Wewe ni mkristo lakini unakuwa mtu wa kusengenya, kila wakati kuzungumzia watu wengine kwa ubaya, kuchukua taarifa za mtu fulani kupeleka kwa mtu fulani, kutoa siri za mtu fulani na kumfunulia mwingine..Kila wakati unakuwa unatoa maneno yasiyokuwa na maana mdomoni, unatoa maneno ya mizaha ambayo ni aibu hata kwa mkristo kutamka, unatoa maneno ya uchochezi na fitna, unatamka matusi hata haionekani tofauti yako na mtu asiyeamini, kila wakati kuchangia mada zisizokuwa na maana, Sasa hapo hata kama unafanya ibada nzuri kiasi gani mbele za Mungu, au unahubiri kiasi gani, au unasaidia maskini kiasi gani, Dini yako ni bure mbele za Mungu..Ni kwasababu gani?..ni kwasababu Umeshindwa kuutawala usukani wa maisha yako ya kikristo, na umempa mwingine autawale naye ni shetani.