UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

UJUE UCHAWI WA MANABII WA UONGO?.

Kuna makundi mawili ya WACHAWI!.

 1. Wachawi wa kawaida wanaojulikana; wanaopaa na Nyungo, na kuloga na kuwanga!. Hawa wanamharibia mtu Maisha yake ya kimwili tu, kufanya mtu awe na kasoro fulani fulani za kimwili, au kimaisha.

2. Manabii wa Uongo: Hili ni kundi la Pili la wachawi!, ambalo ni hatari sana kuliko hilo la kwanza!.. kundi hili haliwalogi watu kimwili bali kiroho.. yaani kazi yake ni kumsababisha mtu aukose uzima wa milele kwa kuiacha Imani au kwa kutoijua imani.

Hili kundi la Pili, ndio lile Mtume Paulo alilolizungumzia katika kitabu cha Wagalatia na lile Bwana alilotuambia tujihadhari nalo.

Wagalatia 3:1 “Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?

2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?

3 Je! Mmekuwa wajinga namna hii? BAADA YA KUANZA KATIKA ROHO, MNATAKA KUKAMILISHWA SASA KATIKA MWILI?

Na Bwana Yesu alituonya tujihadhari na kundi hilo la Pili, Zaidi ya lile la kwanza.

Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali”.

Manabii wa uongo ni wachawi wanaologa roho, ambao wamevaa mavazi ya karama za Mungu, wanajiita wachungaji, waalimu, wainjilisti, waimbaji, wahubiri n.k lakini katika utu wao wa ndani ni waharibifu wa roho za watu!.

Hawa hawatakuonea wivu wewe kuwa Maisha mazuri hapa duniani, tena watakuhubiria hayo!, watakupaka na mafuta, na kukulisha chumvi, na udongo ilimradi tu, upate mafanikio, wala hawataona wivu wewe kuzaa Watoto, wala hawatakuonea wivu wewe kufurahi duniani, kama lile kundi la kwanza, ambalo halitaki ufanikiwe hapa duniani.

Manabii wa uongo!, wenyewe hawana shida na wewe kufanikiwa.. wenyewe wanashida moja tu kwako!.. kwamba USIURITHI UZIMA WA MILELE!!!!. Hilo tu!!

Hebu tujifunze kwa nabii mmoja wa uongo katika biblia, (aliyekuwa mchawi wa roho za watu), na kisha tutapata kujifunza zaidi…

Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, MCHAWI, NABII WA UONGO, Myahudi jina lake BAR-YESU;

7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, MTU MWENYE AKILI. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu.

8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), AKASHINDANA NAO, AKITAKA KUMTIA YULE LIWALI MOYO WA KUIACHA ILE IMANI”.

Umeona hapo kazi ya huyo mchawi (aliye nabii wa uongo) ni ipi?.. Haikuwa kumwangia na kumloga Sergio asiwe Tajiri, au asiwe na akili, au asiwe na Watoto, bali ilikuwa ni KUMTIA MOYO WA KUIACHA IMANI YA BWANA YESU!!!.

Ndugu, Manabii wa uongo hata leo wanafanya kazi hiyo hiyo!.. wanashikilia biblia, wanahubiri, na wana majina ya kikristo (kama huyu Bar-Yesu) na mbaya zaidi wanatoa mpaka pepo, lakini ndani yao ni wauaji wa roho!!..

Kaka/Dada usifurahie kufarijiwa na mhubiri anayekuambia kuwa mambo yote ni sawa na huku hayaoni maisha yako yaliyojaa uzinzi, usifarijiwe na mchungaji yeyote, au nabii, au mwalimu, au padri, anayekuambia kuwa wewe ni mtoto wa Mungu, unayependwa na ilihali wewe ni mwizi, ni mlevi, ni muabudu sanamu, ni mgomvi, ni mtu wa hasira, ni mtu wa kutosamehe, ni mtu wa vinyongo na mtazamaji pornography, ni mtu wa kujichua ni mtu wa kuvaa na kutembea nusu uchi.. Tambua kuwa wewe bado hujawa mtoto wa Mungu katika hiyo hali ya dhambi uliyopo.

Jua huyo mchungaji au mwalimu anayekufundisha hivyo, hakupeleki kwenye Imani, bali anakutoa kwenye Imani..

Hiyo ndio kazi kubwa ya manabii wa Uongo!. KUKUFANYA UKAE MBALI NA ILE KWELI, AU USIIELEWE KABISA!!. Na ubaya ni kwamba hawa manabii wa uongo, WENGI WAO wanaujua ukweli! Lakini kwasababu wapo kwaajili ya kazi waliotumwa na baba yao (ibilisi), basi ndio wanaendelea kuwapotosha watu makusudi..

Neno la Mungu linasema..

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU”.

Itafute kweli yote ya Neno la Mungu..na JIHADHARI NA MANABII WA UONGO!..

Bwana Yesu anarudi na hizi ni siku za Mwisho.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

Usimwache mwanamke mchawi kuishi! Biblia ilimaanisha nini?

Nini maana ya “Torati na manabii”?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
7 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Rois
Rois
2 years ago

Mungu atuhurumia nyakati hizi za mwisho manabii wa uongo wamekuwa wengi Sana makanisani na mikutano ya kishetani.
🙏🙏🙏

Anonymous
Anonymous
2 years ago

Amen sana mwalimu

Lutagomwa
Lutagomwa
2 years ago

Unanifanya kuwiwa kuwa mtumishi was kristo Bwana Yesu, injiri yako ina sisimua na kwa kila anae fatilia page yako hii nakuhakikishi lazima awe na matokeo mazuri
Ubalikiwe mtumishi

Emmanuel Kitengule
Emmanuel Kitengule
2 years ago

Barikiwa sana mwalimu kwa kazi kubwa ya kufundisha ile iliyo KWELI.Binafsi kila ninapopitia masomo haya huwa napiga hatua katika maarifa.