Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 23:27 “Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

28 Naam, huotea kama mnyang’anyi; Huwaongeza wenye hila katika wanadamu”.

JIBU: Kahaba ni mwanamke anayezini na mtu ambaye si mume wake, ni mwanamke mwenye mahusiano na wanaume wengi, akiwa na lengo la aidha kujiburudisha au kuharibu maisha ya wengine, huyu huwa hatafutwi bali yeye ndio anatafuta, kutimiza makusudi yake maalumu.

Lakini Malaya kibiblia ni mwanamke anayefanya uasherati kwa lengo la kujipatia fedha , au kupata upendeleo fulani, au kukubaliwa, mara nyingi huwa hajaolewa. Vilevile mwanamke yeyote anayejiamulia tu kufanya uasherati na mtu yeyote pale anapofuatwa, bila kujali chochote huyo pia ni Malaya.

Sasa Biblia inatuambia wote, ni hatari hakuna hata mmoja mwenye afadhali, ikiwa umenaswa nao.  Kwamfano ukizini na kahaba, rohoni ni kama unazama kwenye shimo. Na heri lingekuwa ni shimo tu, bali biblia inasema ni shimo refu, ikiwa na maana mtu akizama, hana matumaini tena ya kutoka huko. Ndio milele anapotea.

Vilevile anasema Malaya ni Rima jembamba. Rima ni shimo maalumu ambalo linachimbwa kwa ajili ya kunasa kitu, hususani wanyama. Zamani watu walipotaka kuwakamata wanyama wakali kama vile simba au dumu, walikuwa hawawapigi sindano za usingizi kama wanavyofanya sasa hivi,hapana, bali walikuwa wanachimba mashimo marefu sana, na membamba kisha, kwa juu wanayafunika na majani, kiasi kwamba mnyama akipita pale hawezi jua kama chini kuna shimo. Na akishasogea tu pale anatumbukia na kwenda chini sana, baadaye wanakuja kumkamata na kumtoa kirahisi.

Hivyo Malaya naye ndio vivyo hivyo, ukijiingiza kwenye mitego yao, unanasika na kutoka kamwe hutaweza. Soma.

Mithali 22: 14 “Kinywa cha malaya ni shimo refu; Anayechukiwa na Bwana atatumbukia ndani yake”.

Sasa tahadhari hii hawapewi wanaume tu, bali pia na wanawake..Kibiblia, kahaba na Malaya inamaanisha jinsia zote. Wewe ni kijana au binti, ikimbie zinaa kama vile biblia inavyosema katika 1Wakorintho 6:18… Kwasababu dhambi nyingine zote mtu unatenda nje ya mwili wako, lakini zinaa ni juu ya mwili wako mwenyewe.

Na ni dhambi inayowaangusha wengi sana, na inayoshusha viwango vya kiroho kwa kasi sana. Kiasi kwamba kitendo kimoja tu kama hicho kinaweza kukufanya uachwe na Mungu milele. Licha tu ya kuachwa na Mungu, pia yapo magonjwa hatari kama vile Ukimwi, jambo ambalo wengi hawafahamu, ni kuwa ukimwi ni PEPO, kwamfano inawezekana kabisa watu wawili wakakutana   wasiwe na maambukizi, lakini kwasababu kile kitendo kinahasisiwa na pepo la uzinzi, moja kwa moja linawavaa wote, na saa hiyo kila mmoja anapata UKIMWI, baadaye wakijiuliza  wametolea wapi, hawajui. Ndivyo ilivyokuwa kwa watu wa kwanza walioupata huo ugonjwa, hawakuambukizwa na mtu bali lilikuwa ni PEPO liliowavaa.

Hivyo kuwa makini sana, biblia inaposema ni Shimo refu na rima jembamba, inamaanisha kweli. Ukinasika usidhani ni rahisi kutoka. Hizo ni tahadhari kwetu. Lakini ukimpa Yesu maisha yako, atakupa uwezo wa kipekee wa kuweza kuvishinda vishawishi hivyo vyote. Uwezo huo hawezi kutoa mtu yeyote, zaidi ya Yesu Kristo tu peke yake. Watu wa ushauri nasaha, hawawezi kukufanya uushinde uzinzi, Madkatari hawawezi, Bali Yesu tu peke yake. Hivyo ukimwamini, utakusaidia.

Na kumwamini kunakuja kwa kutubu dhambi zako zote, kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha kukubali kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa na kwa maji mengi, na yeye mwenyewe kuanzia huo wakati atakushushia kipawa chake cha Roho wake Mtakatifu kukusaidia kuweza kuyashinda majaribu yote, kama yeye alivyoweza kuyashinda.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments