WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia.

Leo nataka tujifunze umuhimu wa kuchunguza mambo, kwani  tusipokuwa watu wa kuchunguza mambo basi tunaweza tusiuelewe uweza wa Mungu.

Asilimia kubwa ya watu wanaobarikiwa hawajui kuwa mafanikio yao ni kutokana na maombi ya watu wengine (ambao wanawaombea wao pasipo kujua), hivyo ni muhimu sana kufikiri wakati wa kufanikiwa.

Hebu tujifunze katika ile habari ya Kana ya Galilaya pale Bwana Yesu alipofanya muujiza wake wa kwanza wa kugeuza maji kuwa divai.

Maandiko yanasema baada ya Bwana Yesu kubadili yale maji kuwa divai, yule Mkuu wa meza, aliyeteuliwa kuandaa  vinywaji vya wageni wa kawaida na mgeni rasmi, hakujua kama ile divai mpya imetoka kwa Bwana, badala yake alidhani mwenye sherehe ndiye aliyeinunua, na ndipo akaenda kumfuata mwenye sherehe (Bwana harusi) na kumpongeza akidhani kuwa yeye ndiye kainunua ile divai mpya na kuwapa watu wote wanywe.

Na yule Bwana harusi naye akashangaa kupewa sifa ambazo si zake, huenda na yeye akadhani kuna mtu tu katikati ya sherehe kajitokeza na kujitolea kununua divai mpya ili kuimeza aibu.. kwamaana divai kuisha katikati ya sherehe na bado kuna watu wa muhimu hawajapata, ilikuwa ni aibu kubwa sana kwa wenye sherehe. Hivyo mpaka mwisho wa sherehe ni wachache sana ndio waliojua siri ya ile divai, kuwa na Bwana Yesu ndiye aliyeitoa.

Tusome,

Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.

2  Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.

3  Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.

4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia.

5  Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni.

6  Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu.

7  Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu.

8  Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka.

9  Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji), yule mkuu wa meza alimwita bwana arusi,

10  akamwambia, Kila mtu kwanza huandaa divai iliyo njema; hata watu wakiisha kunywa sana ndipo huleta iliyo dhaifu; wewe umeiweka divai iliyo njema hata sasa”.

 Sasa nataka tuone nyuma ya Baraka hizo alikuwa nani?, Nyuma ya muujiza huo alikuwa nani, na nyuma ya aliyetoa aibu alikuwa ni nani?.. kisha na sisi tutapata akili wakati wa kufanikiwa.

MWOMBAJI/ WAOMBAJI.

Kulipoonekana tatizo, Marimu alienda kumwomba Bwana na kumsihi sana. Huyu ndiye aliyekuwa mwanzo wa muujiza wa divai. Kama sio Mariamu watu wangeabika kwenye sherehe hata kama sherehe hiyo Kristo alikuwepo ndani.

Vile vile hata leo, ukiona jambo Fulani la heri limetokea mbele yako lililoziba aibu yako, hebu tafakari sana, usijivune wala usikimbilie kusema wewe ni mwenye bahati, huna bahati yoyote, hayo ni matokeo ya wengine kuomba kwaajili yako..haijalishi Kristo yupo na wewe.. Hata katika ile harusi Kristo alikuwepo ndani, alikuwa ni mwalikwa, lakini bado kama pasingekuwepo mwombaji, hakuna kitu kingefanyika.

Ukiona umebarikiwa kwa jambo Fulani au mambo yako fulani fulani yameenda sawa usikimbilie kujisifu, wala kujivuna, kwamba una bahati!!…fahamu kuwa hayo ni matokeo ya wengine kuomba kwaajili yako, na hao huenda unawajua au huwajui.

Mtoto ukifanikiwa jua wakati mwingine ni matokeo ya maombi ya wazazi wako na si kwasababu wewe una akili sana au una ujanja mwingi, kijana ukifanikiwa jua ni matokeo ya maombi ya ndugu zako, au wapendwa wenzako wanaokesha kwaajili yako pasipo wewe kujua.

Unapoona unapiga hatua kimaisha au kiroho, fahamu kuwa ni matokeo ya wanaokuongoza kiroho kukuombea, wala usidhani ni kwa nguvu zako au una bahati..

Waebrania 13:17  “Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi”

Ukilifahamu hili siku zote utakuwa mnyenyekevu na kumshukuru Mungu kwa kila jambo na pia kufikiri sana kuwaheshimu wanaokuombea na hata wewe kutenga muda kuwaombea!.. Laiti yule mkuu wa Meza na yule Bwana arusi wangejua kitu Mariamu alichowafanyia, kwenda kuwaombea kwa Bwana wangeshangaa sana, na kunyenyekea sana.

Laiti ungejua mambo watu wanayomwambia Bwana kuhusu wewe, usingebaki kama ulivyo..

Amani ya familia yako, Amani ya jamii yako, Amani ya nchi yako, ni matokeo ya maombi ya watu wengine wa Mungu wanaolia mbele zake usiku na mchana.. wala si kwasababu nyingine?, kama si hao ni kitambo sana mambo ya ulimwengu yangeshaharibika..(2Thesalonike 2:7).

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?.

Je! Mwendo wa Sabato ulikuwaje kibiblia?(Matendo 1:12)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments