Pale unaposema leo nimeamua kuwa Mkristo nimeamua kumfuata Mungu kwa moyo wangu wote, pale unaposema maisha yangu ya kale basi, hapo ni sawa na umemwita Mungu aje kuyaongoza maisha yako kuanzia huo wakati na kuendelea, au kwa lugha ki-kibiblia tunasema umeliitia jina la Mungu lije kukuokoa, lakini pale unaposema Nimeokoka, mimi ni mkristo halafu, unaendelea kuyafanya yale yale uliyoyaacha kule nyuma, unaendelea kuiba,unazidi kuzini, unatazama pornography, unasengenya n.k. Hapo ni sawa kabisa na umemdhahaki Mungu kwamba ulimwita akuokoe na kumbe haupo tayari kuokolewa, Hapo umelitaja JINA LA MUNGU wako bure!.. Ni heri usingedhubutu kuujaribu wokovu kabisa maishani mwako ..