Hichi ni kipindi cha dhiki za kitambo, ambacho hakikwepeki kama kweli utakuwa ni mtoto wa Mungu, ndio hapo utaona mtu akiamua kuchukua uamuzi wa kumfuata Kristo, ghafla vikwazo vinaanza kuibuka, pengine ndugu wanaanza kukupiga vita, au kujitenga na wewe, pengine hali yako ya kiuchumi inaanza kuyumba, wengine inafikia hatua hata ya kukosa chakula, wengine pindi tu wanapoamini wanakumbana na misiba kufiwa na wazazi au watoto, wengine magonjwa ya ajabu yanazuka, wengine wanafukuzwa kazi kutokana na imani yao, wengine wanaingizwa magerezani, wengine wanaishia kupigwa, wengine jamii inayowazunguka inakuwa kama mwiba katika maisha yao.
Wengine wanadharauliwa, heshima yao inashuka hata watoto wadogo wanawadharau kisa tu kaamua kuuweka msimamo wake kwa YESU. kiasi cha kwamba mtu anaweza akafikiria yeye ni mtu wa bahati mbaya au ana mikosi, Lakini si kweli, hapo ujue unajaribiwa kama utaiacha ile imani au la.