Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

Katika 1Wakorintho 1:17, Paulo anasema hakuitiwa kubatiza, Je na mimi kama sijaitiwa kubatiza, bali nimeitiwa kuhubiri watu waokoke tu!, nitakuwa na hatia, nisipohubiri suala la ubatizo wala kuligusia kabisa?


Jibu: Ni muhimu kufahamu kuwa  kila mtumishi wa kweli wa Mungu, haijalishi awe nani, ameitiwa KULIHUBIRI NENO LA MUNGU KATIKA UKAMILIFU WOTE, pasipo kubagua kipengele chochote katika maandiko. Huo ndio wito tuliopewa..

Tutatofautiana tu namna ya kuhubiri, kwasababu tunazo karama mbali mbali lakini INJILI NI MOJA KWETU WOTE!, Na wote tutahubiri kitu kimoja.. Hakuna mahali tumepewa maagizo ya kuhubiri tofauti tofauti au kulipunguza Neno la Mungu.

Sasa tukirudi kwenye swali, ni kwanini Paulo aseme sikuitiwa kubatiza?

Hebu tusome, mstari huo kwa utarati kisha tuendelee..

1Wakorintho 1:17 “Maana Kristo HAKUNITUMA ILI NIBATIZE, bali niihubiri Habari Njema; wala si kwa hekima ya maneno, msalaba wa Kristo usije ukabatilika”.

Hapa hakusema “MAANA KRISTO, HAKUNITUMA NIHUBIRI UBATIZO,” lakini badala yake anasema “KRISTO HAKUNITUMA NIBATIZE”. Maana yake kuhubiri Ubatizo Paulo alikuwa anauhubiri kama kawaida,(Soma Matendo 19:1-5 utalithibitisha hilo), lakini kitendo cha kufanya Ubatizo hakuwa anakifanya sana, bali mara moja moja sana… Ndio maana tukirudi juu kidogo katika mistari hiyo tunaona yeye mwenyewe anajishuhudia kubatiza watu baadhi..

1Wakorintho 1:14 “Nashukuru, kwa sababu sikumbatiza mtu kwenu, ILA KRISPO NA GAYO;

15 mtu asije akasema kwamba mlibatizwa kwa jina langu.

16 TENA NALIWABATIZA WATU WA NYUMBANI MWA STEFANA; zaidi ya hao, sijui kama nalimbatiza mtu ye yote mwingine”.

Umeona hapo anasema aliwabatiza Krispo, na Gayo Pamoja na watu wa nyumbani mwa Stefana.. Kuashiria kuwa alikuwa anabatiza, lakini hakuwa anaifanya hiyo huduma mara kwa mara, kulinganisha na huduma ya kwenda kuzunguka huku na huko kuhubiri Neno kwa watu aliyokuwa anaifanya.. Na wote walioamini injili yake aliwaongoza katika makanisa wabatizwe au watu maalumu wakabatizwe!..ili yeye apate nafasi ya kuendelea kuhubiri injili sehemu nyingine…Na ilipotokea hakuna mtu wa kuwabatiza kwa mahali hapo, basi alichukua yeye hilo jukumu la kuwabatiza!. kama hapo kwenye Matendo 19:2-6.

Ni sawa na jinsi Mitume walivyogawanya jukumu la kuwahudumia wajane, kwa wale Mashemasi 7 ili wao wadumu katika kulihubiri Neno.

Matendo 6:2 “Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, HAIPENDEZI SISI KULIACHA NENO LA MUNGU NA KUHUDUMU MEZANI.

3 Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili;

4 na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.

5 Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia;

6 ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba, Hakuna mtu yeyote ambaye ameitiwa kufundisha Neno moja la kwenye biblia na kuliacha lingine…Wote tunapaswa tuhubiri injili yote, iliyo kamili, yaani injili ya toba, ubatizo, Imani, Roho Mtakatifu, na mambo mengine yote ya kiimani, pasipo kupunguza chochote wala kuongeza. sawasawa na (Ufunuo 22:18-19).

Sababu kuu inayowafanya asilimia kubwa ya wahubiri wabague baadhi ya maneno kwenye biblia na kufundisha baadhi tu, ni kwasababu wanaogopa kuumiza hisia za watu au kupoteza waumini!, na wala si kitu kingine!!.. Jambo ambalo ni la hatari sana!.. kuacha kuhubiri Neno la Mungu kwasababu ya kohofia hisia za mtu, atajisikiaje, au atakuonaje.

Ni heri kuonekana hufai, lakini umelizungumza Neno la Mungu katika ukamilifu wote, Ni heri mtu ahuzunike moyoni kwasababu ya kweli ya Neno uliyomweleza, kwasababu itamuumiza moyo sasa, lakini baadaye itakuwa ni tiba kwake na atakuja kumshukuru Mungu sana kwaajili yako..

2Wakorintho 7:10 “Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti”.

Lakini unajua kabisa ubatizo aliobatizwa sio sahihi, mavazi anayovaa sio ya kiimani, kazi anayoifanya sio halali, na kwasababu unaogopa usiumie utakapomwambia ukweli, unaishia kumfariji kuwa wewe hujaitiwa kuhubiri ubatizo au Mavazi au kazi mtu anayoifanya, wewe umeitiwa kumhubiria amwamini Yesu tu!.. Fahamu kuwa ndio unazidi kumpoteza huyo mtu!.

Maran atha!

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

Je! Ni kanisa lipi sahihi kumuabudia Mungu?

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Emmanuel Kitengule
Emmanuel Kitengule
1 year ago

Amina mwalimu,nimepata kitu hapo.

Anonymous
Anonymous
1 year ago

Ni sahihi kumshirikisha kila MTU Jambo lako?