“Lakini nina ubatizo unipasao kubatiziwa” (Luka 12:50) Ni ubatizo gani huo?.

by Admin | 23 June 2022 08:46 pm06

Jibu: Tusome,

Luka 12:49 “Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi?

50 LAKINI NINA UBATIZO UNIPASAO KUBATIZIWA, nami nina dhiki kama nini hata utimizwe!”

Ubatizo Bwana Yesu aliokuwa anaumaanisha hapo, ni kile kitendo cha  KUZIKWA na KUFUFUKA kwake. Kwasababu maana yenyewe ya Neno ubatizo ni KUZIKWA.

Hivyo kwa kupitia mauti ya Bwana Yesu, Deni la dhambi zetu limefutwa/LIMEZIKWA. Na kama vile alivyofufuka katika upya na utukufu, pasipo mzigo wa dhambi zetu, vile vile na sisi tunapomwamini yeye na kubatizwa kwa njia ya maji, kama ishara ya kuakisi ubatizo wake yeye (wa kuzikwa na kufufuka kwake) tunakuwa tunakufa kwa habari ya dhambi na tunafufuka katika upya.

Wakolosai 2:12 “MKAZIKWA PAMOJA NAYE KATIKA UBATIZO; NA KATIKA HUO MKAFUFULIWA PAMOJA NAYE, KWA KUZIAMINI NGUVU ZA MUNGU ALIYEMFUFUA KATIKA WAFU.

13 Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote”.

Kwahiyo ubatizo wa Maji ni kivuli cha Ubatizo wa Bwana Yesu, (wa kuzikwa kwake na kufufuka kwake). Kama vile Bwana alivyozikwa katika makosa yetu na kufufuka pasipo makosa yetu, na sisi tunapozama katika maji na kuibuka juu… katika ulimwengu wa roho, tunakuwa tumekufa katika utu wa kale na tumefufuka katika utu upya. (Dhambi zetu zinakuwa zimeondolewa, Matendo 2:38).

Tunakuwa tunatembea katika utukufu ule ule ambao Bwana Yesu alitembea nao baada ya kufufuka kwake.. Na katika ulimwengu wa roho tunakuwa tumeketi naye..

Waefeso 2:5 “hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema.

6 AKATUFUFUA PAMOJA NAYE, AKATUKETISHA PAMOJA NAYE KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, katika Kristo Yesu”

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Ubatizo Bwana alioumaanisha katika Luka 12:50 ni KUZIKWA na KUFUFUKA KWAKE. Na kabla ya huo kutimizwa ilipasa Bwana apitie mateso mengi (dhiki), kwa kukataliawa na kuteswa Kalvari, ndio maana anamalizia kwa kusema “nami nina dhiki kama nini hata utimizwe!”

Luka 9:22 “akisema, Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi, na kukataliwa na wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa NA SIKU YA TATU KUFUFUKA”.

Kufuatia maandiko hayo utaona ni jinsi gani ubatizo wa maji ulivyokuwa wa muhimu, na wala si wa kuupuuzia hata kidogo, Na maandiko yanasema mtu asipozaliwa kwa Maji na kwa Roho, (Yohana 3:5) hawezi kuurithi uzima wa milele. (na Kuzaliwa kwa maji ni ubatizo wa Maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo).

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/06/23/lakini-nina-ubatizo-unipasao-kubatiziwa-luka-1250-ni-ubatizo-gani-huo/