Title 2025

USIGEUZE JIWE KUWA MKATE.

Je unaujua uhusiano wa JIWE na MKATE kibiblia?.. Hebu leo tujifunze…

Mathayo 7:8 “ kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.

9 Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, MWANAWE AKIMWOMBA MKATE, ATAMPA JIWE?”

Ni hakika, hakuna mzazi yoyote mwenye akili timamu, ambaye mtoto wake akimwomba MKATE atampa JIWE. Hayupo mzazi wa namna hiyo, wala wanyama hawawezi kufanya mambo ya mfano huo wa watoto wao.

Lakini tunaona wakati fulani shetani alijaribu kumchonganisha Bwana YESU na Baba yake wa mbinguni kwa kumwambia, AGEUZE JIWE LIWE MKATE, kana kwamba Baba wa mbinguni alikuwa amemwekea yale mawe kule jangwani kuwa chakula chake (uvunjifu mkubwa wa heshima)!

Luka 4:2 “akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.

3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, LIAMBIE JIWE HILI LIWE MKATE”.

Hili lilikuwa ni jaribu kubwa la shetani kwa Bwana YESU kutaka kumwingizia roho ya kumwona Baba wa mbinguni kama ni mkatili, ambaye anampa mwanae mawe badala ya mkate kupindi cha njaa, na hivyo adui sasa anamfundisha ayageuze yale mawe kuwa mkate.

Na adui alijua kuwa endapo KRISTO angefanya vile (kwaasababu huo uwezo wa kugeuza jiwe kuwa mkate alikuwa nao) angempokonya uhusiano wake mwema aliokuwa nao na Baba yake, na tangu ule wakati angejua Baba anatoa mawe kwa watoto wake badala ya mkate.

Lakini Kristo kwasababu alikuwa amejaa Roho Mtakatifu aliyajua mafumbo yote ya shetani, hivyo hakudanganyika,  na ndio maana hapo baadae katika Mathayo 7:9 akawaambia wanafunzi wake kuwa Baba mwema hawezi kumpa mtoto wake JIWE badala ya MKATE, sasa kwanini alisema vile?..kwasababu alishakutana na jaribu la namna hiyo hiyo jangwani.

Hali kadhalika unapopitia hali Fulani ya majaribu, usianze kutanga tanga na kuruhusu hofu, na kuona kama kila kitu kilichoko mbele yako hata kisicho na uhai ni fursa kutoka kwa MUNGU, sio kila kitu ni fursa kwako wakati wa majaribu!…vingi ni mitego ya ibilisi kwasababu anajua upo katika hali ya uhitaji wa hali ya juuu….hiyo ndiyo kawaida ya shetani.. alitaka pia kumwaminisha Bwana YESU kuwa yale mawe ni fursa ya kuondoa njaa yake.

Si kila kazi inayokuja mbele yako wakati wa vipindi vigumu ni fursa kutoka kwa MUNGU, kazi nyingine ni za Ibilisi (ni mawe). Mungu hawezi kukupa hayo kama riziki, ziache zipite!.. kazi za Bar ni mawe!, kazi ya Saloni za kiduni ni mawe!, kazi inayohusisha rushwa ni jiwe!, kazi inayohusisha kuuza utu wako ni jiwe!, kazi inayohusisha kuabudu miungu mingine ni jiwe!.. usizigeuze MAWE hayo kuwa MKATE!, hata kama una njaa ya kukaribia kufa!..ziache zipite, si majibu kutoka kwa MUNGU, bali ni majaribu kutoka kwa shetani, kwani huwezi kumwomba Baba wa mbinguni MKATE akakupa JIWE.

Huwezi kumwomba akupe kazi nzuri halafu akakuletea kazi ya kujiuza mwili wako!.. huyo sio MUNGU, bali ni ibilisi…Njaa yako, udhaifu wako, changamoto zako ambazo ni za muda tu!, zisikufanye ukaharibu mahusiano yako na MUNGU moja kwa moja.

Je tayari umeshampokea YESU?.. Kama bado fahamu kuwa tunaishi siku za mwisho, na YESU amekaribia kurudi, na dunia inaenda kuisha, ni heri leo ukayasalimisha maisha yako kwake, ili usamehewe dhambi zako na jina lako liandikwe kwenye kitabu cha Uzima cha Mwanakondoo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Je ni kweli Bwana YESU hajui siku ya kuja kwake? (Mathayo 24:36)

IFAHAMU NGUVU YA MAOMBI.

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.

MANENO SABA YA YESU MSALABANI.

Print this post

KUFUTWA KWA ACCOUNT

Ikiwa utahitaji Account yako nzima ifutwe moja kwa moja kwasababu zozote zile, pamoja na maudhui yake yote, basi wasiliana basi tutumie maombi hayo kupitia email yetu hii watakatifuwasikuzamwisho@gmail.com au namba zetu tajwa hapo chini na tutafanya hivyo mara moja.

+255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Print this post

Sera za Faragha (Privacy policy)

Ifuatayao ni Sera ya Faragha ya Tovuti/App ya Nuru ya Upendo (wingulamashahidi.org)

Tarehe ya Mwisho wa Marekebisho: [21/05/2025]

Tunapenda kukushukuru kwa kuchagua kutumia kituo cha Wingulamashahidi, jukwaa la injili ya YESU KRISTO, mafundisho ya Biblia, maombi, na jumbe za wokovu kupitia tovuti yetu na app yetu rasmi. Tunathamini faragha yako na tunajitahidi kuhakikisha taarifa zako zinalindwa kikamilifu.


1. Taarifa Tunazokusanya

Lengo la kukusanya taarifa zako ni kukuletea huduma ya kiroho iliyo bora zaidi. Na taarifa tuzikusanyazo ni:

  • Taarifa  Binafsi (kama utazijaza): ambazo ni Jina lako, barua pepe, namba yako ya simu.

  • Taarifa za Kiufundi: Aina ya kifaa unachotumia, anwani ya IP, aina ya kivinjari, lugha, na mfumo wa uendeshaji.

  • Taarifa za Matumizi: Maudhui unayoyasoma, au kupakua, au kushiriki. Hii inatusaidia kujua aina gani ya masomo yanayopendelewa zaidi na watu.


2. Jinsi Tunavyozitumia Taarifa hizo

Taarifa hizi zinahitajika kwa:

  • Kukurushia masomo mapya kwenye barua pepe yako.

  • Kuboresha muundo na mwonekano wa tovuti pamoja na app

  • Kujibu maswali yako, maombi ya maombi, au mawasiliano mengine ya kiroho..


3. Ulinzi na usalama wa Taarifa Zako

Hatua za kiusalama tunazizingatia  (kama SSL, uthibitisho wa watumiaji, na encryption) kuhakikisha taarifa zako hazidukuliwi na yoyote, wala kupotea, wala kutumiwa bila idhini ya mhusika. Pia tunazingatia kanuni za kimaadili kulingana na ukristo.


4. Ushirikishaji wa Taarifa

Hatutashiriki wala kuziuza, kusambaza, au kugawa taarifa zako binafsi kwa mtu mwingine yoyote bila idhini yako isipokuwa:

  • Kwa mujibu wa sheria au maelekezo ya mamlaka husika.

  • Kwa watoa huduma wanaotusaidia kutoa huduma hizi (mfano: huduma ya kutuma barua pepe), kwa masharti ya usiri.

  • Ikiwa kama utachagua kushiriki jumbe kwenye mitandao ya kijamii.


5. Watoto

Hatukusanyi taarifa za watoto walio chini ya miaka 12 bila idhini ya wazazi au walezi. Ikiwa mzazi ataona kuwa kuwa mtoto wake ametoa taarifa binafsi bila idhini yao, basi tunaomba awasiliane nasi ili tuchukue hatua za kuondoa taarifa hizo mara moja.


6. Haki Zako

Unayo haki ya:

  • Kufahamu ni taarifa gani tulizonazo kuhusu wewe.

  • Kuomba taarifa zako zifutwe au kurekebishwa inapohitajika.

  • Kujiondoa kwenye orodha ya wanaopokea pokea mafundisho kwa njia ya barua pepe au yoyote ile.

  • Kuhoji matumizi ya taarifa zako kwa ajili ya tafiti, chunguzi au matangazo (kama yatakuwepo).


7. Vidakuzi (Cookies)

Tovuti yetu hutumia cookies ili kuboresha matumizi yako. Unaweza kuchagua kuzima kama haitakuwa ni mapendekezo yako, lakini hii yaweza kuathiri usomaji wako wa tovuti.


8. Mabadiliko ya Sera ya Faragha

Patakapotokea mabadiliko ya Sera hizi, tutakujuza mabadiliko hayo kupitia tovuti z. Mabadiliko huanza kutumika mara moja baada ya kuchapishwa.


9. Mawasiliano

Kwa maswali kuhusiana na sera hizi za faragha, tafadhali wasiliana nasi kupitia:

Barua pepe: wingulamashahidi@gmail.com
Tovuti: https://wingulamashahidi.org


Mungu akubariki sana kwa kuwa sehemu ya huduma hii. Tunakuombea baraka za Bwana YESU ziende nawe

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Shalom

Print this post

What Does “Give Strong Drink to Him Who Is Perishing” Mean?

The Question:

Proverbs 31:6–7 says:
“Give strong drink to him who is perishing, and wine to those who are bitter of heart.
Let him drink and forget his poverty, and remember his misery no more.”

Does this verse mean it’s okay for believers to drink alcohol when facing sorrow, pain, or hardship?


Understanding the Context – The Old Covenant and Physical Solutions:
To interpret this properly, we must consider the dispensational context. Proverbs was written under the Old Covenant, a time when God’s dealings with humanity were largely external and physical (Hebrews 8:6–13). Under that covenant, people often turned to physical remedies for emotional and moral issues—including the use of strong drink to dull grief and suffering.

It’s similar to how they were permitted to divorce or marry multiple wives—not because it was God’s ideal, but because of the hardness of their hearts.

Jesus clarifies this:

Matthew 19:7–8 
They said to Him, “Why then did Moses command to give a certificate of divorce, and to put her away?”
He said to them, “Moses, because of the hardness of your hearts, permitted you to divorce your wives, but from the beginning it was not so.”

God tolerated certain human practices in the Old Testament, but they never reflected His original design. The temporary provision to allow strong drink for those in sorrow was just that—a temporary allowance, not a divine endorsement of alcohol as a lasting solution.

Limitations of Alcohol as Comfort:

The thinking behind Proverbs 31:6–7 was that someone overwhelmed by grief might use alcohol to forget their pain, especially during severe distress like death or deep poverty. Even Job’s story (Job 1–2) shows the depth of grief humans face. But the relief from alcohol is fleeting. Once the drink wears off, the pain returns. Alcohol doesn’t heal, it numbs—and only for a short time.

This highlights an important theological truth: Fleshly solutions cannot resolve spiritual or emotional problems.


God’s Better Solution in the New Covenant – The Holy Spirit:
With the coming of Christ, God introduced a new and better covenant (Hebrews 8:6), bringing lasting spiritual transformation through the Holy Spirit. Jesus offers not a temporary escape from sorrow, but living water that satisfies the deepest longings of the soul.

John 7:37–39
“If anyone thirsts, let him come to Me and drink.
He who believes in Me, as the Scripture has said, out of his heart will flow rivers of living water.”

But this He spoke concerning the Spirit, whom those believing in Him would receive; for the Holy Spirit was not yet given, because Jesus was not yet glorified.

The Holy Spirit brings what alcohol cannot: true comfort, lasting peace, freedom from sin, and inner joy.


The Day of Pentecost – The Spirit Misunderstood as Wine:
When the Holy Spirit was poured out at Pentecost, the joy and boldness experienced by the disciples caused some onlookers to think they were drunk. But Peter corrected them:

Acts 2:15–17
“For these are not drunk, as you suppose, since it is only the third hour of the day.
But this is what was spoken by the prophet Joel:
‘And it shall come to pass in the last days, says God,
That I will pour out of My Spirit on all flesh…’”

This wasn’t the intoxication of wine—it was the overflow of the Spirit.


A Clear Command Against Drunkenness:
In the New Testament, believers are commanded not to seek emotional escape or joy through alcohol, but to be filled with the Holy Spirit:

Ephesians 5:18
“And do not be drunk with wine, in which is dissipation; but be filled with the Spirit.”

Paul draws a clear contrast: drunkenness leads to spiritual and moral collapse, but being filled with the Spirit brings life, order, and purpose.

Proverbs 31:6–7 is not a command or justification for alcohol use in times of sorrow. It’s a reflection of an older, less complete way of dealing with pain, rooted in the Old Covenant. Under the New Covenant, we are offered something far better: the Holy Spirit, who brings real healing and lasting joy.

Just as polygamy and divorce were permitted but not ideal, alcohol may have been tolerated—but it is not the believer’s source of comfort today. That role now belongs to the Holy Spirit, the Comforter (John 14:26).

Let us, therefore, understand the times we live in and walk according to God’s perfect will.

“The Spirit helps us in our weakness…”
Romans 8:26 

God bless you.

Print this post

Tafsiri ya Mithali 3:27 inayosema ‘Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao’

SWALI: Nini maana ya Mithali 3:27 ?

[27]Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda.


JIBU: Kuna mambo mawili yaliyogusiwa katika hicho kifungu..

  1. Usiwanyime watu mema yaliyo Haki yao.
  2. Lakini pia, ‘ikiwa katika uwezo wa mkono wako’.

1] Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao.

Hili ni agizo la Bwana kuwasaidia wengine. Lakini pia Bwana anataka tujue ni akina nani wenye haki hiyo ya kusaidiwa.

Kibiblia Makundi ambayo ni haki yao kusaidiwa.(wawapo na shida), ni matatu (3)

 i) Familia (yaani ndugu wa mwilini)

1 Timotheo 5:8

[8]Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

Wazazi wako, wadogo zako, watoto wako. Ni haki yao kuwasaidia, kwasababu ni damu moja na wewe. Usipotimiza wajibu huo unahesabika sawa na mtu aliyeikana imani. Hakikisha jicho lako haliwapiti ndugu zako, ni sehemu ya wajibu.

ii) Ndugu wa rohoni:

Wagalatia 6:10

[10]Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.

Kanisa la kwanza lilitambua jukumu hili la kusaidiana, vivyo hivyo na sisi ikiwa mpendwa mwenzako yupo katika hali na uhitaji mkubwa hupaswi kufumba macho, bali msaidie, watumishi wa Mungu wanaojibidiisha kuhubiri kweli ya Mungu wanastahili kusaidiwa mahitaji yao. (Warumi Romans 12:13, Hebrews 13:16).

1Yohana 3:17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.

Hapa inalenga pia na wajane pia walio ndani ya kanisa wale walio wajane kwelikweli. (1Timotheo 5:3–5, 9–10)

iii) Maskini.

Wapo maskini wengi ulimwenguni, ambao wanashindwa kufikiwa na mahitaji yao ya msingi, wengine wanakuwa mabarabarani walemavu, wagonjwa, majirani maskini, wote hawa pia wanastahili kusaidiwa.

Wagalatia 2:10 ila neno moja tu walitutakia, tuwakumbuke maskini; nami neno lilo hilo nalikuwa na bidii kulifanya.

Hayo ndio makundi yenye haki ya kusaidiwa. Lakini wengine wanaweza kusaidiwa lakini sio haki yao,ikiwa na maana hata wasiposaidiwa hakuna shitaka lolote juu yako kwa Mungu.

2]  Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda:

Lakini Ukiendelea kusoma anagusia tena jambo la pili ambalo ni; “Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda”.

Akiwa na maana gani?

Mtume Paulo kwa uweza wa  Roho aliandika maneno haya;

2 Wakorintho 8:12-13

[12]Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri ya asivyo navyo.  [13]Maana sisemi hayo, ili wengine wapate raha nanyi mpate dhiki;

Yaani kwa jinsi moyo wako unavyoguswa, tenda mema,  lakini pia kulingana na uwezo wako uliokirimiwa na Mungu,  ili upande mmoja usiuache na taabu au kupungukiwa kabisa. Kwamfano umepata rizki kipimo cha watoto wako tu, ukaenda kukichukua na kuwapa maskini huku familia yako ikabaki Kulala njaa.. hapo hujafanya busara kwasababu umehamisha Tatizo sehemu moja kupeleka kwingine, hujatatua tatizo.

Tenda mema, bila kusahau pia kipimo chako ulichopimiwa cha mema.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Masomo mengine:

Elewa tafsiri ya Mithali 27:22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni.

Elewa maana ya Mithali 18:23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali. 

Nini maana ya Mithali 24:11 Uwaokoe wanaochukuliwa ili wauawe?

Print this post

Ipi tofauti ya Falme, Mamlaka na Wakuu wa giza (Waefeso 6:12)

Jibu: Turejee..

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya FALME na MAMLAKA, juu ya WAKUU WA GIZA HILI, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”.

Hapa kuna vitu vinne, vilivyogawanyika katika sehemu mbili.. Kundi la kwanza ni “FALME na MAMLAKA” na kundi la pili ni “WAKUU WA GIZA na JESHI LA MAPEPO” jumla mambo manne (4)

Sasa hebu tuanze na kundi la kwanza la FALME na MAMLAKA.

Mwandishi (ambaye ni Paulo, Mtume wa Bwana YESU) alitumia mfumo wa Tawala za dunia, kutoa picha ya tawala za ufalme wa giza.

Katika Dunia tunajua kunakuwa na Falme za wanadamu… Kwamfano kuna Falme za kiafrika, falme za kiarabu, Falme za kiasia n.k,

Sasa kwa vizazi vyetu nyakati hizi mfano wa Falme ni hizi SERIKALI tulizonazo (ambapo kila nchi inayo serikali yake), lakini zamani za kale Falme zilibaki kuitwa falme..Kwamfano kwenye Biblia utaona kulikuwa na Ufalme wa Umedi na Uajemi, Ufalme wa Babeli, Ufalme wa Uyunani, Ufalme wa Rumi n.k.. Hizi zote zilikuwa ni falme na ziliongozwa na Wafalme.. kwahiyo katika ulimwengu kulikuwepo na Falme Nyingi, zenye wafalme wengi, lakini dunia ni moja.

Tusogee mbele zaidi..

Chini ya kila Falme (au serikali) kunakuwa na Mamlaka, kwamfano katika Serikali ya nchi ya Tanzania, kuna Mamlaka mbalimbali, kuna Mamlaka ya mapato (TRA), Mamlaka ya Maji safi na maji taka, Mamlaka ya mawasiliano, Mamlala ya Hali ya hewa, Mamlaka ya Elimu, Mamlaka ya bandari n.k, hivi vyote ni viungo vya Serikali kwaajili ya kuwahudumu walio chini ya Serikali/Ufalme.

Kwahiyo tunaweza kurahisisha kwa kusema mfano huu, “Vyanzo vya maji vyote vilivyopo katika UFALME wa Tanzania vipo chini ya MAMLAKA ya maji ya maji ya nchi hiyo”… au Ukusanyaji wa kodi za wananchi katika Ufalme/serikali ya Tanzania upo chini ya MAMLAKA ya Ukusanyaji mapato (TRA)….Au jukumu la Ulinzi wa raia na mali zao la Ufalme wa Tanzania lipo chini ya Mamlaka ya ulinzi na usalama kupitia chombo chake maalumu kiitwacho Polisi….Umeona huo muunganiko wa Ufalme na Mamlaka?.

Na kawaida kila Mamlaka inayo Wakuu wake na jeshi.. Ndio hapo utasikia “Mkuu wa mamlaka ya mapato” au Mkuu wa mamlaka ya mawasiliano,  na jeshi zima la mamlaka hiyo ni wafanya kazi wote waliopo chini ya mamlaka hiyo..

Na katika ULIMWENGU wa giza ni hivyo hivyo, kuna FALME na pia kuna MAMLAKA mbalimbali… Zipo mamlaka za uuaji na utekaji (mfano wa hizo ni zile zilizoruhusiwa kumkamata Bwana YESU (Soma Luka 22:53),

zipo mamlaka za uharibifu wa ndoa, zipo mamlaka za uharibifu wa huduma, zipo mamlaka za uharibifu wa familia, kazi n.k n.k,

Na kila mamlaka ya giza inayo Mkuu wake/Kiongozi ambaye ni Pepo (hao Ndio wanaoitwa wakuu wa giza)..  Hapa ndipo tunapofika katika kundi la Pili la WAKUU WA GIZA na MAJESHI YA MAPEPO.

Sasa kama kuna kiongozi au mkuu, ni wazi kuwa kuna Jeshi chini yake, (hakuna kiongozi/mkuu asiye  na jeshi la watu chini yake la kuliongoza)

hivyo mapepo yote yaliyosalia yanayofanya kazi chini ya Wakuu wa giza ndio wanatengeneza kundi la majeshi ya mapepo wabaya.

Kwahiyo Biblia inaposema kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama bali juu ya FALME NA MAMLAKA NA WAKUU WA GIZA NA MAJESHI YA PEPO WABAYA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, imemaanisha kuwa tunapambana na wakuu wa giza (Wakuu wa mapepo) na majeshi yao ambayo yanatumia Mamlaka na Ufalme wa giza kupambana nasi.

Kwahiyo ufalme wa giza, imesimama katika ngazi zake, kuonyesha kuwa vita vyetu si virahisi kama tunavyovichukulia, kupambana na falme si kazi ndogo! Inahitaji msuli wa kutosha wa kiroho, maana yake ni lazima mtu uwe umesimama kwelikweli, umezama kweli kweli kwenye ufalme wenye nguvu kuliko huo wa giza.

Na hakuna ufalme mwingine wenye nguvu kuuzidi ufalme wa giza, zaidi ya UFALME WA MBINGUNI, ambao Mkuu wa Ufalme huo ni YESU KRISTO (Mwamba Mgumu). Huyo ndiye mwenye nguvu za kuuvunja nguvu zote za falme za giza, na hana namba mbili yake!..

Je unaye YESU moyoni na maishani?.. Kama hujaokoka fahamu kuwa upo chini ya ufalme wa giza na mamlaka za giza hata kama ni tajiri, au una afya au una mafanikio mengine yote, bado upo chini ya utawala wa giza, wanaweza kukufanya chochote kwa wakati wowote, na wanaweza kukutumia vyovyote watakavyo, Mgeukie YESU leo na uhame kutoka katika huo ufalme wa giza.

Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;

14 ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;

15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.

16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake.

17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye.

18 Naye ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha kanisa; naye ni mwanzo, ni mzaliwa wa kwanza katika wafu, ili kwamba awe mtangulizi katika yote”.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je mkristo anaweza akawa na mapepo?

Je! tunaweza kuwaamuru Malaika kama tunavyoyaamuru mapepo?

Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?

ONDOKA YESU, TUACHIE MAPEPO.

Wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe. Akawapa ruhusa.

Print this post

Je tamaa ni dhambi kulingana na Yakobo 1:15?

Swali: “Halafu ile tama ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti, (Yakobo 1:15).. je kutamani sio dhambi?”


Jibu: Kwa asili kutamani sio dhambi! Bali kunaweza kuwa ni mwanzo wa dhambi.. ni sawa na “kuongea”..kuongea si dhambi lakini kunaweza kuwa chanzo cha dhambi, kutegemea ni nini unaongea..

Na vile vile “tamaa” kwaasili ..imeumbwa ndani ya Mtu, na hata ndani ya viumbe vyote, ambayo lengo lake ni kuhamasisha jambo fulani jema au baya lifanyike katika mwili wa mtu au maisha ya mtu.

Kwamfano hatuwezi kumtafuta MUNGU kama yeye mwenyewe hajaiweka hiyo tamaa ndani yetu..hatuwezi kuomba kama yeye hatatuwekea hiyo tamaa ndani yetu n.k

Vile vile katika masuala ya mwilini,  tusingependa kula wala kuhamasika kula chakula kama tusingewekewa ndani yetu tamaa ya chakula, ile tamaa iliyowekwa ndani inatuhamasisha kula chakula, na tunapokula miili yetu inapata faida, na kutimiza lengo la kuendelea kuishi.. Lakini tamaa hiyo inapozidi mipaka inazaa ulafi na ulevi ambao ni dhambi (Soma Luka 21:34, Warumi 13:13, Wagalatia 5:21, na 1Petro 4:3).

Vile vile pia mtu kawekewa tamaa ndani yake ya kimwili kwa jinsia tofauti na yake, tamaa hiyo Mungu kaiweka ndani ya mtu kwa kusudi maalumu na wakati maalumu, kwamba wakati utakapofika mtu aweze kukutana na mke/mume wake na kuzaa watoto, kutimiza Baraka  alizozisema katika Mwanzo 1:28

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.

28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi:”.

Lakini tamaa hiyo inapozidi na kuvuka mipaka kiasi kwamba inampelekea mtu kushindwa kujitawala ndipo anapoanguka katika zinaa na hata zinaaa ya jinsia moja na yake.

Kwahiyo tamaa yoyote ile iwe ya chakula, au ya mwili  kwaasili sio mbaya, ila inapozaa matunda mabaya ndipo inageuka kuwa dhambi..Na ndicho Biblia ilichokimaanisha hapo katika  Yakobo 1:15 kuwa “tamaa ikiisha kuchukua mimba inazaa dhambi”..maana yake katika uasili wake sio dhambi!.. ila inapochochewa kwa njia isiyopaswa ndipo inapozaa dhambi.

Unatazama picha chafu mitandaoni, au unaposoma makala zenye maudhui ya zinaa, au unaposhiriki mijadala yenye maudhui ya zinaa  hapo unaizalia matunda ile tamaa ya mwili ndani yako, na hiyo ni dhambi, kwasababu mwisho wa siku itakupelekea kufanya zinaa au kujichua, au mawazo yako muda wote kutawaliwa na zinaa jambo ambalo biblia imesema kuwa ni machukizo kwa Bwana, moyo uwazayo mabaya (Mithali 6:18).

Biblia inatufundisha kutoyachochea mapenzi..

Wimbo 2: 7 “Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe”.

Na tamaa nyingine zote ni hivyo hivyo, hatuna budi kuzitawala ili zisizae dhambi, maana mshahara wa dhambi ni Mauti… na tamaa zinazozaa dhambi zote zinatokana na dunia na si MUNGU..

1Yohana 2:16 kuwa tamaa  ya macho na tamaa ya mwili inatokana na dunia na si Mungu

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI NJIA GANI MTU AITUMIE AWEZE KUSHINDA TAMAA NA VISHAWISHI?

USIWE NA TAMAA YA CHAKULA KINGINE.

USIKATE TAMAA UNAPOPITIA MAGONJWA.

Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.

Roho ya kukata tamaa ni nini na inatendaje kazi?

Print this post

Fahamu maana ya Warumi 7:25 je tunatumikia sheria ya dhambi?

SWALI: Naomba kufahamu Warumi 7:25 ina maana gani?

Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.

JIBU: Katika sura yote ya saba, mtume Paulo, anaeleza kwa kina mapambano yaliyo ndani ya mwamini.  Kwamba nia yake kutoka ndani ni kuitii sheria ya Mungu, lakini mwili wake kwa nje ni kikwazo kikubwa kiasi cha kumfanya ashindwe kabisa kutimiza maadhimio yake.

Warumi 7:19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu

Na ni kweli huo ndio uhalisia wa kila mtu. Na ndio maana mwishoni mwa sura hiyo anahitimisha kwa kueleza hali hiyo, Lakini katika vifungu hivyo, wengi wanatafsiri vibaya wakidhani  Paulo anatetea udhaifu wa mwili hapana.. Kinyume chake alianza kwanza kueleza uhalisia wa kibinadamu, ili atoe suluhisho halisi la namna ya kushinda, ambalo ndio tunalisoma katika sura inayofuata ya nane (8)

Ambapo sasa kwenye sura ya nane(8) inayofuata, anaeleza namna ambayo Kristo anatusaidia kuishinda hiyo hali, kwa sheria nyingine  mpya ya Roho ambayo anaiweka ndani yetu.

Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.

2 Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. Maana yake ni kuwa, Roho Mtakatifu, anatuweka huru katika huo utumwa wa mwili unaotupelekesha.

Inahitaji tu kutii, kwa kumfuata Roho Mtakatifu, kisha yeye mwenyewe atatupa nguvu ya kushinda mambo yote ya mwilini. Lakini sio kwa kutegemea  nguvu zetu tu wenyewe.

Warumi 8: 5 Kwa maana wale waufuatao mwili huyafikiri mambo ya mwili; bali wale waifuatao roho huyafikiri mambo ya roho.6 Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani.

7 Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii. 8 Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.

9 Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.

10 Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.

Hivyo ukiishi kwa kumtii Roho Mtakatifu, basi huwezi tumikishwa tena na  mwili,

Wagalatia 5:16 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. 18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.

Hitimisho:

Warumi 7:25, Paulo analenga hasaa sababu ya sisi kushindwa kutimiza sheria ya Mungu, Ni kwasababu ipo sheria nyingine (ya dhambi iliyojificha ndani yetu) ambayo ni ngumu kutoka kwa namna ya kibinadamu, hivyo anataka hilo tulijue ili tufahamu kuwa kwa nguvu zetu wenyewe hatuwezi kuishinda, Lakini kwa Yesu Kristo atupaye Roho wake ndani yetu, tukienenda kwa kumtii huyo, basi sheria hiyo ya dhambi tutaishinda kabisa kabisa.

Ni wito wa kila mwamini kujifunza kutembea katika Roho.

Je! Unafahamu namna ya kutembea katika Roho kama sio. Basi tutumie ujumbe kwa namba uzionazo chini ya somo hili tukutumie.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NITAUVUTAJE UWEPO WA ROHO MTAKATIFU KARIBU NAMI?

MAANA ROHO HUCHUNGUZA YOTE, HATA MAFUMBO YA MUNGU.

Print this post

Kwanini Nyaraka za Paulo kwa makanisa tuzifanye kuwa nyaraka zetu leo?

Swali: Nyaraka za Paulo tunaona ni barua kwenda kwa makanisa yaliyokuwepo wakati huo, kama Korintho, Efeso, Kolosai na Galatia na nyingine kwenda kwa watu waliokuwepo wakati huo, kama Timotheo, Tito na Filemoni sasa iweje nyaraka hizo zituhusu na sisi na hata ziwe ni neno la MUNGU?, na kuzitumia hizo kufundishia sasa?


Jibu: Swali zuri lakini ili tuweze kupata majibu yaliyojitosheleza, hetu tutafakari mifano ya kawaida iliyopo,

Alikuwepo mwanasayansi mmoja  wa kijerumani maarufu ambaye sasa ni marehemu ajulikanaye kama Albert Einstein (Mgunduzi wa kanuni ya kutengeneza bomu la Nyuklia), huyu wakati wa vita vya pili vya dunia alimwandikia waraka Raisi wa Marekani aitwaye Roosevelt, kwamba atengeneze silaha ya Nyuklia, kabla Adolf Hitler hajaitengeneza, na katika waraka huo alimpa pia hiyo fomula/kanuni ya kutengeneza silaha hiyo. (Waraka huo uliandikwa mwaka Agosti 2,1939).

Na matokeo ya waraka huo ni Raisi Roosevelt kuunda bomu la Nyuklia, na kwenda kulifanyia majaribio katika miji miwili ya nchi ya Japani (Mji wa Heroshima na Nagasaki).

Lakini ajabu ni kwamba baada ya wakati huo, sehemu za waraka huo zilizobeba kanuni za utengenezaji wa nyuklia zilivuja na kufikia mataifa mengine, na mataifa hayo kama Urusi hayakulaza damu bali nayo pia yakaunda mabomu ya nyuklia yenye kanuni ile ile, zilizokuwepo ndani ya ule waraka.

Na cha ajabu zaidi ni kwamba miaka mingine mingi mbele mataifa mengine kama Ufaransa, Pakistani,India, na mengine machache yakaichukua kanuni hiyo hiyo ya kuunda bomu la Nyuklia na kutengeneza mabomu yao,

Na cha kushangaza zaidi na zaidi ni kwamba mataifa mengine mengi leo yanafanya jitihada kuunda mabomu yao kupita kanuni ile ile ya mwanasayansi huyo Albert Einstein aliyetokea miaka mingi huko nyuma kupitia waraka wake aliomwandikia Raisi wa Marekani.

Sasa swali la kujiuliza, ni hili; kulikuwa kuna haja gani ya Mataifa kama Urusi, Ufaransa, na mengineyo kufuatilia waraka Einstein aliomwandikia Raisi Roosevelt na hata kuzitumia kanuni/fomula alizoziandika ndani yake kutengeneza mabomu yao??..

Tulitegemea waraka wa Einstein kwenda kwa Raisi huyo, uishe matumizi baada ya kusomwa na kutumika na Raisi huyo wa Marekani, lakini ajabu ni kwamba mpaka sasa una matokeo katika ulimwengu wetu, ingawa uliandikwa miaka mingi iliyopita.

Kwahiyo Utaona kwamba sababu pekee ya mataifa mpaka leo hii kuitumia kanuni ya mwanasayansi huyo aliyetokea miaka mingi huko nyuma ni kwasababu alichokigundua Albert Einstein ni kitu cha Kweli chenye manufaa na tija si tu kwa wakati wake tu, au Taifa lake tu bali hata kwa mataifa mengine na kwa vizazi vingi vijavyo.

Na ni hivyo hivyo Nyaraka za Mtume Paulo na za Mitume wengine… kwa jicho la nje zitaonekana kama zimeandikwa kwaajili ya makanisa yale ya wakati ule, au kwaajili ya watu wa wakati ule, lakini kwa jicho la rohoni ni ujumbe kwetu zaidi hata ya watu wa wakati ule.

Kwasababu yaliyoandikwa katika nyaraka za Mitume wa kwenye Biblia ni maneno ya kweli yanayoishi katika vizazi vyote, na tena kwa jinsi muda unavyozidi kwenda ndivyo yanavyohitajika zaidi kwasababu yaliyokuwa yanatendeka zamani, sasa hivi yamezidi mara nyingi sana.

Vita vya kiroho walivyokuwa wanapigana watu wa kanisa la Korintho, Galatia, na mengineyo nyakati hizo ndizo tunazopambana sasa, tena wakati huu zimezidi zaidi, kwahiyo tunahitaji fomula na kanuni za wanasayansi wetu wa kiroho (Mitume na manabii wa kwenye Biblia) kutengeneza silaha zetu za kiroho sasa, na kupambana hivi vita mpaka tushinde.

Lakini tukibaki na kusema zile nyaraka zilikuwa ni za wakorintho tu peke yao na wagalatia tu peke yao, na kwamba sisi hazituhusu tutamalizwa vizuri na shetani, ni sawa na Taifa la Urusi liseme ule waraka wa Einstein aliomwandikia Raisi wa Marekani, kuhusu utengenezaji wa Nyuklia uliwahusu Wamarekani peke yao, wangekuwa na akili hiyo, leo wangeisha, au wangetawaliwa!.

Na sisi ni lazima tuiamini Biblia, kuwa ni Neno la MUNGU linaloishi kwa nyakati zote na vizazi vyote, hakuna wakati litaisha matumizi, au litapitwa na wakati, Mafunuo yaliyokuwemo ndani ya Biblia yana nguvu na Uwezo, kwani waliofunuliwa wamefunuliwa kwa uweza wa Roho Mtakatifu na si kwa akili zao.

Mwisho; Je umempokea YESU kwelikweli au kidini?.. kama maisha unayoishi ni ya uvuguvugu bado hunaye YESU, unamhitaji YESU aingie maishani mwako, unahitaji kujikana nafsi na kubeba msalaba na kumfuata YESU, Fanya mageuzi na acha kuishi maisha ya uvuguvugu, kwani tunaishi nyakati za hatari na muda umeenda sana, na parapanda inalia muda wowote, na mambo yote yatapita.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?

Je ni nyaraka zipi mtume Paulo aliziandikia gerezani?

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Print this post

SADAKA INAONDOA MADHARA YA MAUTI

Sadaka inayotolewa kwa mwongozo wa Neno la MUNGU ina matokeo makubwa sana kwa anayeitoa. Yapo madhara yanayoondoka kwa maombi tu peke yake, lakini yapo mengine yanahitaji sadaka pamoja na maombi.

Hebu turejee Biblia kidogo tujifunze jambo..

Wakati ambapo Nabii Samweli anataka kwenda kumpaka mafuta Daudi ili awe mfalme mahali pa Sauli..biblia inatuambia kuwa alipofikiri kwenda tu hofu ilimwingia..

Na hofu hiyo ni kwamba alimwogopa Mfalme Sauli, kwani alijua kabisa endapo Sauli akisikia mtu mwingine anaenda kupakwa mafuta ya kifalme kuchukua sehemu yake, wivu utamwingia na atataka kumwua nabii Samweli na yule atakayeenda kupakwa mafuta.

Sasa ili zoezi la Daudi kupakwa mafuta likamilike bila kuleta madhara yoyote kwa Nabii Samweli na Daudi anayeenda kupakwa mafuta ya kifalme, SADAKA ILIHUSIKA!.

Utauliza ilihusika vipi?…turejee maandiko…

1 Samweli 16:1 “BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.

2 Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi BWANA akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea BWANA dhabihu.

3 Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako”

Je umeiona nafasi ya sadaka katika kuyaokoa maisha ya Samweli na Daudi?.

Hapo MUNGU hakushindwa kumwambia nabii Samweli aende hivyo hivyo na kwamba atamlinda!…La! Hakufanya bali alimwambia aende na dhabihu..

Jambo hilo Bwana MUNGU wetu aliliruhusu pia ili tuelewe umuhimu dhabihu/sadaka.

Unapomtoleo MUNGU kwa ufunuo wa Neno, bila kushurutishwa na mtu wala uchungu, kuna mambo mengi katika ulimwengu wa roho yanafanyika, kama ni nira za mauti zinalegea na kama kuna vifungo vya dhambi pia vinaondoka.

Na kumbuka sadaka kwa BWANA inapelekwa kwa BWANA, maana yake mahali ambapo BWANA anatumikiwa (mfano kanisani au mahali panapofanyika kazi ya MUNGU ikiwemo mikitano ya injili)..hapo ndipo penye neema.

Usipeleke sadaka yako maalumu mahali pengine kama kwa marafiki, au watu au maskini wa barabarani…ni vizuri kufanya hivyo na kuna baraka zake lakini vya Bwana vinapaswa vipelekwe kwa Bwana ndivyo maandiko yanavyofundisha..

Tenga kiasi chako kungine peleka kwa maskini na wenye uhitaji, lakini hakikisha una sadaka yako maalumu kwa BWANA utakayopeleka aidha kanisani au mahali popote kazi ya MUNGU inapofanyika kwa usahihi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post