Tunajifunza nini hapo?…kuna watu watatumiwa na shetani kutujaribu, hususani wanaotumia biblia..pengine ni marafiki zetu au ndugu zetu, na kwasababu Neno la Mungu linakaa ndani yetu, tunazitambua fikra za shetani ndani yao..Na mambo wanayofanya ukaona kabisa yanamchukiza Mungu na Mungu kawakasirikia, sasa huo sio wakati wa kupiga maadui yako!! Sio wakati kusema walaaniwe maadui zangu, wafe maadui zangu, waanguke!! Hapana! Biblia haitufundishi hivyo hata kidogo…inatufundisha kwenda kwenye magoti kutubu kwa ajili yao, kuwaombea msamaha, kulia hata ikiwezekana kutoa sadaka kwa ajili yao…hivyo ndivyo Bwana naye atakavyogeuza UTEKA WETU! Ndugu jitenge na injili za kupiga maadui si za kimaandiko hata kidogo…ukifanya hivyo Mungu hatageuza uteka wako hata kidogo. Tujifunze kwa Ayubu hakuna mtu aliyeumizwa moyo kama Ayubu, kapata msiba na wakati huo huo rafiki zake wanamwambia ana dhambi nyingi…inaumiza kiasi gani, lakini hakuwalaani bali aliwaombea..