba macho ghafla pale hatari inapoyakaribia macho yako, na mapigo ya moyo kuongezeka kasi, na mwili kutetemeka huwezi kusema ni matendo ya sheria uliyojiwekea wewe yanayokuongoza…

La! bali ni sheria mwili uliojiwekea isiyohusisha hiari yako wala maamuzi yako, unajikuta tu unafanya hayo matendo bila kupenda au kuamua au hata kutafakaro… yaani ni matendo yanayotokana na mwitikio wa mwili kutokana na mazingira ya nje yanayoendelea.

Na Lengo ni kuulinda mwili wako usidhurike au usiendelee kudhurika..

Hali kadhalika matendo ya utakatifu ni mwitikio wa nje wa imani iliyopo ndani ya mtu na si matendo ya sheria..

Mtu aliyeipokea imani kweli kweli na kubatizwa na Roho Mtakatifu, anajikuta tu kuna mambo anayafanya pasipo hiari yake.

Anapokaribia mazingira ya dhambi amani inatoweka yenyewe pasipo yeye kuamua na hivyo anayaepuka hayo mazingira haraka sana.

Akisikia masengenyo ni kama vile mtu aliyeketi kwenye mazingira ya takataka na akapata kichefuchefu katika mazingira yale, kile kichefuchefu hakupanga wala kuamia kije, bali kinakuja chenyewe tu, ili utoke katika yale mazingira, ni kwa namna hiyo hiyo mazingira ya usengenyaji, au mazungumzo mabaya ni kichefuchefu kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili kweli kweli.

Na hilo sio jambo linalompa shida sana kulitekeleza, bali linatoka tu lenyewe ndani, dunia nzima inaweza kumwona kama hayupo sawa kiakili au yupo kwenye utumwa mzito wa sheria alizojiwekea, lakini kumbe ni kinyume chake, mambo anayoyafanya yanabubujika yenyewe ndani yake na si sheria alizojiwekea.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba. Matendo ya utakatifu si sheria bali ni matendo yanayotendeka ndani ya mtu pasipo sheria, hata kama yanaonekana kama yamekaa kisheria, na hayo ni mambo ya rohoni yanayotambulika na watu wa rohoni kama maandiko yanavyosema..

1 Wakorintho 2:14 “Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.

15 Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu”.

Mtu kamwe hawezi kuuishi utakatifu kama hatakuwa na ujazo wa Roho Mtakatifu..

Na hiyo inahitaji Maamuzi mazito, yaani kumwamini Bwana YESU, kutubu dhambi na kubatizwa kwa maji mengi na kwa Roho Mtakatifu.

Kwahiyo kama utaamua kufanya mageuzi ya kweli kweli ya kuamua kumfuata YESU kwa kutubu dhambi kabisa na kujikana nafsi na kujitwika msalaba wako na kumfuata na kujazwa Roho Mtakatifu, nakuhakikishia suala la kuutimiza utakatifu kwako halitakuwa sheria bali mwitikio wa hiari.

Hutakuwa unakunywa pombe kwasababu imeandikwa usilewe, bali utakuwa hunywi pombe kwasababu hiyo kiu wala shauku itakuwa haipo ndani yako.

Hutazini kwasababu maandiko yamesema usizini, bali hutazini kwasababu hiyo kiu au msukumo utakuwa haupo ndani yako

Hutasengenya kwasababu maandiko yanasema usisengenye bali hutasengenya kwasababu mazingira hayo kwako ni kichefuchefu.n.k

Sababu kubwa uminayomfanya mtu asipokee hii nguvu ya kuishi maisha masafi?..ni jinsi alivyopokea na alivyoamini.

Kama mtu ameamini au ameaminishwa kuwa hawezi kuishi maisha ya utakatifu duniani, na pia ukienda kwa YESU hakuna haja ya kujitoa wote (kujikana nafsi)..hapo ndipo tatizo linapoanzia..

Utatakaje matunda ya mtu na bado humtaki yule mtu,..utatakaje matunda ya Roho Mtakatifu na bado humtaki YESU??..Unampa asilimia moja ya maisha yako na asilimia nyingine 99 ipo kwa ibilisi na ulimwengu!…hapo kwanini matendo ya utakatifu yasiwe sheria ngumu kwako??.

Jikane nafsi, (hilo jambo usilikwepe)..Dhamiria kumfuata YESU kwa moyo wako wote…. Ingia gharama kubwa kuacha vingi katika maisha yako, jitoe wote halafu uone nguvu itakayoingia ndani yako.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

CHAGUA UTAKATIFU MWAKA HUU.

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI (Sehemu ya pili)

Wabadili fedha ni watu gani kwenye biblia? (Mathayo 21:21)

MGAWANYIKO WA ISHARA ZA UJIO WA BWANA YESU KRISTO.

Kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi, maana yake nini? (Zab.18:26)

Print this post

TOFAUTI KATI MAASKOFU, MASHEMASI, WAZEE WA KANISA NI IPI?

Katika kanisa, Mungu aliweka huduma mbalimbali, karama mbalimbali, na utendaji kazi tofauti tofauti, ili kulikamilisha kanisa lake na kuupanda ufalme wake duniani kama alivyokusudia.

Sasa katika upande wa huduma, Mungu aliziweka huduma kuu tano, ambazo zenyewe zinasimama kama kuliongoza kanisa, kulikuza, kulichunga, ni kama nguzo za kanisa ambazo husimama wakati wote, Nao ni;

Mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji na waalimu. (Waefeso 4:10-12)

Kwa urefu wa maelezo ya huduma hizo jinsi zinavyotenda kazi basi bofya hapa upitie >>> TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?

Lakini sambamba na hizo aliweka wengine katika kanisa, wanaoshirikiana na hawa watano (5).

Ambao ni  WAZEE WA KANISA, MAASKOFU na MASHEMASI

Tuangalie kazi ya kila mmoja;

1) WAZEE:

Tamaduni za kiyahudi tangu zamani walikuwa na desturi ya kuteuwa wazee (watu waliokomaa kiumri), wenye hekima na busara na uzoefu wa Kidini  kufanya maamuzi na Kutoa hukumu mbalimbali katikati ya jamii ya wayahudi Soma (Kutoka 3:16, Kumbukumbu 1:9-18)

Hata baadaye kanisa lilipokuja kuanza, nyakati za mitume, tunaona bado walirithi utaratibu huo katika nafasi za kiuongozi ndani ya kanisa. Isipokuwa haikuhitaji awe ni lazima mzee Kiumri, lakini ni lazima Awe amekomaa Kiroho.

Nafasi hii hasaa iliwahusu wanaume, Kwasababu katika nyaraka za mitume hatuoni mahali popote kama kuna mfano wa mwanamke aliyeteuliwa kuwa  mzee wa kanisa.

Ukisoma Tito 1:6, inaeleza sifa zao, anasema wazee wawe waume wa mke mmoja..

Tito 1:5-6

[5]Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;

[6]ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.

(Matendo 14:23)

Zingatia: Hii haiwafanyi wanawake wasiwe na kazi yoyote katika kanisa hapana, wanaweza kusimama kama huduma-kivuli ambazo zaweza Kuonekana kama za wazee wa kanisa, waalimu, mashemasi, kama wasaidizi wenye huduma hizo, lakini sio rasmi kwao. Mfano wa hawa kwenye biblia walikuwa ni akina Fibi, prisila,

KAZI ZA WAZEE WA KANISA:

1). Kulichunga kundi,

Matendo 20:28

Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.

(Soma pia 1Petro 5:1-4)

ii) Kufundisha vema watu. 

1 Timotheo 5:17

[17]Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.

Tito 1:9

[9]akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.

iii) Kutatua migogoro ya kiimani ndani ya kanisa.

Utakumbuka wakati ule makanisa ya mataifa yalikuwa yakitaabishwa, na wayahudi juu ya kushika torati, hivyo  kukatokea mkanganyiko mkubwa, na kuwalazimu wawafuate wazee kule Yerusalemu ili walitatue tatizo hilo, na kama tunavyosoma baada ya hoja nyingi, walifikia hitimisho sahihi la Roho Mtakatifu.

Matendo 15:6 Mitume na wazee wakakusanyika wapate kulifikiri neno hilo.

7 Na baada ya hoja nyingi Petro akasimama, akawaambia, Ndugu zangu, ninyi mnajua ya kuwa tangu siku za kwanza Mungu alichagua miongoni mwenu ya kwamba Mataifa walisikie neno la Injili kwa kinywa changu, na kuliamini

iv) Kuwaombea wagonjwa.

Yakobo 5:14-15

[14]Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.

[15]Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.

2) MAASKOFU.

Maana ya Askofu ni mwangalizi.

Kazi yake kubwa ni kuliangalia kanisa,/ kulisimamia, mfano kusimamia malengo ya kikanisa, kulinda fundisho, na kusimamia uchungaji ulio bora.

Japokuwa mahali pengine maaskofu wanatajwa kama wazee wa kanisa. (Tito 1:5-9).

Lakini tofauti yao hasaa ni kwamba wazee wanayasimamia makanisa madogo madogo, lakini maaskofu ni waangalizi wa makanisa (yote/baadhi), Wazee wanaweza kuwa wengi, lakini maaskofu ni cheo, cha uangalizi hivyo aweza kuwa mmoja au wachache, wazee wanaweza kuwa na wajibu wa kufundisha, na kuchunga, lakini maaskofu hasaa katika kuongoza. Vilevile kwenye maandiko hatuoni mahali popote nafasi hii ikihusisha wanawake.

Sifa za maaskofu na wazee, wa kanisa zinafanana.

Sifa za mtu kuwa mzee wa kanisa. (Tito 1:5-9, 1Timotheo 3:1-7)

  1. Awe mtu asiyelaumika
  2. Awe Mume wa mke mmoja,
  3. Mwenye kiasi
  4. Mwenye busara
  5. Mtu wa utaratibu
  6. Mkaribishaji
  7. Ajuaye kufundisha
  8. Si mtu wa kuzoelea ulevi
  9. Si mpiga watu
  10. Awe mpole
  11. Si mtu wa kujadiliana
  12. Asiwe mwenye kupenda fedha
  13. Awezaye kuisimamia nyumba yake vema
  14. Asiwe mwongofu mpya.

3) MASHEMASI.

Mashemasi ni mtumishi wa kanisa.  Huduma hii ilitokea katika kanisa kwa mara ya kwanza, mitume walipokuwa wanahudumu na kuona kuwa baadhi ya mapungufu kwamba wajane wanasahaulika katika huduma ya kila siku, ndipo ikalazimika wateue watu saba, ndani ya kanisa watakaoweza kusimamia mambo yote ya kimahitaji ya kundi.  (Matendo 6:1-7), mmojawapo alikuwa ni Stefano.

Kazi za mashemasi:

i) Kulihudumia kundi katika masuala ya mahitaji ya mwilini ya kundi:

Hususani kwa maskini, wajane, wenye mahitaji,  mayatima.

ii) Kuongoza kwa mifano:

Lazima wawe kipaumbele kitabia, uaminifu, na nidhamu Na kuonyesha roho ya kiutumishi

iii) Kusimamia shughuli za kikanisa:

Ujenzi, taratibu za kiibada na mikutano, kusimamia hazina na mali za kanisa.

Sifa za mtu kuwa shemasi:

Zinatajwa kwenye 1Timotheo 3:8

1Timotheo 3:8 Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu.

9 wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. 10 Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia.

11 Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; si wasingiziaji; watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.

12 Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao.

13 Kwa maana watendao vema kazi ya shemasi hujipatia daraja nzuri, na ujasiri mwingi katika imani iliyo katika Kristo Yesu

Hivyo wazee, maaskofu na mashemasi, ni nguzo muhimu za kulifanya kanisa kusimama, katika nidhamu ya kitabia na kimapokeo, pamoja na kihuduma.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.

Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?

JINSI BWANA ALIVYOWACHAGUA MITUME WAKE.

Print this post

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI (Sehemu ya pili)

Maombi ya shabaha kwaajili ya Kazi/kibarua/shughuli/biashara/elimu.


UTANGULIZI: Ni muhimu kujua hili: lengo kuu au kiini cha Wokovu ulioletwa na BWANA YESU KRISTO sio sisi tuwe matajiri au tupate mafanikio ya huu ulimwengu!.

Mafanikio ya dunia hii ni moja ya faida za mwisho mwisho kabisa za kusudi la msalaba wa Bwana YESU kwasababuwalikuwepomatajiri kabla ya Bwana YESU kuja duniani, hivyo KRISTO asingeweza kuja kutegua mtego aukutatua tatizo ambalo lilishatatuliwa huko nyuma.

Ingekuwa lengo lake ni ili tufanikiwe tuwe matajiri, angetuambia tu tusikilize hekima za Sulemani na tungefanikiwa, hakukuwa na haja ya kuja kumwaga damu yake.

Lakini suala la ondoleo la dhambi hilo halikuwahi kufanyika huko nyuma, hakuna aliyewahi kuondolewa dhambi, kwani dhambi zilikuwa zinafunikwa tu! (Soma Waebrani 10:3-4)..

Sasa hiko ambacho kilishindikana kutendeka huko nyuma (katika Agano la kale) ndicho kilichokuwa cha kwanza na cha msingi kilichomleta BWANA YESU duniani, na kitu hiko si kingine zaidi ya ONDOLEO LA DHAMBI.…kiasi kwamba mtu akikosa ondoleo la dhambi hata awe na vitu vyote ulimwenguni bado anayo hasara kubwa soma (Mathayo 16:26).

Kwahiyo ni muhimu kujua msingi huu, ili tunapokwenda kujifunza juu ya MAOMBI JUU YA KAZI au BIASHARA, Usiweke moyo wako wote huko!.. Yatumie tu maarifa haya kama sehemu ya maisha, lakini jali zaidi hatima ya roho yako, kupitia damu ya YESU na UTAKATIFU.

Sasa tukirudi katika kiini cha somo!.. Ikiwa unafanya kazi za mikono, labda tuseme biashara, tumia kanuni hii ya Maombi kupata FAIDA YA KILE UNACHOKIFANYA!!.

Badala ya kuombea bidhaa zako, kama sabuni unazouza, au dawa unazouza, au kingine chochote kwamba kiwe na mvuto, kuanzia leo punguza kuomba maombi ya namna hiyo, badala yake omba maombi yafuatayo.

– Kila mteja anayekuja kwako mwombe neema ya Wokovu, ikiwa bado hajampokea YESU, maombi ya namna hiyo yanamtoa yule mtu kutoka katika vifungo vya ibilisi na hatimaye kumfungua kabisa, na anapofunguliwa aweza kuwa mteja wako wa ajabu sana, au akawaleta na wengine wengi mahali ulipo.

– Ikiwa tayari ameshampokea YESU mwombee azidi kusimama katika imani, na mwombee akawe Nuru kwa wengine wengi, ombea na familia yake kama unaijua, hiyo ndio njia bora ya kuombea kazi yako au biashara yako..

– Unafanya biashara ya chakula, na wateja wako ni watu wa kidunia, badala ya kuombea madishi na chakula unachokipika kwamba wakipende, hebu waombee wampende YESU, halafu uone kama hiko chakula chako hawatakipenda, zaidi ya vyakula vya wengine wote.

– Pale ofisini acha kuombea uso wako kwamba upate kibali, sawa waweza kuomba hivyo, lakini isizidi sana kiasi kwamba hujui kitu kingine cha kuomba zaidi ya hicho, badala yake anza kuomba watu wa ofisini kwako wamjue MUNGU, wakimjua MUNGU wewe utapata kibali tu!, wala hutatumia nguvu nyingi.

– Pale shuleni acha kuombea walimu wakupende, hebu waombee wamjue YESU na kumpenda, halafu uone kama hawatakupenda na wewe.

– Unauza bidhaa, waombee wateja wako wamjue YESU na kumpenda zaidi ya bidhaa zako, halafu uone matokeo.

Ukitaka kufunga kwaajili ya biashara yako!, Funga kwa maombi ya kuwaombea wateja wako wokovu na Neema zaidi, kama unayo list, anza mmoja baada ya mwingine, wapatanishe na KRISTO hivyo uone kama KRISTO pia hatakupatanisha nao, utaona kazi zako zinaenda, shule yako inaenda, biashara yako inaenda, kazi yako inaenda.

Lakini ukijikita tu kuziombea bidhaa kama vile waganga wanavyotoa dawa za kwaajili ya biashara, matokeo yake yatakuwa ni madogo sana.

Hivyo OMBA lakini omba kwa shabaha/target.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI:

MWONGOZO WA MAOMBI YA FAMILIA

KWANINI MUNGU HAJIBU MAOMBI?

Mistari ya biblia kuhusu maombi.

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Print this post

Kwanini Mungu alimfunga tumbo Raheli, ilihali Yakobo alimtesekea miaka 14?

Jibu: Hakuna kosa lolote Raheli alilolifanya, lililomfanya afungwe tumbo asizae.. Lakini tukisoma maandiko twaweza kuona sababu kama mbili zilizopelekea yeye kufungwa tumbo na MUNGU mwenyewe.

 1. KUMNYENYEKEZA RAHELI na KUMTIA NGUVU LEA.

Tunasoma kuwa Lea ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa, na Yakobo alimpenda zaidi Raheli kuliko Lea, (na jambo hilo lilikuwa wazi linaonekana) kwahiyo labda ingetokea Yakobo aliyebeba ahadi za MUNGU kumuoa Raheli, na tena akazaa naye mtoto wa ahadi, huenda jambo hilo lingemfanya Raheli kujivuna/kujigamba mbele ya Lea dada yake, na hivyo Lea angekuwa duni/mnyonge mbele ya mdogo wake, kwahiyo MUNGU akamfunga tumbo.

Mwanzo 29:28 “Yakobo akafanya hivi, akatimiza siku zake saba. Naye akampa Raheli binti yake kuwa mkewe.

29 Labani akampa binti yake Raheli mjakazi wake Bilha, awe mjakazi wake.

30 Akaingia kwa Raheli naye, AKAMPENDA RAHELI KULIKO LEA, akatumika kwa ajili yake miaka saba mingine

31 Bwana akaona ya kwamba Lea hakupendwa, naye akafungua tumbo lake; bali Raheli alikuwa hazai.

32 Lea akapata mimba akazaa mwana, akampa jina lake, Reubeni, maana alisema, Kwa kuwa Bwana ameona teso langu; sasa mume wangu atanipenda.

33 Akapata mimba tena akazaa mwana, akasema, Kwa kuwa Bwana amesikia ya kwamba mimi sikupendwa, amenipa na huyu; akamwita jina lake Simeoni.

34 Akapata mimba tena, akazaa mwana, akasema, Basi wakati huu mume wangu ataungana nami, kwa sababu nimemzalia wana watatu. Kwa hiyo akamwita jina lake Lawi.

35 Akapata mimba tena, akazaa mwana. Akasema, Mara hii nitamsifu Bwana; kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; akaacha kuzaa”.

2. KUKITHAMINISHA KITAKACHOZALIWA BAADAYE.

Hii ni sababu ya pili ya Raheli kufungwa tumbo: Tunasoma ijapokuwa Raheli alifungwa tumbo muda mrefu, lakini ulifika wakati akazaa, na mwana aliyemzaa alikuwa wa tofauti na wale wengine 10 waliotangulia, kwani ndiye aliyekuwa YUSUFU, ambaye alikuja kuwa Mkuu zaidi ya ndugu zake wote, na tena Mkuu juu ya nchi yote ya Misri, baada ya Farao.

Ikifunua kuwa si kila kinachochelewa kina laana!.. Vingi vinavyochelewa ni kwasababu ya Utukufu wake, hivyo usimwone mtu kachelewa kupata mimba ukamdharau!.. Hujui atakayekuja kumzaa ni nani!..
Vile vile usihuzunike unapoona unachelewa kupata mtoto, kwani vizuri na vya thamani, vina gharama, na gharama yenyewe yaweza kuwa fedheha, matusi, kejeli na masimango.. Lakini vinavyokuja baada ya gharama hizo vinakuwa ni vizuri, endapo tu utazidi kusimama katika imani, haijalishi muda, vitatokea tu!.

Wagalatia 4:27 “Kwa maana imeandikwa, Furahi, wewe uliye tasa, usiyezaa; Paza sauti, ulie, wewe usiye na utungu; Maana watoto wake aliyeachwa pekee ni wengi Kuliko wa huyo aliye na mume”.
Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini Raheli aliiba miungu ya Baba yake, (Labani) Mwanzo 31:19.

Kwanini Labani aseme Yakobo ni Mfupa wake na nyama yake?(Mwanzo 29:14)

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

Zeri ya Gileadi ni nini?

Tunguja ni nini katika biblia? (Mwanzo 30:14).

Print this post

“Akaiona imefagiwa na kupambwa” Maana yake nini (Luka 11:26).

Swali: Bwana YESU alisema pepo anapomtoka mtu na baadaye akirudi na kukuta nyumba yake imefagiliwa na kupambwa huenda kuchukua pepo wengine saba,.. maaa yake nini kusafishwa na kupambwa?.. je mapepo wanapenda sehemu safi?


Jibu: Awali ya yote tuisome mistari hiyo.

Luka 11:24 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika; asipoona, husema,

25 Nitairudia nyumba yangu niliyotoka.

26 Hata afikapo, akaiona imefagiwa na kupambwa, ndipo huenda akachukua pepo wengine saba, walio waovu kuliko yeye mwenyewe, wakaingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza”.

Sasa kabla ya kujua nini maana ya “kufagia na kupambwa” hebu tuelewe kwanza maana ya nyumba kiroho..

Maandiko yanasema Miili yetu ni Hekalu la Roho Mtakatifu..

1 Wakorintho 6.19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;

20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.

Soma pia 1Wakorintho 3:16 utaona jambo hilo hilo..

Sasa kama miili yetu imekusudiwa iwe Hekalu/nyumba ya Roho Mtakatifu, maana yake ni kwamba isipokaliwa na Roho Mtakatifu basi itakaliwa na roho chafu za mapepo, maana yake badala ya mwili kuwa Nyumba ya Roho Mtakatifu, sasa inakuwa ni nyumba ya mapepo.

Hivyo mpaka hapo tumeshaelewa kuwa Nyumba inayozungumziwa hapo katika Luka 11:25-26, si nyingine zaidi ya miili yetu.

Sasa swali la pili: Nini maana ya kupambwa na kufagiliwa.

Hebu tena tutumie maandiko tujue mapambo ya nyumba ya Mungu (yaani miili yetu) ni yapi, na mapambo ya mapepo ni yapi.

1Petro 3:3 “Kujipamba kwenu, KUSIWE KUJIPAMBA KWA NJE, YAANI KUSUKA NYWELE; NA KUJITIA DHAHABU NA KUVALIA MAVAZI;

4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.

5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao”.

Angalia mstari wa tatu (3) anasema.. Kujipamba kwenu KUSIWE!, Zingatia hilo neno KUSIWE!!.. Maana yake ni kwamba mapambo yake ni kwamba mapambo yafuatayo si ya ki Mungu bali ni ya Ibilisi, ndio maana anasema hapo KUSIWE!.. Sasa hebu tuendelee tuangalie hayo mapambo..

…”Kujipamba kwenu, KUSIWE KUJIPAMBA KWA NJE, YAANI KUSUKA NYWELE; NA KUJITIA DHAHABU NA KUVALIA MAVAZI..”

Oo kumbe! kuweka wigi, kuvalia mavazi (ya kikahaba), na kuvaa dhahabu masikioni na shingoni na vikuku miguuni na mikononi ni mapambo ya mapepo, na tena tumeshaona kuwa “nyumba” tafsiri yake kiroho ni “miili yetu”, hivyo tunapoweka hereni masikioni, wigi kichwani, cheni shingoni na vikuku miguuni, tafsiri yake ni kwamba nyumba zetu (yaani miili yetu) tumeipambwa kwa mapambo ya kipepo, ambayo yale mapepo yakiona yanafurahi na kwenda kutafuta pepo wengine saba, na kurudi kumwingia mtu.. Hii ni ajabu sana!.

Na ndio maana wengi (wanaume na wanawake) wanaopamba miili yao na kuvaa kikahaba wanakuwa wanasumbuliwa na mapepo na ndoto mbaya!, kwanini?..kwasababu miili yao ni nyumba iliyofagiliwa na kupambwa..

Sasa utauliza kufagiliwa ni kufanya nini?…Kufagiliwa ni maandalizi ya mapambo!..Maandalizi yote ya kiroho na kimwili kabla ya mtu kujitia mapambo ya nje ni “kufagia”..

Lakini hebu tuangalie mapambo ya ki MUNGU ni yapi!.. Tuendelee na mistari ile..

“Kujipamba kwenu, KUSIWE KUJIPAMBA KWA NJE, YAANI KUSUKA NYWELE; NA KUJITIA DHAHABU NA KUVALIA MAVAZI;

4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu”.

Bali anasema mapambo yetu yawe Utu wa moyoni, yaani Roho ya Upole, na utulivu (kwa ufupi utakatifu).
Je! mama, dada, au kaka ni mapambo gani unayo?..ya nje au ya ndani??.. ni kweli utaonekana wa kisasa, unayekwenda na wakati, lakini fahamu kuwa mapambo hayo ndio mapepo wanayoyaangalia.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10 atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Print this post

VUNJA MADHABAHU, ANGUSHA NGUZO, KATA ASHERA NA CHOMA SANAMU.

Haya ni mambo manne yanayopalilia matatizo kuanzia ngazi ya kifamilia mpaka ya kitaifa!. (Madhabahu, Nguzo, Ashera na Sanamu).


Kumbukumbu 7:5-6 “Lakini watendeni hivi; zivunjeni madhabahu zao zibomosheni nguzo zao, yakateni maashera yao, ziteketezeni kwa moto sanamu zao za kuchonga.

6 Kwa maana wewe u taifa takatifu kwa BWANA, Mungu wako; BWANA Mungu wako, amekuchagua kuwa watu wake hasa, zaidi ya mataifa yote walioko juu ya uso wa nchi”

Labda utauliza mambo haya ni mambo gani kwa undani wake na yanaathiri vipi maisha.

   1. Madhabahu:

Madhabahu ni mahali popote panapotolewa dhabihu (sadaka).

Sadaka ina nguvu, ndio maana hakuna mganga anayetoa huduma bila sadaka,

Sasa si kwamba sadaka anahitaji tu  kwaajili ya mahitaji yake..La! bali anajua uchawi wake hautafanya kazi ipasavyo pasipo sadaka, kwahiyo madhabahu ni mahali mahususi kwa sadaka..

Katika biblia BWANA MUNGU aliwaagiza wana wa Israeli wazivunje madhabahu za wakaanani..

Na zilikuwa ni nyingi na za aina tofauti tofauti…na pasipo kuchagua waliambiwa wazivunje zotewasibakishe hata moja, kwani zitakuwa ni chanzo cha matatizo..

Ikimaanisha kuwa madhabu za mashetani ni za kuvunja si za kuziacha, kwani zinapeleka harufu mbaya mbele za MUNGU, na hivyo kuleta matatizo mengi…

Ikiwa kuna mahali ipo madhabahu wanapotolea sadaka karibu nawe, na hiyo madhabahu inakuhusu kwa namna moja au nyingine (kimila), ivunje bila kuogopa!..kama alivyofanya Gideoni, usiiache kwani yaweza kukuletea matatizo.

     2. NGUZO

Nguzo ni miimo ya Mahekalu ya ibada, yaweza kuwa Hekalu la MUNGU (soma 1Wafalme 7:21 na Mwanzo 28:22),  au yaweza kuwa hekalu la mashetani (Soma 2Wafalme 10:26-27).

Maana yake mahali popote penye msingi wa hekalu la miungu ni lazima pabomoshwe.

   3. ASHERA.

Ashera ni miti na maua yaliyokuwa yanazunguka mahekalu ya miungu, ambapo mimea hiyo iliaminika na kuabudiwa kama sehemu ya miungu.

Bwana aliwaambia wana wa Israeli wakate-kate maashera yote lisibaki hata moja (Kutoka 32:12-14).

Hali kadhalika yapo maashera hata sasa, utakuta upo mti fulani unaaminika kama ni wa kiungu na watu wanaenda kufanya matambiko hapo (hiyo ni ashera), ni ya kukata, wengine si miti bali maua tu…

Ondoa maashera katika nyumba yako, ondoa katika nyua yako na uzio wako kwani yaweza kuwa chanzo cha matatizo mengi.

   4. SANAMU.

Sanamu ni kitu chenye umbile la mtu kinachowekwa katika mahekalu na kuabudiwa.

Hizi nazo Bwana aliagiza zichomwe moto,

Sasa swali linakuja, vipi kama Madhabahu hizi, na ashera, na nguzo na sanamu zipo mbali?.

Kama zipo mbali na upeo wa kuzifikia, tunazo silaha zinazosafiri masafa marefu zaidi ya silaha zote zilizowahi kutengenezwa na mwanadamu au zitakazokuja kutengenezwa.

Silaha hiyo ni Maombi.

Maana yake katika maombi Unazivunja madhabahu kwa Imani, unaangusha Nguzo kwa imani, unakata maashera kwa imani, na unazichoma moto hizo sanamu kwa imani kupitia jina la YESU.

Na kwa jinsi utakavyotamka, zitateketea kule zilipo kwa namna hiyo hiyo, lakini usiingie kwenye maombi ya vita kama wewe si askari mwenye silaha hizi za Waefeso 6:10-15.(utajitafutia matatizo zaidi).

Pia usiache kuzibomoa kwa mikono yako kama zipo mbele ya upeo wa macho yako. (Upo unaziona sio tu kuombea, bali kuzimoa kwa mikono kabisa).

Ukifanya hivyo utakuwa umeusafisha uwanda, hakuna laana juu ya mahali ulipo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI.

Sehemu ya kwanza.

Zaburi 66:20 “Na ahimidiwe Mungu asiyeyakataa maombi yangu, Wala kuniondolea fadhili zake”.

Maombi ni zaidi ya silaha yoyote ile yenye ubora inayofahamika, leo nataka tujifunze kupitia mfano mdogo sana wa simu ya mkononi.

Kawaida ili uweze kuongeza uwezo wa simu yako, huna budi kujiunganisha na internet..

Vichochezi

Internet ni mtandao usiookana kwa macho, unaoratibu mawasiliano ya haraka na taarifa za haraka.

Sasa simu yako inapoungwa na internet ndipo unapoweza kupakua (kudownload) vichocheo vya simu vinavyoitwa application.

Applications zile zinasaidia kuongeza uwezo wa simu yako..

Kama unataka simu yako iweze kusoma baadhi ya makala unahitaji kichocheo husika cha kusomea makala hizo.

Vile vile kama unahitaji simu yako iwe na uwezo wa kucheza nyimbo kwa mpangilio, itakugharimu kupakua (download) vichocheo hivyo n.k

Simu zenye vichocheo (applications) nyingi mbalimbali ndizo zenye uwezo mkubwa..na zile zisizo na vichocheo kabisa huwa zina uwezo mdogo na changamoto nyingi.

Sasa na mwili wa Mtu ni hivyo hivyo, kuna mambo hatuwezi kufanya wala kuwa nayo pasipo hivi vichocheo vinavyoongeza uwezo.

Kwamfano huwezi kusoma biblia na kuielewa kama hujaongezewa nguvu.. Utakuwa ukishika tu unalala!.

Huwezi kuhubiri kama hujaongezewa nguvu, utakuwa unaona aibu tu!.

Huwezi kuishi maisha masafi kama hujaongezewa nguvu utajaribu lakini utashindwa…n.k.

Sasa kazi ya Roho Mtakatifu ni kutuunganisha sisi na mtandao wa kimbinguni, kama vile simu inavyoungwa na internet.

Na tunapoungwa na mtandao wa kimbinguni basi tunaweza kupakua (download) vichocheo vya kimbinguni..

Na tunavipakua vichocheo hivyo kwa njia moja tu ya MAOMBI!.

Unapoomba maana yake unapakua (download) visaidizi vya kimbunguni, ambavyo vinakuongezea nguvu katika utu wa ndani.

KUMBUKA: Maombi hayakupi kitu! Balia YANAKUONGEZEA NGUVU YA KUFANYA NA KUPATA KITU.

Ndio maana baada ya maombi utaona ile nguvu ya kusoma Neno inaongezeka, ile nguvu ya kuhubiri inaongezeka, ile nguvu ya kushinda dhambi inaongezeka, ile nguvu ya kuendelea na wokovu inaongezeka..

Utaona ile nguvu ya kuendeleza maono yako inaongezeka,..ukiona hivyo jua ni vichochezi vya kimbinguni vimeingia ndani yako vinafanya kazi..HIYO NDIO NGUVU YA MAOMBI!!.

Na kawaida hata vichochezi vya simu (application) vinakuwa updated mara kwa mara, vivyo hivyo na mwombaji huwa haombi mara moja na kuacha, bali anakuwa na desturi ya kuomba mara kwa mara ili kuimarisha vichochezi vyake.

Lakini usipokuwa mwombaji, utabaki, hutaona mabadiliko yoyote katika eneo lolota la kiroho na kimwili…kila kitu kitakuwa kigumu hakiendi..

Na kama ulikuwa mwombaji na ukapunguza kuomba, na vile vichocheo pia vinapungua nguvu.

Anza kuwa mwombaji, kuna mambo hayawezekaniki pasipo maombi hususani yale ya mfungo.

Mathayo 17:21 “Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

NI KWA NAMNA GANI KRISTO ALIZIBEBA DHAMBI ZETU?

Ili kuelewa Msamaha wa dhambi jinsi unavyofanya kazi, kwamba ni kwa namna gani Bwana YESU alibeba dhambi zetu, twaweza kuelewa kwa kutafakari mfano huu mrahisi.

Katika sheria za Mahakama inapotokea mfungwa aliyehukumiwa  kifungo, akafariki katikati ya kifungo hiko, na ikathibitishwa na jeshi la magereza pamoja na ripoti za madaktari, na akazikwa basi kile kifungo chake kinakuwa kimefika mwisho, na kesi yake inakuwa haiendelei tena (inafutwa)..

Sasa ikitokea yule mtu akafufuka baada ya siku kadhaa anakuwa hana kesi tena (yupo huru) kwani  kesi yake ilishafutwa, kutokana na ripoti za mahakama na madaktari..

Na zaidi sana mahakama haziamini ufufuo, hivyo itaendelea kuamini kuwa yule mtu alishakufa na taarifa zilithibtishwa na jeshi la magereza pamoja na madaktari.

Sasa ni hivyo hivyo kwa Bwana YESU, yeye alikubali kubeba hatia zetu na makosa yetu yaliyo mengi na akakubali kuhukumiwa kama yeye ndiye aliyeyatenda yale makosa..

Lakini alipokuwa anaanza kukitumikia kile kifungo kwa mateso makali (ambayo kiuhalisia yamgekuwa ya daima)..alikufa katikati..

Na sheria ya hukumu ni kwamba kifo kinahitimisha kifungo cha Mtu, hivyo Kristo alipokufa kifungo chake cha adhabu na mateso kikafikia mwisho, akawa hana hatia tena wala ule mzigo wa dhambi (yupo huru na dhambi sawasawa na maandiko).

Warumi 6:7 “kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi”

Lakini muujiza ni kwamba baada ya siku tatu akaonekana yu hai, na kwasababu hukumu yake ilishafutwa kwa kifo chake, akawa huru na kifungo hiko baada ya kufufuka, ndio maana hatuoni akilia kwa uchungu wa maumivu baadaa kufufuka, bali tunaona ana utukufu mwingi.

Kwahiyo laiti Kristo asingekufa angeendelea kuhesabika laana na mwenye hatia kwaajili ya dhambi zetu nyingi alizozobeba, ingempasa aendelee kukaa katika hali ya adhabu daima, na aendelee kutengwa na MUNGU daima.

Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti”

Lakini kifo chake kimehitimisha hukumu yake, ambayo sisi ndio tungepaswa tuitumikie.

Sasa tunapomwamini ndipo tunaingia katika huo mkondo wa kuondolewa dhambi..

Lakini tunapomkataa basi dhambi zetu zinabaki palepale..ni rahisi tu hivyo!.

Je umemwamini Bwana YESU?..Je umebatizwa kwa ubatizo sahihi wa Maji mengi na wa Roho Mtakatifu?.

Kama bado unasubiri nini?…je bado huoni tu gharama kubwa Bwana YESU aliyoingia kwaajili yetu ili tupate ondoleo la dhambi?.

Mpokee YESU leo wala usingoje kesho.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Fahamu Maana ya Mithali 15:24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;

SWALI: Nini Maana ya Mithali 15:24?

Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.

JIBU: Hapo yapo mambo matatu,

  1. Mtu mwenye akili.
  2. Njia ya uhai,
  3. Na uelekeo wa njia hiyo.

Mtu mwenye akili ni mtu mwenye uwezo wa kufikiri/kupambanua vema na kufanya maamuzi sahihi katika maeneo mbalimbali ya maisha yake. Hivyo hapo anasema mtu mwenye akili anajua vema kuichagua njia yake ya uhai.

Anasema njia yake hutoka chini kuelekea juu. Kwa lugha ya picha ni barabara iliyopinduliwa na kusimamishwa wima kama ngazi,  na sio mfano wa barabara hizi tulizonazo zilizolala chini, ambazo uelekeo wake ni aidha kaskazini na kusini, au mashariki na magharibi.

Sasa hapa anasema njia yake ya uhai huenda juu, ili atoke kuzimu chini. Akiwa na maana husafiri kutoka kuzimuni kuelekea uzimani juu kwa Mungu.

Hufunua nini?

Safari ya mtu mwenye akili, hufikiri kumtafuta Mungu juu alipo,

Wakolosai 3:1 Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. 2 Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.

Hufikiri ukuaji wa kiroho, atokea hatua moja ya utakatifu kwenda nyingi, kiwango kimoja cha Imani kuelekea kingine kama Kristo (2Petro 1:5-10, Waefeso 4:13). Ni mtu ambaye kila siku anakwenda mbali na njia ya mauti. Mawazo yake yapo juu sikuzote kumjua Kristo na mapenzi yake yote.

Lakini kinyume chake ni ukweli, mtu asiye na akili barabara yake haijasimama wima, bali imelala. Atawaza atoke hatua moja kwenda nyingine lakini hakuna ukuaji wowote au kuongezeka kokote. Huwenda anachowaza tu sikuzote ni kutoka katika umaskini kwenda katika utajiri, kutoka katika kiwango kimoja cha elimu kwenda kingine, kutoka katika cheo kimoja kwenda katika kingine..Hatua zake ni za kidunia tu, akidhani ndio uzima wake upo hapo. Kumbe kapotea njia.

Si kwamba vinapingwa vya dunia hapana, ni vizuri na vinafaa, lakini havina uzima wa milele ndani yake. Ili uwe na akili hakikisha unampokea Kristo, kisha unaanza kukua kiroho, kila siku unafikiri njia ya kuyakimbia machafu ya kidunia. Hapo barabara yako itakuwa umesimama kama ngazi na hivyo utaiponya nafsi yako.

Je! Umeokoka?. Kama ni la! Basi wakati ndio sasa fungua moyo wako mkaribishe Yesu akuokoe hizi ni nyakati za hatari, tubu leo upokee wokovu. Ikiwa upo tayari kumkaribisha Kristo moyoni mwako, basi waweza kubofya hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba. Bwana akubariki. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha. 

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Biblia inasema nini kuhusu mtu ‘Mwenye kujipendekeza (Mithali 29:5)

Print this post

Kuonja ni kufanya nini? (Kutoka 15:25).

Swali: Kuonja kunakozungumziwa katika kitabu cha Kutoka 15:25 kunamaanisha nini?.

Jibu: Turejee mistari hiyo..

Kutoka 15:24 “Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema,Tunywe nini? 

25 Naye akamlilia BWANA; BWANA akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, AKAWAONJA HUKO

Kuonja kunakozungumziwa hapo ni kuonja kiroho na si kimwili, siku zote mtu anayeonja kitu, lengo lake ni kukipima ubora wake, kilingana na vigezo anavyovitaka.

Na kiroho MUNGU anatuonja sisi mara kwa mara kwa kuangalia matendo yetu kama tupo sawa mbele zake…

Kwamfano utaona Bwana YESU anatumia lugha hiyo ya kiroho katika kitabu cha Ufunuo kuyapima matendo yetu..

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu”

Umeona hapa?…matendo yetu yanapimwa kwa kinywa cha Bwana..kama tu Moto mbele zake basi tuna heri, lakini kama tu baridi au vuguvugu ni Ole!.

Kwahiyo hata kipindi wana wa Israeli wakiwa wanatoka Misri kuelekea nchi ya ahadi.. Mungu alikuwa anawaonja matendo yao…

Na kuna kipindi aliwatapika walipomjaribu na kumnun’unikia.

Lakini si tu Bwana akiyekuwa anawaonja, bali pia aliwaambia kuwa hiyo nchi wanayoiendea itawaonja matendo yao, na kama yakiwa mabaya itawatapika, kwa kuwa pia iliwatapika wenyeji waliokuwa wanaiishi kutokana na mateendo yao maovu.

Walawi 18:25 “na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi YATAPIKA wenyeji wake na kuwatoa. 

26 Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu; 

27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;) 

28 ili kwamba hiyo nchi ISIWATAPIKE NA NINYI PIA, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu”.

Je umempokea YESU?.

Je wewe ni moto?, au baridi au una uvuguvugu?…Uvuguvugu maana yake ni kuwa upo mguu mmoja nje!…mguu mmoja ndani!, leo unaenda kanisani kesho unaenda Bar, leo unatoa sadaka kesho unabeti, leo unavaa nguo ya sitara kesho nguo ya aibu..hapo Bwana amesema atatapika mtu wa namna hiyo.

Bwana atusaidie tumtii ili tusiwe miongoni mwa watakaotapikwa.

Maran atha!.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post