Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

Mungu ni mmoja tu, lakini katika umoja wake amekuwa akijifunua katika majina mengi, kulingana na  uweza wake alionao, au majira Fulani yaliyopita, au matukio ya namna tofauti tofauti  yaliyotokea. Ni sawa, ni raisi Fulani aitwe JOHN, lakini huyo huyo anaweza akaitwa baba sehemu fulani, akaitwa mjomba sehemu nyingine , mhandisi kwa watu fulani, amiri jeshi mkuu eneo Fulani, babu sehemu nyingine n.k.

Unaona utaona vyeo vyote hivyo vimekuja aidha kulingana na wakati, au matukio, au nafasi aliyopo au ujuzi alionao n.k. Na vivyo hivyo Mungu wetu , alijifunua katika  majina mengi, ambayo leo hii tutayatazama kwa ufupi.

ELOHIMU: Mungu mwenye uweza, muumbaji  wa milele, mwenye nguvu (Mwanzo 1: 1, 17:7, Yeremia 31:33)

ADONAI: Mungu Mwenye enzi yote,kimbilio imara Mwa 15:2‐8, Kut 6:2‐3

EL-ELYONI:  Mungu Aliye juu zaidi ‐Mwa14:18, Dan 4:34

YEHOVA-RAFA: Mungu-Atuponyaye. (Kutoka 15:26.).

YEHOVA EL – SHADAI: Mungu Ututoshelezaye (Mwanzo 17:1)

YEHOVA-NISI: Mungu ni Bendera yetu (Berani ya vita) (Kutoka 17:13-16).

YEHOVA-YIRE: Mungu atupaye (Mwanzo 22:14)..

YEHOVA-ROHI: Bwana ndiye mchungaji wangu (Zab 23)

YEHOVA-MEKADISHKEMU: Bwana atutakasaye (Kutoka 31:13)

YEHOVAH SABAOTHI: Bwana wa Majeshi (1 Samweli 1:3)

YEHOVA SHAMA: Bwana Yupo Hapa (Ezekiel 48:35).

YEHOVA EL-OHEENU: Bwana Mungu Wetu (Zaburi 99:5,8,9)

YEHOVA SHALOM: Bwana ni Amani Yangu (Waamuzi 6:24)

YEHOVA TSIDKEMU: Bwana ni Haki Yetu (Yeremia 23:6)

YEHOVA OLAMU: Mungu wa milele Zaburi 90:1-3

YEHOVA  EL- GIBBORI: Mungu Mwenye Nguvu ( Isaya 9:6-9)

YE-SHUA (YESU): Mungu utuokoaye.(Mathayo 1:21 )

Jina Hili la YESU ndio jina tulilonalo mpaka sasa. Kwa kupitia hili ndio tunapata wokovu, kwa jina hili ndio tunamshinda adui, kwa jina hili ndilo tunapata Baraka, na kwa jina hili ndio tunaishi.

Lakini biblia inatuonyesha pia jina hili sio la kudumu, Upo wakati Kristo atakuja na jina jipya,(Ufunuo 19:12 ) jina hilo wakati huo litakuwa sio la Ukombozi tena, sio la kurehemu tena, bali litakuwa ni jina la kifalme. Na ndio maana wakati huu ambao angali bado neema ipo, usiruhusu, ikupite ikiwa wewe ni bado mwenye dhambi, Leo hii Kristo bado yupo kama kuhani mkuu akitupatanisha sisi na Mungu, ikiwa na maana kuwa mlango wa rehema bado upo wazi kwa kila mtu atakayetaka kuuingia, Lakini hautakuwa wazi sikuzote. Kwani dalili za kurudi kwa Yesu mara ya pili zimeshatimia zote, tunachongojea ni unyakuo tu.

Ikiwa upo tayari leo kumpa Yesu maisha yako leo ayaokoe basi huo utakuwa ni uamuzi wa busara sana kwako, Hivyo fungua hapa, kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
James
James
6 months ago

Asante kwa maubiri