USIMFANYIE JEURI ROHO WA NEEMA.

USIMFANYIE JEURI ROHO WA NEEMA.

Kuna hatari kubwa sana kuidharau Neema ya Bwana YESU KRISTO, Katika agano la kale, kule jangwani Mungu alipokuwa anazungumza na wana wa Israeli katika mlima SINAI, Utukufu wa Mungu ulikuwa ni mkubwa kiasi kwamba hata watu wenyewe walikataa kuukaribia ule mlima kwa jinsi ulivyokuwa unatisha, kwa hofu na kwa kutetemeka walifikia hatua ya kumwambia Musa azungumze nao lakini sio Mungu. Mlima ule ulitisha sana hata kwa mnyama yoyote aliyeusogelea ilikuwa ni kifo.

Biblia inasema; katika Waebrania 12:18-25

18 Maana hamkufikilia mlima uwezao kuguswa, uliowaka moto, wala wingu jeusi, na giza, na tufani,

19 na mlio wa baragumu na sauti ya maneno; ambayo wale walioisikia walisihi wasiambiwe neno lo lote lingine;

20 maana hawakuweza kustahimili neno lile lililoamriwa, Hata mnyama akiugusa huo mlima atapigwa kwa mawe.

21 Na hayo yaliyoonekana jinsi yalivyokuwa ya kutisha, hata Musa akasema, Nimeshikwa na hofu na kutetemeka.

22 Bali ninyi mmeufikilia MLIMA SAYUNI, NA MJI WA MUNGU ALIYE HAI, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,

23 mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika,

24 na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili.

25 Angalieni msimkatae yeye anenaye. Maana ikiwa hawakuokoka wale waliomkataa yeye aliyewaonya juu ya nchi, ZAIDI SANA HATUTAOKOKA SISI TUKIJIEPUSHA NA YEYE ATUONYAYE KUTOKA MBINGUNI;”.

Kama biblia inavyosema sisi tulio kwenye AGANO lililo bora la DAMU YA YESU KRISTO, tunaukaribia mlima wa mbinguni(SAYUNI YA MBINGUNI) mbali na wana wa Israeli wao waliukaribia mlima wa duniani(SINAI),.. Ni dhahiri kuwa wale walioukaribia mlima wa mbinguni, ambao maelfu ya malaika wamekusanyika ndio walio karibu zaidi na Mungu kuliko hao wengine.Hivyo hawa wa mbinguni ndio wanapaswa wawe na hofu kubwa zaidi na wawe makini zaidi, kwasababu wapo karibu na Mungu, hivyo kosa moja linaweza likakugharimu mauti ya kiroho.

Na ndio maana biblia inasema 

Wafilipi 2:12b-13 “ UTIMIZENI WOKOVU WENU WENYEWE KWA KUOGOPA NA KUTETEMEKA. 13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.”

Hii tunayoiita NEEMA, ni kweli ni NEEMA lakini sio neema kwa wakati wote, Inapochezewa au kutupiliwa mbali inageuka kuwa laana mbaya kuliko zote. Biblia inasema hali ya mtu Yule aliyeidharau hali yake ya mwisho inakuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.

2Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.

21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.

22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni.”

Pale unapojiita mkristo halafu bado unakwenda kwa waganga ili upate kitu Fulani, ukijifariji kwamba utatubu tu siku moja, kwasababu neema bado ipo!! Usidanganyike NEEMA haifanya kazi kwa namna hiyo shetani anataka ufikirie hivyo ili ukumbane na mauti ya kiroho kutoka kwa Mungu mwenyewe.

Unapojiita mkristo halafu bado ni mwasherati, mlevi, mwabudu sanamu, na huku unafahamu kabisa hayo uyafanyayo sio sawa, ukijifariji utatubu, kwasababu tunaishi chini ya NEEMA, biblia inasema ingekuwa heri kwako kama usingeijua ile haki, Ndugu utaangukia hukumu ya kifo cha kiroho,na ukishafikia hiyo hatua, ndio pale injili kwako inageuka kuwa upuuzi tu masikioni mwako au hadithi za kutunga, ROHO MTAKATIFU anakuacha na kuondoka, na ile hali ya kuugua ndani juu dhambi inaondoka kwako, kutenda dhambi kunageuka kuwa ni kitu cha kawaida, hapo hata uhubiriweje injili huwezi kugeuka unasubiria moto wa jehanum.

Shetani ndiyo agenda yake sasa hivi, kuwapofusha watu na hili Neno “tunaishi chini ya neema” na kusema Mungu ataturehemu tu! Hata tuwe watenda dhambi.. Kumbuka Neema ina pande mbili, kwa Yule anayeikubali ndio italeta manufaa chanya kwake, lakini kwa Yule anayeidharau na kuitupilia mbali inageuka kuwa LAANI kubwa mno.

Waebrania 10:26-29 “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, HAIBAKI TENA DHABIHU KWA AJILI YA DHAMBI;

27 BALI KUNA KUITAZAMIA HUKUMU YENYE KUTISHA, NA UKALI WA MOTO ULIO TAYARI KUWALA WAO WAPINGAO.

28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni KITU OVYO, NA KUMFANYIA JEURI ROHO WA NEEMA?”.

Unaona hapo usitende dhambi za makusudi ukidhani neema itaendelea kudumu siku zote maishani mwako, Ndugu huu ni wakati wa kujitazama tena maisha yako ni wapi haujakaa sawa, unalega lega au vuguvugu. Fanya bidii usimame imara angali bado Roho wa NEEMA analia ndani yako uache dhambi, fanya hima usimfanyie jeuri kabla haujachelewa, kwa maana wakati wa wokovu uliokubaliwa ni sasa.

Tubu mgeukie Kristo aliye mkuu wa uzima wako, naye ni mwaminifu atakuosha na kukupa uzima wa milele.

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Kwa mawasiliano, maombi/ushauri/ubatizo/ whatsapp: Namba zetu ni hizi: +255693036618/ +255789001312


Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

USIMFANYIE JEURI ROHO WA NEEMA.

Je Malaika Mikaeli ndiye Yesu mwenyewe?

HABARI ILE YA PILATO KUCHANGANYA ZILE DAMU ZA WAYAHUDI NA PAMOJA NA DHABIHU ZAO,(LUKA 13) ILIHUSU NINI?


Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
JEAN PAUL NDUWARUGIRA
5 months ago

Join

REUBEN PINDO SAGUDA
REUBEN PINDO SAGUDA
3 years ago

Kwaimani yangu Mungu hakika nawabariki azidi kuwafunulia zaidi kwa maana nimejifuza masomo yenu tungu mwaka jana sasa wakati huu.