BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO”;

Mwishoni mwa mstari huo wa 18 biblia inatuambia ‘”bali mjazwe Roho”.. Hili Ni neno endelevu, Sasa kumbuka Mtume Paulo alipokuwa anazungumza na kanisa hili la Efeso Alijua kabisa walishapokea Roho Mtakatifu tangu zamani walipoamini, na ndio maana likawa kanisa kubwa lilolitwa Efeso, Lakini hiyo haikumfanya mtume Paulo aone wamefika, bali aliwaasa siku baada ya siku wajazwe Roho, kwasababu alijua kuwa Roho anaweza kuzimishwa ndani ya mtu, hali kadhalika pia anaweza kujaa na kupungua kwa jinsi mtu atakavyokuwa makini au mzembe katika wokovu wake.

Hata sisi wakristo wa zama hizi ambazo uovu wetu ni mkubwa kuliko ule wa kanisa la Efeso, kusema tu, tumeokoka, au tumepokea Roho Mtakatifu, na huku bado uhusiano wetu na Mungu haueleweki haitoshi kutufikisha mbinguni, bali tunapaswa tujazwe Roho Mtakatifu siku baada ya siku mpaka siku ile ya Unyakuo itakapotukuta..

Kwasababu tukipuuzia jambo hilo, tutafananishwa na wale wanawali wapumbavu tunaowasoma katika Mathayo 25 ambao walikuwa wanamngojea Bwana wao lakini hawakuwa na mafuta ya kutosha ya kuwafikisha hadi ule wakati wa kumlaki Bwana wao.. matokeo yake saa ile ilipofika ya Bwana wao kutokea, ndio wakajishtukia kuwa taa zao zinakwenda kuzima…Sasa wakati wanakwenda kununua huku nyuma tayari Bwana arusi ameshawasili na kuwachukua wale aliowakuta wapo tayari na kuingia nao karamuni..Na wale wengine waliokwenda kuchukua mafuta waliporudi wakajikuta wameshachelewa.. Hasara ikawa ni kwao na taabu yao yote ya kumngojea Bwana ikiwa ni bure.. Japokuwa nao pia walikuwa ni wanawali (mabikira) yaani wameokoka, ambao wanamngojea tu Bwana wao kwa saburi kama wale wengine.. Lakini kwasababu ya kupuuzia jambo la msingi la mafuta katika chupa zao ikawafanya wakose karamu..

Siku zote mafuta yanafananishwa na Roho Mtakatifu..Tunapompokea Roho Mtakatifu siku zile za kwanza tulipookoka, tulipokea mafuta ya kuwasha tu vyombo vyetu vya usafari..Lakini tukiridhika na yale tu, hatutafika mbali. Ndugu ili kukivuka hichi kipindi cha Uovu uliokirithiri duniani sasa..Tunapaswa tuendelee kujazwa Roho..

Pengine utauliza nifanye nini ili nijazwe Roho Mtakatifu?

Roho Mtakatifu anaweza kuendelea kujaa ndani yetu, kwa walau mambo makuu manne.

  1. Kwa kuomba;

Biblia inasema, Luka 13:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”

Ukiwa mtu wa kuomba, na kukataa uvivu kwa kutokusali walau saa moja kwa siku, ndivyo utavyojiongezea mafuta yako ya rohoni na hivyo Roho Mtakatifu atapata wigo mpana wa kuyatawala maisha yako siku baada ya siku.

    2.  Kwa kujifunza kwa bidii Neno la Mungu..; Neno ndio chakula cha uzima wa mtu. Usipojibidiisha kujifunza Neno la Mungu, kutafuta habari za uzima, usidhani kuwa Roho Mtakatifu atapata nafasi ya kukufundisha kitu chochote ndani yako. Kwasababu Mungu yupo katika Neno lake(Sauti ya Mungu ni Neno lake). Ukiwa umeokoka, halafu unaona uvivu kujifunza Biblia basi ujue Roho wa Mungu ameshazimika ndani yako kitambo..Na hivyo hata wakati wa unyakuo utakapofika utafananishwa na wale wanawali wapumbavu.

     3.  Kaa mbali na uovu; Siku zote dhambi inavutia, lakini mwisho wake ni mbaya..Tunapoivumilia dhambi katika maisha yetu ndivyo Mungu anavyouficha uso wake. Na matokeo yake Roho Mtakatifu anazimika, au anaondoka kabisa ndani yetu.(Isaya 59:2)

    4.  Tangaza habari njema: Ukiwafundisha wengine, na wewe hapo hapo Roho wa Mungu anakufundisha, ukiwafungulia wengine hazina ya maneno ya uzima, Roho Mtakatifu anapata nafasi ya kukufunulia wewe Zaidi na kukutumia, ili kuwaokoa watu wake..Na hivyo ni sharti atakaujaza tu Roho wake, kwasababu siku zote unafanya kazi yake..Na hapo utakuwa na nafasi nyingine ya kuwa karibu na yeye.

Hivyo tusiridhike tu, na hali za kiroho tulizopo, tukajificha nyuma ya kivuli cha Neno nimeokoka..Tunapaswa tujiulize Je! Mafuta tuliyonayo yanatutosha mpaka wakati wa kuja kwa Bwana? Kama sivyo basi huu ndio wakati wa kuzitengeneza upya taa zetu..kwa kuhakikisha kuwa kila siku Roho Mtakatifu anapata nafasi maishani mwetu..Ili ile siku ambayo hatujui ni lini itakapotujilia kwa ghafla basi tuwe na uhakika kuwa UNYAKUO hautatupita.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

RABI, UNAKAA WAPI?

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments