Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

 Habari ya UZIMA? Naomba unisaidie tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu Kwa Sisi Tumwaminio/wafuasi wake. Je! Damu ya Yesu inakazi ya Kutulinda sisi au Mali zetu pale tunapoomba kupitia Damu? Ni sahihi kuomba hivyo? Je! Damu ya Yesu inatumikaje Kwa sisi wakristo?

JIBU: Ili kuelewa tofuati ya utendaji kazi wa damu ya YESU na Jina Jina la Yesu, Ni vizuri kwanza tukajifunza katika maisha ya kawaida…Katika maisha ya kawaida mtu anayo DAMU na vilevile analo JINA…Jina la mtu linaelezea utambulisho wa mtu yule, cheo alicho nacho, heshima aliyo nayo, nguvu aliyo nayo na mamlaka aliyonayo.. Kwamfano katika nchi yoyote mtu mwenye jina kubwa na lenye nguvu kuliko wote ni Raisi wa nchi hiyo…

Vilevile katika upande wa pili DAMU ya mtu inaelezea Uzima wa huyo mtu, asili ya mtu huyo, Undugu alionao na wanafamilia wenzake, na inaelezea pia Urithi alionao..yaani watu atakaowarithisha mali zake.

Na kila Raisi wa nchi au Mfalme, anayo DAMU na vilevile analo JINA.

Sasa tukirudi katika mamlaka ya kimbinguni ambayo hiyo ni kuu kuliko ya kiduniani…Tunaye Mfalme mmoja, naye ni Yesu Kristo (Huyo ni Zaidi ya Raisi yeyote wa nchi)…Na huyu analo JINA vilevile na anayo DAMU.

Kama tulivyosema damu inaelezea undugu wa mtu, yaani uana-familia.….na Bwana Yesu pia anao ndugu zake wa damu,..ambao ni wale wote waliozaliwa mara ya pili…Hao wanayo mamlaka ya kumsogelea katika meza yake na kula naye, na kumwomba lolote kwa jina lake na kupewa…Mtoto wa mfalme akiomba apewe jimbo fulani kutoka kwa Baba yake…haitachukua mlolongo mrefu kupewa haja ya moyo wake..mara moja tu baba yake atamwandikia hati ya nakala kwa jina lake na kuipeleka mahali husika kupata anachokihitaji…Na huyo mtoto kwa jina la Baba yake anaweza kupata lolota katika nchi…..Lakini hebu mtu wa kawaida tu amsogelee mfalme wa nchi na kumwomba apewe hicho kipande cha ardhi uone mlolongo wake!…anaweza kufukuzwa au hata asipofukuzwa basi ombi lake linaweza kuchukua muda mrefu sana kujibiwa…

Sasa yote hayo ni kutokana na nini?

Ni kutokana na kwamba mtoto wa Mfalme anatumia DAMU kupata lolote kwa JINA la Baba yake…wakati wengine wanatumia bahati tu!..kwamba ombi lao likikubaliwa ni kama wamepata bahati tu!..wangeweza kukataliwa…lakini mtoto wa Mfalme anauhakika kwasababu anatumia damu.

Kwahiyo tukirudi kwenye swali: Tofauti kati ya damu ya Yesu na jina la Yesu ni ipi? Tumeshaiona hapo juu na …na je ni sahihi kuomba kutumia damu ya Yesu kutulinda sisi na mali zetu? (damu ya Yesu inatumikaje)

Jibu: Mtu aliyeokoka tayari damu ya Yesu inanena mema juu yake..kama kwa hiyo mifano tuliyoiona hapo juu…Haihitaji kumweleza sana Baba wa mbinguni kwamba unahitaji ulinzi..kitendo tu cha kuwa mwanawe wa damu tayari ni jukumu lake kukulinda wewe na mali zako..na kwa jina lake kupewa chochote katika huu ulimwengu..Tofauti na mtu ambaye hajaokoka…huyo si mwana wa Mungu,..huyo hana uhusiano wowote na damu ya Mungu…Kwahiyo hata akiomba lolote kwa jina la Yesu kwake ni bahati nasibu kupata anachokiomba…

Je umeokoka?…

Umefanyika kuwa mwana wa Mungu?..umekuwa damu moja na Mungu?..Kama hujaokoka basi fahamu kuwa ni ngumu wewe kupokea upendeleo wowote kutoka kwa Mungu..Kwasababu Mungu anawaangalia kwanza wanawe kuwapatia mema (Soma Warumi 8:28-29)..na hao ndio atakaowarithisha uzima wa milele…hawezi kuwarithisha watu wasio wanawe…hata wewe mwenyewe ni ngumu kumrithisha mtoto asiye wako mali zako na kuwaacha wanao bila urithi…

Sasa kwanini uwe kama Yatima siku ile?..wakati wenzako wanairithi mbingu…wewe unarithi ziwa la moto kutoka kwa baba yako ibilisi?..mwache shetani aende kuzimu mwenyewe wewe mgeukie Kristo, mwenye urithi udumuo.

Hivyo unachopaswa kufanya ni kutubu kama hujatubu, kama ulikuwa ni mwasherati unatubu kwa kuacha kufanya hivyo, kama ulikuwa unaweka make-up unaacha, kwasababu mabinti wa Mungu waliozaliwa kwa damu ya Mungu hawafanyi hivyo, ..kama ulikuwa unasuguliwa kucha na wanaume saloon, utubu na kuacha,.., kama ulikuwa unavaa vimini, unapamba uso, unavaa surali, unatubu na kuacha kama ulikuwa ni mlevi, mvutaji wa sigara na mfanyaji masturbation na mtazamaji wa picha chafu katika mitandao unatubu na kuacha, kama ulikuwa ni mwizi vivyo hivyo…

Na baada ya kutubu kwa kudhamiria kabisa na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu. …utakuwa umezaliwa mara ya pili na kuhesabika mwana-familia wa familia ya kimbinguni. Na hivyo kuwa mrithi, na ile damu ya thamani isiyoisha muda wa matumizi, damu ya Yesu Kristo itaanza kunena mema juu yako.

Na hivyo hata ukiitamka jambo lolote kwa jina lake utapata.

Bwana akubariki.

Tafadhali share na wengine Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Sarah
Sarah
1 year ago

Amina barikiwa sana mtumishi