Title March 2025

Fahamu Maana ya Mithali 15:24 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;

SWALI: Nini Maana ya Mithali 15:24?

Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu; Ili atoke katika kuzimu chini.

JIBU: Hapo yapo mambo matatu,

  1. Mtu mwenye akili.
  2. Njia ya uhai,
  3. Na uelekeo wa njia hiyo.

Mtu mwenye akili ni mtu mwenye uwezo wa kufikiri/kupambanua vema na kufanya maamuzi sahihi katika maeneo mbalimbali ya maisha yake. Hivyo hapo anasema mtu mwenye akili anajua vema kuichagua njia yake ya uhai.

Anasema njia yake hutoka chini kuelekea juu. Kwa lugha ya picha ni barabara iliyopinduliwa na kusimamishwa wima kama ngazi,  na sio mfano wa barabara hizi tulizonazo zilizolala chini, ambazo uelekeo wake ni aidha kaskazini na kusini, au mashariki na magharibi.

Sasa hapa anasema njia yake ya uhai huenda juu, ili atoke kuzimu chini. Akiwa na maana husafiri kutoka kuzimuni kuelekea uzimani juu kwa Mungu.

Hufunua nini?

Safari ya mtu mwenye akili, hufikiri kumtafuta Mungu juu alipo,

Wakolosai 3:1 Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. 2 Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.

Hufikiri ukuaji wa kiroho, atokea hatua moja ya utakatifu kwenda nyingi, kiwango kimoja cha Imani kuelekea kingine kama Kristo (2Petro 1:5-10, Waefeso 4:13). Ni mtu ambaye kila siku anakwenda mbali na njia ya mauti. Mawazo yake yapo juu sikuzote kumjua Kristo na mapenzi yake yote.

Lakini kinyume chake ni ukweli, mtu asiye na akili barabara yake haijasimama wima, bali imelala. Atawaza atoke hatua moja kwenda nyingine lakini hakuna ukuaji wowote au kuongezeka kokote. Huwenda anachowaza tu sikuzote ni kutoka katika umaskini kwenda katika utajiri, kutoka katika kiwango kimoja cha elimu kwenda kingine, kutoka katika cheo kimoja kwenda katika kingine..Hatua zake ni za kidunia tu, akidhani ndio uzima wake upo hapo. Kumbe kapotea njia.

Si kwamba vinapingwa vya dunia hapana, ni vizuri na vinafaa, lakini havina uzima wa milele ndani yake. Ili uwe na akili hakikisha unampokea Kristo, kisha unaanza kukua kiroho, kila siku unafikiri njia ya kuyakimbia machafu ya kidunia. Hapo barabara yako itakuwa umesimama kama ngazi na hivyo utaiponya nafsi yako.

Je! Umeokoka?. Kama ni la! Basi wakati ndio sasa fungua moyo wako mkaribishe Yesu akuokoe hizi ni nyakati za hatari, tubu leo upokee wokovu. Ikiwa upo tayari kumkaribisha Kristo moyoni mwako, basi waweza kubofya hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba. Bwana akubariki. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Maana ya Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha. 

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Biblia inasema nini kuhusu mtu ‘Mwenye kujipendekeza (Mithali 29:5)

Print this post

Kuonja ni kufanya nini? (Kutoka 15:25).

Swali: Kuonja kunakozungumziwa katika kitabu cha Kutoka 15:25 kunamaanisha nini?.

Jibu: Turejee mistari hiyo..

Kutoka 15:24 “Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema,Tunywe nini? 

25 Naye akamlilia BWANA; BWANA akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, AKAWAONJA HUKO

Kuonja kunakozungumziwa hapo ni kuonja kiroho na si kimwili, siku zote mtu anayeonja kitu, lengo lake ni kukipima ubora wake, kilingana na vigezo anavyovitaka.

Na kiroho MUNGU anatuonja sisi mara kwa mara kwa kuangalia matendo yetu kama tupo sawa mbele zake…

Kwamfano utaona Bwana YESU anatumia lugha hiyo ya kiroho katika kitabu cha Ufunuo kuyapima matendo yetu..

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu”

Umeona hapa?…matendo yetu yanapimwa kwa kinywa cha Bwana..kama tu Moto mbele zake basi tuna heri, lakini kama tu baridi au vuguvugu ni Ole!.

Kwahiyo hata kipindi wana wa Israeli wakiwa wanatoka Misri kuelekea nchi ya ahadi.. Mungu alikuwa anawaonja matendo yao…

Na kuna kipindi aliwatapika walipomjaribu na kumnun’unikia.

Lakini si tu Bwana akiyekuwa anawaonja, bali pia aliwaambia kuwa hiyo nchi wanayoiendea itawaonja matendo yao, na kama yakiwa mabaya itawatapika, kwa kuwa pia iliwatapika wenyeji waliokuwa wanaiishi kutokana na mateendo yao maovu.

Walawi 18:25 “na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi YATAPIKA wenyeji wake na kuwatoa. 

26 Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu; 

27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;) 

28 ili kwamba hiyo nchi ISIWATAPIKE NA NINYI PIA, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu”.

Je umempokea YESU?.

Je wewe ni moto?, au baridi au una uvuguvugu?…Uvuguvugu maana yake ni kuwa upo mguu mmoja nje!…mguu mmoja ndani!, leo unaenda kanisani kesho unaenda Bar, leo unatoa sadaka kesho unabeti, leo unavaa nguo ya sitara kesho nguo ya aibu..hapo Bwana amesema atatapika mtu wa namna hiyo.

Bwana atusaidie tumtii ili tusiwe miongoni mwa watakaotapikwa.

Maran atha!.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

ELOI ELOI LAMA SABAKTHANI?

Zaburi 22:1 Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu? 2 Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati.

Maneno haya ukiyatafakari, utagundua ni ya mtu aliyefikia hatua mbaya sana ya kukaribia kukata tamaa kwasababu ya aidha magumu, au huzuni, au mateso yasiyoelekeza anayoyapitia, akiangalia kulia, haoni  tumaini lolote, akiangalia kushoto haoni mkono wowote wa Mungu ukimsaidia licha ya kuomba na kulia sana, kwa muda mrefu.

Sehemu nyingine anasema, amekataliwa kila kona, amekuwa kama msikwao kwa ndugu zake.

Zaburi 69:10 Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa laumu juu yangu.

11 Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, Nikawa mithali kwao. 12 Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi hunidhihaki. 13 Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.

14 Uniponye kwa kunitoa matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika vilindi vya maji. 15 Mkondo usinigharikishe, wala vilindi visinimeze, Wala shimo lisifumbe kinywa chake juu yangu.

16 Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema, Kwa kadiri ya rehema zako unielekee. 17 Wala usinifiche uso wako, mimi mtumishi wako, Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi.

Mwandishi huyu alikuwa ni  Daudi, alipitia kipindi kirefu sana cha kujiona kama vile Mungu kamtupa, hadi kuna wakati akaona heri aende kuomba hifadhi kwa maadui zake wafilisti ambao hapo mwanzo aliwafukuza na kuwaita makafiri (wasio tahiriwa), lakini safari hii kwa unyenyekevu wote, anaenda kuwa mmoja wa askari wao, ili tu apate hifadhi, asiangamie kabisa. Huyo ni mtu ambaye maji ya shingo yalimfikia kwelikweli.

Sio kwamba alikuwa haombi, au hamlili Mungu?. Au kwamba ana dhambi kuliko wengine, mpaka awe mtu wa bahati mbaya hivyo Hapana, nyakati zote alikuwa mwombaji, lakini akafika mahali katika uhalisia wa kibinadamu aliona kama Mungu amemwacha kabisa.

Lakini kwasababu huruma za Mungu zilikuwa nyingi juu yake alimpa moyo mkuu, wa kuendelea kumngoja Bwana. Ndio maana  sehemu nyingi katika Zaburi anasisitiza sana Neno hili ‘mngojeeni Bwana’ (Zaburi 37:7, 25:3, 31:24,38:15, 40:1).

Sasa moja ya  maneno machache ya Daudi yaliyonikuliwa na Bwana Yesu lilikuwa ni hili.

Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?

Mathayo 27: 45 Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa.

46 Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

Je! Unadhani kauli hiyo Yesu aliyoitoa alimaanisha kweli ameachwa?

Hapana, tangu mwanzo alikuwa anajua Mungu yupo pamoja naye, na kwamba saa yake imekaribia, muda si mrefu anakwenda kuinuliwa na kutukuzwa, tena sehemu nyingine anasema alishangalia pale msalabani (Wakolosai 2:15). Lakini kuinukuu kauli ile ni kuonyesha ubinadamu wetu, unavyoweza kutuhubiria tuwapo katikati ya shida, kwamba Mungu ametuacha hususani pale tunapopitia shida, na mateso.

Yesu alinukuu ubinadamu wetu kukumbuka mfano wa yale aliyoyapitia Daudi..

Lakini tunaona dakika chache baada ya pale, pindi tu alipokata roho, makaburi yakapasuka, wafu wakatoka makaburini, pazia la hekalu likapasuka, na baada ya siku tatu akafufuka, ukombozi wetu mkuu ukapatikana, ‘Lakini ni kwa maneno ya kudhaniwa kuwa Mungu amemwacha’.

Mathayo 27:50 Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.

51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka;

miamba ikapasuka; 52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; 53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.

Ndugu, upitiapo hatua hizo ambazo mawazo yako yanakufundisha kuwa Mungu hayupo na wewe tena, amekuacha, kwasababu ya shida unazozipitia muda mrefu, magonjwa yasiyokoma, umeomba mpaka umechoka, umelia hadi ukomo,wewe ona ni kawaida,…. Piga moyo konde Mngojee Bwana. Daudi alistahimili hatimaye akathibitishwa kwenye ufalme ambao ulidumu pamoja na vizazi vyake vingi tofauti na wafalme wengine wa Israeli. Mngojee Bwana, kimaombi, kwasababu baada ya joto huja mvua.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI YESU ALIMUITA BABA YAKE “ABA”?

kiaramu ni lugha gani? je ilizungumzwa na Yesu?

Nzi wa Misri, na Nyuki wa Ashuru vilimaanisha nini? (Isaya 7:18-20).

Print this post

Biblia inaposema sisi ni ukuhani wa kifalme, maana  yake nini?

1Petro 2:9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;


JIBU: Katika vifungu hivyo biblia inaeleza kwa ukubwa sifa zetu sisi tuliomwamini Yesu Kristo, jinsi zilivyo kuu, anasema sisi ni mzao mteule, na pia watu wa milki ya Mungu. Lakini sifa nyingine ndio hiyo ya ukuhani wa kifalme.

Angeweza kusema sisi ni  ukuhani wa kisomi, au ukuhani wa kiroho, au ukuhani ki-mbingu, au ukuhani wa kitajiri. Lakini anatumia Neno ukuhani wa kifalme. Ikiwa na maana kuwa tunao ukuhani lakini si ukuhani tu bali wenye asili ya kifalme.

Sifa kuu ya kuhani, ni kuweza kumkaribia Mungu kusema naye, na kufanya upatanisho kwa ajili ya watu wengi. Mfano wa Haruni na uzao wake. Tunaona hawa tu ndio waliopewa neema ya kuweza kumkaribia Mungu katika kiti chake che rehema, kuzungumza naye na kuomba rehemu kwa taifa zima. Wengine wote walikaa nje ya hema.

Lakini pia sifa ya mfalme ni uweza, mamlaka, nguvu, na utajiri.  Mfalme anatawala, mfalme ana nguvu ya kijeshi, mfalme ni lazima awe tajiri na mwenye utiisho.

Sasa tukirudi kibiblia, Haruni na walawi wote ambao waliopewa sifa ya kikuhani, hawakuwa na ukuhani wa kifalme ndani yao. Waliishia tu kukaa hemani, na sio ni makuhani na wakati huo huo ni wafalme, lakini pia wafalme wengi (Mfano wa Daudi, Sulemani n.k.)hawakuwa na ukuhani pia ndani yao.. Hivyo waliishia tu kutawala lakini sio kuingia hekaluni kuvukiza uvumba. Alitokea mfalme mmoja kujaribu kufanya kazi hizo mbili kwa wakati mmoja, aliishia kupata ukoma kwasababu hakukuwahi kutokea mtu mwenye uwezo huo wa kutembea katika vyeo vyote viwili kwa wakati mmoja (2Nyakati 26:16-21).

Lakini yupo aliyetabiriwa na manabii kuwa atakuwa kuhani mkuu lakini pia mfalme. Na huyo si mwingine zaidi ya Bwana wetu Yesu Kristo. (Waebrania 7:11-17), Yeye alikuwa kuhani lakini pia alitokea katika kabila la kifalme la Yuda, kwa jinsi ya mwili.

Na mpaka sasa anatawala kama kuhani mkuu wetu, lakini pia mfalme wetu. Amewazidi makuhani wote, amewazidi wafalme wote.

Hivyo na sisi tuliozaliwa na yeye, tunarithi vyote alivyonavyo, maandiko yanasema hivyo (1Petro 1:3-4), Tunafanyika sio tu makuhani, ambao tunamkaribia Mungu kusema naye ana kwa ana, na kuwapatanisha wengine na yeye, lakini pia  tunafanyika wafalme wenye mamlaka yote, na nguvu, na utajiri.

Sisi tumepewa mamlaka ya kukanyaga nge na nyoka, na nguvu zote za Yule mwovu, mamlaka ya kupooza kila aina ya magonjwa na madhaifu, mamlaka ya kufungua na kufunga jambo lolote. Vilevile tumepewa na utajiri wote wa hekima na maarifa ndani ya Yesu Kristo (Waefeso 1:3).

Na zaidi mamlaka ya ufalme tuliyonayo itakuja kudhihirika vema mbeleni kwenye utawala wa miaka 1000 wa amani wa Yesu Kristo duniani. Jinsi tutakavyo milika na kutawala na yeye kama wafalme, na yeye akiwa kama mfalme wa wafalme. (Ufunuo 19:16)

Ufunuo 5:10 ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi.

Je!, umeipokea neema hii?

Ni nini unachosubiri usimpe Kristo maisha yako? Tafakari ahadi kubwa namna hii unapewa bure, ni nani anayeweza kufanya hivyo? Saa ya wokovu ni sasa, na wakati uliokubaliwa na Mungu ndio huu, okoka leo, usamehewe dhambi zako, jina lako liandikwe katika kitabu cha uzima.

ikiwa upo tayari kumpokea Yesu, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya “Uweza wa kifalme utakuwa begani mwake” (Isaya 9:6)?.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Ulimwengu wa Roho ni nini? Na mtu anawezaje kuwa wa rohoni?

Print this post

Je mkristo anaweza akawa na mapepo?

JIBU: Swali la kwanza la kujiuliza, je! mkristo ni mtu gani?..Mkristo ni mtu aliyemwamini,Yesu Kristo, kisha akapokea msamaha wa dhambi,kwa toba ya kweli, ubatizo na kutiwa muhuri na Roho Mtakatifu.

Mtu wa namna hiyo anakuwa na Kristo ndani yake. Na mtu mwenye Kristo Hawezi kuwa na mapepo, kwasababu Yesu hana pepo.

Vifungu hivi vinatuthibitishia kuwa hilo jambo haliwezekani;

1 Yohana 4:4

[4]Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia.

2 Wakorintho 6:14

[14]Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?

Kuonyesha kuwa giza na nuru haviwezi kuwepo sehemu moja, wakati mmoja.

Lakini swali linakuja inakuwaje kuna baadhi ya watu waliokoka wanaonekana kuwa na mapepo ndani yao?

Kama tulivyoona mkristo hawezi kuwa na mapepo, lakini ni vema kufahamu kuwa kuna tofauti kati ya kukaliwa na mapepo, na kushambuliwa na kipepo. 

Mtu aliyeokoka hawezi kukaliwa na mapepo, lakini anaweza akashambuliwa au kusumbuliwa na  uwepo wa mapepo, hicho ndicho kinachoweza kumtokea, lakini sio kwamba ana mapepo ndani yake.

Sababu zinazoweza mpelekea asumbuliwe nayo, ni hizi kuu tatu;

  1. Kutoijua kweli vema
  2. Uchanga wa kiroho
  3. kutenda dhambi.

Tukianza na sababu ya kwanza.

  1. Kutoijua kweli.

Kukosa kujua nafasi na mamlaka uliyo nayo ndani ya Kristo, shetani anaweza kukusumbua kwelikweli. Na wakati mwingine kukutesa. mapepo yanaweza kuwasumbua watu kifikra na kwa kuwawekea mawazo machafu akilini mwao, kuwashitaki, kwa kuwatupia ndoto mbaya, au kuwakaba usiku, au kuwaletea majaribu mbalimbali, lakini huyu mtu akijua kuwa ameshakabidhiwa mamlaka yote ya kukanyaga nge na nyoka na nguvu zote za yule mwovu,(Luka 9:1), akaitumia vema, shetani atamwogopa kumsogelea kwasababu anajua nguvu ya kimamlaka iliyo ndani yake ni thabiti haitoki mdomoni bali inasukumwa na ufalme wa Mungu ulio nyuma yake.. Ni sawa na mtu anayetoa amri kwa kinywa chake mwenyewe na yule anayetoa kwa agizo la raisi watu watamwogopa yule anayetoa kwa mamlaka aliyopewa na raisi. Hivyo ni muhimu sana kuitafakari na kuiamini mamlaka uliyopewa na Kristo ndani yako ili hayo maroho  unapoona dalili ya kutaka kukusumbua unatamka jina la Yesu mara moja tu yanatetemeka na kukimbia. Mamlaka hiyo amepewa mkristo yoyote aliyeokoka, haijaishi ni mchanga au mkomavu.

2) Sababu ya pili ni uchanga wa kiroho.

Ukiokolewa, kwasababu ya kutoondoka mara moja kwa baadhi ya tabia, au msingi au mienendo ya kale, hivyo tabia hizo mara nyingine zinakuwa ni upenyo wa uwepo wa kipepo kuzunguka zunguka karibu yako. Vitu vichanga sikuzote hushambulika kirahisi, unyasi ukiwa mdogo hutikiswa sana na upepo, Ndio maana ni lazima uanze kuukulia wokovu, kwa kujifunza Neno, kujizoesha utakatifu, maombi, ibada, mambo ambayo adui hapendi kwasababu ni kama moto kwao.  Mtu asipokuwa mkristo wa vitendo, sikuzote atasumbuliwa na roho za kidunia, na hatimaye atajiona kama ni ana mapepo kabisa, na akiendelea kuishi hivyo, mpaka kurudi nyuma atakufa kiroho, na Roho Mtakatifu kuondoka ndani yake, na mapepo ndio yatapata nafasi ya kumtawala kabisa.  (2Petro 1:5-10)

3) Kutenda dhambi

Mtu aliyeokoka, akaanza kutenda dhambi za makusudi, anarudia yale yale kila siku, jambo hilo ni upenyo mwingine wa mapepo kumsumbua, kwasababu anakuwa ameyapa nafasi, na maandiko yanasema tumsimpe ibilisi nafasi. (Waefeso 4:27).

Kwamfano umeacha ulevi, baada ya kuokoka, na umekuwa hivyo kwa muda mrefu sasa, halafu ghafla unaanza tena kuwa mlevi, Mungu anakuonya uache hutaki, unaendelea kunywa pombe..kitendo hicho kinaweza kukupelekea kusumbuliwa sana na mapepo. Mfano tu wa Yule ambaye anatawaliwa nayo.

Mathayo 12:43 Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika,asipate.

44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na

kupambwa.

45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye

mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.

Hivyo kwa hitimisho, ni kuwa mtu aliyeokoka, hawezi kukaliwa na mapepo, yaani kutawaliwa au  kupagawishwa, au kuendeshwa nayo.. Isipokuwa anaweza kushambuliwa, kusababishiwa madhara, lakini kuvamiwa na uwepo wao. Ndio maana tumeambiwa tuvae silaha zote za haki, ili tuweze kumpinga shetani (Waefeso 6:10). Kwa kulijua Neno, utakatifu, maombi, na ibada.

Bwana akubariki.                                                               

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?

DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.

Je mtu anaweza akawa hajaokoka akaombea mtu na Pepo likamtoka,

 

Print this post

Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)

Je huu mji mtakatifu shetani aliomchukua Bwana katika Mathayo 4:5 ni mji gani?.. maana tunajua shetani hawezi kumiliki vitu vitakatifu?


Jibu: Turejee..

Mathayo 4:5 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mji mtakatifu, akamweka juu ya kinara cha hekalu.
6 akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu jitupe chini; kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake; Na mikononi mwao watakuchukua; Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

7 Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako”.

Mji Mtakatifu unaozungumziwa hapo ambao shetani alimpeleka Bwana YESU ni YERUSALEMU (Ya duniani) iliyopo pale Israeli..

Kumbuka ipo YERUSALEMU YA MBINGUNI, ambayo itakuja kushuka baada ya hukumu ya mwisho, na Yerusalemu hiyo Mpya shetani hawezi kufika wala watu ambao hawajamwamini Bwana hawataingia (kulingana na maandiko).

Ufunuo 21:1 “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.

3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao”.

Ruka mpaka mstari wa 23-27..

“23 Na mji ule hauhitaji jua wala mwezi kuuangaza, kwa maana utukufu wa Mungu huutia nuru, na taa yake ni Mwana-Kondoo.

24 Na mataifa watatembea katika nuru yake. Na wafalme wa nchi huleta utukufu wao ndani yake.

25 Na milango yake haitafungwa kamwe mchana; kwa maana humo hamna usiku.

26 Nao wataleta utukufu na heshima ya mataifa ndani yake.

27 Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”.

Lakini Mji shetani aliompeleka Bwana ulikuwa ni Yerusalemu ya duniani, (ule mji ule wa Daudi), mahali pale ambapo Hekalu la Sulemani lilijengwa..Yerusalemu hii ya duniani shetani anaweza kufika wakati wowote na mtu mwingine yoyote anaweza kufika, (awe mtakatifu au asiwe mtakatifu), anaweza kufika, na hata leo watu wanafika pale..

Na shetani alimpomfikisha Bwana YESU katika Hekalu, alimpandisha mpaka kwenye kinara chake, na kumwambia ajirushe chini, kwa maana imeandikwa atawaagiza malaika nao watamwokoa na ajali ile (sawasawa na Zaburi 91:11-12).

Lakini Kwakuwa Bwana YESU alikuwa amejaa Roho Mtakatifu, alizijuza hila na mbinu zote za ibilisi, na aliweza kumjibu kwa Neno, kuwa imeandikwa tusimjaribu Bwana MUNGU wetu.

Ni jambo gani tunaweza kujifunza hapo?

shetani anapotaka kumjaribu mtu anayemcha MUNGU hampeleki kwa waganga wa kienyeji, wala hampeleki kwenye mazingira ya dhambi ili atende dhambi, bali anampeleka sehemu takatifu, kama kanisani, au katikati ya watu wanaomtafuta MUNGU,
Ndio maana utaona leo mtu amesimama lakini anaanguka/anaangushwa katika dhambi na mtu/watu wa kanisani.

Utaona Askofu, au mchungaji, au mwinjilisti, au Nabii, au Mtume au mwimbaji wa kwaya anaanguka katika uzinzi na watu wa kanisani, ni mara chache sana na watu wa nje, kwanini?.
Kwasababu shetani anajua sehemu pekee ya kumjaribu mtu aliyeokoka na kusimama ni kanisani, akimletea wanaojiuza huko barabarani ni ngumu kuanguka..

Ndicho alichotaka kujaribu kufanya kwa Bwana YESU kumpeleka Hekaluni, kwanini asingempekeka kwenye vinara vingine vya mahali pengine, badala yake akachagua Hekalu?.. ni kwasababu alijua hapo ni rahisi kumwangusha Bwana.

Hivyo na sisi tuliookoka ni muhimu kuwa makini katika nyumba ya MUNGU kwani huko huko shetani anaweza kupata nafasi.

Bwana atusaidie.
Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 3)

MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)

Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?

Print this post

Filipo ni nani na je! Kuna Filipo wangapi katika biblia?

Katika biblia wapo watu wanne Wanatajwa Kwa jina la Filipo.

1) Filipo mtume

Huyu ndiye anayetambulika sana, ambaye alikuwa ni mmoja wa mitume wa Yesu Kristo

Yohana 1:43-44

[43]Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate.

[44]Naye Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mwenyeji wa mji wa Andrea na Petro.

Soma pia (Marko 13:18)

2) Filipo mwinjilisti

Huyu ni moja ya wale watu saba (mashemasi), waliochaguliwa na mitume wasimamie shughuli za kanisa. Habari yake tunaisoma Katika..

Matendo ya Mitume 6:2-5

[2]Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani.

[3]Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili;

[4]na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.

[5]Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia;

Huyu ndiye alikwenda kumbatiza yule towashi mkushi, na baadaye Kunyakuliwa na kupelekwa sehemu nyingine kwa ajili ya injili (Matendo 8).

Lakini pia anaonekana kuja kuishi Kaisaria ambapo alikuwa na mabinti wake wanne waliokuwa wanatabiri (Matendo 21: 8-9)

3) Filipo mfalme (Iturea)

Huyu alikuwa mtoto wa Herode Mkuu.

Luka 3:1

[1]Mwaka wa kumi na tano wa kutawala kwake Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alipokuwa liwali wa Uyahudi, na Herode mfalme wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania mfalme wa Abilene,

Kulingana na historia Huyu hakuonekana na sifa za chuki au ukatili bali mtenda haki, ndiye Aliyekuja kujenga mji wa Kaisari-Filipi, ulioitwa kwa jina lake (Mathayo 16:13).

4) Filipo mume wa Herodia

Alikuwa mtoto mwingine wa herode mkuu, wengine humchanganya na Filipo mfalme wa Iturea. Herode mkuu alikuwa na watoto.wawili walioitwa Filipo. Huyu hakuwa mfalme kama ndugu zake, ndiye aliyekuwa mume wa Hedoria, Ambaye alimwacha na kwenda kuolewa na kaka yake Herode, kitendo ambacho kilikemewa Na Yohana mbatizaji? Ikampelekewa yeye kufungwa na baadaye kukatwa kichwa. (Marko 6:17-19).

Nini tunaweza kumulika katika Filipo hawa wote.

Ijapokuwa walifanana majina Lakini tabia zao zilikuwa tofauti, Filipo wawili Wa kwanza walikuwa wakristo, lakini wawili wa mwisho hawakuwa wakristo.

Kuonyesha kuwa majina sio yanayowageuza watu. Bali Ni mwitikio wa injili. Ni vema kuwa na majina mazuri, Lakini ikiwa hakuna mwitikio wa kweli haiwezekani kubadilika hata tupewe majina mazuri namna gani.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii.>>>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

BWANA, SISI TUNATAKA KUMWONA YESU.

Je! ile habari ya Herode kutaka kumwua Yohana mbatizaji inajichanganya?(Mathayo 14:5 na Marko 6:20).

Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.

Print this post

Nzi wa Misri, na Nyuki wa Ashuru vilimaanisha nini? (Isaya 7:18-20).

Jibu: Awali turejee mistari hiyo..

Isaya 7:17 “Bwana ataleta juu yako, na juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako, siku zisizokuja bado, tangu siku ile aliyoondoka Efraimu kutoka katika Yuda; yaani, mfalme wa Ashuru.

18 Tena itakuwa katika siku hiyo Bwana atampigia kelele INZI ALIYE KATIKA PANDE ZA MWISHO ZA MITO YA MISRI, na NYUKI ALIYE KATIKA NCHI YA ASHURU.

19 Nao watakuja na kutulia katika mabonde yaliyo ukiwa, na katika pango za majabali, na juu ya michongoma yote, na juu ya malisho yote.”

Huu ni unabii ambao Mungu alimpa Nabii Isaya ili amweleze Mfalme wa Yuda aliyeitwa Ahazi, endapo akitegemea msaada kutoka kwa Mataifa makubwa na kuacha kumtegemea MUNGU kuwa baadaye yatampata mabaya badala ya mema anayoyatazamia.

Ikumbukwe kuwa Mfalme Ahazi alikumbwa na hofu kubwa baada ya kuona Mataifa mawili (ambayo ni Israeli na Shamu) yamegeuka kinyume naye, yanataka kumpiga na kumtoa katika ufalme..

Na mfalme Ahazi badala ya kumtegemea Mungu, alitaka kwenda kutafuta msaada kutoka kwa mfalme wa Ashuru, na Mungu alimwonya kupitia nabii wake Isaya, kwamba msaada kutoka kwa mataifa ya kigeni hautamsaidia, bali utaleta uharibifu zaidi, Lakini Mfalme Ahazi wa Yuda hakusikia na matokeo yake alikwenda alituma wajumbe kwa Mfalme wa Ashuru, kutaka msaada kwao (soma 2Wafalme 16:7-9)

Ingawa msaada huo ulionekana kama ulileta unafuu kwa Mfalme Ahazi, kwani kweli Mfalme wa Ashuru alikubali kumsaidia na kumwangamiza Mfalme Resini wa Shamu.

Lakini matokeo yake baada ya hapo yalikuwa ni makubwa, kwani Yuda walilazimika kuwa tegemezi kwa Ashuru baada ya hapo, na mfalme Ahazi alilazimika kuonyesha utii kwa mfalme wa Ashuru kwa kufuata taratibu zao za kidini na kisiasa (soma 2Wafalme 16:10-18).

Na Uovu wa ibada za kipagani uliongezeka Yuda mpaka kufikia hatua ya Ahazi kujenga madhabahu ya kipagani mfano wa ile iyokuwepo Dameski, jambo ambalo ni machukizo makubwa kwa MUNGU (rejea 2 Nyakati 28:3).

Katika Isaya 5:8-5, Nabii Isaya aliwaonya kwa Neno la MUNGU kuwa kutegemea Ashuru kungeleta taabu zaidi kwa Yuda badala ya msaada.

Sasa “Inzi walio watokao katika kijito cha Misri” ni nini?, na “Nyuki wa Ashuru”.

Hizi ni lugha zinazowakilisha “uharibifu na magonjwa”

Moja ya kitu kilichoiharibu Misri wakati Farao anapigwa na Bwana ni pamoja na wale Inzi, katika ..

Kutoka 8:24 “Bwana akafanya; wakaja wingi wa mainzi kwa uzito sana, wakaingia nyumbani mwa Farao, na katika nyumba za watumishi wake, tena katika nchi yote ya Misri; nayo nchi iliharibiwa kwa ajili ya wale mainzi”.

Kama vile Inzi walivyoiharibu Misri, (kwa zile kero) vile vile Bwana ataleta kero kubwa kwa watu wa Yuda..
Hali kadhalika Nyuki ni wadudu waumao na wanaofukuza, (Kumbukumbu 1:44) ambao ghasia zake ni zaidi ya zile za nzi, na hapo Bwana anawaonyesha kuwa watafukuzwa kwa maumivu kutoka katika nchi yao..

Mambo hayo yalikuja kutokeo huko mbeleni kama yalivyo, Kwani maovu ya Yuda yalipozidi alikuja Nebukadreza mfalme wa Babeli na kuwaondoa katika nchi yao, kwa maumivu makali kama ya nyuki.
Funzo kuu tulipatalo kutoka katika habari hii, ni kumtegemea MUNGU na si wanadamu, Mfalme Ahazi alimwacha MUNGU wa Israeli na kuwategemea wanadamu, ikawa laana kwake na kwa watu wa YUDA wote.

Bwana atusaidie tumtegemee yeye peke yake wala tusirudi nyuma.
Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Je wazo la Herode kutafuta kumuua mtoto YESU lilitoka wapi?

Wakati Herode anaua watoto kule Bethlehemu baada ya kuzaliwa YESU je roho iliyokuwa ndani yake ilikuwa inatoka wapi?.. Kama ni shetani, je shetani hakujua kama Yusufu na Mariamu wametoka na wameelekea Misri?.


Jibu: Awali ya yote ni muhimu kujua kuwa roho iliyokuwa ndani ya Herode ni ya “shetani” na wala hazikuwa akili zake Herode..Kwasababu kitabu cha Ufunuo kinaonyesha wazi kuwa ni Joka (yaani shetani mwenyewe) ndiye alikuwa anatafuta kumwangamiza Bwana YESU wakati anazaliwa na si Herode (Herode alitumika tu kama chombo)

Ufunuo 12:3 “Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.

4  Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka AKASIMAMA MBELE YA YULE MWANAMKE ALIYE TAYARI KUZAA, ILI AZAAPO, AMLE MTOTO WAKE.

5  Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi”.

Sasa swali kwanini shetani asiahirishe ajenda yake ya kuua watoto Bethlehemu baada ya kujua kuwa mtoto hayupo tena Bethlehemu?..

Kikawaida uwezo wa shetani si kama wa MUNGU.. MUNGU anaweza kufanya pasipo ushirika na yoyote, na anaweza kufanya jambo likabadilika kwa muda mfupi, lakini si shetani..

shetani anaposhindwa kufanikisha jambo lake lolote baya kupitia mapepo wake, huwa anatumia wanadamu.. kwamfano akishindwa kumuua amtu kimazingara, basi anaweza  kutumia mtu/watu kufanikisha adhimio lake hilo,  hivyo anaweza kuweka wazo ndani ya mtu la kuua, na huyo mtu akaanza maandalizi ya mauaji (jambo ambalo linaweza kuchukua muda mrefu) tofauti na hiyo njia ya kwanza ya kimiujiza-ujiza ambayo ni ya haraka tu ikiwa mtu huyo hana ulinzi wowote wa kiMungu.

Lakini njia ya kumtumia mtu kuua inachangamoto kubwa kwa shetani, Kwasababu ni lazima kwanza amwandae huyo mtu (atakayemtumia kuua), pengine amwekee wivu ndani yake au hasira, na pia amshawishi vya kutosha na kumfundisha njia, sasa mpaka yule mtu aelewe na kutenda kama shetani anavyotaka inaweza kuchukua muda,

Na vile vile si rahisi kulitoa wazo ndani ya mtu (alilokwisha kumwekea), na kubadilisha mpango kwa haraka, kwamfano kama alikuwa amemfundisha mtu aue kwa sumu, na akataka ambadilishie wazo hilo amwekee lingine la kumuua kwa kumchoma kisu, haiwezi kuwa ni jambo la haraka, itamgharimu shetani muda mwingine wa kutosha kufuta wazo la kwanza na kupandikiza wazo la pili ndani ya mtu.

Ndio maana utaona baada ya mtoto kukimbizwa Misri, bado wazo lile la ibilisi ndani ya Herode la kumuua mtoto halikutoka, matokeo yake Herode aliendelea na mauaji….hivyo kubadilisha mpango kwa haraka ilikuwa ni ngumu, zilihitajika taarifa zimfikie Herode kwamba mtoto hayupo kakimbilia Misri, na Herode aamini, na kuahirisha wazo lile.

Kwahiyo shetani alishajua mtoto kakimbilia Misri, lakini kulibadilisha wazo kwenye kichwa cha Herode halikuwa jambo jepesi la dakika moja.

Hiyo pia ikifunua kuwa dhambi ndani ya mtu inayo maandalizi, huwa haiji ghafla, ni lazima kwanza shetani apandikize magugu ndani ya mtu ndipo mwisho aitekeleze, Hivyo ni lazima tuikatae dhambi katika msingi wake, Laiti Herode angeikataa dhambi katika msingi wake pale wivu ulipoingia ndani yake, bila shaka asingeendelea na hatua zinazofuta za mauaji, lakini aliporuhusu wazo la ibilisi lichipue ndani yake ndipo akawa kifaa tosha cha ibilisi.

Vile vile Kaini alionywa na MUNGU, juu ya dhambi ya wivu inayochipuka ndani yake, laiti kama angemsikiliza MUNGU asingefikia hatua ya mauaji, lakini alidharau maonyo ya MUNGU na mwisho akawa kifaa cha ibilisi cha mauaji.

Mwanzo  4:6 “Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana? 

7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

8 Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani,Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua”.

Vile vile na sisi ni lazima tuikatae dhambi katika uchanga wake, mawazo mabaya yajapo ni wakati wa kuyakataa kabla hayajatupeleka katika matendo, fikra mbaya zijapo ni wakati wa kuzikataa katika uchanga wake, hasira ijapo, chuki zijapo, uchungu ujapo na mambo mengine yote mabaya ni wakati wa kukataa, kama hayajafikia kukomaa..

Vile vile dhambi ikiisha kukomaa ni ngumu kuiacha, ndio maana ilikuwa ni ngumu shetani kumbadilishia Herode mpango kwa haraka, kwasababu tayari ile dhambi imeshikamana naye.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

YULE JOKA WA ZAMANI.

Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)

CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO:

Print this post

NITAACHAJE DHAMBI?.

Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia, Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa njia zetu (Zab.119:105).

1 Petro 4:1 “Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; KWA MAANA YEYE ALIYETESWA KATIKA MWILI AMEACHANA NA DHAMBI”.

Kumbe KUTESWA KATIKA MWILI ndio kanuni ya KUACHANA NA DHAMBI!

Sasa ni nani aliyewahi kuteswa katika mwili na akaachana na dhambi,ili tuuige mfano wake?..

Huyo si mwingine zaidi ya Bwana wetu YESU KRISTO, yeye aliteswa katika mwili na kuachana na dhambi…

Sasa hakuteswa kwaajili ya dhambi zake kwasababu yeye hakuwahi kufanya dhambi, bali Baba alimtwika dhambi zetu na hivyo akahesabika mwenye dhambi kuliko watu wote…..na akateswa kwaajili ya dhambi hizo (za ulimwengu),

Na baada ya kuteswa alikufa,na baadaye akafufuka bila zile dhambi (huo ni muujiza mkubwa sana), kwani aliziacha zile dhambi zote kaburini.

Warumi 6:10 “Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu”.

Na sisi ili tuachane na dhambi ni lazima tufuate kanuni hiyo hiyo, ya KUTESWA, KUFA na KUFUFUKA.

Lakini kwa kuwa hakuna mwanadamu yoyote anayeweza kutembea katika ile njia ya BWANA YESU asilimia mia moja, yeye Bwana katurahisishia zoezi zima hilo la KUTESWA, KUFA na KUFUFUKA.

Kwamba tunapomwamini na kubeba misalaba yetu, na kuukataa ulimwengu (Hapo ni sawa na KUTESWA)..

Vile vile tunapozama katika yale maji mengi wakati wa ubatizo (Hapo ni sawa tumekufa pamoja naye)

Na tunapoibuka kutoka katika yale maji wakati wa ubatizo (Hapo ni sawa tumefufuka pamoja naye).

Wakolosai 2:12 “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu”.

Na kama hatua hizo tatu (kujikana nafsi na ubatizo) zinalinganishwa kisahihi kabisa na Kuteswa, kufa na kufufuka..basi lile andiko la kwamba “YEYE ALIYETESWA KATIKA MWILI AMEACHANA NA DHAMBI (1Petro 4:1)”.  Linafanya kazi hapa hapa..

Wagalatia 5:24 “Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake”.

Sasa ukiona bado dhambi inakutawala kiasi kwamba uasherati una nguvu juu yako, ulevi una nguvu juu yako, uuaji una nguvu juu yako, uchawi, udui, wivu, husuda na mambo mengine yote yaliyotajwa katika Matendo 5:19-20, ni ishara kuwa bado haujausulibisha mwili wako kwa KRISTO, na hiyo ndio sababu dhambi inakutawala.

Suluhisho ni Kujikana nafsi na kubeba msalaba, kisha kutafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU (Matendo 2:38) na ubatizo wa Roho Mtakatifu.

Ukiyapata mambo hayo matatu dhambi haina nguvu tena juu yako!, kwasababu unakuwa umeifia dhambi..

Warumi 6:2 “Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi?”

Ni sawa na mgonjwa aliyekuwa anasumbuliwa na homa, baada ya kupata dawa, ile homa yote inaondoka…Naam ni hivyo hivyo mtu anayejikana nafsi kweli kweli na kumfuata YESU, anakuwa amemeza kidonge cha kwanza cha matibabu ya dhambi inayomtesa, kidonge cha pili na cha tatu ni ubatizo wa maji mengi na ubatizo wa Roho Mtakatifu.

Warumi 6:10 “Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu

11 Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu

12 Basi, dhambi isitawale ndani ya miili yenu ipatikanayo na mauti, hata mkazitii tamaa zake”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post