Nini maana ya “Torati na manabii”?

Nini maana ya “Torati na manabii”?

SWALI: Tukisoma katika maandiko tunaona sehemu kadha wa kadha likitajwa neno “Torati na manabii”. Sasa hii torati na manabii maana yake ni nini? Kwamfano  Mathayo 7:12  inasema

“Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii”.

JIBU: Bwana Yesu aliposema Torati na manabii, alimaanisha Agano la kale, ambalo ndio limeundwa na vitabu vya Musa (Torati), ambavyo ni vitano (5), Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na Kumbukumbu la Torati.  Pamoja na vitabu vyote vya manabii, kama vile, Yeremia, Isaya, Danieli, Ezekieli, Hababuki, Amosi, n.k. hapa ikijumuisha pia, vile vingine kama  Waamuzi, Zaburi, Ayubu, Wafalme,  Mithali, Ruthu n.k. Ambavyo sio moja kwa moja vya manabii, lakini vimebeba nabii za Mungu ndani yake.

Kwahiyo torati na manabii kwa ufupi ni lile agano lote la kale. Hivyo Pale Bwana Yesu alipokuwa anawafundisha juu ya kanuni za kufuata, alirejea biblia yao, akiwaambia kuwa kiini cha biblia hiyo ni UPENDO. Wala hakuna siri nyingine nyuma yake, Torati yote, pamoja manabii wote, walichokuwa wanahubiri ni Upendo, (Ambao umegawanyika, wa Mungu na wanadamu)

Hata sisi wa leo tulio katika agano jipya, tunaposoma biblia yote tujue Ujumbe mkuu tunaoupata katika agano letu ni ule ule UPENDO. Na ndio maana Mtume Paulo alisema.

1Wakorintho 13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.

2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.

3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu”.

Hivyo na sisi, tunapaswa tuutafute huu, kwa bidii zote, ili tuonekane kuwa wakamilifu mbele za Mungu.

Shalom

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments