Lakini biblia inatuambia YESU KRISTO, Ndiye Mfalme ambaye atakuja kuubatilisha ufalme wote wa hii dunia na kisha atauweka UFALME mpya wa milele usioasika, Biblia inasema yeye atakuwa ni MFALME WA WAFALME, na BWANA WA MABWANA. Ataitawala dunia yote kwa fimbo ya chuma, pale dunia wakati huo itakaporejeshwa katika hali yake ya mwanzo ya uzuri, basi chini yake kutakuwa na wafalme wengi na makuhani wengi, na mabwana wengi sana. Kumbuka wakati huo bahari haitakuwepo, kwani tunajua bahari imechukua asilimia 75% ya dunia, sasa bahari ikiondolewa unaweza ukaona kama ni mabara duniani yatakuwa mangapi?, kadhalika majangwa nayo hayatokuwepo, na wala hakutakuwa na sehemu yoyote ya dunia itakayokuwa ukiwa, sehemu zote zitakuwa zimejaa utukufu wa Mungu na wanadamu.