JIRANI YANGU NI NANI?

JIRANI YANGU NI NANI?

Amri ya kwanza tuliyopewa na Bwana, ni kumpenda yeye kwa mioyo yetu yote, kwa nguvu zetu zote na kwa akili zetu zote, na nyingine inayofanana na hiyo ni kupendana sisi kwa sisi. Kila mmoja kumchukulia mwenzake bora kama nafsi yake mwenyewe. Lakini mtu mmoja alimuuliza Bwana, jirani yangu ni nani…akiwa na maana kuwa nini maana ya ujirani?.

Ndipo Bwana akatoa mfano ambao tunausoma katika Luka 10.

Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?

26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?

27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.

28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.

29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, NA JIRANI YANGU NI NANI?

30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.

31 Kwa nasibu KUHANI mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.

32 Na MLAWI vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.

33 Lakini, MSAMARIA mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,

34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.

35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.

36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni yupi aliyekuwa jirani yake yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?

37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.

 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, NA JIRANI YANGU NI NANI?  30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang'anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.

Katika mfano huu tunajifunza, makundi matatu ya watu, wa kwanza ni KUHANI, wa pili MLAWI, na watatu ni MSAMARIA.

Kama tunavyofahamu kuhani ni mtu aliyekuwa ametiwa mafuta na Mungu kuhudumu katika nyumba ya Mungu, ni mtu aliyemkaribia Mungu sikuzote, kwa kazi ya kufukiza uvumba na kufanya upatanisho kwa makosa ya watu wa Mungu, katika patakatifu. Ni mtu mwenye bidii ya kumtumikia Mungu usiku na mchana, kiufupi ni mtu aliyeheshimika mbele za Mungu na mbele za wanadamu. Lakini ilipokuja katika jambo dogo kama hili, aliikosa shabaha, pengine alijua kumtumikia Mungu ni hekaluni tu na kwenye masinagogi! mahali penye mikusanyiko mikubwa ya watu wengi. Hakufanya vibaya, ni kwasababu hakupata ufunuo wa neno “JIRANI HASA NI NINI?”. Yeye alidhani kuwa kule aendako ndipo majirani zake walipo.

Kadhalika na yule Mlawi nae, kumbuka mlawi naye anafanya kazi zinazofanana na za kikuhani katika nyumba ya Mungu, isipokuwa yeye haingii katika patakatifu pa Mungu, tofauti ya Mlawi na Kuhani ni kwamba Kuhani yeye ni Mlawi aliyeteuliwa kutenda kazi katika patakatifu pa Mungu, hivyo kwa cheo huwa anaanza Mlawi, kisha kuhani, na mwisho kabisa ni Kuhani Mkuu. Sasa huyu naye alipomuona yule mtu mwenye majeraha, pengine huruma ilimjia kidogo, lakini alipogundua kuwa hizo sio kazi za Walawi, akaamua naye kupita kando. Naye pia hakufanya kosa, ni kwasababu tu hakupata ufunuo wa “JIRANI HASA NI NANI?”.

Lakini tunamsoma mwingine wa mwisho ambaye ni MSAMARIA. Kumbuka katika Israeli kulikuwa na Eneo linaloitwa Samaria na watu waliokuwa wanaishi kule walikuwa ni watu ambao sio wayahudi kamili, ni kama mchanganyiko wa watu wa mataifa na wayahudi, hivyo walikuwa nao wanaishika torati ya Musa japo wayahudi walikuwa hawawaatambui wala kuchangamana nao. Ni watu ambao hawakuruhusiwa kuingia au kuhudumu katika nyumba ya Mungu kwa namna yoyote ile, ni kama watu-baki au najisi mbele za wayahudi lakini walikuwa wanamjua Mungu na baadhi yao wanamcha.

Hivyo huyu Msamaria naye alipokatiza katika njia ile. alimuona yule mtu mwenye majeraha na “KUMUHURUMIA”, na pasipo kujali yule mtu ni wa namna gani, au ni kwasababu gani kapata hayo matatizo, yule msamaria akaghairi yote, pengine shughuli zake za kumwingizia kipato, ili tu aokoe maisha ya yule mtu kwa ule wakati. Hivyo kama tunavyosoma akayafunga majeraha yake, na kuyatia MAFUTA NA DIVAI. Kisha akaona hiyo tu haitoshi akampeleka hospitali, kwa gharama zake mwenyewe akamuuguza mpaka alipopona.

Na ndipo baada ya mfano huo Bwana Yesu akamuuliza yule mwanasheria ni yupi aliye JIRANI YAKE?. Naye akajibu; NI yule aliye MUHURUMIA(Msamaria).

Na sisi tunajifunza nini hapo?.

Katika hali tulizopo ni rahisi kudhani kuwa kuhudumu katikati ya umati mkubwa ndio chachu ya kudhani Mungu anakuona una upendo kwa jirani zako! lakini nini maana hasa ya kuwa JIRANI kwa mwenzako?.. Tukijifunza katika hiyo mifano hapo tunaona ni yule aliyekaribu sana na wewe, na unaona anahitaji msaada wa haraka sana kutoka kwako huyo ndiye jirani yako. Yule Kuhani na yule Mlawi walidhani umati mkubwa wa watu wanaowatumikia kule kila siku ndio wanaweza wakawa majirani zao. Lakini mtu alipotokea mbele yao ghafla mwenye uhitaji mkubwa na wa haraka kuliko wale, wakapita kando. Na mtu asiyemjua Mungu sana ndiye akaja kumsaidia.

Vivyo hivyo na sisi hatuhitaji tuwe wahubiri wakubwa, tunahubiria mamilioni ya watu ndipo tuonekana tuna upendo mkubwa kwa ndugu zetu mbele za Mungu.. Hauhitaji kwenda masafa ya mbali kuhubiri ukidhani kuwa hichi ni kipimo cha kuonyesha kuwa una upendo mkubwa kwa ndugu zako wakati jirani yako hapo karibu nawe yupo katika hali ya dhambi, na hamjui huyo Mungu unayekwenda kumuhubiri ulaya.

Unao rafiki zako ni makahaba, au walevi au waabudu sanamu. unawaacha waangamie unasema mimi nataka nikahubiri makanisani na kwenye makongamano tu…unachofanya sio dhambi lakini bado hujaonyesha ule upendo kwa jirani yako kama Mungu anavyotaka.

Lakini yule msamaria alimpaka mafuta na divai na kufunga majeraha yake, na baadaye akampeleka kwa matabibu wamtunze. Kadhalika na sisi tunapaswa tuwatazame ndugu zetu wote waliokaribu na sisi sana ambao wapo katika dhambi wamepigwa na kutiwa majeraha na shetani, tunapaswa kuwatia mafuta na divai, kwa kuwahubiria habari njema ili wapokee Roho Mtakatifu kisha wakishapokea Roho ndipo tuwapeleke kwa viongozi wa kiroho wawakuze. Na kwa kufanya hivyo Tutakuwa tumekidhi vigezo vya kuwapenda jirani zetu kama nafsi zetu. Japo mbele za wanadamu unaweza ukaonekana hujafanya kitu lakini mbele za Mungu, ni mtu mwenye maana sana.

Mungu akubariki.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

JE! BIKIRA MARIA NI MALKIA WA MBINGUNI?

WALE WATU AMBAO SHETANI ATAWADANGANYA KATIKA MWISHO WA UTAWALA WA MIAKA 1000, WATATOKA WAPI, ANGALI TUNAJUA UTAWALA ULE UTAKUWA UMEJAWA NA WATAKATIFU TU?

Rushwa inapofushaje macho?


Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
5 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Frank Shoo
Frank Shoo
1 year ago

Amina watumishi. Kazi yenu ni njema sana.

Alex
Alex
1 year ago

Mungu awabariki Walimu wote wa Wingu la mashahidi.
Nabarikiwa sana nimefaham mambo mengi nisiyoyajua sasa najua.

Gibson msuva
Gibson msuva
2 years ago

Hisia… Feeling ni msukumo unaotoka ndan juu ya jamb Fulani.. waweza kuwa mzur au mbaya….

Christian jakoracha
Christian jakoracha
3 years ago

Ningependa kujua maana ya neno hisia kwa undani zaidi