JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

Je! ni dhambi kuimba wimbo wa Taifa hata kama umetungwa kidunia?.Na je ni dhambi kwa watoto wa kikristo kuimba zile nyimbo za chekechea?

JIBU: Nyimbo karibia zote za kitaifa hazijatungwa kidunia… Nyingi zilitungwa wakati au baada kidogo ya uhuru wa Taifa husika..Zilikuwa ni nyimbo za Kumshukuru Mungu na kulitakia amani, baraka na mafanikio Taifa husika. Hivyo nyimbo nyingi zilitungwa kama sala iliyo katika mfumo wa kama wa wimbo hivi.

Hakuna wimbo wowote wa Taifa lolote duniani..unaiombwa kwa lengo la kunyanyua hisia za uasherati, wala kutukana kama nyimbo zinazotungwa siku hizi, wala kwa lengo la kujiburudisha, wala kutafuta fedha, wala kujulikana…Hata wengi wa watunzi wa nyimbo hizo hazikuwa mali zao wenyewe kwamba wana hati miliki nazo..bali zilikuwa ni mali za Taifa.

Lengo lingine pia la nyimbo hizo, zimetungwa kuinua morali ya kufanya kazi, kuishi kwa umoja, upendo na kuliheshimu Taifa.

Hivyo hakuna ubaya wowote wa kuimba wimbo wa Taifa mahali popote.

Na sio tu nyimbo za Taifa, bali hata nyimbo za Chekechea (Nursery) kwa watoto wa kikristo.

nyimbo za chekechea

Mtoto wa kikristo si dhambi kushiriki nyimbo za shuleni na watoto wengine..Maadamu nyimbo hizo zimejulikana ni za kimaadili na za kujifunza na zipo katika mtaala wa shule!..Lakini nyingine zozote zilizosalia za kidua ambazo si za kielimu wala si za kiheshima, wala hazipo katika mtaala wowoe wa kishule watoto wa kikristo hawaruhusiwi kushiriki wa vyovyote vile.

Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NYIMBO ZA WOKOVU

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

TENZI ZA ROHONI

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments